UCHIZI katika Nchi: Kauli ya Mch. Gwajima...

UCHIZI katika Nchi: Kauli ya Mch. Gwajima...

Mhandisi wangu
Nchi hii Hakuna mwenye hati miliki nayo, ni Mali yetu sote, hakuna mwenye maamuzi ya nchi kwamba Yeye ni mnene zaidi Kwenye hatma Za Utanzania Na wengine followers, Hakuna kizazi kilichobatizwa haki ya kuimiliki nchi, NCHI NI YETU SOTE, so siwezi kaa Kwenye Nyumba mbovu ikaniangukia siku moja ya mvua eti Kwa sababu ya makosa ya ujenzi wa baba yangu mzazi. No no no..!! Baba yangu ni Mwanadam, SIO Mungu, alikosea tu Kama mwanadam wa kawaida akaweka mfumbati Kwenye kiuno Cha nyumba Na wakati ule wake was fine alijua kuucontroo mfumbati wake but he pass away. Mfumbati wake umeoza, nyumba inaslide sasa, eti tuache mpaka tuangukiwe Na Jengo Kwa Sababu 'baba alikosea kujenga??' shit hii ni zaidi ya mawazo hatari zaidi. Makosa yalitendeka embu tuyarekebishe sasa.. Muungano ulikuwa Na Hira nyingi Na wasiwaSi wa vamizi Za kikoloni Leo hii ni ndoto kuongelea Kwamba mwarabu atavamia ZANZIBAR .. Tuacheni kikariri mambo jamani
wewe unaongelea mifano ya baba na binadamu,mimi naongelea kitu kinaitwa MKATABA,na ndio maana hata matatizo ya mipaka na malawi watu wanaongelea MKATABA,ktk maswala ya madini watu wanaongelea MIKATABA,hata zile pesa nyingi walizo daiwa Tanesco ni kuhusu kukwepa MIKATABA.
Kiongozi MKATABA unalindwa na zipo sheria za kimataifa na ukienda kinyume na mikataba hiyo itatatuliwa ktk mahakama.sasa basi,kuhusu muungano wetu kuna makubaliano na hatuwezi tu kupiga kelele bila hata kwanza kuondoa makubaliano hayo ili baadae yasije kutufunga.huu muungano ni lazima una MKATABA sasa huo mkataba upo wapi?
 
Maisha yetu ni mabadiliko,kila sekunde ,dakika,saa, siku, mwaka na hadi karne ina mambo yake>>> ninachoweza kusema ni kwamba muungano huu ulikubaliwa kuwa hivi ulivyo kwa wakati huo, nina uhakika kabisa kwamba kulikuwa na sababu ya kuuweka hivi ulivyo sasa>>> lakini kwa sababu ya wakati hatuwezi kuendelea na muungano wenye mfumo huu usiozingatia hesabu ndogo tu za kijografia na za kitakwimu, lakini kama tutaendelea kufanya kwa mazoea, kuishi kwa mazoea,kuamua kwa mazoea bila kufanya hesabu kido ambazo wanasiasa wetu hawapendi kuzisikia maana ndizo zinazofafanua ukweli kuhusu jambo lolote au uamuzi wowote, mwisho wa Muungano huu utakuwa ni mbaya!!!
:grouphug:
 
..
Tony hakuna anayepinga Hilo but embu tafakari, Kama muungano ulishatendeka from those 1964 years, ok today we have Tanzania, hatuna tena Zanzibar Na Tanzania bara, ??? Hili unaliona???

Kwanini mpaka Leo serikali inatulazimisha tuongelee Zanzibar as a separate state Na Tanzania bara as another separate state???!!?? Kama tunataka kuunda katiba la Nchi kwanini tusiunde tume ya Tanzania Na si Tanzania bara Na Visiwani?, Kama inshu ni uwakilishi wa maeneo KWANINI wasichaguliwe wajumbe kutoka kila Mkoa au kila Jimbo la uchaguzi wenye Vigezo vya utaalam unaotakiwa?

Tanzania Ina Mikoa 26 fine let choose the members according to maeneo haya Kwa Sababu kila mkoa una vionjo vya kiutamaduni, kiuchumi Na kielimu ambavyo AMA vingepatiwa nafasi Na ulinzi Ndani ya Katiba.. Hatuundi katiba la Kisiasa Kama maoni mengi yanavyoelekezwa, tunaunda katiba Kwa maendeleo ya nchi..

So Tonny open your mind, Serikali inajitahidi sana kuuvunjilia mbali Muungano wetu Kwa kutubagua kila siku kila Leo sasa ubaguzi unapenya kwenye mioyo ya wazawa Leo watu wanasema gesi yetu itufaidie kwanza sisi, kesho ziwa letu litufaidie kwanza sisi hili ni Janga Tonny ..

Mkuu, unaeleweka sana, hapa dhana inayoletwa ndo potofu ya kuangalia idadi ya watu! Issue hapa ni mfumo wa Muungano ndo unaonekana haukubaliki, lakini kuibagua Zanzibar kwa kigezo cha Idadi ya watu siyo sahihi! Kwani duniani hakuna nchi zenye watu Million Moja?????
 
Ukweli mtupuuuuuuuuuu! Hajapepesa macho, hajang'ata maneno wala kutikisa maskio.
 
Angalia msijemkawa mnatukana baba wa taifa aliyeunganisha nchi mbili hizi! Ohoo, Mwalimu Nyerere ndiye aliyeunganisha hizi nchi mbili na kwa wakati huo population ya ZNZ ilikuwa ndogo zaidi kuliko ilivyo sasa!

Muungano haukufanywa kwa kuangalia idadi ya watu bali hadhi ya nchi zilizounda muungano.
kwa hapa alichemka sijui alikuwa anawaza nini?ila nasikia lilikuwa ni shinikizo kutoka magharibi ila kwa kweli alichemka
 
wewe unaongelea mifano ya baba na binadamu,mimi naongelea kitu kinaitwa MKATABA,na ndio maana hata matatizo ya mipaka na malawi watu wanaongelea MKATABA,ktk maswala ya madini watu wanaongelea MIKATABA,hata zile pesa nyingi walizo daiwa Tanesco ni kuhusu kukwepa MIKATABA.
Kiongozi MKATABA unalindwa na zipo sheria za kimataifa na ukienda kinyume na mikataba hiyo itatatuliwa ktk mahakama.sasa basi,kuhusu muungano wetu kuna makubaliano na hatuwezi tu kupiga kelele bila hata kwanza kuondoa makubaliano hayo ili baadae yasije kutufunga.huu muungano ni lazima una MKATABA sasa huo mkataba upo wapi?

Hapana , ukiongelea mkataba unakwenda pembeni raia, mkataba ni mfumu wa makubaliano kati ya pande mbili Na una quantities Na moja kati ya quantities ni Time frame(kipindi maalum), substance of the Contract, breaching of contract Na Hitimisho lake.. Sidhani Muungano ni Contract.

Unapoongelea Contract mwananchi ni Kwamba hapa ---- Element A inayojitegea Na pale kuna element B inayojitegemea, sasa Elemen A anakiwa Na interest Kwa Element B Kwa kidaraja flan(Contract) Kwa vitu flan(project), Kwa makubaliano flan (terms or Statement of requirements) Kwa Muda flan (contractual duration). Na iwapo member moja atapindisha makubaliano Kwa makusudi au bahati mbaya moja Kwa moja atakuwa amebomoa daraja (breach) Na Kwa mantiki hiyo zipo sheria sasa ndani ya Mkataba huo Kwamba mmojawapo akijifanya ndumila Basi atendewe hivi -Na vile.. Lakini Muungano sasa it is an assembling of element A and B , and we no longer call it by its separate Elements but we call it a new Unit C, now formal Element A and B, Consrtuct an Union Statements as a single body, after that Element A and B Dissolve completely to form an element body C.. We no longer naming it as element A & B , but a Unit C. Huo ndio Muungano..

Serikali yetu inatulazimisha everyday tuendelee kurumia neno Tanzania Bara Na Zanzibar.. Ni UHAINI HUU... WAFUNGWE VIONGOZI HAWA, wanavunja Muungano HADHARANI..
 
- Huyo Mchungaji hamuwakilishi anybody zaidi yake mwenyewe, ameonyesha kwamba uwezo wake wa kufikiri unaanzia wapi na kuishia wapi, siku hizi Makanisa yamekuwa sehemu ya Biashara na kutafuta kuwa-blackmail wanasiasa wasiojitambua ndio wanahangaika kila siku Makanisani, I mean ndio maana mimi siku hizi nayaogopa sana haya Makanisa Uchwara ambayo kwa Viongozi wake kutafuta mlo yameacha mafundisho ya dini na kililia siasa kila siku!

- Waumini wa hilo Kanisa ni bure tupu na Maskini Mchungaji wao!!, kama anataka agombee uongozi wa siasa otherwise ya Kaizari amuachie Kaizari!!

- CCM OYEEE!! KIDUMU CHAMA TAWALA!!

LE MUTUZ

Wewe na baba yako ulikwishasilimishwa na fedha za Iran kusaka Uriais mwaka 1995, na mzee akiitwa Jumanne badala ya John, hivyo hata usipokuwa na imani na Kanisa ni sawa tu maana mlikwisha hasi kwa ujira wa shekeli na uroho wa madaraka mkawa wafuasi wa Yuda Escariote.
 
Lakini iliniuma sana aliposema bado ana kadi ya Machizi.

Siku hizi kuwa Na Kadi Ndo fasheni.. Lazima Mtu umiliki mikadi yao, unawatumbulia humo Kwa Humo.. Kadi kitu gani. Mx Kadi tulizomazo si Za CCM, ni Za Tanu
 
juma lililopita nimeshuhudia kwa macho yangu watu wawili tofauti waliookota simu na katika hali ya kushangaza wakatumia muda na gharama nyingi kuwatafuta wenye nazo na kuwarejeshea bila hata ya kudai chochote, ilimradi waonekana ni binadamu wema tu na chini chini nikaanza kuhisi kuwa wale Watanzania wenye roho za ajabu taratibu tunaanza kubadilika!
Na hii kauli kwa njia moja au nyingine naweza kuilink na hayo matukio hayo mawili kuwa pamoja na matatizo, dhiki, woga (nk) tulivyonavyo lakini inafika sehemu "1+1=2" na si vinginevyo, ukweli uitwe ukweli!
Nampongeza Mch. Gwajima kwa kuongea anachokiamini badala ya kuongea asichoamini ili watu wa mataifa wafurahi tu!!
 
- Huyo Mchungaji hamuwakilishi anybody zaidi yake mwenyewe, ameonyesha kwamba uwezo wake wa kufikiri unaanzia wapi na kuishia wapi, siku hizi Makanisa yamekuwa sehemu ya Biashara na kutafuta kuwa-blackmail wanasiasa wasiojitambua ndio wanahangaika kila siku Makanisani, I mean ndio maana mimi siku hizi nayaogopa sana haya Makanisa Uchwara ambayo kwa Viongozi wake kutafuta mlo yameacha mafundisho ya dini na kililia siasa kila siku!

- Waumini wa hilo Kanisa ni bure tupu na Maskini Mchungaji wao!!, kama anataka agombee uongozi wa siasa otherwise ya Kaizari amuachie Kaizari!!

- CCM OYEEE!! KIDUMU CHAMA TAWALA!!

LE MUTUZ
1. Je wewe unattend services za Anglican (kama alivyo Mzee baba yako) kama inavyotakiwa?
2. Na je, hiyo 'logic' ya 1 million/43 million kuwa na nafasi sawa kwa sawa unaielezeaje?? (jifanye unanielezea mimi mtoto wa darasa la nne ili niielewe) badala ya kuponda bila kujua ni jinsi gani kapuku wa kawaida anabeba gharama za huu Muungano kwa kuhudumia mashangingi (V8) na mahoteli ya five stars ya makamu wa sita wa rais na makatibu wa manaibu wa mawaziri viongozi!

 
Sasa mchungaji analalamikia uchizi upi? Huyu mchungaji anapaswa kuhojiwa na polisi kwa kuwadhalilisha waasisi wa muungano kwa kuwaita machizi.
Mchungaji ana hoja ya msingi mno, tusimhukumu na wala hajawadharau waasisi wa muungano huu maslahi.
 
wewe unaongelea mifano ya baba na binadamu,mimi naongelea kitu kinaitwa MKATABA,na ndio maana hata matatizo ya mipaka na malawi watu wanaongelea MKATABA,ktk maswala ya madini watu wanaongelea MIKATABA,hata zile pesa nyingi walizo daiwa Tanesco ni kuhusu kukwepa MIKATABA.
Kiongozi MKATABA unalindwa na zipo sheria za kimataifa na ukienda kinyume na mikataba hiyo itatatuliwa ktk mahakama.sasa basi,kuhusu muungano wetu kuna makubaliano na hatuwezi tu kupiga kelele bila hata kwanza kuondoa makubaliano hayo ili baadae yasije kutufunga.huu muungano ni lazima una MKATABA sasa huo mkataba upo wapi?
Hivi ARTICAL OF THE UNION kwa kiswahili ni nini?
 
Mi niliyasema haya, huu ni ujinga (nimetumia neno zuri la kiswahili).

Huu muungano inabidi upitiwe upya la sivyo uko mbeleni hakutokuwa Salama.

Hiyo tume ya kushughulikia kero za muungano inatumia fedha nyingi za walalahoi ambazo zingetumika kutatua migogoro ambayo utatuzi wake ungelisaidia taifa, mfano mgogoro wa wakulima na wafugaji katika bonde la Usangu n.k.
Tatizo baadhi ya wanasiasa wakikosolewa na viongozi wa dini wanahamaki kweli kweli, ila wanasiasa wanapenda mno kuwakosoa viongozi wa dini.
 
Wanasiasa wetu wanaogopa kuwaaambia Wazanzibari haya maneno. Na wazanzibari sababu ya kuzoea kulelewa na watanganyika wamekuwa jeuri kweli kweli! Midomo yao ni mepesi kutamka kejeli,dhihaka nk.
Watanganyika taratiiibu wamenza kuchoshwa! Haya mambo yasiposemewa kwa style hii yatatusumbua. Semeni, yaishe!
 
Kuyafananisha maneno ya mch. Gwajima na kauli za kikundi cha UAMSHO ni uchizi! Mheshimiwa mmoja wa sehemu fulani alitamka kuwa waheshimiwa wa sehemu fulani wanafikiria kwa kutumia makalio, ni sawa na huyu anayemfananisha mch. na wanaojenga chuki za kidini. Huyu mch. amefunguka. Maulid Kitenge husema; hakuna kupepesa macho, kumung'unya maneno, kung'atang'ata ulimi wala kutikisa masikio. Each and everything should be in black and white! Watanzania wa leo si wa zama zile, kusukumwasukumwa tu, wa leo wanaelewa....
 
Mchungaji umesema kweli.
Kweli kabisa, sote tunafahamu kuwa tarehe 9/12/1961 TANGANYIKA ilipata UHURU lakini tunasherehekea nchi ambayo hapa duniani haipo kabisa (Tanzania bara), huu ndio UCHIZI pia.
 
Ni watu wachache sana wasiotaka uwepo wa kura ya maoni kuhusu muungano. Lakini mafuriko hayazuiwi kwa mikono.
 
Back
Top Bottom