Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Kampeni za kumgeuzia kibao Rais Kikwete zaanza





Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye watu wake wa karibu wanadaiwa kumgeuka n a kuanza kumfanyanyia kampeni za kumchafua.
*Baadhi ya wabunge watumika kufanya kampeni
*Wana CCM wahoji ukimya wa Kikwete


Na Mwandishi wetu


KAMPENI za kusafisha watuhumiwa wa kashfa mbalimbali za ufisadi nchini sasa zimechukua sura mpya baada ya kikundi cha baadhi ya wabunge na watu wengine kufanya kampeni za chini chini za kumgeuzia kibao Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.


Habari zilizopatikana mjini Dodoma, zinaeleza kuwa kampeni hiyo inafanywa na baadhi ya watu na wabunge waliopo karibu na watu wanaotuhumiwa kwa kashfa za ufisadi nchini kwa kuwafuata wabunge wenye ushawishi mkubwa.


Mbunge mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa hivi karibuni alifuatwa na mmoja wa wabunge wenzake akimshawishi ajiunge katika harakati za kusafisha mtuhumiwa mmoja wa kashfa ya kampuni ya kuzalisha umeme wa Dharura ya Richmond.


Alimweleza kwamba kimsingi watu wanaotajwa katika kashfa hiyo hawahusiki na kwamba walitolewa kafara kumlinda Rais Kikwete.


Alipomwuliza kwa nini rais aingizwe katika kashfa hiyo alisema kwamba alijua utaratibu mzima na kwamba kuwawajibisha mawaziri pekee haitoshi lazima watu wote waende na maji.


Mbunge huyo alisema alimwambia wazi kwamba hawezi kujiunga katika harakati hizo kwa sababu anajua rais hakuhusika kwa lolote na suala hilo na kwamba walioaguka kutokana na kashfa hiyo wamewajibika kutokana na nafasi zao.


"Nchi hii inaelekea kubaya kuanza kufanya kampeni za kusafisha viongozi kwa kutumia njia za kutaka kumchafua rais ni hatari sana," alisema.


Alisema kama serikali na Rais Kikwete hawasimama kuhakikisha kuwa watuhumiwa ufisadi wanachukuliwa hatua ipo hatari kwa vikundi hivi vinavyoibuka nchini kufanya kampeni chafu zikaivuruga nchini.


Mbunge mwingine alidokeza Mwananchi Jumapili kampeni hizi za kuwasafisha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi zinaendelea na kwamba sasa zinafanyika chini chini baada ya hapo awali kufanyika kwa njia ya wazi kabla ya kupigiwa kelele na wananchi.


Alisema baada ya watu hawa kushindwa kujitokeza wazi bungeni kuwatetea watuhumiwa wa ufisadi kutokana na kuogopa macho ya wapigakura wao, sasa wanamfuata mbunge mmoja mmoja kumshawishi kujiunga na kambi yao.


Mbunge huyo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) alisema kitendo cha Rais Kikwete kushindwa kutumia vikao vya juu vya chama kuwadhibiti mafisadi, kimetoa mwanya kwa watu hao kuanza kumgeuzia kibao kuwa hawezi kuwafanyia kitu.


"Unajua kama baadhi ya makada wanaoendesha kampeni za kumchafua rais wana uwezo wa kuzungumza naye kwa simu na kumtumia message akajibu, lakini hivi sasa wanamsliti, ni hatari sana lazima awe mkali sasa rais wetu watammaliza," alionya.


Baadhi ya watu nchini walipoulizwa maoni yao kuhusiana na kampeni hizo, walisema Rais Kikwete hana njia nyingine zaidi ya kuwabana ndani ya CCM na serikalini na kwamba watakaobainika wachukuliwe hatua kali.


Kwa upande wake Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema mjadala wowote kuhusu suala la Richmond kuendelea kufanyika sasa hauna maana kwani suala hilo limefungwa baada ya kufanyiwa kazi na kumalizika.


Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Kapteni George Mkuchika aliliambia gazeti hili jana kuwa chama hakuna maelezo yoyote ya ziada kuhusu suala hilo kwani kinaamini kuwa limefungwa na kinachosubiriwa sasa ni utekelezaji wa kazi iliyofanyika.


"Bwana kuhusu Richmond suala limemalizika na kazi imefanyika sina maelezo ya ziada na mjadala wowote sasa hauna maana," alisema Mkuchika.


Mbunge wa Njombe Kaskazini, Jackson Makweta alisema viongozi lazima waelewe kwamba hii ni nchi yetu sote lazima tuonyeshe mapenzi.


Alisema viongozi ni sawa na gari ambalo kama tutazembea tutalifanya liache njia na kunguka na kuua watu wasoiokuwa na hatia.


Makweta alisema uchambuzi wa kina kuhusu mafisadi lazima ufanyike ili ukweli wa mambo ufahamike .
 
Siku za Kikwete kwa kweli zinahesabika, kama ataendelea kukaa kimya kama vile hayamhusu basi ategemee kurudi kijijini siku si nyingi. What a president!!! kama vile haishi nchini au hajui kuwa kimya nacho ni jibu?

Kikwete na ufisadi ni chanda na pete. Kamwe hawezi kuwachukulia hatua mafisadi kwani na YEYE ni FISADI.

Ufisadi umemfikisha ikulu, kitu ambacho ilikuwa ni ndoto na nia yake toka muda mrefu sana, hivyo nina hakika 1000% hawezi hata chembe kuwachukulia hatua mafisadi.

Mafisadi ndiyo wanaongoza nchi na yeye yupo tu kufuata amri na matakwa ya mafisadi.

Mafisadi yameteka nchi na yanafanya yatakavyo.

Wananchi ni lazima tutafute njia mbadala kwani Jakaya nchi imemshinda hiyo si siri.
 
Hiyo hoja haina uzito uliokusudiwa. Kwa ufupi ni kuwa dini na imani ya mtu siyo jina tu. Wengi wana majina yanayo suggest dini fulani wakati hawana mwelekeo wa kufuata maadili ya dini hiyo. Binafsi naona kuwa suala la udini kwetu watanzania siyo suala la kutupotezea muda. Ukweli ni kuwa nchi nzima ni masikini na inahitaji kuendelezwa kwa kiwango kikubwa. Huwezi kusema kuwa kwa kuwa kamati kuu ya ccm, au popote pale wenye vyeo vya juu ni wa dini fulani kwa hiyo watu wa dini hiyo wana unafuu fulani ktk maisha yao! Umeme ukikatika hauwakatikii watu wa dini moja tu. Maji yanapokuwa hayatoki mabombani, ni kwa watu wa dini zote, na wasiokuwa na dini pia! Petrol, diesel, nauli za daladala zinapopanda bei haziwagusi watu wa dini fulani tu! By the way hoja ni hizo hizo unapokuja ukabila. I hope nimeeleweka!
 
Last edited:
CCM? ni chama cha wakulima na wafanya kazi. CHADEMA cha wachaga na wafanyabiashara. CUF? Chama cha wafanya fujo na wasioamini muungano na serikali zake. NCCR chama cha viongozi ambao ni qualified political and social pathologists waliobobea kufanya postmortem ya matukio mbalimbali ndani ya jamii. Always reactive and never proactive!!!!
 
CCM? ni chama cha wakulima na wafanya kazi. CHADEMA cha wachaga na wafanyabiashara. CUF? Chama cha wafanya fujo na wasioamini muungano na serikali zake. NCCR chama cha viongozi ambao ni qualified political and social pathologists waliobobea kufanya postmortem ya matukio mbalimbali ndani ya jamii. Always reactive and never proactive!!!!

Haya ni maoni yako tu yaliyojaa itikadi za chama fulani cha kifisadi vile. Mbona na chama chako pia hakiamini hayo niliyo bold hapo juu kwa wino mwekundu? Si unajua sasa hivi ndiyo hot debate kwenye hicho chama chako cha mafisadi na wezi? Ondoa propaganda hapa maana sasa hivi sisi si wadanganyika tena!
 
Originally Posted by suleimani
CCM? ni chama cha wakulima na wafanya kazi
Ulisahau? CCM ni chama cha wezi na mafisadi nadhani hii ndiyo term sahihi.
 
HOJA zimekuwa zikijengwa kuwa nchi yetu imefanikiwa kujenga utaifa ambapo hakuna ubaguzi wa kidini au kikabila. Aidha, Mtanzania yeyote ukimuuliza atakuambia kuwa serikali yetu haina dini. Kwa mtazamo huo viongozi hawaongozi kwa utashi wa dini zao kuwahujumu wananchi wasio katika dini moja.

Wanasiasa wanapotoa shutuma dhidi ya watu, wanaodai wana udini, taswira inayojengwa ni kuwa Muislamu ndiye mdini, bali Mkristo hawezi kuwa mdini.

Ndio maana japo serikali na taasisi zake zaweza kuwa imejaa Wakristo ikilinganishwa na Waislamu, haionekani kuwa ni tatizo.

Aidha, ndio maana uongozi wa juu wa CCM ulipokuwa na Wakristo wengi (!?), lakini hausikii CCM ikiambiwa ni chama cha Wakristo au kina udini. Lakini inapotokea chama hicho hicho au kingine, kuwa na viongozi Waislamu basi hubatizwa kuwa chama cha kidini.

Wananchi tunahoji, iweje? Wazandiki hao wadai kwamba baadhi ya vyama au Tassisi ni vya kidini, kwa sababu tu ya kuongozwa na Waislamu, wakati hata vyama au Taasisi wanazo ziongoza wao wenyewe, vimejaa viongozi Wakristo watupu? Au ndio tuseme sasa ndio wananchi wanatakiwa kujua kwamba ndani ya vyama vyao au Taassisi hamna Waislamu? Na kwa maana hiyo ni vyama vya wakristo? Matamshi ya baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa yanatia kichefuchefu. Kama ni ushahidi, sasa umepatikana kumbe yaliyokuwa yakisemwa ni kweli, udini upo tu pale ambapo Mwislamu ni kiongozi au anaposhika madaraka katika taasisi za umma.

Mayowe yote tunayosikia ya udini na mara nyingine na ukabila, yanayopigwa na walaghai, ni katika kuendeleza hila za kuwalaghai wananchi, ambao bado wanadhaniwa kuwa ni punguwani, hasa wale wanaoambiwa kwamba hawakusoma.

Wananchi wamekwisha baini kwamba, kumbe wale wanaodai kuwa wanaupiga vita udini, ndio hasa wanaouendeleza nchini. Upitizi wa makini wa kitabu "Kanisa Katoliki na siasa Tanzania Bara 1953-1985" unatoa habari za ndani zisizo za kawaida juu ya kampeni dhidi ya Uislamu.

Kwa sababu zisizoeleweka kitabu hiki kimeandikwa na kuchapishwa na waumini wa Kanisa hilo. Yaliyomo ndani ya kitabu hicho hayajakanushwa wala kubishiwa na serikali ya Muungano ya Tanganyika au CCM, huu ukiwa ni ushahidi kamili juu ya ukweli wa kukiri juu ya neno hilo.

Kwa sababu na malengo yoyote ya kutolewa kitabu hicho, na lazima ziwepo sababu za msingi za kufanya hivyo, kitabu hiki ni ufunuo mzuri juu ya mbinu za chini kwa chini za Kanisa katika medani ya kisiasa Tanzania.

Kitabu kinaeleza ni Kanisa Katoliki lililojenga njia ambazo ziliwawezesha kuwa na mahusiano ambayo kitabu hicho inaeleza yalikuwa ya karibu kabisa na TANU wakati wa miaka ya kupigania uhuru. Kinaonesha ni vipi Kanisa lilitayarisha waumini wake shupavu ambao walikuwa wameshika karibu nafasi zote muhimu katika serikali mpya ya Kiafrika ya Tanganyika. Lakini hatukusikia wanachi wakilalamika kuwa serikali ina udini, japokuwa wakristo ndio waliokuwa wamejazana kwenye nafasi kubwa kubwa za uongozi na ndio walio kuwa wengi wenye madaraka.

Kwa wale viongozi, wawe wa Kanisa, CCM au serikali ya Muungano ambao walikuwa wakijipigia kelele kutenganisha kwa siasa na dini, lakini wao wenyewe wakiwa ndio waendelezaji wakubwa wa hilo, wana kazi ngumu ya kuelezea kwa umma kwa ujumla lakini zaidi kwa Waislamu. Sivalon anaelezea juu ya mpango na njama zinazoendelea zikishirikisha Kanisa Katoliki, Chama (TANU-CCM) na serikali ya Muungano.

Tangu njama hizo ziwekwe wazi 1992 hapakuwa na kauli moja ya kupinga au kutolea maelezo juu ya hilo. Huku ni kukiri kwa dhahiri juu ya mipango na njama za Kanisa zinazofanywa hali zikiwa zinaeleweka na mkono wa chama na serikali yake.

Yafuatayo ni baadhi ya madondoo kutoka kitabu hicho:

"Mwishowe tutakuja kuonesha jinsi Rais mstaafu Nyerere alivyokuja kuwa kiungo cha pekee kati ya chama/kanisa na Kanisa Katoliki. Uhusiano huo unaelezwa kwanza kama msingi wa kuelewa jinsi gani na kwa kiasi gani viongozi wa Kanisa walivyoingilia kati maendeleo ya siasa hapa Tanzania (uk. 5).

Huo uhusiano ukawaweka viongozi wa Kanisa katika nafasi nzuri ya kuelekeza maelekezo ya siasa Tanzania. (uk. 9).

Kinyume na kampeni inayosambazwa, Waislamu sio chanzo ila wao ni waathiriwa wa mbinu za makusudi za kujenga mfumo wa uhasama ambao unawanyonya watu wa dini zote mbili na siasa ili kuwabana Waislamu na pia kupata uwezo wa kuwakandamiza.

Wananchi wamekwisha kujua kwamba, vyama vingi vya siasa hapa nchini ni matawi ya Chama Cha Mapinduzi, vilivyobuniwa makusudi, ili kuwagawa wananchi wasiwe na nguvu za kuleta mabadiliko ya uongozi wa chama cha siasa nchini.

Na kwa kumalizia wakristo hao waliokuwa wameshika madaraka makubwa na kuiongoza serikali ya Tanganyika na sasa serikali ya Jamhuri ya Tanzania ndio walio tuletea umaskini huu, tulio nao hivi leo. Wao ndio waliokuja na sera ya Azimio la Arusha na kuiba mali za wanachi, wao ndio walio kuja na sera ya vijiji vya ujamaa na kusababisha maafa makuwa kwa wanachi.

Je tukisema kuwa Wakristo wameiangamiza nchi hii ya Tanzania tutakuwa tumekosea?
 
Huyu bwana Mwanakijiji anataka kuturudisha kwenye enzi za zama za mawe!!!!!. Kesho utatuambia hata Taifa stars imejaa udini..... Ushauri wangu: tuangalie uwezo ktk utendaji and not otherwise. Au unataka kuwa-criticize CCM (aka chama cha mafisadi) wanapotumia hoja ya kibaradhuli kwa kusema Chadema au CUF ni vyama vya udini ....kwa wewe nawe kujifanya baradhuli? Mbwa akikung'ata na wewe utachuchumaa umng'ate?????

Mkuu Macho_Mdiliko,

Mimi nakubaliana na mawazo yako kwa asilimia mia. Falsafa ya Wangwe ni falsafa iliyojaa udini na ukabila. Vyama vya siasa nchini Tanzania havisajiliwi vikiwa na udini, ukabila hata ueneo. Lakini, vile vile ni ubaguzi kuwazuia watu wa dini moja, kabila moja, rangi moja, umri mmoja au eneo moja kujiunga kwa wingi katika chama chochote kimoja wanachokitaka kwa hiari yao wenyewe.

Kwa mtaji huo huo, huwezi kuwazuia watu wa dini moja, kabila moja, rangi moja, umri mmoja au eneo moja kuchukua uongozi katika chama chochote kimoja kama watu hao wanao uwezo wa uongozi huo.

Vinginevyo, ni fitna, choyo na husda. Wote hao ni Watanzania ndani ya chama na ndani ya uongozi. Kama pana malalamiko, tulalamikie uwezo au jinsi walivyochaguliwa kama demokrasia na katiba ya vyama vyao ilivunjwa.
 
tatizo nini sasa ikiwa zenji ni asilimia 100 niwaislam na mmejitia kuungana nao si lazima na wao watoe asilimia yao au huu muungano ni kumfanya yule alie changia asipape sawa madhali umeukubali muungano wa nchi 2 kitakacho patikana kigaiwe sawa usiangalie ukubwa wa sehemu umetoa moja na nimetoa moja sasa kwakuwa ni mdogo ndio unipe rebo
 
Rais wetu ameshindwa kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo katika kiapo alichokitoa wakati anaingia ikulu.
Vuguvugu la Zanzibar ni nchi au la pamoja na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuamua kukaa kimya ni dhahiri kuwa amevunja kiapo alichokitoa cha kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa nini rais anapata kigugumizi kuitetea katiba? kina tambwe hiza na raza ni nani mpaka watolee kauli hatma ya muungano?
 
He is out of words.Mwambie achangie mada kuhusiana na watoto wa shule kupewa mimba hapo atachangia na kuhusu wadada wadogo wazuri yeye hapo humtoi!
 
He is out of words.Mwambie achangie mada kuhusiana na watoto wa shule kupewa mimba hapo atachangia na kuhusu wadada wadogo wazuri yeye hapo humtoi!
sasa naona spika sita nae kajitosa...
ni jukumu la nani kutolea kauli suala la muungano? kwikwi na kigugumizi cha rais kikwete kinatoka wapi?
 
Rais wetu ameshindwa kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo katika kiapo alichokitoa wakati anaingia ikulu.
Vuguvugu la Zanzibar ni nchi au la pamoja na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuamua kukaa kimya ni dhahiri kuwa amevunja kiapo alichokitoa cha kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa nini rais anapata kigugumizi kuitetea katiba? kina tambwe hiza na raza ni nani mpaka watolee kauli hatma ya muungano?
kwa kauli za karibuni bado raisi wetu yuko kimya.... inatisha
 
Ochu Suala Na Muungano Halimuhusu Na Hawezi Kusema Chochote Kuhusu Muungano Znz Inajulikana Sio Nchi , Kwahiyo Huu Mjadala Wa Muugani Ufutwe Haraka Ikiwezekana , Kama Wewe Ni Mznz Basi Umeuwawa
 
Ochu Suala Na Muungano Halimuhusu Na Hawezi Kusema Chochote Kuhusu Muungano Znz Inajulikana Sio Nchi , Kwahiyo Huu Mjadala Wa Muugani Ufutwe Haraka Ikiwezekana , Kama Wewe Ni Mznz Basi Umeuwawa

suala la Muungano liko kwenye katiba aliyoapa kuilinda na kuitetea kumbuka. mbaya zaidi wazanzibar ndio hawataki muungano
 
Rais wetu ameshindwa kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo katika kiapo alichokitoa wakati anaingia ikulu.
Vuguvugu la Zanzibar ni nchi au la pamoja na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuamua kukaa kimya ni dhahiri kuwa amevunja kiapo alichokitoa cha kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa nini rais anapata kigugumizi kuitetea katiba? kina tambwe hiza na raza ni nani mpaka watolee kauli hatma ya muungano?

bunge linatakiwa limwajibishe rais: impeach the president now.
 
bunge linatakiwa limwajibishe rais: impeach the president now.

Kwa lipi? La kutozungumzia Muungano au kuwawajibisha wanaotoa maneno ya kutaka kuuvunja? maana mashitaka ya Impechment siyaoni. Kufuatana na katiba yetu Sura ya kwanza Ibara ya 46B kifungu cha 2 inabidi tujiulize yafuatayo kabla ya kufikiria hiyo impechment Je ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; Je ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba, au amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano? Kama majibu ni hapana, katiba haitoi nguvu kwa Bunge kumwondoa Raisi.

Sasa hii sio kusema nakubaliana na ukimywa wake katika choko choko za muungano zinazoendelea
 
Rais wetu ameshindwa kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo katika kiapo alichokitoa wakati anaingia ikulu.
Vuguvugu la Zanzibar ni nchi au la pamoja na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuamua kukaa kimya ni dhahiri kuwa amevunja kiapo alichokitoa cha kulinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa nini rais anapata kigugumizi kuitetea katiba? kina tambwe hiza na raza ni nani mpaka watolee kauli hatma ya muungano?

mbona hajatoa jibu muafaka la hatma ya muungano? mbona anaogopa kuongea waziwazi?
 
Ochu hicho kiapo alichokula alikula mbele yako au mbele ya watanzania ? Je watanzania wanajua kilichomo ndani ya hicho kiapo ? Inawezekana mambo yanayoendelea sasa hivi ndio kiapo chake alichokula kama ni tofauti naomba utupe kiapo alichokula ambacho wewe unafikiri ni sahihi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom