UCHIZI katika Nchi: Kauli ya Mch. Gwajima...

UCHIZI katika Nchi: Kauli ya Mch. Gwajima...

- Eti ni wapi Yesu aliitukana Serikali kwamba ina maamuzi ya kichizi, unapoteza muda mwingi sana bila hoja onyesha ni wapi yesu aliitukana Serikali?

- Yesu alisema ya kaziari muachie kaizari siku alipoulizwa kuhusu Serikali, sasa wewe hii bilblia yako ni ya wapi? Au yako mwenyewe?

le mutuz

hivi hujui Yesu alikuwa crucified kwa kujiita mfalme huku nchi ina mfalme! Kosa la uhaini hili. TAYADI kakuweza
 
Last edited by a moderator:
tatizo lenu wazee wa kujilipua hamkumbuki fadhila shule za wakristo zimewasomesha zilipotaifishwa leo mna elimu mnasahau mlikotoka ingekuwa pilau msingesahau

Hiyo lugha ya kujilipua ndiyo wanayoielewa watenda uovu. Mimi sikusoma shule ya kanisa kwa bahati mbaya tangu chekechea mpaka nilipofikia kwa hiyo sina fadhila ya kulipa.
 
- Mchungaji wako ni simply mjinga na hafai hata kuwa Mchungaji, maana ya siasa hayamuhusu anatakiwa kuwa busy kutafuta wananchi na kuwapa imani ya Mungu huwezi kuwa Mchungaji Kanisani na hapo hapoa ukawa Professor wa Muungano,

- Yesu aliyajua haya mapema sana ndio maana akasema ya Kaizari Muachie Kaizari, huyu Mchungaji ni hopeless inaweza kuwa hata waumini wake ni kama yeye ama sivyo wangemfukuza, mimi ningekuwepo hapo kanisani ingekuwa ni balaa maana nisingemuacha!

- Kuhusu maisha yangu binafsi please wachana nayo maana huu mfupa umesmhinda Fisi, wamejaribu mpaka magazeti ya udaku wameshindwa, kuna we nzako hapa wamejaribu sana kunichafua wameshindwa wewe huwezi huuu ni ukuta, nina Three Combination za masomo niliyoyasoma sana kule USA, nilisomea sana Dini ya Christian, Criminology na Political Science so kwenye hii Combination kucheza na mimi kisaikolojia unajichezeaa mwenyewe, so think again kama ni worhty!!

Le Mutuz

hivi huyu mzee ndio yule mtoto wa mheshimiwa malecela au kuna mtu kajisajili kwa jina lake? P'se wanaomjua wamtaarifu kuna mtu anamchafua huku! Kama ni yeye Sipati picha ujana wake!
 
Mchungaji huyu ana akili sana na nimemuamini sana kwa kauli hii. Kuna wakati mtu unapata hasira kiasi cha kuumia
 
...teh teh...Tanganyika bwana ...kazi yake kulalamika tuuuuuuuuu...
 
- Mchungaji ni hopeless huwzi kusimama mbele ya waumini wanaowasikiliza wanasiasa kila siku na kuwaambia eti maamuzi ya Serikali ni Uchizi, ndio maana nasema hata hilo Kanisa nina wasi wasi nalo sana kama wapo powa!

le mutuz

kama watu wenyewe viongozi wa magamba wenye akili kama za kwako kwa nn mchungaji asiwaite machizi.!
 
"Kipande cha nchi Chenye idadi ya wakaazi Milioni Moja Tu Kinaungana na Kipande kikubwa cha nchi chenye zaidi ya watu zaidi ya Milioni arobaini na Tatu, halafu vipande hivi viwili vinakuwa na Nguvu sawa kwenye Kuunda Hatma ya Nchi (Katiba), Huu ni Uchizi.. "Mch Gwajima, Sunday speech Leo.


Miaka yote hiyo alikuwa wapi kutueleza haya,yawezekana yeye uchizi ndio unaanza kipindi hiki.

Kwa hiyo ndio kusema hata wale waumini wanaomweka mjini ni machizi sio,maana haiwezekani kuwahubiri wenye utimamu
bali waliopotea.

Si ayafuate yale ambayo ametumwa na Mungu wake kuhubiri watu wake,sasa haya ya siasa ameyatoa wapi?

Wakiambiwa waachane na siasa katika dini/imani zao wanakuwa wabishi kikitokea cha kutokea katika imani zao wanalalamikia siasa wakati wao wenyewe ndio wanang'ang'ania kuhubiri siasa.
 
Wazanzibari ni wasumbufu sana, usiombe ukawa na jirani kama huyu tena akiwa na uhuru kamili wa kuamua anavyotaka, bora uungane naye ili umdhibiti.
 
...Nadhani ni muafaka nikianza kwa nukuu ya Mwalimu Nyerere kutoka kwa kijitabu cha TUJISAHIHISHE (1962, ukurasa wa 8):
Watu walio hatari ni wale ambao wanafikiri kuwa wanajua kila kitu, wala hawana haja ya kujifunza zaidi.
Inawezekana Mch. Gwajima hakuwahi kusoma kitabu hiki cha Mwalimu Nyerere (1962) na inawezekana Mch. Gwajima ana matatizo ya "ugonjwa" wa ubinafsi zaidi ya tunavyodhani! Nina sababu ya kudhani hivyo; na siwezi kuuma maneno juu yake, hoja zifuatazo zina kila sababu ya kujibu madai yake juu ya UCHIZI anaouona yeye (Mch. Gwajima). Hoja zangu ni hizi:

  1. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni zao la Mkataba wa Muungano (Articles of Union) baina ya nchi mbili;
  2. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliridhiwa Tanganyika na kupitishwa kwa Sheria Na. 22 ya mwaka 1964 inayotambua kwamba, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni "muungano" wa nchi MBILI (Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar)...rejea Kifungu cha 3 na 4 cha Sheria Na. 22, 1964...kwa jinsi hiyo, MUUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar si muungano wa WATU isipokuwa ni muungano wa JAMHURI mbili (Tanganyika na Zaznibar).

Nadhani Mch. Gwajima anahitaji "aelewe" kwamba: ZILIZOUNGANA NI NCHI MBILI; NA SI WATU WA NCHI MBILI! Kwa kuwa nchi mbili (Tanganyika + Zanzibar) ndizo zilizoungana hakuna sababu yeyote kudhani kwamba kwa wingi wa WATU wa sehemu moja ya muungano ndivyo tunavyoweza kufanya maamuzi juu ya MUUNGANO ambao asili yake (kwa mujibu wa Articles of Union na Sheria Na. 22 ya 1964) ni mkataba wa kisheria baina ya NCHI MBILI HURU (NA ZILIZO SAWA MBELE YA SHERIA).

Hata kama kulikuwa na jitihada za makusudi za kupora UHURU wa nchi moja (Tanganyika) na kuipoteza kwenye ramani ya nchi za dunia kwa kisingizio cha MUUNGANO; bado sehemu ya wenye AKILI za upembuzi ulikuwa ukitafuta wakati wa kuliweka jambo hilo sawa na kulitafutia MUAFAKA (Zanzibar walipofanya Marekebisho ya Katiba 2010 waliamua kuandika wazi kwamba: Zanzibar ni NCHI inayounda MUUNGANO)...huu ndio mwanzo, na tamko (kauli) ya Mch, Gwajima inaonyesha wazi "agenda" iliyojificha nyuma ya tamko (kauli) lake/yake na hatuwezi kudhani kwamba amefanya hivyo akiwa na AKILI TIMAMU, au kama hajui kwamba MUUNGANO uliundwa kwa mujibu wa "makubaliano" yaliyoridhiwa na watu wawili (NYERERE na KARUME) kwa niaba ya NCHI MBILI (Tanganyika na Zanzibar).

Mwisho, kama Mch. Gwajima anadhani kwamba Watanganyika milioni 43 (sasa, kwa mujibu wa Matokeo ya Idadi ya Watu, 2012) wanaweza kuwameza Wazanzibari milioni 1+; hii ni dhana HASI (-) inayohitaji kukemewa kwa NGUVU (za UHURU, HAKI na USAWA) kwa kuwa Zanzibar ilikuwa NCHI na bado ni NCHI kama ilivyo TANGANYIKA. Kama dhana ya idadi ya watu ndio kigezo cha kufanya maamuzi ya kisiasa kuhusu MUUNGANO, basi Articles of Union (1964) na Sheria Na. 22 zingaliweka kipengele hicho kwenye nmuktadha wa sheria ili kwa sheria hiyo muafaka wa kisiasa baina ya watu wa Tanganyika na watu wa Zanzibar waamue justakabali wao kwa njia hiyo. Uchizi wa dhana hiyo unaweza kusomeka kwa mtu asiyehoji kisheria kwa MUUNGANO uliyofanywa kisheria; isipokuwa anataka (huyo mtu) kuhoji kwa utashi wa atakavyo yeye au kama anavyoona yeye pasipokuwa na hoja zenye mashiko ya kisheria na au rejea rasmi zilizokubaliwa na NCHI mbili (Tanganyika na Zanzbiar).


Muungano umefanyiwa marekebisho mengi; na wasomi wa SHERIA wameandika sana juu yake, kwa hiyo namuomba Mch. Gwajima (na wenye mawazo kama yake) warejee rejea za kisomi juu ya sherehe (upembuzi na usanifu) wa tasnia ya MUUNGANO kwa mtazamo wa UHURU, HAKI na USAWA. Tusitengeneze wafuasi juu ya kuchukia jambo (au mambo) usiyoyajua...na kwa anayejiita "mtu wa mungu" kama Mch. Gwajima lazima atambue kwamba MUUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar haukuwa "muungano wa watu" ulikuwa muungano wa kisheria baina ya NCHI MBILI HURU; na si kinyume chake - HUU NDIO UKWELI...kinyume chake Mch. Gwajima anataka atuaminishe UONGO (kwa maslahi yake).
Bakari..
asalaam

Bandiko lako umelinyima uhuru wako, kumbuka ulichobandika ni mawazo tu ya wazee tokea 1964, Na matamshi ya watanzania waliotutangulia lakini wewe Binafsi hujatoa maoni yako zaidi ya Kushutumu semi Kwa ghani Za kihistoria..

Embu funguka kifikra jaribu kujiuliza mwenyewe mbali Na hizo Article Za Muungano ambazo kwangumie ni Historia Na Historia haiwezi kunambia Leo kuna Nini. Embu jiulize ni lini Tanganyika Na Zanzibar ziliketi kuunda KATIBA TOKEA muungano???? Zaidi ya katiba hii ya Chief Adam Na Kombo JE kuna katiba ya Kimuungano??????? Kama waunganaji hawa hawajawahi kuketi kuunda mustakabali wao Sababu yake ni Nini ????

Unajua Hata ndoa zina 'instruction Manual' sasa iweje Nchi mbili ziungane Na zisiketi kutengeneza mstakabali wa maisha Yao?

Hembu acha uoga jaribu tu kuwaza Kwa sauti Kama from 1964 waunganaji hawa hawajaketi kujenga Katiba Lao Ndo waje walijenge 2012, inaingia akilini mwako BAKARIIII???

Tuache kulaumu historia embu tuje Kwenye uhalisia hii Tume ya Katiba inakusanya maoni ya nchi ngapi?, Muungano Gani?, na what shall be its compilation..

Tutapokuja Kwenye common fact, ok let's Vote.. What shall be the nature of votes .. Nchi hazipigi votes Bali wananchi, sasa 43:1 vote line unadhani kitu hiyo ipo.. Embu tuache kufumbia macho majanga, Wazanzibar wana interest zao Na kama kura Za watanzania 43:1 zitawafunika wana visiwa hao hujui tayari tumeshawakwida matakwa Yao ?????!!??

Twendeni Mbele mziki huu hauwezekani JAMANI, tafadhali tujadilini kwanza ni Muungano gani Watanzania tunautaka, kisha ichorwe mistari halisia ya wazi Kwenye Muungano kisha ndipo tuingie zoezi la kujenga mustakabali wa Nchi. Kama maamuzi ni Serikali Tatu, mbili, Moja Basi tujadili Kwa Uwazi hili.

Tungekuwa Na Muungano Leo usingesikia upuuzi Wa pande mbili au tatu.. Ingeundwa tume ya Jamhuri ya Muungano bila Kutaja pande Za ushiriki, ukishasema tu wajumbe 14 from Zanzibar haya wangine 14 from where???? Ukisema Tanzania Bara umeshavunja Muungano wewe, neno lenyewe Tanzania manaake (tanganyika + Zanzibar)

Unaposema unaunda tume ya katiba 14 members from Zanzibar hawa ni solid members from ZANZIBAR, but ukisema 14 from Tanzania Bara, this means 14 members from (Tanganyika Na Zanzibar walioko bara) hii unaiona Bado iko sawa BAKARI..?!!???

Ok tuje Kwenye kiinimacho kingine Unamwitamwitaje 'HUYU MZANZIBAR' 'HUYU MTANZANIA BARA' UNAMWITAMWITAJE?????, unatumia IDENTITY GANI, rangi?, lunga, Makazi?, Kuzaliwa ? Unatumia Nini Kama si viinimacho !?! Watanzania ni Watanzania tu, hatunaga ma Identity au Tatoo mwilini Kama alama Za Uzanzibari au uzanzibara wetu, ni total Confussion..
Mambo serikali inayoyafanya ni Kuvunja Muungano Na Kuleta roho Za kibaguzi mie Sijui akili hizi nani kawasaidia..??!! Wamrudishie akili zake walomwazima

BAKARI Haya unakubaliana nayo kweli..

Mie Binafsi Hoja yangu tuondoe uzanzibar Na utanganyika Tuunde katiba ya Tanzania.. Futeni ubaguzi Nchi zilishaungana Leo kuanza kuzibagua tena as if Ndo zinaungana ITAWACOST..
 
ni uchizi kweli kweli, uwa nashindwa kuelewa kwa nini zanzibar isiitwe mkoa wa tz? yani mawazo yangu ni kuwa siku yoyote gsana akiwa rais ni kuamuru watu wote walio zanzibar wagawiwe ardhi dodoma , singida ,kibaha na mtwara alafu ardhi yote ya zanzibar tufuge kenge, mamba na nyani ili kumaliza mgogoro huu wa kipuuzi badala ya kuangaika na mambo ya kimaendeleo...kuendelea kuijadili zanzibar ni kulea uchizi....
 
napinga muungano wa watu 43mil kwa watu 1mill na mwisho wa siku mnakuwa na equal say and rights...HELL NOOO.

KWA SIASA NA HALI YA DUNIA YA MWAKA 1964 NYERERE NA KARUME WALIKUWA SAHIHI...SAHIVI 2013...HUO MUUNGANO HAUNA DEAL NA HAUFAI HATA KUZUNGUMZIKA...

UVUNJWE NA KAMA NI MUUNGANO ZANZIBARI WAUNGANE NA WILAYA YA ILALA NDANI YA DAR ES SALAAM.
 
Angalia msijemkawa mnatukana baba wa taifa aliyeunganisha nchi mbili hizi! Ohoo, Mwalimu Nyerere ndiye aliyeunganisha hizi nchi mbili na kwa wakati huo population ya ZNZ ilikuwa ndogo zaidi kuliko ilivyo sasa!

Muungano haukufanywa kwa kuangalia idadi ya watu bali hadhi ya nchi zilizounda muungano.
Hata baba Huwa anakosolewa na kushauriwa eti....
 
Huyu alikuwa na Roho Mtakatifu katika maneno yake. Nachelea kusema haya ni maneno ya Roho Mtakatifu kupitia kwa Mchungaji Gwajima
 
tulishakubaliana kuungana pasipo kuangalia idadi ya watu ama ukubwa wa nchi,kwa hiyo hatuna budi kuwa wavumilivu ktk hili na hata wakati huo tunaungana walioengineer muungano huu waliyaona haya.
Wewe
Kama tulishaungana.. Fine Tulishaungana.. Sasa KWANINI chizi Mwingine leo aseme wajumbe 14 from Zanzibar Na wajumbe 14 From Tanzania Bara.. Muungano uko wapi hapo ????!!??
Muongo huu wa 90' Ndo kelele Za Zanzibar ..!! Bara !! Zimezidi, hazikuwepo Hizi tulikuwa Na Tanzania Leo Tuna Tanzania bara.. Unajua Tanzania bara manaake ni nini? Unapasema 14 members from zanzibar Na 14 members from Tanzania Bara unamaanisha (Tanganyika Na zanzibar) Kwa hiyo tunasema tume imeundwa Na 14 members from Zanzibar and 14 members from Zanzibar and Tanganyika ratio wise 14 members from zanzibar, 7 members from zanzibar stays in Tanganyika and 7 members from tanganyika .. Truth..
 
Mchungaji kasema kweli lakini sifa kubwa ya wanaotawala ni unafiki,mchungaji sio mnafiki.Niliwahi kuuliza humu kuwa una wake wawili mke mmoja anawatoto 6 mwingine anawatoto 2 ukitoa pesa sawa ya matumizi ni haki kwakuwa wote ni wake zako?
 
ndo maana tunasemaga wachungaji wengine ni mabogas tu kama sadaka anazokula hazimtoshi ajiuwe haiwezekani mtu mwenye akili timamu akaongea haya nchi yeye anatafsiri vipi??? ndo shida ya vikanisa vinavyomea kama uyoga
 
UAMSHO wakisema hawataki muungano wanafunguliwa kesi za kuhatarisha usalama wa nchi! Mchungaji akisema, serikali inapiga makofi. Kweli mfumo kristo unafanya kazi yake mchana kweupe ndani ya serikali.

Umeanza upuuzi wewe..Huwezichangia bila kuweka udini? Kweli ningekuwa mwislam kwa hizi comment zenu ningeukana hadharani na matarumbeta juu
 
Hivi ili uwe mchungaji ni lazima kuhubiri siasa kanisani?


Yawezekana mchungaji ameingiliwa na mapepo wachafu wa ubinafsi,wivu na usahaulifu wa kule alikotoka.

Ila tunashukuru kwa kile alichokitoa maana amekitokea muda mwafaka na kama bado wapo wengine nao wajitokeze mapema kabla ya katiba yetu haijapatikana waeleze dukux2 zao ili nyongo na vitu vingine vya kibinadamu vitulie.
 
Back
Top Bottom