Uchawi niliowahi kuushuhudia!

ngoja kwanza nikupe stori ya kweli kwenye shughuli za watu.

mie naish uswaz nusu sasa huku shughuli ni almost kila wiki. kuna katabia kale ka watu kusoma dua kwenye menu ya sherehe like wengi wanaopenda mambo ya ushirikina wanatafuta mganga wa vitabu anasoma dua kwenye vyakula kabla havija pikwa na kuandika dua nyingine kwenye maji.

sasa bana hata kama ni watu mia mbili ukapika kg 20 zinaenea kabisa manake mtu akipewa upawa mmoja tu hawez kula tena yaani vinakinaisha usipime halafu unaviona vitam mno. kumbe vimesomewa ma dua ya kiganga nyie mnakinai mnapokula.

binafsi huwa kula kwenye shughuli ni kitu cha mwisho kwangu.
Hiyo dua hata mie naikumbuka, hebu subiri nimuulize binamu yangu hapa maana yeye ni bingwa wa haya mambo.
 
Kuna mtu alikula vya watu Kigoma basi siku hiyo kenda kukojoa kando ya ziwa Tanganyika, aliyeliwa vyake akamkuta hapo akamwambia "utalijaza" hilo, basi naam, mkojo haukukatika mpaka kafa. Kisa cha barza ya gahwa.
 
Eti kuna uliyoona na uliyosikia, halafu unataka kuandika uliyosikia.

Mpaka hapo ushashindwa tayari.

Matokeo yake mtu ana epileptic bouts mnasema kalogwa!

Sijawahi kuona a convincing case for uchawi, some mumbo jumbo and abracadabra mind games maybe, actual witchcraft, no.
Kiranga tungekuwa na watawala kama wewe ingekuwa raa sana manake tungejifunza kuwa na akili za kufikiri na sio za kushkiwa. napenda sana jinsi ulivyo
 
Last edited by a moderator:
Kiranga tungekuwa na watawala kama wewe ingekuwa raa sana manake tungejifunza kuwa na akili za kufikiri na sio za kushkiwa. napenda sana jinsi ulivyo

Huyu jamaa Kiranga mie namuita mzee wa kufikiria nje ya box, maana yeye hulitazama jambo kwa jicho la tatu, ni watu wachache sana wenye kipawa hicho
 
Last edited by a moderator:
umenikumbusha msiba mmoja niliwah kwenda manzese. basi ilibingwa kura ya upish pish la pilau lilimwangukia mtu tofauti kumbe yule mma alotaka apike ule msosi hakupenda. basi kila pilaua likikolezwa viungo aaah wappy halitokelezei mmh! tukajiuliza jamani kunanii hapa??

mama mmoja ambaye alikuwa ni mwenyeji wa eneo lile akasema hebu jamani mwiten mama fulan aje atusaidie ni mpish mzuri basi yule mama kuja tu alishika ukuni akasogeza jikoni. pilau likatokelezea......... nilichoka mie na haya mambo lol!
mpaka leo nikienda msibani sipiki vyakula vya watu najikalia pembeni bingwa wa kuleta maji na kukata vitunguu ila ukoroga mwiko hunikamati lol!

Hii wanadai dawa yake kumwaga chumvi kidogo motoni kabla hujaanza upishi. Sijui inasaidia or not, sie huwa tunaona hatuna cha kupoteza so tunajitupia chumvi motoni tunaendelea. Au sijui bado hatujakutana na hilo jicho!
 
Kuna mtu alikula vya watu Kigoma basi siku hiyo kenda kukojoa kando ya ziwa Tanganyika, aliyeliwa vyake akamkuta hapo akamwambia "utalijaza" hilo, basi naam, mkojo haukukatika mpaka kafa. Kisa cha barza ya gahwa.

mie nilisha wahi kumwona mtu mafia alivunja amri ya sita na mke wa mtu. mwenye mke akamuuliza umefanya hivi akagoma akamwambia haya bana ila siku ukirudia basi hutapanda boti tena.

kijana alikuwa katokea mitaa ya kibaha basi akaona huyu mzee ni **** halafu ananitisha ngoja mie niendeleze na mkewe basi wakendeleza na mkewe. iyo sku alipigwa """CHUMA LIMOTO""" ngoma hailali. analia kwa maumivu lkn wapi nenda hosp wapi hkupanda tena boti kweli alikufa.
 
Kiranga mwanagenzi, usambe mkurugenzi.

Ha ha ha haaaa, kule Tanga mtu mwenye KIHEREHERE wanamwita ana Kiranga, sijajua connection ya ID yako na hiyo dhana ya Kiherehere LOL
 
Last edited by a moderator:
the man is smart up stairs aisee.
huwa nampenda sana manake ananifanyaga niwaze sana
Seam tu watu wa namna ya Kiranga wana kasoro moja.
Sio watekelezaji, ni watu wenye maono na wabunifu wazuri but it is very difficult for them to put into action
 
Last edited by a moderator:
mie nilisha wahi kumwona mtu mafia alivunja amri ya sita na mke wa mtu. mwenye mke akamuuliza umefanya hivi akagoma akamwambia haya bana ila siku ukirudia basi hutapanda boti tena.

kijana alikuwa katokea mitaa ya kibaha basi akaona huyu mzee ni **** halafu ananitisha ngoja mie niendeleze na mkewe basi wakendeleza na mkewe. iyo sku alipigwa """CHUMA LIMOTO""" ngoma hailali. analia kwa maumivu lkn wapi nenda hosp wapi hkupanda tena boti kweli alikufa.

Hiyo kule Tanga wanaita TEGO, mkaka mmoja alilala na mke wa mtu akafia kinenani baada ya kufika mshindo, basi dudu haikulala mpaka anazikwa, ilibiri ifungwe na kamba na kuzungushiwa kiunoni wakati anaoshwa
 
Hiyo kule Tanga wanaita TEGO, mkaka mmoja alilala na mke wa mtu akafia kinenani baada ya kufika mshindo, basi dudu haikulala mpaka anazikwa, ilibiri ifungwe na kamba na kuzungushiwa kiunoni wakati anaoshwa

hilo tego litamfaa sana @ asprin duh!
ila ni adhabua mbaya sana kwa mwizi wako lol!
 
vipi na wale wazee wanaocheza bao kuanzia asubuhi mpaka jioni lakini huwaoni wakienda kujisaidia, ila sasa mtazamaji anayeangalia bao utaona kila baada ya muda anaenda haja kubwa au ndogo lakini wale wazee hawanyanyuki wanaendelea kucheza tu kumbe wanakupasia mizigo yao! Mimi ishanipata miaka ya nyuma pande za mwananyamala nilikuwa nazuga kwenye bao wakati namlia mingo dem flani, wewee si mchezo kila wakati wazee wananisakizia kupeleka mizigo yao, bahati kulikuwa na bar jirani nikawa najisevia kwenye toilet yao nilipokuja kushtukia mchezo washantesa sanaa! nikawa sikai tena nikawaacha wasakiziane mizigo yao wenyewe kwa wenyewe!
 
Hiyo kule Tanga wanaita TEGO, mkaka mmoja alilala na mke wa mtu akafia kinenani baada ya kufika mshindo, basi dudu haikulala mpaka anazikwa, ilibiri ifungwe na kamba na kuzungushiwa kiunoni wakati anaoshwa

Wabondei na Wazigua wanaita USINGA,Zinduna,dudu huwa 'linavunjwa' hasa kwa waislamu ili wakati wa kuzikwa lisije nyanyua Sanda.Mwalimu gfsonwin, kule Majani mapana hukuwahi kuona hiyo?
 
Eti kuna uliyoona na uliyosikia, halafu unataka kuandika uliyosikia.

Mpaka hapo ushashindwa tayari.

Matokeo yake mtu ana epileptic bouts mnasema kalogwa!

Sijawahi kuona a convincing case for uchawi, some mumbo jumbo and abracadabra mind games maybe, actual witchcraft, no.

Mtu ana delusional paranoia watu wanadai kalogwa huyo!

Wakati delusional paranoia ni serious mental illness.

Kuendekeza uchawi mimi huwa nasema ni dalili za mental illness.

Yeyote anayeendekeza uchawi huenda anasumbuliwa na manic depression, schizophrenia (tena hii hufanya watu wasikie voices kwa sababu auditory hallucinations are common in schizophrenic people...labda ndo hapo wanadhani wamerogwa!), autism, selective mutism, obsessive compulsive, na mengineyo.

Ni wangapi Tanzania wanakuwa diagnosed na hayo magonjwa? Hata wataalam (psychologists, psychiatrists, etc.) waliobobea hakuna wa kutosha.

Tunaishia kusingizia uchawi.
 
mie nilisha wahi kumwona mtu mafia alivunja amri ya sita na mke wa mtu. mwenye mke akamuuliza umefanya hivi akagoma akamwambia haya bana ila siku ukirudia basi hutapanda boti tena.

kijana alikuwa katokea mitaa ya kibaha basi akaona huyu mzee ni **** halafu ananitisha ngoja mie niendeleze na mkewe basi wakendeleza na mkewe. iyo sku alipigwa """CHUMA LIMOTO""" ngoma hailali. analia kwa maumivu lkn wapi nenda hosp wapi hkupanda tena boti kweli alikufa.

Mwalimu gfsonwin sasa kwenye mpira enzi zile za African Sports na Coastal Union,ilikuwa balaa,kuna mechi moja mwaka 89,Yasini Napili alipiga shuti mpira umempita kipa halafu ukapasuka vipande viwili na vile vipande havikuvuka goal line kuamanisha kwamba sio goli,na mechi hiyo hiyo kulikuwa kuna babu alikuwa amepelekwa ufukweni mwa bahari wakati maji yamekupwa, wakawa kama wamemzika kwa kusimama isipokuwa kichwa na shingo ,baada ya mpira kwisha matokeo yalikuwa nunge, basi watu wakasahau kwenda kumfukua kule ufukweni mpaka maji yakawa yanajaa bahati nzuri wavuvi wakasikaa kelele alizokuwa anapiga ndio wakaenda eneo la tukio ndio wakamfukua.Nilikuwa kambini usiku kabla ya mechi hii basi vitu vingine siwezi simulia kwani huwezi amini mambo yaliyokuwa yanafanyika.Mungu alinisaidia niliacha mpira msimu uliofuata kwani nilikuwa nimechaguliwa kwenda form five toka Usagara Secondary,oops isije id ika.........Sarikoki sikjui kama ulikuwa kishazaliwa..... ha ha ha
 
Mwalimu gfsonwin sasa kwenye mpira enzi zile za African Sports na Coastal Union,ilikuwa balaa,kuna mechi moja mwaka 89,Yasini Napili alipiga shuti mpira umempita kipa halafu ukapasuka vipande viwili na vile vipande havikuvuka goal line kuamanisha kwamba sio goli,na mechi hiyo hiyo kulikuwa kuna babu alikuwa amepelekwa ufukweni mwa bahari wakati maji yamekupwa, wakawa kama wamemzika kwa kusimama isipokuwa kichwa na shingo ,baada ya mpira kwisha matokeo yalikuwa nunge, basi watu wakasahau kwenda kumfukua kule ufukweni mpaka maji yakawa yanajaa bahati nzuri wavuvi wakasikaa kelele alizokuwa anapiga ndio wakaenda eneo la tukio ndio wakamfukua.Nilikuwa kambini usiku kabla ya mechi hii basi vitu vingine siwezi simulia kwani huwezi amini mambo yaliyokuwa yanafanyika.Mungu alinisaidia niliacha mpira msimu uliofuata kwani nilikuwa nimechaguliwa kwenda form five toka Usagara Secondary,oops isije id ika.........Sarikoki sikjui kama ulikuwa kishazaliwa..... ha ha ha

jamani kwanza naomba nitumie salam za x-mass nilipoteza simu mwenzo.

haya ya mpira sitak hata kuyasema manake namkumbuka mzirai(rip) aliwah kuruka ukuta na wachezaji wake badala ya kuingilia mlangoni pale uhuru.
 
Back
Top Bottom