Hivi hakuna mchawi humu anirushie hilo zongo nione linakuwaje? Hizi hbr za uchawi kila siku naishia kuziskia tu.
Uchawi na dini kimsingi havina tofauti maana vyote msingi wake mkuu ni imani. Labda tofauti iliyopo ni kwenye application tu ingawa hii nayo yaweza kuwa debatable.
Uchawi mtu unaweza kusema lengo lake ni ubaya wakati dini/imani kwa mungu lengo lake ni wema/ uzuri.
Ngoja wakusikie wenyewe...
vipi na wale wazee wanaocheza bao kuanzia asubuhi mpaka jioni lakini huwaoni wakienda kujisaidia, ila sasa mtazamaji anayeangalia bao utaona kila baada ya muda anaenda haja kubwa au ndogo lakini wale wazee hawanyanyuki wanaendelea kucheza tu kumbe wanakupasia mizigo yao! Mimi ishanipata miaka ya nyuma pande za mwananyamala nilikuwa nazuga kwenye bao wakati namlia mingo dem flani, wewee si mchezo kila wakati wazee wananisakizia kupeleka mizigo yao, bahati kulikuwa na bar jirani nikawa najisevia kwenye toilet yao nilipokuja kushtukia mchezo washantesa sanaa! nikawa sikai tena nikawaacha wasakiziane mizigo yao wenyewe kwa wenyewe!
Nyani Ngabu kimsingi mambo ya uchawi hayawezi kuthibitishwa,lakini hii haimaanishi kuwa uchawi haupo.
Wazungu ni wachawi kuliko sisi,tena uchawi wao ni kiboko zaidi.
Obama na Hillary ni wachawi sana.
Uchawi wao ni black Magic ambao una asili ya Kabalah.Usidhani huko haupo.
Hata kuipata nafasi ya kuwa mgombea uraisi wa Marekani achilia mbali kuwa raisi,ni lazima uwe mchawi na unashiriki uchawi.
Tatizo tumeaminishwa Ulaya na Marekani hakuna uchawi na uchawi upo Africa tu,kuamini hivi ni jambo la ajabu sana.Hakuna jamii isiyokua na uchawi.Na uchawi ukifanyika kokote ni uchawi tu!
We nawe, sasa na ile Halal Badri ina wema au ubaya?
Hahahahahahahahahaha
Zinduna hapo kwenye kula alaf ana shiba mwingine umeniacha hoi sana!
kwa nia njema tu, nijishuhudilie hayo mautaalam
By the time unahisi utashuhudia, unajikuta hata hizo guts za kushuhudia huna tena maana wataalam washafanya ya kufanya!
ila sasa ntajuaje kama ndio washanifanyia mambo?
Hivi hakuna mchawi humu anirushie hilo zongo nione linakuwaje? Hizi hbr za uchawi kila siku naishia kuziskia tu.
Mwalimu gfsonwin sasa kwenye mpira enzi zile za African Sports na Coastal Union,ilikuwa balaa,kuna mechi moja mwaka 89,Yasini Napili alipiga shuti mpira umempita kipa halafu ukapasuka vipande viwili na vile vipande havikuvuka goal line kuamanisha kwamba sio goli,na mechi hiyo hiyo kulikuwa kuna babu alikuwa amepelekwa ufukweni mwa bahari wakati maji yamekupwa, wakawa kama wamemzika kwa kusimama isipokuwa kichwa na shingo ,baada ya mpira kwisha matokeo yalikuwa nunge, basi watu wakasahau kwenda kumfukua kule ufukweni mpaka maji yakawa yanajaa bahati nzuri wavuvi wakasikaa kelele alizokuwa anapiga ndio wakaenda eneo la tukio ndio wakamfukua.Nilikuwa kambini usiku kabla ya mechi hii basi vitu vingine siwezi simulia kwani huwezi amini mambo yaliyokuwa yanafanyika.Mungu alinisaidia niliacha mpira msimu uliofuata kwani nilikuwa nimechaguliwa kwenda form five toka Usagara Secondary,oops isije id ika.........Sarikoki sikjui kama ulikuwa kishazaliwa..... ha ha ha