Ally Kombo
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 11,429
- 2,653
ngoja kwanza nikupe stori ya kweli kwenye shughuli za watu.
mie naish uswaz nusu sasa huku shughuli ni almost kila wiki. kuna katabia kale ka watu kusoma dua kwenye menu ya sherehe like wengi wanaopenda mambo ya ushirikina wanatafuta mganga wa vitabu anasoma dua kwenye vyakula kabla havija pikwa na kuandika dua nyingine kwenye maji.
sasa bana hata kama ni watu mia mbili ukapika kg 20 zinaenea kabisa manake mtu akipewa upawa mmoja tu hawez kula tena yaani vinakinaisha usipime halafu unaviona vitam mno. kumbe vimesomewa ma dua ya kiganga nyie mnakinai mnapokula.
binafsi huwa kula kwenye shughuli ni kitu cha mwisho kwangu.
nyingi ni simulizi tu ambazo hazina uthibitisho. Tanga ni moja ya mikoa mbayo mungu ameibariki vitu vingi vzr... Panafaa kuishi kwani maisha ni rahisi, plan nzuri ya mji nk
Nini Mnyuzi wewe, maneno iko MSAMBIAZI bwana!
Kuna vizee vnapiga zongo mpaka vifaranga, Korogwe inatisha nyie acheni tu
Ukifika hapo maeneo ya MSAMBIAZI unaweza kushangaa kukuta kuku kafungwa hirizi, kwani vifaranga wanweza kupigwa zongo visikue kabisa vinadumaa mpaka vinakufa...Mkuu hii ya vifaranga kiboko ! Daaaah ! Sasa vifaranga vinakuwaje ?
Enzi hizo bwana kila kitu mzee ilikuwa ni Coastal Union tu kila siku lazima niende mazoezini kwao huko mzee wakali kama kina Mwameja,Carreca,Yasin Napili,Mgaza,Muhani,joseph razaro na kingslay marwilo walikuwa wanatisha ukja huku African Sports ndio unawakuta kina Juma Mgunda dah Tanga bwana ilikuwa inavutia sana enzi hizo.
Basi wewe huijui Tanga, Je unamkumbuka Sheikh Omari Vikapu?
Huyu alikuwa na shamba lake la minazi basi kuna vjana walikwenda kuiba nazi, shambani kwake. Akatangaza na kuwapa siku saba wezi wajisalimishe la sivyo atasoma hiyo Halal Badri, wezi wakakaidi. Basi Mzee Omari Vikapu akashusha dua ya Halal Badri, kilichotokea ilikuwa ni maafa, wale vijana wote walifariki isipokuwa mmoja alisalimika, punda waliobeba zile nazi waliangamia, minazi iliyotumika kufungwa wale punda ilikauka, vyuma vilivyotumika kufulia zile nazi vilivunjika vipande vipande. aliyesalimika ni kijana mmoja aliyekwenda kujisalimisha kwa huyo mzee na kuomba radhi, lakini aliambiwa ni too late dua ishasomwa. hata hivyo alimshika kichwani na kumuombea dua. alisalimika, lakini alioza pua na mdomo na baada kuhangaika sana akapona lakini alikuwa ameharibika sura kwani sehemu ya pua na mdomo ilikuwa imeondoka na hivyo kuacha kinywa wazi, alikuwa anafunga kigozi ili kuficha meno yasionekane. watu wakawa wanamwita Omari Kigozi na shughuli zake zilikuwa ni pale Soko la Ngamiani. Naamini waliowahi kuishi hapo miaka ya 80, watakuwa wanamkumbuka.
Wakati mwingine watu hao wenye macho mabaya hukiri kabisa kuwa wana macho mabaya ili watu waliomzunguka wafahamu hivyo, kuepusha lawama. Naomba Mzee Asprin ayaweke sawa maelezo yangu kama nitakuwa nimekosea.
Hii wanaita 'KOPERA' nikipata muda nitaweka kisa cha kweli kilichonikuta na hawa chuma ulete...Dah hatari.
Hii wanadai dawa yake kumwaga
chumvi kidogo motoni kabla hujaanza upishi. Sijui inasaidia or not, sie
huwa tunaona hatuna cha kupoteza so tunajitupia chumvi motoni
tunaendelea. Au sijui bado hatujakutana na hilo jicho!
Ukifika hapo maeneo ya MSAMBIAZI unaweza kushangaa kukuta kuku kafungwa hirizi, kwani vifaranga wanweza kupigwa zongo visikue kabisa vinadumaa mpaka vinakufa...
Kuku anayetaga anaweza kupigwa zongo hadi atamie mwaka mzima, wewe achana na mkoa wa Tanga, na hapo hujaenda mahali panaitwa MARAMBA au MAGOMA, kuna wachawi hapo mwana ukome, unaweza kupigwa kitu ukajikuta uko Congo DRC wakati ulikuwa Tanga, wenyewe wanaita SAKIRIZI.
Ngoja nikipata muda nitasimulia ushuhuda kuhusu uchawi wa Tanga na vitongoji vyake.
Juma Mgunda alikuwa anachezea Coastal Union BosS
Mmh! Zinduna umeenda Tokomwile au Mwakizaro kwa bibi nini?
Tanga hapo kuna eneo moja karibu na Kwa Minchi kulikua na kimsitu flani hivi kinaitwa "Mtupie"....maana yake kila anayepita mtupie uchawi. Hilo eneo lilikua halikauki mauzauza, ulipita eneo hilo lazima nywele zisimame kama kama mkia wa jogoo linalomchobea mtetee!
Je yale mahirizi yanayochomelewa na mabati kwa mafundi vibatari ili mtoto akikogeshwa hirizi isilowane.
Unajua kilichomo humo ndani ya hizo hirizi?
Nitakuja kusimulia hapa siku nyingine kwa ID nyengine maana hii kuna mkuda anaijua, akisoma atamwambia nyanya yake anizulie balaa
Hivi unajua kwamba wewe ni kihele hele sana?? au unataka nikupige madogori ujikute umeangukia Mwembe Basha umelala nini??usinichezee.