Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.

Kilitime,

Mimi nimekuwa napinga sana suala la udini hapa na utakumbuka ugomvi wangu na Mchambuzi kuhusu mgombea wa ccm kuwa mkristo.

The same standard imekuwa inatakiwa kutumika kwa wanaccm hapa ambao wamekuwa wanakiita chama cha CUF kama cha kidini na cha waislam. Ni juzi tu hapa wanasisiemu tena wameanza issue kuwa chama cha CHADEMA ni cha watu wa kaskazini na cha kikabila.

Hii generalization ilikuwa tamu kwenu wanaccm na hata wewe you never said a thing about it. Leo kwa sababu ni ccm ndio inasemwa then unaiita upuuzi.

Haijalishi formula gani imetumika, ukweli ni kwamba members wa CC na NEC ya ccm ni asilimia 75 au zaidi waislam. Kubishana kuhusu formula sio tatizo wala solution.

Issue iwe kwamba, udini iwe kwa CUF au CCM usitumike kugeneralize mambo. Mimi nauona huo ukweli kuwa viongozi wengi wa ccm sasa ni waislam lakini ugomvi wangu hauko dhidi ya dini zao au mambo yao ya kikubwa. Ugomvi wangu ni juu wa wizi na ufisadi. The same standard from you guys should be used wakati mnapotumia mbinu chafu dhidi ya upinzani!
 

Lakini jamani kwani tatizo letu ni namba ya waislamu kuzidi kuongezeka? Kwani katika hiyo kamati unayotaja, kuna mwongozo unaosema iwe na waislamu wangapi? Maana mwongozo kama huo ungekuwapo, basi ingekuwapo pia njia (methodology) ya kuhakikisha kwamba ratio inakuwa hivyo. Mimi nadhani suala la kuanza kuhesabu kuna waislamu wangapi na wakristo wangapi katika chama au serikali ni paranoia. Upuuzi mtupu. Watu wanachaguliwa kwa mujibu wa sifa zilizowekwa katika katiba. Zinapofuatwa sifa hizo na kanuni zilizopo kuna uwezekano wa kupata kiongozi mwanaume au mwanamke, mwenye dini au asiye na dini, mweusi au aso mweusi, kabila hili au lile, alimradi wote walishiriki katika mchakato wa kupata kiongozi. Sasa hapo tatizo liko wapi?
 

Kithuku soma tena hiki alichoandika Mwanakijiji katika hiyo quote ulotumia hapo juu:


Kinachokataliwa hapa ni ubaguzi wa aina yoyote maana ukishatumika utaendelea bila kukoma. The same standard inayotumiwa na ccm kusema kuwa cuf ni chama cha kidini (kwa sababu tu viongozi wake wengi ni waislam) inabidi iachwe kabisa kwa sababu ikiendelea matokeo yake ndiyo yanakuwa haya ya kuona nani ni nani hata ndani ya hiyo ccm yenyewe!
 
 
Siye wa TZ ni watu wa ajabu sana, hizi topiki za udini zinapamba moto kama moto wa vifuu, nawauliza je tutafika kweli?

Kutoaka na nionavyo mimi nikuwa wengi wetu ni wadini na wakabila wa kutupwa, ila tunajifanya hatujali, ndiyo maana hizi topiki zinapendwa sana na tunazishabikia.

Mimi napinga ubaguzi wa aina yeyote ile. Na deep down najua ukweli uko wapi, ila sipendi kuongezea petroli hapa na naamua kukaa kimya ili mada kama hizi ziishe mapema lakini wapi.

Nawaomba wote wanaopinga ubaguzi wa aina zote tusichangie hapa, kwani kuna topiki nyingi ambazo tunaweza kuchangia na kusidia taifa zaidi kuliko hii.

Nilikuwepo!
 
Mimi nashangaa sana , kwa nini watu wengi wanashughulika na Imani za viongozi badala ya kushughulikia nini wanatenda kwa jamii?? Tusiwe na upeo mdogo wa kutazama muhimu ni kua kiongozi anawajibika vipi ktk kazi zake (wajibu ) na tukitazama hayo Udini na ukabila hatutoviona na tutamkosoa kiongozi kwa mabaya yake na sio Imani yake nadhani haya ndio maendeleo kinyume tutabaki kila mara kutazama majina (dini) na hakuna maendeleo tutapata ila kuzidisha chuki na hali sote ni nchi yetu na hakuna wa kuondoka ila haki sawa kwa wote
 
Kuna mtu aliwahi kusema hapa kuwa kuna makubaliano ndani ya ccm kuwa na uwakilishi sawa wa dini kubwa nchini za uislam na ukristo. Matokeo ya uchaguzi dodoma yanaonyesha kuwa waislam sasa wana-nafasi asilimia 75 ya uongozi wa ccm.

NOTE: Uongozi (Ukiondoa nafasi ya Mnykt na Katibu mukuu)Katika CCM (nadhani hata vyama vingine itabidi waige hivyo) umegawanywa sawia kati ya Tanganyika na Zenji.

Tanzania = Tanganyika + Zanzibar
.
. . Tanganyika = Zanzibar = 1/2 Tanzania

Muslims(Tanganyika) = 50% (population)

Muslim(Zanzibar)=100% (Population)

Viongozi Muslims(Toka Tanganyika) = 50% (Ya viongozi toka Tanganyika)

Viongozi Muslims(Toka Zanzibar)=100% (Ya viongozi toka zanzibar)

Viongozi MUslim(Tanzania)= 1/2( 100% + 50%) = 75%

A miracle!!! no just! arithmetical computations!!!


NB: Equal sign inawakilisha uwiano unaokaribiana tu, na sio sawasawa kabisa.
 
Jamani tuache kuendekeza mambo ya UDINI!!!! Tuhoji tu tutapoona mtu anachaguliwa kwa dini yake na si vigezo vingine vya kiuongozi.

Ni ujinga na uzuzu mtupu mtu kusema eti chama fulani ni cha kidini kwasababu viongoziwe wengi ni wa dini fulani bila kuangalia sababu za msingi kwanza!! eti serikali ni ya kikristu etu tu kwasababu viongozi wengi ni wakristu !! Chaa! hamuoni kuwa wengi wao wameenda shule??!!

Kuendekeza mambo hayo mwishowe mtakuwa si watu wa DINI tena bali watu DUNI!!!
 

babu, we have a long way to go !

vizuri sana uliposema kwa nini hatuangalii utendaji wa kazi na sio dini zao, vil vile kama nilivyosema kwa nini tusiangalie maendeleo ya nchi bila kujali viongozi wametoka chama gani, lakini watu wakaniona ovyo !
 

kula 5 bokassa !
 

UNCLE USISAHAHU HILI VUGUVUGU LA MJADALA HUU LIMEKUWA DERIVED FROM THE CURRENT SITUATION BONGO YA MAHAKAMA YA KADHI!SO, KAMA VIONGOZI WOTE NI WAISLAM JE WATASIKILIZA HOJA AMBAYO NI YA TOAUTI NA INAYOKUBALIANA NA MAHAKAMA YA KADHI?MAYBE LAKINI POSSIBILITY NI NDOGO SANA!USISAHAU MVUTIA KAMBA....
 
 
Gamba la Nyoka is being objective. AS 4 the REV, Mhh, you better think twice.
 

Yani hapa ndio nimechoka kabisaaaaa.

Population ya bara na zanzibar ni tofauti kabisa lakini tunapata nafasi sawa? niite mdini lakini mimi nitakiita ccm kama chama cha waislam kama wao walivyokiita cuf kwa muda wote huu.
 
 
Halafu Jamani HUYU MTU ANAEITWA KADA kwa nini aruhusiwe kujisajili mara mbili? Admin. tafadhali hebu liangalie hili na Kada uje ueleze huu utovu wako wa nidhamu unakusaidia nini hapa jamvini
Ben,usiseme Kada tu hata wewe yawezekana umejisajili nick zaidi ya moja.Hapa wapo kibao tu wamejisajili majina zaidi ya moja.

je ni kosa kujisajili hivyo?

Hata moderators na may be Adm mwenyewe anaweza kuwa kajisajili zaidi ya mara moja
 
katika dini ambayo haina mgogoro ni dini ya Pagan.Karibuni mjumuike nami.Hizo dini zisiwatishe ni kama Chama Cha Siasa tu
 
Ben,usiseme Kada tu hata wewe yawezekana umejisajili nick zaidi ya moja.Hapa wapo kibao tu wamejisajili majina zaidi ya moja.

je ni kosa kujisajili hivyo?

Hata moderators na may be Adm mwenyewe anaweza kuwa kajisajili zaidi ya mara moja

mtu huyu shalow naona anakuja na kuchungulia hapa, halafu anamchokonoa kada sijui kwa nini ! yaani he is used to it !
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…