Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Udini CCM? - viongozi waislam ni 75

Status
Not open for further replies.
Ochu hicho kiapo alichokula alikula mbele yako au mbele ya watanzania ? Je watanzania wanajua kilichomo ndani ya hicho kiapo ? Inawezekana mambo yanayoendelea sasa hivi ndio kiapo chake alichokula kama ni tofauti naomba utupe kiapo alichokula ambacho wewe unafikiri ni sahihi

aliapa mbele ya Jaji Mkuu wa tanzania na mbele ya watanzania wote kuwa atailind ana kuitetea katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania. suala la muungano liko ndani ya katiba na ameshindwa kulitetea
 
Karume ni rais mjinga sana na hana la kusema kwa kuwa kama walivyo wazenj wengi uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana

Huwezi kuwatukana wazanzibar kuwa wanauwezo mdogo, haya ni matusi na hakika hayavumiliki kwa jinsi yeyote ile .

Naami ni kuwa unapaswa kuomba radhi mara moja.
 
CUF yafanya mkutano wa aina yake Zanzibar na yasema Zanzibar ni nchi hata nje ya Tanzania ,mazonge na mikwara ya Serikali ya Muungano iliyojaa waTanganyika ndio waliyoiuwa Zanzibar katika medani ya Kimataifa kwa kungeuka Mkataba wa Muungano.
Habari zaidi zitaelezwa na waandishi wa habari lakini inasemwa hakuna aliebakia nyumbani hata viongozi wa ngazi za juu wa CCM walihudhuria kiaina lakini walionekana na kukaribishwa katika jukwaa la waheshimiwa.
 
lini yametokea mambo hayo? Mbona saa hizi ni asubuhi hapo zenji? Mkutano umefanyika alfajiri?
 
CUF yafanya mkutano wa aina yake Zanzibar na yasema Zanzibar ni nchi hata nje ya Tanzania ,mazonge na mikwara ya Serikali ya Muungano iliyojaa waTanganyika ndio waliyoiuwa Zanzibar katika medani ya Kimataifa kwa kungeuka Mkataba wa Muungano.
Habari zaidi zitaelezwa na waandishi wa habari lakini inasemwa hakuna aliebakia nyumbani hata viongozi wa ngazi za juu wa CCM walihudhuria kiaina lakini walionekana na kukaribishwa katika jukwaa la waheshimiwa.

Pole Mheshimiwa Mwiba. Nilikwambia miye unachupia gari hivyo!. Sasa unaona. Zanzibar ni Nchi ndani ya Tanzania. Siyo Nchi asilani nje ya Tanzania. Kwani wewe hujui hivi? Pole yako Bwana Mwiba. Na ujue tu hakuna suala la Serikali Tatu - ingawa pia hakuna la Serikali moja. Ukiona gari inakwenda usikurupuke kuchupia tu -Mwiba. Upo hapo?
 
Pole Mheshimiwa Mwiba. Nilikwambia miye unachupia gari hivyo!. Sasa unaona. Zanzibar ni Nchi ndani ya Tanzania. Siyo Nchi asilani nje ya Tanzania. Kwani wewe hujui hivi? Pole yako Bwana Mwiba. Na ujue tu hakuna suala la Serikali Tatu - ingawa pia hakuna la Serikali moja. Ukiona gari inakwenda usikurupuke kuchupia tu -Mwiba. Upo hapo?

Wakati ndio utasema ,mkutano umeanza saa nne au kama badu basi wamekuwa wanafanya makolombwezo tokea asubui ,ni mkutano wa asie na mwana abebe jiwe.

Subirini mkutano ukimaliza , naona ndio wakati mtapata ya kusema kama ni mbivu au mbichi.
 
Cuf ni sleeping giant katika politics za Tanzania, hawa jamaa wapo makini sana kwenye kusimamia issues husikii mambo ya kugombea ruzuku na upuuzi wa aianhiyo na uongozi wote wa juu umeshikamana sawasawa kwa hili nawafagilia sana hawa jamaa
 
Na pale kulipoanza dalili za wenye tamaa kuwaletea upuuzi wa ufisadi ndani ya chama chao hawakuwakawiza ndio maana Tambwe Hizza akakimbia...alivumiliwa sana angekiharibu sana km angeendelea kuwepo saa hizi tulii na mafisadi wenzie anaongeza ukubwa wa ngozi mwilini! kwi kwi kwi
 
Kwangu mimi sioni tatizo lolote kwa Kamati Kuu kuwa na idadi kubwa ya watu wa dini moja. Hali hiyo haiashirii udini. Kwa kipindi kirefu hapa nchini waliosoma sana ni Wakristu kutokana na utaratibu wao wa kujenga shule pamoja na makanisa yao. Hivyo kwa usomi wao wanazo sifa za kushika nyadhifa mbalimbali katika taifa. Huo si udini hata kidogo. Mimi ninachokiona katika CCM ni kuwa kumejaa mafisadi wasioitakia mema nchi yetu na siyo udini. Kumejaa watu wanaopenda ubinafsi na hawajali hali duni ya mamilioni ya watanzania. Sidhani kama dini ni kigezo cha kugombea ujumbe katika Kamati Kuu ya CCM.
 
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, WAKATI WA KUPOKEA MAANDAMANO YA KUPINGA MAUAJI YA MAALBINO, UKUMBI WA KARIMJEE,
DAR ES SALAAM, TAREHE 19 OKTOBA, 2008
corrected
Ndugu Ernest Kimaya, Mwenyekiti wa Chama cha Maalbino,
Waheshimiwa Viongozi;
Wanaharakati wote mlioko hapa;
Wageni waalikwa;
Mabibi na Mabwana:

Nawashukuru viongozi wa Chama cha Maalbino kwa kunialika. Mwaliko wenu umenipa fursa nzuri ya kufahamiana na kusikia maoni na ushauri wenu juu ya kiini cha tatizo la mauaji ya watu wa jamii ya Maalbino hapa nchini na namna ya kukabiliana na tatizo hilo.

Nawashukuru kwa ngonjera na igizo lililosisimua na kuleta simanzi kubwa.

Nawashukuru kwa risala yenu iliyosheheni maoni na ushauri muafaka. Tumeyapokea mapendekezo yenu na tutayafanyia kazi. La kuwawezesha kutembea tutafanya hivyo. Aidha, nawashukuru kwa maelezo ya ziada yaliyotolewa na wawakilishi wa vikundi mbalimbali.

Mawazo yenu na yetu yanashabihiana kuhusu kiini cha tatizo na nini kifanyike. Kwa jumla sote tunataka kuona unyama wanaofanyiwa ndugu zetu hawa unakomeshwa.


Kila mtu ana haki ya kuishi
Ndugu zangu;
Katika suala hili la mauaji napenda kuwahakikishia kuwa Serikali ni mdau mwenzenu katika mapambano haya. Serikali inatambua wajibu wake wa kulinda haki ya msingi ya raia wa nchi hii ambayo ni ya kuishi na kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. Albino ni raia kama alivyo raia mwingine yoyote, hivyo anayo haki sawa na anastahili apatiwe haki hiyo kama apatavyo raia mwenzake wa nchi hii. Napenda kuwahakikishia kuwa hivyo ndivyo ilivyo Serikalini kwa raia wote na hakuna anayebaguliwa: awe Albino au siyo Albino; awe mwanamke au mwanaume, au wa dini au rangi, kabila lolote.

Mbele ya Serikali raia wote ni sawa. Wote wanayo haki sawa ya kuhakikishiwa uhai wao. Kwa kuzingatia ukweli huo mauaji yanapofanywa kwa raia yeyote utaratibu wake wa kushughulikia matukio ya namna hiyo nao ni mmoja na sawa. Hauna ubaguzi wowote na unaongozwa na sheria moja. Hali kadhalika adhabu nazo zinalingana, hazibagui Alibino na asieyekuwa Albino. Adhabu kwa aliyeua kwa makusudi ni kifo.

Mahakama haijatoa adhabu tofauti kwa aliyeua Albino na aliyemuua mtu ambaye si Albino. Tena haki hiyo si kwa raia tu ni kwa mwanadamu yeyote hata kama si raia wa nchi hii anapouawa hapa nchini na kama aliyehusika ni Mtanzania raia mwenzetu huyo atapata adhabu hiyo hiyo bila kubagua.


Nayasema hayo kusisitiza ukweli kwamba Albino hajabaguliwa na Serikali kwa namna yoyote ile. Amekuwa anatendewa na kupewa haki zake stahili kama raia popote na wakati wowote. Isitoshe kwa kutambua mahitaji maalum ya Albino Serikali haijasita kutoa upendeleo pale ulipostahili.

Napenda kuwahakikishia kuwa pale palipojitokeza tukio hilo tulichukua hatua na kama kutatokea Albino kufanyiwa vitendo vya kubaguliwa popote pale tupeni taarifa na hatua zipasazo zitachukuliwa dhidi ya wahusika.


Kiini cha matatizo yanayowakabili watu wa jamii ya Maalbino nchini ni mila potofu za makabila yetu. Kwa makabila yetu mengi nchini kama siyo yote kuzaliwa mtoto Albino katika ukoo ni balaa ambalo halikubaliki. Kwa mujibu wa mila za makabila mengi mtoto albino anapozaliwa huuawa.

Tena kazi hiyo hufanywa pale pale anapozaliwa na wakunga na huzikwa kimya kimya kwa siri kubwa. Hata sisi Wakwere tumekuwa tunafanya hivyo. Ndiyo maana kwa watu wa umri wangu tuliozaliwa mikononi mwa wakunga wa jadi hatukuti Albino.


Siku hizi kwa sababu ya kuenea kwa zahanati, vituo vya afya na hospitali na kina mama wengi kujifungulia hospitali mauaji ya watoto Albino yamepungua kwa kiwango kikubwa. Kwa wale waliozaliwa hospitalini hayapo kabisa na kwa wale wanaozaliwa chini ya mikono ya wakunga wa jadi nao kama yapo ni kidogo sana. Elimu imesaidia wengi kumuona mtoto Albino kuwa ni mtoto sawa na mwingine.

Wengi wenu nyie waliozaliwa vijijni kwa wakunga wa jadi hawakupata bahati hiyo. Serikali na jamii kwa jumla haina budi kutambua nafasi ya elimu katika kukomesha mauaji ya Maalbino katika mazingira haya. Tutaendelea kuelimisha jamii na wakati huo huo tutaendelea kueneza huduma ya hospitali ili mama wajifungulie hospitalini. Hayo mawili ndiyo majawabu.

Lakini elimu ndiyo itakayosaidia kuondoa tatizo la unyanyapaa wa Albino. Tatizo hili nalo linapungua sana siku hizi kuliko ilivyokuwa zamani. Katika mazingira yale yale ya kumuona Albino balaa, hata kuishi na yule ambaye alibahatika kutokuuawa ni jambo la mashaka mashaka.

Kiserikali hatuwabagui Albino kwa haki zao za msingi wanazostahili kupata kutoka katika serikali na jamii kuhusu maisha yao na mali zao. Serikali haiwabagui kwenye upatikanaji wa huduma za msingi kama vile elimu, afya, maji na ajira. Na iwapo itatokea mtu yeyote atabaguliwa na mtumishi wa Serikali kwa sababu ya kuwa Albino nawahakikishia kuwa matendo hayo ni yake binafsi siyo sera wala mwongozo wa Serikali. Tuarifuni tuchukue hatua zipasazo.

Ndugu Wananchi;
Hiyo ndiyo sura moja ya mila potofu zinazohusiana na mauaji ya Albino hapa nchini tunayoijua sote. Lakini, siku za hivi karibuni imejitokeza sura mpya ya mauaji ya Albino ambayo kiini chake ni ushirikina. Ushirikina unaojenga imani ya kijinga ati kuwa ukipata kiungo cha Albino unapata mafanikio katika uvuvi na uchimbaji wa madini. Nasema ni ya kijinga kwa sababu hakuna ukweli wowte kwamba kiungo cha Albino ndicho kitakufanya ufanikiwe katika biashara yako badala ya kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.

Kama ingekuwa viungo vya Albino ni chanzo cha utajiri, basi Maalbino leo ndiyo wangeongoza kwa utajiri duniani. Jambo hilo si kweli hata kidogo. Nawashangaa sana wale wanaoamini hivyo kwa upande wa wafanyabiashara na wale waganga wa jadi wanaowadanganya watu kuwa wakipata viungo vya Albino watapata mafanikio makubwa. Najua wanajua kuwa wanawadanganya lakini kwa vile waliotayari kudanganywa wapo wanautumia mwanya huo kujipatia mapato haramu yanayosababisha mauaji ya kikatili na mateso makubwa kwa wenzetu wa jamii ya Albino.


Ni maoni yangu na ya Serikali kuwa tunayo mambo mawili au matatu ya kufanya. Kwanza kabisa kuelimisha kuwa utajiri hautapatikana kwa kuwa na kiungo cha Albino bali kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Hii nayo si kazi rahisi kwa sababu wengi wetu bado tunaamini katika uwezo wa nguvu za giza katika kutuwekea sawa mambo yetu. La pili, ni kuwatambua waganga wa jadi wanaoeneza imani hiyo na wale watu wanaotumika kuua na kupata hivyo viungo. Kazi hii tunaendelea nayo na tumekuwa tunachukua hatua. Kuna mafanikio yanayoendelea kupatikana. Ugumu mkubwa ni ule usiri unaoambatana na suala lenyewe. Hata hivyo hatutachoka mpaka tulidhibiti.

Msako dhidi ya wahusika
Ndugu wananchi;
Mtakumbuka kuwa katika hotuba yangu ya kuhitimisha na kuuaga mwaka 2007 niliyoitoa kupitia vyombo vya habari tarehe 31 Desemba, 2007 nilielezea masikitiko yangu na dhamira yetu ya kupambana na watu wanaojihusisha na mauaji ya Maalbino kwa imani za kishirikina. Nilisema kuwa, Jeshi letu la Polisi litafanya kila liwezalo kuwasaka watu hao waovu pamoja na kuvunja mtandao wao wa uhalifu.

Kazi hiyo inaendelea na haitasimama hadi hapo tutakapotokomeza kabisa mauaji haya. Kama tulivyofanya kwenye suala la ujambazi, tutaendelea kuimarisha uwezo wa vyombo vyetu vya usalama katika kukabiliana na tatizo hili.

Tayari Jeshi la Polisi limewakamata watu 47 wanaotuhumiwa kujihusisha na uharifu huu kati ya mwaka 2007 na Oktoba, 2008 ambako matukio ya mauaji yalikuwa ni 28. Kati ya hayo matukio 18 yametokea kati ya Januari na Oktoba, 2008. Watuhumiwa 17 wamekamatwa Mwanza ambao ndio mkoa unaoongoza kwa vitendo hivi vya mauaji ya Albino. Watuhumiwa wengine sita (6) wameshatiwa nguvuni mkoani Mara. Jeshi la Polisi pia limewatia nguvuni watuhumiwa wawili (2) mkoani Kagera na mmoja Shinyanga. Na hivi karibuni watuhumiwa wawili wamekamatwa Mkoani Mbeya.

Aidha, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mabaraza ya Ulinzi na Usalama ya Mikoa na Wilaya linaandaa mkakati endelevu wa kupambana na uharifu huu. Pia linaandaa orodha ya Maalbino wote nchini na kutambua sehemu wanazoishi ili kuimarisha usalama na ulinzi wao.

Shanjari na hilo, Polisi wameanza kutekeleza dhana ya ulinzi shirikishi kwa kuwashirikisha wananchi katika kuwatambua waganga wa jadi wanaopiga ramli chonganishi ambazo ni moja ya sababu kubwa zinazopelekea kuwepo kwa mauaji ya ndugu zetu Maalbino.



Wajibu wa kila mmoja wetu

Pamoja na hayo ni vyema sote tukatambua kuwa, vita hii haiwezi kuachiwa Jeshi la Polisi peke yake. Hii ni vita yetu sote, jamii nzima. Kwani wanaohusika na mauaji hayo ya kinyama tunaishi nao na baadhi yetu huenda tunawafahamu. Tunawajua waganga, wauaji na wafanyabiashara wanunuaji wa viungo.

Naomba tuendelee kuwafichua. Tuwape Polisi taarifa zitakazosaidia kuwakamata ili wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria. Tulifanya hivyo katika mapambano yetu dhidi ya ujambazi tukafanikiwa; tufanye hivyo sasa katika vita hii, naamini pia tutafanikiwa.

Nasema tuendelee kufanya hivyo kwani hata hawa waliotiwa nguvuni sasa ni matokeo ya ushirikiano huo. Tuuzidishe.


Ndugu zangu,napenda kusisitiza kuwa katika vita hii sote ni wadau. Hivyo ushirikiano wetu ni jambo muhimu kama tunataka (Tusi)(Tusi)(Tusi)(Tusi)liza tatizo hili mapema. Raia washirikiane na vyombo vya dola ipasavyo, tutafanikiwa.

Vyombo vya Habari

Katika mapambano haya vyombo vya habari vina mchango mkubwa. Hivyo tunaviomba vitusaidie kuelimisha jamii kuachana na mila potofu. Pia wasaidie vyombo vya dola kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kuwapata wahusika na uhalifu huu.

Wanaharakati nao endeleeni kutusaidia katika kuelimisha umma. Tayari mnafanya kazi nzuri lakini bado haitoshi kwani tatizo bado lipo na kubwa. Kulaumu hakuna tija katika mapambano haya.

Mwisho, napenda kuwahakikishia ndugu zetu wa jamii ya Maalbino nchini kote kuwa, Serikali ipo kuwalinda, kuwatetea na kusimamia haki zenu zote kama inavyofanya kwa raia wengine wa nchi yetu. Natambua haja ya mtazamo maalum kwa ajili ya Albino. Tuyatafakari pamoja na tutaendelea kupambana na wale wote wanaojihusisha na mauaji haya ya kinyama na wengine wote wanaohusika katika kuwapotosha kwa imani za kishirikina.

Na katika mapambano haya hatukubali kushindwa pamoja na ugumu wake. Lazima tutashinda kwa mshikamano na umoja wetu. Hivyo nawaomba wananchi muendelee kushirikiana na Serikali hususan vyombo vyake na kutuunga mkono.

Mwenyekiti alilisemea suala la uwezeshaji kiuchumi: naomba mtengeneze mawazo yenu ili tuone namna ya kusaidiana. Meya amenihakikishia kuwa katika jengo Wamachinga walemavu wakiwemo Albino wanahakikishiwa kupata nafasi ya kufanya biashara.
Naomba nimalize kwa kusema kuwa mauaji ya Albino yanatuuma, yanatusikitisha sana. Tutaendelea kupambana na uovu huu bila kuchoka mpaka tuutokomeze.

Asanteni kwa kunisikiliza!
 
watakaothibitika kuhusika/kushiriki kuua/kudhuru albinos............kama si kunyongwa wafungwe maisha.........damn!!
 
Hii ni kawaida na itakuwa kawaida.Katika jamii pofu, iliyojaa ujinga , jamii isiyoelimika, jamii inayowaza uchawi na kuwa watapata utajiri kichawi, SI SWALA LA KUANGALIA UPANDE MMOJA TU, serikali wanayopart ya kuplay.

Katika karne hii ya 21 wakati watu hawaruwazi hata kusikia uchawi na uuaji wa namna hii, Tanzania unapatikana, serikali inapaswa kuwaondoa watu gizani, pamoja na nguvu kama hizi , lakini bado watawaacha maalbino wataamia wenye upara..,vitambi..

Jamii imekata tamaa,inaamini utajiri utapatikana kwa uchawi, yes maana maana amemuona jirani katajirika kwa ufisadi pengine, na wanawaona wako mitaani wakitutambia kwa maprado yao.Wanaona solution ni hiyo.

Siwatetei ila tuangalie kwa mapana na marefu.

Sidhani kuwa polisi wameshindwa kazi yao, mpaka muungwana atoe hukumu hiyo..maana kama ni hivyo wanagpi wanakufa hospitali kwa ufisadi, wangapi wanakufa kwa kukosa malazi, madawa, barabara..kisa fedha zimepote kifisadi.

waberoya
 
Hili siyo suala la kisheria tu; mara nyingi sheria hazi deter watu kufanya uovu hasa wakipima risk na faida inayopatikana na vitendo vyao. Kama vitisho vya sheria vingekuwa vinazuia watu kufanya uovu wezi wa EPA wangaliacha zamani!
 
Leo hii dunia nzima inajua kuwa watanzania ni wauaji wa albino! Tutajificha wapi?
 
sio watanzania wote hata kuhusu ufisadi sio kila mtanzania ni visadi kila mtu abebe mziko wake
 
ni vipi hotuba kwa albino imepatikana wakati ile aliyo itoa bungeni mwezi juni bado ina karabatiwa ikulu?

macinkus
 
Hili siyo suala la kisheria tu; mara nyingi sheria hazi deter watu kufanya uovu hasa wakipima risk na faida inayopatikana na vitendo vyao. Kama vitisho vya sheria vingekuwa vinazuia watu kufanya uovu wezi wa EPA wangaliacha zamani!

....hapana bana...........ni utekelezaji tu sheria........check Nigeria for example uhalifu uliopo south na ule wa North...........

...kuna wakati niliona video clip.......jamaa anakatwa uume hadharani baada ya kubambwa/kugundulika amebaka.........matukio ya ubakaji ni almost nil.....

Albino must be protected.........by any means......Mh Rais JK....hao watakaopatikana na hatia.......nao wanyonge mapaka wafe......hakuna cha huruma....eti haki ya kuishi...wakti watu wanaua wenzao!!!.....damn
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom