Boramaisha
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 820
- 18
..uzoefu wa Salim Salim ni ktk masuala ya diplomasia tu. katika nafasi zake zote za uongozi alizopata kushika hakuna hata moja inayohusiana/inayogusa moja kwa moja maisha ya mwananchi wa kawaida.
..uzoefu wake kama waziri mkuu na baadaye waziri wa ulinzi ni wa muda mfupi sana, na alitumikia hapo muda mrefu uliopita, kuweza kunishawishi kwamba anayafahamu na anaweza kuyakabili matatizo yanayoisibu nchi yetu leo hii.
..tunahitaji Raisi atakayesimamia mapinduzi ya KILIMO, VIWANDA,MIUNDO MBINU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA. tunahitaji Raisi ambaye yuko capable and comfortable dealing with the details and nuances za masuala niliyoyataja hapo juu.
..pia tunahitaji Raisi Mzalendo mwenye imani ktk uwezo na vipaji vya Watanzania. Raisi ambaye atahamasisha na kuimarisha wawekezaji wazalendo wa ndani.
JokaKuu,
Salim anaijua nchi hii vizuri kuweza kuitawala/kuiongoza kwa mafanikio. Shida za wananchi Salim anazijua na amewahi kuzishughulikia akiwa Waziri Mkuu. Kwa mfano aliwahi kwenda mikoa ya kusini akakuta wananchi wanavaa nguo za vi-sulphate ile mifuko ya mbolea ya chumvi-chumvi. Salim akaagiza nguo zinazotengenezwa viwandani Urafiki n.k. - kaniki, kanga, vitenge etc zipelekwe mikoa hiyo. Salim ni chimbuko la ruksa ya kuingizwa mitumba kutoka nje inayosaidia walalahoi hadi leo.
Kama uliweza kufuatilia harakati za mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005 Salim alikuwa wa pili. Kwa nini aliweza kupata nafasi hiyo kama maisha yake hayakuhusiana moja kwa moja na wananchi? Aliwezaje kukubalika mikoani na akapata watu wengi waliomuunga mkono kwenye mikoa ya mbali kama Songea? Jeshini pia anakubalika vyema kwa sababu kwa kipindi kifupi unachozungumzia aliweza kuleta mabadiliko na kushughulikia maslahi ya wanajeshi. Wale waliokuwepo wakati huo wanamkumbuka mpaka leo.
Matatizo ya leo ambayo yamechanganyika na effects za Utandawazi mtu kama Salim ndiye haswa mahali pake kwa sababu kutokana na kufanya kazi ya ubalozi nje hususan Marekani hadi jina lake kupendekezwa kwa nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, anaijua dunia anajua intrigues za nchi tajiri na anaweza kujua namna ya kushughulika nao kuliko akina Dr. Slaa ama Magufuli.
Salim ni mzalendo, anayo imani kwa Watanzania wenziwe wenye vipaji. Wakati akiwa Waziri Mkuu hakuwahi kulete 'mitumba' ya wataalamu kutoka nje kuchukua nafasi za Watanzania! Salim anajua fika Tanzania inahitaji nini ili iweze kujikwamua kutoka hapa tulipo. Kutokana na uelewa wake na usomi wake Salim anaweza sana kusimamia mapinduzi hayo uliyoyataja ya KILIMO, VIWANDA, MIUNDOMBINU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA. Kama alipokuwa nje aliwanyima Watanzania nafasi kwenye sehemu alizokuwa akiziongoza k.m. OAU ni kwa sababu hana hulka ya upendeleo na ubinafsi.
Ninavyoelewa mimi mtu anapoomba kazi CV yake ndiyo kigezo cha kwanza kinachoangaliwa ili kuweza kupata mtu anayefaa kwa kazi hiyo. CV ya Salim imesheheni vigezo vya kumfanya afae kuwa rais wa Tanzania.
FMEs anatuambia Dr. Slaa anafaa kwa sababu anaweka 'Maslahi ya Taifa Kwanza'. Je tuna sababu gani za msingi za kudhani kwamba Salim ambaye amewahi kushika nyadhifa za juu - ubalozi, uwaziri na kuwa Waziri Mkuu wa nchi yetu na hana dhambi yoyote ya ufisadi hawezi kuwa Rais anayetufaa? Katika kinyang'anyiro cha kutafuta mgombea wa CCM jina la Salim lilipitishwa na Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu na aliweza kushika nafasi ya pili, tunasema hafai? Kwa maana nyingine waliompa kura zao hawana akili timamu?!
Mtu kudhihirisha kwamba anaweka maslahi ya taifa kwanza si lazima awe dramatic asimame Mwembe Yanga kutangaza majina ya mafisadi ama kuongea Bungeni kwa sauti ya juu kuhusu ufisadi na kuwa na mbinu za kuiba nyaraka nyeti etc! Kwa kuwa Salim hana wadhifa wowote wa ngazi ya juu kichama ama serkalini amekuwa mara kwa mara akitoa mawazo yake na msimamo wake kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mustakabali wa nchi yetu kupitia vyombo vya habari. Kosa lake kubwa ni kwamba hataji, hatukani na hadhalilishi watu hadharani na kwa sababu hiyo anaonekana si mzalendo, hafai!