Zinduna
JF-Expert Member
- Nov 6, 2011
- 2,378
- 3,392
- Thread starter
- #161
Nilikuwa nasimamia Canteen pale halmashauri ya wilaya Korogwe,kazi ilikuwa inakwenda vizuri lakini ghafla ilitokea hali ya kigeni,chakula na na vinjwaji vilikuwa vinakwisha lakini nikija katika hesabu nakuta hatuna akiba na hata pesa ya kununua mahitaji haitoshelezi......kwa kuwa nilikuwa naweka akiba Benki,nilianza kuchukua pesa Benki kuziba mapengo,amini usiamini akiba niliimaliza ikawa sasa nimegonga ukuta, at the time nilikuwa bado mdogo ndio kwanza nimemaliza O level na pale nilikuwa nimewekwa na marehemu kaka yangu...kichwa kikawa kinaniuma nitaanza vp kumfahamisha kaka kwa kuwa pesa Benki nimemaliza na pale kazi inafanyika kama kawaida na sitoweza kulipa mishahara wala kwenda kuchukua stock ya kundeshea kazi.....Ikabidi nijisingizie ugonjwa.
Kiasi cha siku tatu nakumbuka marehemu kaka akaja nyumbani kuniuliza 'wewe pale unafanya vipi kazi?' nikamuuliza kwa nini? Akaniambia mbona mimi nikifunga kazi chakula hakibaki lakini nikitaka mahitaji mpaka niongeze pesa zangu nje ya kazi ile...ndio nikaona sasa hata nikimueleza ile hali atanielewa.
Nikamwambia A-Z mpaka sababu ya mimi kupumzika ni kwa kuwa nilikuwa naogopa nitaanza vipi kusema nafanya kazi lakini pesa hazionekani,nani ataniamini? Ndio wakahangaika jahazi likakaa sawa.
Sijaribu kuhalalisha au kulazimisha kuamini lakini huu ni UCHAWI NILIO WAHI KUUSHUHUDIA.
Hiyo ni chuma ulete na dawa yake ni ndogo tu, kama ukimjua mtu ambaye ni chuma ulete, na mara nyingi ni rahisi kumjua, kwani huja jioni kununua kitu cha bei rahisi halafu anakupa hela kubwa ili arudishiwe chenji, sasa ukishamshitukia ile hela yake usiichanganye na hela nyingine za biashara, na kwa kuwa lengo lake ni kutaka wewe uichanganye noti yake na fedha zako za biashara ili ziweze kuhamia kwenye mfuko wake, hataondoka akijaribu kukuangalia kwamba utafanya nini. wengine wanaweza kudiriki hata kukuliza kwamba kwanini unaitenge noti yake, wewe mpe kubwa na wala usimuogope mwambie kabisa wewe ni chuma ulete nimesha kushitukia, na hatakaa arudi tena na atakuogopa.
Lakini pia ipo njia nyingine, unaipokea ile hela kisha unaikunja mkononi kama vile umekunja ngumi halafu unapiga ngumi kwa upande wa nyuma wa mkono kwenye ardhi, hata uichanganye hiyo noti na fedha zako za biashara hapati kitu na akikuona anaweza kukulalamikia maana atajua umeshamjua.
Msishangae nilifundishwa mbinu hiyo na mjomba wangu.
Wakati mwingine nitawafundisha namna ya kumtega mchawi anase kwenye paa la nyumba au mlangoni.