Ufafanuzi wa tukio lilotokea jioni ya leo kwenye Anga la Tanzania, Teknolojia inazidi kukuwa, Watanzania tunaachwa nyuma tunabaki kushangaa

Uncle bright

JF-Expert Member
Feb 9, 2023
1,040
4,080
Siku ya leo jioni kumekuwa na taharuki baada ya watu kuona vitu vilivyopita angani mithiri ya nyota zinazoongozana katika mstari mmoja, wapo waliodhani ni nyota, wapo waliodhani ni vimondo, mpaka waliodhani ni miujiza.

Pia soma > Mliopo Dar es Salaam kuna kitu kinapita maeneo yenu angani

1708991816996.png


Ukweli ni kwamba hizi zilikuwa ni satelaiti za kampuni ya internet ya starkink inayomilikiwa na Elon Musk.

1708992035105.png


Internet hii inapatikana hata uwe bondeni, milimani, porini, kijijini, n.k. Internet haina kikomo utatumia unavyotaka (Unlimited), Kuna takribani satelaiti elf 5 za starlink zinazunguka juu ya anga la dunia kuhakikisha internet inapatikana sehemu zote duniani,

1708968794511.png


Tanzania tulikua moja ya nchi za mwanzo kabisa kuhusishwa na hii internet lakini mpaka leo vibali vinashughulikiwa, Tangu mwaka jana mwezi wa pili Waziri wa Teknolojia, Nnape Nauye amekuwa akisema starlink hawajakamilisha vibali,. >> source <<

jpg (3).jpeg


Internet hii imepewa vibali nchi nyingi, Nchi jirani zinazofaidi huduma hii ni Kenya, Rwanda, Malawi, Zambia na Msumbiji. Kwa sasa sisi tutabaki kushangaa hizo satelaiti angani lakini wanaozitumia ni majirani,

1708991335057.png
 
Wengi wameelezea tukio hilo kama vitu vilivyounganika vinavyowaka waka, kuna wengine wamehusisha tukio na miujiza.

Ni satelaiti za kampuni ya internet ya starkink inayomilikiwa na Elon Musk.

Internet hii inapatikana hata uwe bondeni, milimani, porini, kijijini, n.k. Internet haina kikomo utatumia unavyotaka (Unlimited)

Elon Musk aliwahi kuja Tanzania kuomba vibali ili alete ofisi zake watanzania tunufaike na hii huduma lakini waziri wetu wa teknolokia Nnape Nnauye alituangusha

Internet hii imepewa vibali nchi nyingi, Nchi jirani zinazofaidi huduma hii ni Kenya, Rwanda, Malawi, Zambia na Msumbiji. Sisi tutabaki kuwa watazamaji wa hizo satelaiti tukizishangaa angani lakini wanaozitumia ni majirani,

Kuna takribani satelaiti elf 5 za starlink zinazunguka juu ya anga hapa duniani, hakuna haja ya mnara ukiwa na starlink, popote duniani utapata intenet, wenzetu wanafaidi teknolojia za kisasa.

View attachment 2917421

View attachment 2917422
Zilikuwa kwenye maandamano?
1708965547510.jpg
 
hakukuwa na haja ya hii taharuki ya kuonesha ushamba wa wazi wazi kama Nnnape Nnauye anagemruhusu Elon Musk
You mean Nape angeruhusu Starlink hii inamaanisha watu wangeona hizo satellite juu wangejua ni satellite za starlink....HOW??

Unadhani watu ambao hawakujua kinachopira juu ni nini hawajui kuhusu Starlink, Elon, Space X and such stuffs ??

Hakun asiyeju satellite humu wewe umeju hizo satellite za starlink baada ya kusachi tu kama sisi instant ulivyoziona hukujua ni nini
 
Wengi wameelezea tukio hilo kama vitu vilivyounganika vinavyowaka waka, kuna wengine wamehusisha tukio na miujiza.

Ni satelaiti za kampuni ya internet ya starkink inayomilikiwa na Elon Musk.

Internet hii inapatikana hata uwe bondeni, milimani, porini, kijijini, n.k. Internet haina kikomo utatumia unavyotaka (Unlimited)

Elon Musk aliwahi kuja Tanzania kuomba vibali ili alete ofisi zake watanzania tunufaike na hii huduma lakini waziri wetu wa teknolokia Nnape Nnauye alituangusha

Internet hii imepewa vibali nchi nyingi, Nchi jirani zinazofaidi huduma hii ni Kenya, Rwanda, Malawi, Zambia na Msumbiji. Sisi tutabaki kuwa watazamaji wa hizo satelaiti tukizishangaa angani lakini wanaozitumia ni majirani,

Kuna takribani satelaiti elf 5 za starlink zinazunguka juu ya anga hapa duniani, hakuna haja ya mnara ukiwa na starlink, popote duniani utapata intenet, wenzetu wanafaidi teknolojia za kisasa.

View attachment 2917421

View attachment 2917422
Tanzania ukiwa na akili kama za Lucas mwashambwa unakuwa mteule in waiting.

Watu kama kina Mwijaku, Kitenge, Masanja, Dotto Magari, Mpoto, Aristote, Juma Lokole na fananizi nao ndo unaonekana thinktank wa nchi.

Tuendelee kupambania watawala ili watawale vizuri hata kama hawana nia njema na nchi
 
Back
Top Bottom