GLOBALIST
Member
- Aug 20, 2021
- 9
- 10
Nimeona maandiko kadhaa yenye kumsifu aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo baada ya mahojiano yake ya video na Daily News Digital kuhusu namna alivyo-play role yake katika dakika za majeruhi za uhai wa Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli.
Nilichokipenda katika stori ile ni jinsi alivyoshiriki kiuadilifu kwa nafasi yake ya CDF kwa wakati huo hasa katika suala la utii.
Hatahivyo, sijafurahishwa na “cheap politics” za yeye (Jen. Mabeyo) kuja kujianika katika media na kujuza mambo ambayo kimsingi hayakupaswa kuwa sehemu ya siasa.
Ninasema sehemu ya siasa kwa sababu, masuala mengi ya kimaudhui yamefuatia kwa jina la mabeyo, kila mmoja mwenye kujiita “mchambuzi” amemsifia CDF huyo kuwa aliinusuru nchi dhidi ya machafuko ambayo wanaamini yangetokea.
Ni cheap and immature politics kwa nafasi yake kama Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kufanya alichofanya katika media.
Katika hatua zote hizo za final tensions kuelekea kifo cha Mheshimiwa Rais, CDF hakuwa pekee, bali Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Nyakoro Sirro, na Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DGIS) Diwani Athuman Msuya pia walikuwepo. Wao hawajawahi kujitokeza na kusema chochote katika media.
Katika interview yake, CDF Mabeyo ametumia zaidi nafsi ya kwanza umoja (mimi / nili-, nika-, nk) ilihali chochote kilichofanyika kilikuwa ni matokeo ya maamuzi yaliayofikiwa na pande zote: CDF, IGP na DGIS. Je, ni nini ex-CDF huyu anatuonesha au anakitafuta?
Kama ilikuwa ni kupata mileage kwa “burning content” haikuwa lazima kusema chochote kwa media katika kila kumbukizi ya Hayati JPM. Mfano mzuri ni Ofisi ya Rais - IKULU, ambao hawajasema chochote kuashiria kumbukizi ya Hayati JPM kwa mwaka huu wa 2024.
Kiufupi, mstaafu huyu ameendelea kulazimisha uwepo wake kwa njia hii aliyoiona kuwa inafaa. Bragging about what he did literally translates to kwamba wenzake hawakufanya chochote, au wangefanya maamuzi mabaya na hatari kwa taifa bila uwepo wake. This is unhealthy.
Ikumbukwe CDF Mabeyo huyuhuyu aliwahi kutamka kionjo cha statement ambayo hakuisema hadharani alipokuwa akitoa salamu wakati wa mazishi ya kitaifa ya Hayati JPM kule Chato, kwamba ana ujumbe aliopewa na Hayati Rais ambao asingependa kuusema pale, bali angemwambia moja kwa moja Mheshimiwa Makamu wa Rais (ambaye ni Rais wa sasa).
Je, kulikuwa na haja gani ya kuyatamka yale hadharani yamkini akijua ni yenye kumhusu VP pekee? Ni kipi alikuwa anakitafuta? Binafsi yangu nahisi ni “distinctiveness”
UTII AU SIO UTII?
At one story moment, Rais JPM alimuamuru CDF Mabeyo amuondoe hospitalini alipokuwa akipata matibabu na kumpeleka nyumbani kwake. Hii ina tafsiri kwamba Mzee alihisi hawezi kupona kwa hatua aliyofikia (unganisha na tukio la kuitwa Askofu na Kardinali kwa ajili ya upako wa mafuta)
Kwanini Rais amuamuru Mabeyo, sio the rest?
Hapa kwa mtazamo wangu, naziona nadharia mbili:
Ustawi na Amani ya nchi hii ni matokeo ya ushirikiano wa vyombo, majeshi yote, taasisi na raia wenyewe.
Nilichokipenda katika stori ile ni jinsi alivyoshiriki kiuadilifu kwa nafasi yake ya CDF kwa wakati huo hasa katika suala la utii.
Hatahivyo, sijafurahishwa na “cheap politics” za yeye (Jen. Mabeyo) kuja kujianika katika media na kujuza mambo ambayo kimsingi hayakupaswa kuwa sehemu ya siasa.
Ninasema sehemu ya siasa kwa sababu, masuala mengi ya kimaudhui yamefuatia kwa jina la mabeyo, kila mmoja mwenye kujiita “mchambuzi” amemsifia CDF huyo kuwa aliinusuru nchi dhidi ya machafuko ambayo wanaamini yangetokea.
Ni cheap and immature politics kwa nafasi yake kama Kamanda Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kufanya alichofanya katika media.
Katika hatua zote hizo za final tensions kuelekea kifo cha Mheshimiwa Rais, CDF hakuwa pekee, bali Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Nyakoro Sirro, na Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DGIS) Diwani Athuman Msuya pia walikuwepo. Wao hawajawahi kujitokeza na kusema chochote katika media.
Katika interview yake, CDF Mabeyo ametumia zaidi nafsi ya kwanza umoja (mimi / nili-, nika-, nk) ilihali chochote kilichofanyika kilikuwa ni matokeo ya maamuzi yaliayofikiwa na pande zote: CDF, IGP na DGIS. Je, ni nini ex-CDF huyu anatuonesha au anakitafuta?
Kama ilikuwa ni kupata mileage kwa “burning content” haikuwa lazima kusema chochote kwa media katika kila kumbukizi ya Hayati JPM. Mfano mzuri ni Ofisi ya Rais - IKULU, ambao hawajasema chochote kuashiria kumbukizi ya Hayati JPM kwa mwaka huu wa 2024.
Kiufupi, mstaafu huyu ameendelea kulazimisha uwepo wake kwa njia hii aliyoiona kuwa inafaa. Bragging about what he did literally translates to kwamba wenzake hawakufanya chochote, au wangefanya maamuzi mabaya na hatari kwa taifa bila uwepo wake. This is unhealthy.
Ikumbukwe CDF Mabeyo huyuhuyu aliwahi kutamka kionjo cha statement ambayo hakuisema hadharani alipokuwa akitoa salamu wakati wa mazishi ya kitaifa ya Hayati JPM kule Chato, kwamba ana ujumbe aliopewa na Hayati Rais ambao asingependa kuusema pale, bali angemwambia moja kwa moja Mheshimiwa Makamu wa Rais (ambaye ni Rais wa sasa).
Je, kulikuwa na haja gani ya kuyatamka yale hadharani yamkini akijua ni yenye kumhusu VP pekee? Ni kipi alikuwa anakitafuta? Binafsi yangu nahisi ni “distinctiveness”
UTII AU SIO UTII?
At one story moment, Rais JPM alimuamuru CDF Mabeyo amuondoe hospitalini alipokuwa akipata matibabu na kumpeleka nyumbani kwake. Hii ina tafsiri kwamba Mzee alihisi hawezi kupona kwa hatua aliyofikia (unganisha na tukio la kuitwa Askofu na Kardinali kwa ajili ya upako wa mafuta)
Kwanini Rais amuamuru Mabeyo, sio the rest?
Hapa kwa mtazamo wangu, naziona nadharia mbili:
- Amri ilitolewa kwa wote, isipokuwa kwa sababu CDF ndiye Kiongozi wa ile squad ndiye literally alikuwa kama msemaji wao.
- Hayati JPM alikuwa na mapenzi na imani ya wazi kwa Jeshi katika kipindi cha uongozi wake, hivyo alihisi kwa kumtumia CDF, ujumbe huu ungetekelezwa kwa haraka.
Ustawi na Amani ya nchi hii ni matokeo ya ushirikiano wa vyombo, majeshi yote, taasisi na raia wenyewe.