Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

Nisamehe sana,nilikuwa vijijini kwa muda mrefu kidogo kwa ajili ya mambo yetu haya ya kilimo. Miezi mitatu iliyopita niliweka sato 26 vifaranga,mpaka jana tumerecord sato mmoja kafa,kwa hiyo imenipa nguvu kwamba bwawa langu liko mahali sahihi kabisa kilichobaki ni maboresho,hasa aina ya chakula.

Mwezi juni nilipata Kambale 52,nimewaweka ktk visima vidogo,huku nasubiri bwawa jipya likae sawa,yaani lijijenge kupokea wageni. Kwa mwezi mzima sasa hakuna kambale aliyekufa. Nitakwenda Mbegani/ kunduchi nikachukue shule zaidi ili nifuge kwa wingi. Hapo nitapata mbegu ya kuuza. Mwaka jana kigogo mmoja alikosa mbegu ya kambale,tulitafuta sana bila mafanikio.

Pili,pale Kinguruila gerezani pana mbegu ya samaki inauzwa kwa bei nzuri sana,kifaranga kimoja Tsh 30/ sio 300 kama huku Mkuranga. Contact za mhusika nimepata,kwa aliye tayari aniambie nimpe.

Kwa ujumla ninafurahia kufaulu mtihani wa kwanza,yaani pilot trial niliyofanya.
Karibuni SUA Morogoro utalaam wote utapata free idara ya uzalishaji wanyama (DASP)
 
Sokoine University of Agriculture idara ya uzalishaji wanyama (DASP) ndo inaongoza kwa sasa hapa Morogoro kwa vifaranga bora vya sato na kutoa elimu buree kwa wafugaji wanaoanza na wanaoendelea
 
bado tupo under experimental phase, hatuna sera iliyowazi juu ya ufugaji wa hivi viumbe vya majini, aquaponics ni nzuri, cage farming ni nzuri pia lakini vyote hivi athari za kimazingira bado utafiti haujafanywa kwa hapa Tanzania. Mabwawa kwa sasa ndo kila kitu.
 
Habari wakuu!
Naomba ushauri juu ya ufugaji wa samaki, uandaaji wa bwawa na upatikanaji wa chakula. Pia nifahamishwe utunzaji wa bwawa hasa maji je hubadilishwa? Sehemu ya kichanga je yafaa kwa bwawa?

Gharama za uandaaji bwawa zipoje? Hasa bwawa la kuhifadhi samaki walau 3000 hadi 5000 hivi.

Nawasilisha kwa ushauri wenu.
 
Mpendwa hongera kwa mawazo mazuri. Mimi ndiyo niko kwenye pioneering stage ya huo mradi ila nilijifunza mengi toka kwa wadau mbalimbali humu JF. Samaki wangu wana kama miezi 3hivi.

Nakushauri kwenye search box uandike ufugaji wa samaki au pia unaweza ku-google utapata materials nzuri za kuanzia.
 
Mpendwa hongera kwa mawazo mazuri. Mimi ndiyo niko kwenye pioneering stage ya huo mradi ila nilijifunza mengi toka kwa wadau mbalimbali humu JF. Samaki wangu wana kama miezi 3hivi. Nakushauri kwenye search box uandike ufugaji wa samaki au pia unaweza ku-google utapata materials nzuri za kuanzia.

Mkuu vifaranga ulichukua wapi? Nataka tushee kitu kwa manufaa ya wote
 
Muda si mrefu naanza huu mradi, ila nahitaji mtaalam wa kukagua eneo langu, useful sred indeed.
 
Ukitaka working demo ya hii kitu ipo inafanya kazi hapa Dar so welcome to have a look at it
Pia ukiitaji automatic system ya kuzalisha vitoto vya samaki(full Automatic) tuwasiliane mkuu

Nashkuru kwa ukaribisho wa kuona at least demo ya iyo acquaphonic system. Mi nipo dar natamani kuona
 
Habari. Kumekua na uhadimu wa watu wenye utaalamu wa maswala ya ufugaji wa samaki.wengi wamekua wakifuga pasipo kujua namna halisi ya kufanya ili kufuga kwa faida...hivyo nikiwa kama mtaalamu wa secta iyo kutoka chuo kikuu cha dar es salaam.napenda kuwaarifu yoyote mwenye uhitaji wa huduma hiyo awasiliane na mimi..kwa namba zifuatazo 0717451771..tutakusaidia kupata mbegu bora.jinsi ya kujenga bwawa na kutengeneza chakula bora cha samaki wako..ili upate faida kwa wakati..ushauri pia unapatikana..kwa uhitaji wasiliana na mimi.
 
Habar ndugu.binafsi ni mtaalamu wa maswala ya ufugaji wa viumbe wa majin wakiwmo samak.toka chuo.kikuu cha dsm..Sikushauri utumie gogle kupata ufahamu ni mana mazingira yanatofautiana baina ya eneo na eneo.ninawez kukusaidia vifaranga bora.vya monosex wa tilapia.na mambo mengne kama.ulishaj.na kadhalika.wasiliana.na mm.0717451771 muhala fadhili
 
Back
Top Bottom