Kwa wengi tunajua Franco alifariki kwa ukimwi,
Lakini kuna taarifa zingine zinakinzana na taarifa hiyo.
Kuna baadhi ya taarifa zinasema kifo hicho kilisababishwa na maelewano mabaya kati yake na Mobuttu,
Na mtu aliyefanikisha mipango ya kuweka sumu katika mic ya Franco ni MTU wake aliyempenda sana Madillu.
Ukiangalia Franco aliugua na kupungua haraka sana, mashavu yake yalibonyea kwa ndani kwa haraka sana pia kama mtakumbuka wakati wa kutoa albam ya forever akiwa na Sam Mangwana alikuwa kapungua ghafra.
Inasemekana Madillu alipewa cheki tupu na kutakiwa ajaze mwenyewe kiasi anachohitaji toka kwa Mobutu, alijaza US$ 500,000 na kazi akaifanya,
Na kuhamia Marekani, na kuna baadhi wanasema baada ya kifo cha Franco, Madillu aliimba nyimbo nyingi za kumuomboleza rafiki na kiongozi wake wakati akijua ni yeye alihusika kwa tamaa ya pesa.
Kifo cha mtu maarufu huacha simulizi nyingi za kweli na zisizo na ukweli, hivyo kila mmoja anaweza kuamini sehemu au chanzo cha habari anachokiamini.