Uhusiano wa Franco na Mobutu

Uhusiano wa Franco na Mobutu

Kwa wengi tunajua Franco alifariki kwa ukimwi,
Lakini kuna taarifa zingine zinakinzana na taarifa hiyo.

Kuna baadhi ya taarifa zinasema kifo hicho kilisababishwa na maelewano mabaya kati yake na Mobuttu,
Na mtu aliyefanikisha mipango ya kuweka sumu katika mic ya Franco ni MTU wake aliyempenda sana Madillu.

Ukiangalia Franco aliugua na kupungua haraka sana, mashavu yake yalibonyea kwa ndani kwa haraka sana pia kama mtakumbuka wakati wa kutoa albam ya forever akiwa na Sam Mangwana alikuwa kapungua ghafra.

Inasemekana Madillu alipewa cheki tupu na kutakiwa ajaze mwenyewe kiasi anachohitaji toka kwa Mobutu, alijaza US$ 500,000 na kazi akaifanya,
Na kuhamia Marekani, na kuna baadhi wanasema baada ya kifo cha Franco, Madillu aliimba nyimbo nyingi za kumuomboleza rafiki na kiongozi wake wakati akijua ni yeye alihusika kwa tamaa ya pesa.

Kifo cha mtu maarufu huacha simulizi nyingi za kweli na zisizo na ukweli, hivyo kila mmoja anaweza kuamini sehemu au chanzo cha habari anachokiamini.
Historia ya africa ina complications nyingi,,nimependa conclusion yako mkuu
 
dah Jamaa alikula bata
Sana,,alikua na nyumba zingine inapita hata miaka 3 hajazitembelea,

Mkewe anatajwa kuwa na nguo zaidi ya elfu moja,
Mkuu ukitaka mengi kitafute kitabu kinaitwa a la cour de mobutu,kimeandikwa na pierre jansen,mpwa wake
 
naam huyu ukimwi ulimuua mwaka 1998 pale Monaco
aligegeda kila aina ya binti aliempenda na alikuwa na uwezo wa kwenda shule fulan anaopoa binti anaenda Ku gegeda bila MTU yoyote kumuiliza,alikuwa moja ya ma body guard wa Mobutu Babae
Jamaa naitafuta historia yake mtandaoni ipo fupi mno,but siku moja ntaenda kinshasa nikapige stori na jamaa zake nimjue vizuri
 
Mkuu Lucas Mobutu sina nia ya kukosoa bandiko lako but hapo kwenye wimbo Candidat Na Biso Mobutu naomba niongeze nyama kidogo kuhusu huu wimbo.

Baada ya kutoa wimbo wa kumtuhumu rais Mobutu kwa uongozi wake wa mkono wa chuma iliamriwa Frànco akamatwe atiwe jela,kisha Mobutu akampa options mbili either atumie kipaji chake kutunga wimbo mzuri utakaomfanya azidi kupendwa na wananchi wake au aendelee kukaa jela{tukumbuke huu wimbo wa kum-dis Mobutu ulipokelewa vizuri sana na masahabiki wa Frànco so nikama aliambiwa atafute kitu cha kuyafuta yale mawazo mabaya kwa wananchi kisha apandikize mazuri yanayomuhusu yeye}.

Ndipo alipotunga huu wimbo canditad na biso Mobutu na inasemekana Mobutu alipousikiliza kwa mara ya kwanza tu aliamuru Frànco atolewe jela upesi sana na apelekwe ikulu ambako ilifanyika sherehe ya kukata na shoka kwa muda wa siku tatu kisha Mobutu akataka ampe Frànco madaraka ya kisiasa ambapo aliyakataa akaomba apewe ruhusa ya kufanya shughuli zake za kimuziki kwa uhuru tu.

Copied.......
 
Wakuu habarini za muda huu,

View attachment 717548
View attachment 717549

Zimeanzishwa thread nyingi kuhusu Franco na Mobutu, historia ya Mobutu imeelezwa na ya Franco pia, leo naleta historia ya uhusiano wa watu hawa wenye majina makubwa Africa na ulimwenguni, mwanasiasa na gwiji la muziki.

View attachment 717532
View attachment 717529

KUNYONGWA KWA KINA EVARISTE KIMBA

Mnamo mwaka 1965 Mobutu anakua rais wa Zaire na kuagiza kunyongwa kwa watu zaidi ya 6 wengi wao wakiwa mawaziri wa serikali aliyoipindua katika eneo la matonge jijini Leopold Ville (Kinshasa) kwa kosa la uhaini, mamilioni ya watu wanashuhudia hadharani, mmoja wao ni Franco, baada ya hapo Franco akatunga nyimbo iitwayo Luvumbu Ndoki (Luvumbu mchawi) hii ni hadithi ya kikongo kuhusu Mfalme Luvumbu aliyeuwa ndugu zake wa karibu kwa ajili ya kujinufaisha.

Nyimbo hii inaonekana na mamlaka kama dhihaka kwa mobutu kutokana na kitendo chake cha kunyonga mawazili wale Franco anakamatwa na kuachiwa alafu anakimbilia Brazaville kwa miezi 6 mpaka pale mambo yalipokuwa shwari.

AUNTHENTICATION POLICY (Zairenisation)

Mnamo mwaka 1971 mobutu anabadili jina la Congo kuwa Zaire, sarafu kua Zaire, pamoja na miji kuitwa majina ya kiafrika, Leopoldville inakua Kinshasa, Elizabeth Ville inakua Kisangani na kadhalika, kutokana na sera ya uafrika mpaka majina ya watu yanabadilishwa.

Bendi ya Franco, Tp Ok jazz inaandamana na mobutu nchi nzima kueneza sera ya mobutu na kutoa album iitwayo belela unthenticite na congress ya mpira.

MALIPO YA KAZI

Mobutu anampa Franco eneo la ardhi pale Kinshasa, Franco anajenga night club iliyoitwa un Deux trois, pia Mobutu baada ya kubinafsisha kampuni za kigeni anampa Franco kampuni ya muziki iitwayo mazadi.

JACKY NA HELEINE(nyimbo za Franco)

Franco añatoa nyimbo mbili Jacky na heleine ambazo serikali iliziona hazina maadili na kumpa Franco kifungo cha miezi 6 jela, na bar yake kufungwa miezi 2, alivobisha kua hazina maadili mama yake alisikilizishwa, yote haya yalifanywa na Kengo wa Dondo aliyekua attorney general.

Mobutu anamtoa jela Franco baada ya week 3 na kumshusha cheo Kengo wa Dondo kua balozi wa Zaire nchini Ubelgiji, Franco anaimba nyimbo ya kumponda Kengo iitwayo trailleur (anasema fundi nguo akikinyanganya sindano utawachomaje watu? Yaani kengo kaporwa madaraka na Mobutu)

Franco anaimba lettre a mr le directeur general (barua kwa director general) nyimbo ambayo añawaponda viongozi wa serikali kwa rushwa na usimamizi mbovu, hii inachukuliwa na wengi kama diss song kwa Mobutu.

Mwka 1984 anaimba nyimbo ya kumsifu Mobutu iliyoitwa Candida na biso, wakati wa uchaguzi ambapo watu walitakiwa kujibu ndio au apana kama wanamtaka Mobutu, hakukua na wapinzani.

Mobutu alifadhili band nyingi kubwa za muziki nchini Zaire, ikiwemo TP OK JAZZ


KIFO CHA FRANCO

Franco anafariki jijini Ubelgiji mwka 1989, Mobutu akiwa Ufaransa ziarani,
Mobutu anatangaza siku 4 za maombolezo na radio zote kupiga nyimbo za Franco tu, mwili wa Franco unapelekwa Palais du people kuagwa
View attachment 717547

Mobutu aliporudi aliitembelea familia ya Franco pamoja na kaburi.

Kwa kiasi kikubwa Mobutu alimtumia Franco katika ku mobilize watu kwenye siasa zake na pia Franco alinufaika sana kwa kuendesha magari ya kifahari kama mercedes benz na kuishi vizuri, kuliko wanamuziki wengi wa Congo na nje ya Congo
Sor buroho ivi Mobutu ni mzee wako wa kukuzaa?
 
Mkuu Lucas Mobutu sina nia ya kukosoa bandiko lako but hapo kwenye wimbo Candidat Na Biso Mobutu naomba niongeze nyama kidogo kuhusu huu wimbo.

Baada ya kutoa wimbo wa kumtuhumu rais Mobutu kwa uongozi wake wa mkono wa chuma iliamriwa Frànco akamatwe atiwe jela,kisha Mobutu akampa options mbili either atumie kipaji chake kutunga wimbo mzuri utakaomfanya azidi kupendwa na wananchi wake au aendelee kukaa jela{tukumbuke huu wimbo wa kum-dis Mobutu ulipokelewa vizuri sana na masahabiki wa Frànco so nikama aliambiwa atafute kitu cha kuyafuta yale mawazo mabaya kwa wananchi kisha apandikize mazuri yanayomuhusu yeye}.

Ndipo alipotunga huu wimbo canditad na biso Mobutu na inasemekana Mobutu alipousikiliza kwa mara ya kwanza tu aliamuru Frànco atolewe jela upesi sana na apelekwe ikulu ambako ilifanyika sherehe ya kukata na shoka kwa muda wa siku tatu kisha Mobutu akataka ampe Frànco madaraka ya kisiasa ambapo aliyakataa akaomba apewe ruhusa ya kufanya shughuli zake za kimuziki kwa uhuru tu.

Copied.......
Ahsante sana mkuu kwa mchango wako
 
Kama kumbukumbu zangu ziko vizuri ni kwamba UKIMWI uliingia Afrika miaka ya 80, sasa ikawaje UKIMWI huo huo ambao tunambiwa na watalaam huchukua miaka nane tangu kuambukizwa ndo dalili zake zionekane ukagharimu maisha ya Franco ndani ya miaka hiyo ya 80..Niko tayari kurekebishwa..Vinginevyo shukrani zimwendee aliyetuletea historia hii na pia wale wote ambao hawakusita kuchangia pale ambapo waliona wana cha kuchangia na wale pia waliouliza maswali yaliyopelekea historia hii kuongezewa nyama.
Mkuu ktk hili una point ila tusisahau hata sasa ukipimwa ukakutikana na maradhi haya doctor ktk moja ya masharti atakayokusisitiza sana ni wewe kuifunga zipu yako na kufanya yale ya muhimu tu kwa ajili ya afya yako.

Hawa wazee wetu kwa umaarufu waliokuwa nao na nyimbo za mapenzi walizokuwa wanaimba ziliwafanya wanawake wawapende mno,mnoo!ilifikia kipindi wakishuka jukwaani tu wanawake wanawagombania mpaka kuchaniana nguo ili wakawape mzigo.

Sasa ktk mazingira kama haya angekaaje miaka 10 hali yakuwa kila siku alikuwa anachuja nafaka na lady's tofaut tofauti huku akiishi maisha ya starehe pombe na misigara,kuna mwaka nilisikiliza interview ya marehem Dr Remmy akisema kipindi anawika ilikuwa kawaida kwenda msalani na kukutana na mrembo akimsalimia tu anam'bong'olea mzee anapiga show kisha anamwachia pia wakati wa kuondoka anakokota mmoja au wawili wa kuspend nae mpaka asubuhi.

Zamani watu walijitoa ufahamu sana...
 
Mkuu ktk hili una point ila tusisahau hata sasa ukipimwa ukakutikana na maradhi haya doctor ktk moja ya masharti atakayokusisitiza sana ni wewe kuifunga zipu yako na kufanya yale ya muhimu tu kwa ajili ya afya yako.

Hawa wazee wetu kwa umaarufu waliokuwa nao na nyimbo za mapenzi walizokuwa wanaimba ziliwafanya wanawake wawapende mno,mnoo!ilifikia kipindi wakishuka jukwaani tu wanawake wanawagombania mpaka kuchaniana nguo ili wakawape mzigo.

Sasa ktk mazingira kama haya angekaaje miaka 10 hali yakuwa kila siku alikuwa anachuja nafaka na lady's tofaut tofauti huku akiishi maisha ya starehe pombe na misigara,kuna mwaka nilisikiliza interview ya marehem Dr Remmy akisema kipindi anawika ilikuwa kawaida kwenda msalani na kukutana na mrembo akimsalimia tu anam'bong'olea mzee anapiga show kisha anamwachia pia wakati wa kuondoka anakokota mmoja au wawili wa kuspend nae mpaka asubuhi.

Zamani watu walijitoa ufahamu sana...
Hahahaha,,
 
labda umesahau,hebu fwatilia historia ya mpongo love,mwaka 1977 Franco alimsajili mpongo ktk band alikaa miaka miwili okk jazz,hata wimbo wake "ndaya"aliutunga kwa msaada wa Franco,hebu fwatilia
mpongo love alifariki 1994
Google wanasema alikata moto 1990 nadhani ilitokana na shock ya mzee baba nae kuonekana ameenda kwa maradhi yasiyo ya starabu.walipishana miezi tu!
 
Huu uzi mtamu sana baada ya miaka mingi kupita na wote kuwa marehemu leo ndani ya jf nakutana na Lucas mobutu(akiwakilisha rais mobutu)
na wewe bwana luambo makiadi (ukimwakilisha franco luambo makiadi)

Long live jf
..........Bila kumsahau Thomas @sankara,huyu walimuuwa ila alikuwa rais kijana mwenye muono wa mbali sana.inafurahisha sana mkuu na hawa ni watu kwa kiasi kikubwa wametupa heshima kubwa kimataifa ila Mobutu alizingua sana.
 
..........Bila kumsahau Thomas @sankara,huyu walimuuwa ila alikuwa rais kijana mwenye muono wa mbali sana.inafurahisha sana mkuu na hawa ni watu kwa kiasi kikubwa wametupa heshima kubwa kimataifa ila Mobutu alizingua sana.
Thomas sankara kiongozi kijana kabisa mwenye maono ya mbali sana akishika uongozi wa juu kabisa wa burkina fasso wakati huo ikiitwa upper volta akiwa na miaka 31 tu.

Huku akitawala miaka 4 tu 1983-87
Akiuwawa na rafiki yake kipenzi aliyekuja baadae kuwa rais wa nchi hiyo blaise compaore.

Lakini angalia ajabu ya mungu nae baada ya miaka 27 ya kutawala Compaore ndani ya mwezi ule ule wa oktoba aliompindua na kumua rais Sankara ndani ya mwezi huo huo japo miaka na siku tofauti naye alipinduliwa na kulazimishwa kukimbia burkina fasso.

Kwa hakika ndani ya maisha ya rais huyu kijana Thomas Sankara tunayo ya kujifunza mengi.
 
Back
Top Bottom