Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Ukikuta wajinga wawili wanafanya ujinga na wewe ukamuona mmoja tu na kumuita mjinga, basi unachofanya ni kuthibitisha ujinga wako. Hivyo wajinga wawili wakifanya wote ujinga, wote wawili wanaitwa wajinga, hiyo ndiyo inaitwa hekima.

Kwa maneno yako Chadema wajinga kwani ndio kwao imethibitika wakabila kwa makamu mwenyekiti kutoa kauli hiyo. CCM hakuna ushahidi wala tetesi za udini zaidi ya jungu lako wewe lilikosa ushahidi.

tuambie wabunge wa CCM wengi waislam au wakrsitu? nenda kwa spika Sitta na wasaidizi wake hadi namba ya wabunge waislam na hasa viti maalum wote wakristu.
Lakini chadema wachagga watupu.
 
Wakati utnaendea na hizi hate spinnings tukumbuke kuwa mwisho wa siku ni Tanzania nditi itakayoripuka na hata kama wewe ni wa "just landed" class wapo wanaokuhusu watakaogeuka kama wakina mama na watoto wa Somalia......

Unaweza ukadhani unawakomoa wao (CCM) kumbe ukawa unaneemesha mbegu za maangamizo yako mwenyewe.......

Suala la wenye majina ya kislamu kuonekana kuwa wengi katika CCM-CC ni inakuwa factored wa nafasi maalum ya Zanzibar. Ukipiga mahesabu ya CCM-Tanganyika ni wazi wenye majina ya kikristo ni wengi Zaidi ya Waislamu.

Tanzanianjema

Kama hajaelewa Mwanakijiji haelewi tena, atizame wabunge wa Tanzania Bara,mawaziri,makatibu wakuu,wakuu wa mikoa na wilaya wakristu ni wengi nadhani anataka kuamsha mambo ya mwembechai au mabucha ya nguruwe kwani waislam wamelala anataka kuwaamsha wapige hesabu kuona wanavyobanwa kwenye teuzi nyingi.
 
Mimi nimesha msamehe mwankijiji, Hajui alisemalo

Lakini Mkuu Wangwe naye huoni katumwa kuleta vurugu?
Sasa kama ni umoja anataka ni kwa style ya kukigeuza chama kiwe cha kabila gani?
Maana hata yeye maslahi yake ni kuhusu MARA tu!
Akizungumza anasema ni wachagga hawataki kupeleka pesa huko MARA!
Afadhali angekuwa anaongea kwa niaba ya mikoa yote kwasababu si mikoa yote wala wajumbe wa mikoa yote wanaotoa tuhuma nzito nzito kama zake!
Sasa hata akitokea mtu akizungumzia kuhusu EPA yeye anarudi tena na RACIAL SLURS!
Hapa simtetei MKJJ lakini simtetei WANGWE NEITHER!
Lakini nikilazimishwa ni take side basi ofcourse nitatake side ya MKJJ kwani at least anajenga hoja na ana make sense licha ya kwamba we dont see eye to eye all the times.
 
Changia na mada nyingine basi mgagagigikoko.. au utaalamu wako umeishia kwenye haya tu. ? Mchango wako unahitajika na mawazo yako pia.
 
lakini Mkuu Wangwe Naye Huoni Katumwa Kuleta Vurugu?
Sasa Kama Ni Umoja Anataka Ni Kwa Style Ya Kukigeuza Chama Kiwe Cha Kabila Gani?
Maana Hata Yeye Maslahi Yake Ni Kuhusu Mara Tu!
Akizungumza Anasema Ni Wachagga Hawataki Kupeleka Pesa Huko Mara!
Afadhali Angekuwa Anaongea Kwa Niaba Ya Mikoa Yote Kwasababu Si Mikoa Yote Wala Wajumbe Wa Mikoa Yote Wanaotoa Tuhuma Nzito Nzito Kama Zake!
Sasa Hata Akitokea Mtu Akizungumzia Kuhusu Epa Yeye Anarudi Tena Na Racial Slurs!
Hapa Simtetei Mkjj Lakini Simtetei Wangwe Neither!
Lakini Nikilazimishwa Ni Take Side Basi Ofcourse Nitatake Side Ya Mkjj Kwani At Least Anajenga Hoja Na Ana Make Sense Licha Ya Kwamba We Dont See Eye To Eye All The Times.

Ana Make Sense Kwa Kuwafagilia Wachagga? Vipi Sense Ya Wangwe Kuwakilisha Kilio Cha Wanacahama Wote Wa Chadema?
 
Hadi hivi sasa sijasikia mwanachama mwingine yoyote wa Chadema aliyemuunga mkono Wangwe na kama wapo kwanini sauti yao haisikiki sana. Inabidi wakusanye kwanza wanachama wenye chuki na wachagga ndio watafanikiwa.
 
Mzee Mwanakijiji naona sasa kijijini umeamua kufuatilia kotekote kujua kile kinachoendelea ndani ya siasa za Tanzania.

Swali kubwa sana ambalo limekuwa linaulizwa hapa bila kupata majibu toka kwa wana ccm. Kama kuna uwezekano wa kuangalia majina ya watu na kujua makabila, mikoa, lugha, wake/waume, wakwe, watoto, dini na mengine mengi katika chama kikubwa cha upinzani Tanzania - CUF au chama kinachochipuka cha Chadema, basi kipimo hicho chaweza kutumika kabisa kujua kama kuna udini au hata ukabila ndani ya chama tawala cha ccm.

Kazi kweli kweli Mzee Mwanakijiji.

wengine mnafikiri kwa kutumia mbongo zenu,wapinzani wenu wanatumia miyoyo yao!

hoja hii si kwamba Mwanakijiji au wewe mnashabikia udini au vita dhidi ya dini nyingine bali kupingana au kutumia siasa za propaganda za CCM kuishambulia CCm yenyewe

kama wao kwa bayana ua kwa siri wanasema CHADEMA ni chama cha wachaga au watu wa kaskazini ua kudai kwamba CUF ni chama cha waislamu basi kwa mantiki hii CCM pia ni chama cha waislamu tena wa Pwani!
 
Date::7/19/2008
Kampeni za kumgeuzia kibao Rais Kikwete zaanza

Rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye watu wake wa karibu wanadaiwa kumgeuka na kuanza kumfanyia kampeni za kumchafua.
*Baadhi ya wabunge watumika kufanya kampeni
*Wana CCM wahoji ukimya wa Kikwete

Na Mwandishi wetu
Mwananchi

KAMPENI za kusafisha watuhumiwa wa kashfa mbalimbali za ufisadi nchini sasa zimechukua sura mpya baada ya kikundi cha baadhi ya wabunge na watu wengine kufanya kampeni za chini chini za kumgeuzia kibao Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.

Habari zilizopatikana mjini Dodoma, zinaeleza kuwa kampeni hiyo inafanywa na baadhi ya watu na wabunge waliopo karibu na watu wanaotuhumiwa kwa kashfa za ufisadi nchini kwa kuwafuata wabunge wenye ushawishi mkubwa.

Mbunge mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake aliiambia Mwananchi Jumapili kuwa hivi karibuni alifuatwa na mmoja wa wabunge wenzake akimshawishi ajiunge katika harakati za kusafisha mtuhumiwa mmoja wa kashfa ya kampuni ya kuzalisha umeme wa Dharura ya Richmond.

Alimweleza kwamba kimsingi watu wanaotajwa katika kashfa hiyo hawahusiki na kwamba walitolewa kafara kumlinda Rais Kikwete.

Alipomwuliza kwa nini rais aingizwe katika kashfa hiyo alisema kwamba alijua utaratibu mzima na kwamba kuwawajibisha mawaziri pekee haitoshi lazima watu wote waende na maji.

Mbunge huyo alisema alimwambia wazi kwamba hawezi kujiunga katika harakati hizo kwa sababu anajua rais hakuhusika kwa lolote na suala hilo na kwamba walioaguka kutokana na kashfa hiyo wamewajibika kutokana na nafasi zao.

"Nchi hii inaelekea kubaya kuanza kufanya kampeni za kusafisha viongozi kwa kutumia njia za kutaka kumchafua rais ni hatari sana," alisema.

Alisema kama serikali na Rais Kikwete hawasimama kuhakikisha kuwa watuhumiwa ufisadi wanachukuliwa hatua ipo hatari kwa vikundi hivi vinavyoibuka nchini kufanya kampeni chafu zikaivuruga nchini.

Mbunge mwingine alidokeza Mwananchi Jumapili kampeni hizi za kuwasafisha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi zinaendelea na kwamba sasa zinafanyika chini chini baada ya hapo awali kufanyika kwa njia ya wazi kabla ya kupigiwa kelele na wananchi.

Alisema baada ya watu hawa kushindwa kujitokeza wazi bungeni kuwatetea watuhumiwa wa ufisadi kutokana na kuogopa macho ya wapigakura wao, sasa wanamfuata mbunge mmoja mmoja kumshawishi kujiunga na kambi yao.

Mbunge huyo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) alisema kitendo cha Rais Kikwete kushindwa kutumia vikao vya juu vya chama kuwadhibiti mafisadi, kimetoa mwanya kwa watu hao kuanza kumgeuzia kibao kuwa hawezi kuwafanyia kitu.

"Unajua kama baadhi ya makada wanaoendesha kampeni za kumchafua rais wana uwezo wa kuzungumza naye kwa simu na kumtumia message akajibu, lakini hivi sasa wanamsliti, ni hatari sana lazima awe mkali sasa rais wetu watammaliza," alionya.

Baadhi ya watu nchini walipoulizwa maoni yao kuhusiana na kampeni hizo, walisema Rais Kikwete hana njia nyingine zaidi ya kuwabana ndani ya CCM na serikalini na kwamba watakaobainika wachukuliwe hatua kali.

Kwa upande wake Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema mjadala wowote kuhusu suala la Richmond kuendelea kufanyika sasa hauna maana kwani suala hilo limefungwa baada ya kufanyiwa kazi na kumalizika.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, Kapteni George Mkuchika aliliambia gazeti hili jana kuwa chama hakuna maelezo yoyote ya ziada kuhusu suala hilo kwani kinaamini kuwa limefungwa na kinachosubiriwa sasa ni utekelezaji wa kazi iliyofanyika.

"Bwana kuhusu Richmond suala limemalizika na kazi imefanyika sina maelezo ya ziada na mjadala wowote sasa hauna maana," alisema Mkuchika.

Mbunge wa Njombe Kaskazini, Jackson Makweta alisema viongozi lazima waelewe kwamba hii ni nchi yetu sote lazima tuonyeshe mapenzi.

Alisema viongozi ni sawa na gari ambalo kama tutazembea tutalifanya liache njia na kunguka na kuua watu wasoiokuwa na hatia.

Makweta alisema uchambuzi wa kina kuhusu mafisadi lazima ufanyike ili ukweli wa mambo ufahamike.
 
Siku za Kikwete kwa kweli zinahesabika, kama ataendelea kukaa kimya kama vile hayamhusu basi ategemee kurudi kijijini siku si nyingi. What a president!!! kama vile haishi nchini au hajui kuwa kimya nacho ni jibu?
 
Hili sula la kusema mbunge fulani bila ya kutaja jina lake ni taarifa zisizo na uhakika kwa maana hiyo basi ni bora kwa waandishi kama habari hamuwezi kuzieleza kwa uwazi bora zisiandikwe
 
Hawa wazushi tu wala hawana lolote la maana, CCM tumewazoea mara walijiandaa kumkimbia kikwete bungeni mara hili mara lile hakuna lolote hapa. Wanatanguliza maslahi mbele kwanza hawa ila siku zao tunazihesabu sisi hatujali watakuwa na JK au wanajiandaa kumuangusha, kama walikuwa na uchungu mbona wamekumbatia ufisadi wote huu bila kusema lolote, wanatafuta kura hawa mahesabu ya mbali haya.
 
Haa RAIS JK ni Kiboko bwana asikwambie mtu si unaona jinsi anavyofanya kazi kwa Kasi mpya, hari mpya na nguvu mpya nafikiri mpaka mwaka 2010 hahitaji kuchafuliwa na mtu yeyote. Historia tu itamuhukumu kwa maendeleo aliyowaletea Watanzania.

Sisi tunasubiri tu, tuko tayari kutembea mpaka vijijini kuhakikisha watanzania wanamsaidia kurudi jimboni kwake kwa kishindo kama walivyomsaidia kuingia Ikulu kwa kishindo. Vinginevyo nitawaona Watanzania kama hawana maana.

Kenya pamoja na RAIS Kibaki kubadilisha uchumi wao na kufanya mambo mengi ambayo hata walikuwa wakijivunia kwa miaka mitano tu aliyokaa madarakani, lakini mliona jinsi walivyo mtoa makamasi mpaka akahamua kuingia tena kwa hila. Sasa sisi Watanzania kwa kazi yoote aliyoifanya RAIS wetu kweli kuna haja ya kumchafua?

Mimi sioni haja hapa isipokuwa Watanzania kama kweli wanahitaji maendeleo uelekeo wameisha uona. Katika maendeleo huwa hakuna miujiza!.

Huwezi kupeleka timu uwanjani kipindi tu cha kwanza ikapigwa mabao kama Ishirini ukaendelea kujipa moyo kuwa huko mbeleni kuna ushindi. Kwa hili watanzania tumepigwa mabao (timu imechemsha hapa) tayari hakuna haja ya kuendeleza timu ile ile tunahitaji kuondoa timu uwanjani na kuweka timu yenye wachezaji wapya kabisa, vinginevyo kipindi cha lala salama kinaweza kutuweka pabaya sana.

Pia nafikiri JK kweli ni muungwana wakati anaingia madarakani alikuwa kweli amedhamilia kuwakomboa watanzania, lakini pia yeye mwenyewe akiulizwa kama kweli aliyokusuadia kuwasaidia watanzania ameweza nafikiri hata yeye anaona hivyo anajibu zuri sana.

Tunategemea 2010 awe wa kwanza kutusaidia kuleta summary ya archivements zake. Mwaka mmoja tu umebakia pamoja na kwamba nina wasiwasi tunaweza kuongezwa mabao mengine
 
Kuna msemo unaoenda hivi ' utavuna ulichokipanda' hence he/she has to face the music. Siku zote watu wanatakiwa wawe waangalifu na waweke mbele maslahi ya taifa.

Live and let others live, lakini vingozi wetu believe in live and let others DIE

Mungu tubariki waTZ na utunusuru na mafisadi, Amen
 
Ina maana hawa mafisadi haiwezekani kuwashughulikia mpaka JK atishwe????????? Tz kweli nakatisha tamaa..........
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom