Nchi nyingi za wenzetu vyakula vya kikwetu ambavyo miaka ya nyuma ilikuwa ni ngumu sana kuvipata labda mpaka kwenye maduka ya wahamiaji siku hizi vimejaa belele tena kwenye supermarkets ni pumzi yako tu kama unathamini kula vyakula vya kikwetu au kama unataka kula uchafu wa vyakula vinavyotengenezwa kwa dakika tatu burger na fries. Huwa nawashangaa sana wanaosema ugali ni chakula cha kimaskini, sasa sijui ni kipi ni chakula cha kitajiri. Na kama unapenda kula ugali hata ukiwa tajiri bado utautamani tu ugali kwa nyama choma nzuri sana/samaki pembeni kuna mchicha....Acha unashusha mlima taratibu tena kwa raha zao siyo haya mavyakula hata ukiwa na njaa bado havikutamanishi.