Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Sababu mojawapo ni kwamba siasa imekua utamaduni Tanzania. Watu wengi ambao wana uwezo wa kuongoza nchi na kipaji hawako kwenye siasa. Kitu kingine ni ukweli kwamba Watu wengi wa pwani wanapenda siasa ingawa wengi wao hawana uwezo wa kuongoza na hawana utamaduni wa maendeleo.Ukiangalia vizuri utakuta wanasiasa ni watu wenye vipaji vya kuongea lakini wengi wao hawana kipaji cha kuongoza. Makamba ni mfano mzuri wanapiga kelele lakini kule Lushota hakuna bababara wala maji! ingawa wamejaliwa maeneo mazuri sana. Moshi vijijini kuna kila kitu barabara, maji, shule na zimezidi hata za miji mingine mikubwa kwasababu wana wanalazimisha maendeleo.
 
Hivi mnaamini kweli kwa kufunga mijadala kama hii ndio udini utatokomea katika jamii yetu? Mijadala kama hii mingapi imefungwa lakini udini unazidi kuibuka kila kukicha kwa njia moja au nyingine? Ni lazima tujifunze kuongea na kujadiliana tofauti zilizopo katika jamii yetu. Dawa ya jeraha si kulificha bali kulitibu!

Kama kweli mnataka ufungwe kwa nini msi "report post" badala ya kungoja wengine wawafanyie? Ni rahisi tu. Bonyeza hicho kitufe cha tatu (koko kama triangle) kutoka kile cha "thanks".

Amandla........
 
Kweli huu ni wakati wa shetani, Chadema ilizushiwa kuwa ni chama cha wachaga,aikutosha baadaye kikazushiwa kuwa ni chama cha wakristu.CUF ikazushiwa kuwa ni chama cha Waislamu na pia walikuwa wakifanya kampeni hadi misikitini.Sasa CCM nayo zamu yake ya kuthurubiwa imefika basi mimi sina la kusema!
 
Mgaya, hawa CCM siku zote hutumia ujanja wao na umbumbumbu wa Wtz kwa maslahi yao kisiasa; ni hao hao ndiyo huanzisha propaganda chafu dhidi ya wapinzani wao kisiasa kwa kuwaita CUF ni chama cha kidini na CHADEMA chama cha kifamilia!

Nijuavyo mimi siku zote composition ya NEC ya CCM na CC yao wengi wao ni Waislam kwa maana ya kuwa NEC ya CCM huwa na idadi sawa ya wajumbe toka pande zote za Muungano. Mara nyingi utakuta upande wa Bara Wakristo wanazidi kidogo au inakuwa 50:50 lakini kwa sababu nusu ya Wajumbe wengine hutoka Zanzibar basi kule utakuta 99% ya wajumbe niu Waislam na hapo lazima NEC ya CCM inakuwa na Waislam wengi vivyo hivyo CC.

Kwa miaka mingi hilo halikuwa tatizo hadi pale Mwalimu Nyerere alipofariki ndipo likanza kuw issue maana hatuna tena mtu wa kukemea upuuzi huo. Sasa hili suala la kazi linapata nguvu kwa kuwa Mwalimu hayupo na Serikali kwa influence ya Waislamu wengi kuwepmo katika NEC na CC ya CCM usishangae hayo unayosema yakawa kweli maana hili suala halikuwahata la kujadiliwa, lingekemewa mapema lakini kwa kuwa wanahisi umaarufu wao (CCM) umepungua wemelazimika kuweka hilo katika Ilani kwa ahadi ya kulitafutioa ufumbuzi suala hilo na ukweli ni kuwa hawawezi kulipatia ufumbuzi sahihi hadi pale watakaporuhusu Mahkama ya Kadhi ianzishwe.

Kwa maoni yangu, madai hayo yanatiwa nguvu na udhaifu uliomo katika Serikali hii ya CCM.

Doh!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mwisho wa siku wote tutabaki kuwa watanzania ndugu wa baba na mama mmoja.
 
Who cares if 75% of leadership belongs to Masjid? the question is not their religion but their organizational skills, efficiency, capability to lead and standing tall to deliver.

Dini ni hisia and as long as people continue to feel inferior, they will always be inferior in their minds and actions.

Wanaolalamika hata mkiwapa viti vyote vya Bunge kamwe hawataweza kuwa na maendeleo bali ni kubadilisha mbinu za kisisasa na kutumia udini badala ya kuleta maendeleo ya kweli kuondoa Ujinga, Umasikini na Maradhi!

Do not worry, let them be 100%

Wanaolalamika hata mkiwapa viti vyote vya Bunge kamwe hawataweza kuwa na maendeleo bali ni kubadilisha mbinu za kisisasa na kutumia udini badala ya kuleta maendeleo ya kweli kuondoa Ujinga, Umasikini na Maradhi!

Do not worry, let them be 100%

May be CHADEMA with 98.78 ya viongozi na wanachama wakristo,theycan deliver something. hivi mtawatukana waislamu katika nchi hii mpaka lini? udhaifu wa MKAPA haukuwahi kuambatanishwa na ukatoliki wake hata siku moja ila udhaifu wa KIKWETE unaambatanishwa na uislamu wake,, why????
mnaangalia mambo kama wapumbavu wasijua kusoma wala kuandika, mnayachanganua kwa upeo mdogo kuliko hata watoto wa chekechea..
nenda kaulize au fanya utafiti kuanzia mawaziri, makatibu wakuu wa wizara, wakurugenzi wa taasisi za serikali na mashirika ya umma, wenyeviti wa bodi za mashirika pamoja na sehemu mbalimbali za maamuzi halafu uje na detailed document hapa uone jinsi utakavyoonekana mpumbavu.idadi kubwa ya watendaji wa serikali hadi hivi sasa ni wakristo na hawapo huko kutokana na dini zao bali ni kutokana na uwezo wao. nani alijiuzia mgodi wa kiwira, nani alihusika na kashfa ya rada,ndege ya rais je? vipi kuhusu mikataba ya richmond na dowans? meremeta na deepgreen nayo?? ni nanialibadili mitaala ya shule za msingi na sekondari akiwa waziri,, vp kuhusu tanzanite one?
kama wote hao wamefanya kwa sababu ya ukristo wao basi hiyo dini hata bwana yesu angeikimbia......
ila kwa sisi wenye akili zetu na tunaozitumia vizuri kufikiri huwa tunaamini waliyafanya maovu yao kwa tamaa zao na wala sio kwa vile wao ni dini fulani. tukitaka tusambaratike kama taifa!! just bring your filth segregation and you will see if any of us will remain safe.
 
Notradammus, you are wrong! angrish words and allogance of any nature cant solve the issue. people here are discussing jk and his CCM showing biasness in the mentioned two religions. JK is a man of vengeance, hipocrites and christmaphobia. am not abusing bse his history is very clear. a wise man always think for the people and foolish one think for himself and subordinates. go in every government institution and ask who is the CEO, Muslim,muslim, muslim......................................why? start with NSSF!!!! the truth is i was denied a position of internal auditor bse am not a muslim. IPO SIKU, KWANI HATA MJUSI UKIUKIMBIZA SANA HUGEUKA NYOKA.
 
Ndg zangu hili suala la dini lisituchanganye. Dini ya mtu kama dini haitaweza kutusaidia kama Watz!
Kama alivyosema mchangiaji mmoja, hatuwachagui viongozi ili waje watuhubirie makanisani au misikitini, bali tunawahitaji viongozi wanaokuja kutuongoza kama watanzania. Mie hata % 100 wakiwa wa dini moja hainipi shida, cha muhimu je hawa watu wapo tayari kuilinda katiba?
Katiba ya nchi ikilindwa na kuiheshimu haya mambo yote ya ufisaji na ukengeufu mwingine hayawezi kutokea. Nawasilisha hoja!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom