- Mkuu heshima mbele, kwanza ungeweza kuweka hoja zako bila ya kunitafuta na wala hukuhitaji kutumia maneno ya Mkulu MMJ, mimi sihitaji malumbano na wewe kama unavyoyatafuta hapa, mimi nilisha-conclude siku nyingi sana kwamba Salim hana uwezo wa kuwa Rais wa Tanzania kwa sababu moja muhimu alizoea kubebwa na Mwalimu, hana ubavu wa kusimama mwenyewe, vita vya mafisadi vinahitaji kiongozi kama Magufuli au Dr. Slaa wanaoweza kusimama wenyewe,
- Mambo ya kubebwa sasa hayana nafasi tena katika uongozi tunaoutafuta kuliokoa taifa letu, majuzi Warioba na Butiku wamejaribu sana kumbeba wakidhani ile nguvu ya Mwalimu bado ipo, lakini tizama yaliyomkuta ni aibu sana. Kiongozi wa kweli na unayemsema angesimama kidete na kupambana na mtandao mpaka kieleweke, lakini akaishia kujifungia ndani na kulia, majuzi Mama Kahama naye walimpomtwanga UWT naye alijifungia ndani na kulia, unaona sasa mkuu unasema huyu ndiye atapigana na mafisadi? Maneno kidogo tu anajifungia ndani na kulia?
- Salim amekuwa Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi, pamoja na nje, lakini sikumbuki anything serious alichokifanya kwa taifa zaidi ya kuwapa wananchi kusini mitumba, sitaki kusema sana kwa sababu bado ninamheshimu sana Salim as a person, lakini kuwa Rais wa vita ya mafisadi hapana!
es!