Ufugaji wa Samaki: Pata ushauri, mawazo na michango kuhusu ufugaji samaki. Jifunze changamoto, utaalamu na masoko ya Samaki

kama kichwa cha habari kinavyosema ninataka kusaidiwa juu ya ufugaji huu kwenye haya mambo
1; hali ya hewa inayowafaa hawa samaki hususani sangara
2; kina cha maji kwenye bwawa
3; upatikanaji wa chakula pia chakula gan kinawafaa
4; wanahitaji madawa pia wanaweza kushambuliwa na wanyama wengine kwenye maji
5; changamoto katika ufugaji huuu
pia kama kuna mtu ambae tayari ana miliki bwawa na hawa samaki mkoa wa pwani a PM nikajifunze zaid site
 
Wakuu kwema humu? Nahitaji kujua gharama ya sasa ya vifaranga vya samaki monosex bei kwa kifaranga ni sh ngapi sasa? na reliable dealer anapatikana wapi? na chakula chao bei yake ni sh ngapi kwa sasa mimi napatikana DSM, mkuu bukoba boy msaada wako unahitajika kama unataarifa yoyote najua wewe ni mdau mkubwa kwenye sekta hii.
 
je hali ya hewa ni ipi zuri kwa mfano iringa mufindi inafaa kwa samaki au kilimanjaro moshi hali ya hewa inafaa kwa ufugaji samakii? Naomba msaada wenu.
 
Mkuu mleta mada naomba kujua kwanini vifaranga vya kambare vinabei kubwa yaani 500?wakati sato ni 300?
Vifaranga hivyo vina bei kwa sababu kwanza uzalishaji wake unahitaji uangalizi wa juu, pia wanalelewa kwa muda mrefu mpaka kufikia umri wa kuweza mkulima kwenda kufuga.

Hata, hivyo ukifuata uhalisia gharama ya kuzalisha vifaranga haiwezi kuwa ghali kama tunavyouziwa kwa hao kambale na sato
 
Wakuu kwema humu? Nahitaji kujua gharama ya sasa ya vifaranga vya samaki monosex bei kwa kifaranga ni sh ngapi sasa? na reliable dealer anapatikana wapi? na chakula chao bei yake ni sh ngapi kwa sasa mimi napatikana DSM, mkuu bukoba boy msaada wako unahitajika kama unataarifa yoyote najua wewe ni mdau mkubwa kwenye sekta hii.
Gharama ya monosex ni sh 300 kwa kifaranga. Wapo dealers wengi mfano Mzee Noni yupo vikindu (huyu mnapigiana gharama ya usafiri anakuletea hadi shambani); yupo mzee Eden yupo Chanika; yupo ruvu fish farm yupo ruvu bagamoyo. Hao wote wapo vizuri. Wapo wa mikoani lakin kwakuwa upo Dar basi pokea hao.

Chakula wapo Farmers Centre Buguruni (1,800-2500/kg); Ruvu fish farm (3500/kg); Noni ( 2900/kg), Hills (4000/kg). Good news kuna kiwanda kinajengwa Moshi itakuwa chini ya hapo.
 
je hali ya hewa ni ipi zuri kwa mfano iringa mufindi inafaa kwa samaki au kilimanjaro moshi hali ya hewa inafaa kwa ufugaji samakii? Naomba msaada wenu.
Mkuu samaki aina ya sato na kambale wanahitaji jotoridi kati ya 26-33 ili waweze kukua vizuri. Chini ya hapo kasi ya ukuaji inakuwa ya chini. Katika Mikoa tajwa unawza kufuga kwa msimu kwa samaki hao tajwa.

Isipokuwa kuna samaki anaitwa trout unaweza kufuga lakn vifaranga ndio shida. Tembelea kwa afisa huska hapo Kilimanjaro na kwa Iringa nenda Songea
 
  • gharama kwa ujumla kama mimi nataka kufuga kulimo cha biashara . gharama average(general) zinakuwaje?
  • na sehemu ninapoweza pata hao samaki wa kuanzia? nipo morogoro.
Morogoro tembelea kituo cha serikali pale Kingolwira. Gharama inategemea na aina ya udongo katika eneo lako. Mfano ukipata eneo lenye udongo wa mfinyanzi basi bwawa ni la kuchimba tu hivyo gharama ni ya excavator au vibarua tu.

Sasa hapo itatofautiana kulingana na ukubwa wa bwawa. Udongo ukiwa wa kichanga itabidi ujengee bwawa au kuweka nylon sheet kuzuia upotevu wa maji, hivyo gharama ni kubwa.

Kwa bwawa la ukubwa wa 20m kwa 30m bwawa la kujengea kwa cement ni kama mil 5 hadi 6. Tafadhali waone wataalam kituo cha kingolwira
 
natamani sana kufuga samaki,je maeneo ya rufiji yanafaa?na upatikanaji wa maji vibali naazaje?na mtaji wa wastani sh ngapi ili uweze uza kwa faida angalau?
Maeneo ya rufiji kando ya maeneo ya mto yanafaa na yana udongo wa mfinyanzi.

Hivyo gharama ya kuchimba bwawa ni ndogo (hapa tafadhali muone bukoba boy akuchanganulie). Vibali- kwanza pata eneo kwa kununua au kupitia serikali ya kijiji. Halafu, kama mradi ni mkubwa utaomba kibali cha maji kupitia bonde la mtu rufiji ila kama mdogo chini ya hekta tano za mabwawa una haja.......tafadhali tembelea wizara ya kilimo
 
Gharama ya monosex ni sh 300 kwa kifaranga. Wapo dealers wengi mfano Mzee Noni yupo vikindu (huyu mnapigiana gharama ya usafiri anakuletea hadi shambani); yupo mzee Eden yupo Chanika; yupo ruvu fish farm yupo ruvu bagamoyo. Hao wote wapo vizuri. Wapo wa mikoani lakin kwakuwa upo Dar basi pokea hao. Chakula wapo Farmers Centre Buguruni (1,800-2500/kg); Ruvu fish farm (3500/kg); Noni ( 2900/kg), Hills (4000/kg). Good news kuna kiwanda kinajengwa Moshi itakuwa chini ya hapo.
Unaweza nisaidia contacts zao mkuu?? nasikia huwa wanatabia ukitaka monosex wanakuchanganyia hii changamoto unaweza epuka nayo vipi ndugu?

Na kwenye chakula hivyo vyakula vyote huwa vipo in form of pallets maana niliwahi sikia Hills wao ndio chakula chao huwa in form of pallets hiyo imekaeje ndugu??
 
Helo wadau.. niko dar kuna eneo langu lina maji ya kutosha yasiyo kauka kwa mwaka mzima...sasa nimefikiria kuanza ufugaji wa samaki, je nitapata wapi vifaranga kwa hapa dar na ni bei gani kwa kifaranga?na kati ya sato na sangara samaki gani ni mzuri kufugwa hapa dar? Na vipimo kina na sides vya bwawa ni kiasi gani kwa samaki 200?
 
Eden fish farm-pugu, Tsh 300@samaki
Polopolo fish farm Tsh 300@samaki
Utakopeshwa na vifaa vya kubebea,

Udsm ilikua 150, sijui kwa sasa hivi,.. ubebaji unajitegemea.

NB. Hiyo ni kwa kifaranga cha sato

Kina cha bwawa ni 1m,
Kwa ufugaji wa kawaida 1m square inabeba samaki 3-7,
 
Mahesabu ya kwenye karatasi matamu sana! Ila bahati mbaya hayajawahi kumwacha MTU salama!
Unafukua makaburi? Kumbuka ule msemo mali bila Daftari hupotea... So Biashara lazima uiandike mkuu... acha kujidanganya labda uwe na biashara ya kukata vimeo
 
Back
Top Bottom