Uamuzi wa kuwaondoa Machinga mitaa ya Dar es Salaam urejewe upya

Tafakari haya:-

1. Je, Wamachinga ni matokeo au zao la mfumo wa elimu tulio nao?

2. Je, Wamachinga ni zao la Economic Model inayoongoza nchi na sayari?

3. Je, Mamlaka za Kodi zime-engage vipi Wamachinga kwenye mfumo wa kodi maana wako wengi sana?

4. Je, kwanini hakuna Sheria ya Bunge (Act of Parliament) inayoratibu shughuli za Wamachinga kwa tija ya taifa? Ikumbukwe idadi yao ambayo hatujaijuwa ni kubwa kiasi kwamba taifa halipaswi kukosa sheria ya kuwaratibu zaidi ya ile sheria ya uzururaji inayobana madadapoa na mission-town (wapiga misele).

5. Je, Sheria ya Nguvu Kazi ya 1984 inasema nini kuhusu Wamachinga? Au wakati sheria hiyo inatungwa Wamachinga hawakuwepo lakini kwamba sasa wapo ni kwanini sheria hiyo isifanyiwe marekebisho ili iwaongelee na wao pia?

6. Je, kwakuwa Umachinga ni zao la mfumo-liberali wa dunia hasa kwenye uchumi ambapo Ujamaa uliokuwa unasisitiza dola kuzalisha na kuwalisha je, ujio wa mfumo mpya uliowazalisha (siyo Ujamaa) unaowataka wale kwa jasho lao umewaandaliaje mazingira wezeshi na jumuishi ili waendelee kula kwa jasho lao wasijekuitegemea dola?

7. Nachelea kuamini kwamba kama sensa ya Wamachinga nchini ikifanyika idadi yao itazidi idadi ya watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja.

8. Je, mbona uamuzi wa kuwaondoa huwa unafanyika tu baada ya uchaguzi na serikali kusimikwa? Karibu na uchaguzi hawaondolewi? Serikali inakuwa wapi? Bajeti ya kuwaondoa kipindi hicho inakuwa wapi?

9. Mbona ilani za uchaguzi hazisemi moja kwa moja kwamba tukishika madaraka ya nchi tutawaondoa Wamachinga; ili utekelezaji wa kuwaondoa unapofanyika basi ionekane wazi kwamba Ilani inatekelezwa?


10. Je, kama Wamachinga wanachafua miji vipi magereji na vituo holela vya mafuta kwenye makazi vinapamba miji?

11. Pana tofauti gani kati ya Wamachinga waliovamia mitaa nchi nzima na watu waliowekeza na kuishi kwenye hifadhi za barabara za Tanroads na Tarura nchi nzima kwa miaka nenda miaka rudi?

12. Wamachinga walianza mwaka 1985. Wakati wa uchaguzi 1990 Wamachinga hawakuondolewa, 1995 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2000 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2005 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2010 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2015 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2020 hawakuondolewa muda wote wa uchaguzi na ule usio wa uchaguzi. Maswali:-

1. Tatizo ni warasimu au Wamachinga?

2. Tatizo ni Demokrasia mbovu?

3. Tatizo ni ombwe la sheria, sera, kanuni, miongozo, ubovu wa sera ya taifa ya vijana, mfumo wa elimu au nini?

4. Sheria (kama ipo) inayowaondoa muda usio wa uchaguzi kwanini isiwaondoe muda wa uchaguzi pia?

5. 2025 wakati wa mchakato wa uchaguzi hasa kampeni Wamachinga watarejea tena mitaani (na hawataguswa) kwa sababu hatuna utaratibu mzuri endelevu kuhusu Umachinga. Mama atatafuna mfupa huu bila shaka.

NB.
Fikiria, taifa liwe na kundi dogo la watu wa idadi ya nchi za Eswatini na Lesotho ambao hawalipi kodi kutokana na kwamba hakuna mazingira/mfumo wezeshi ulioandaliwa kwa ajili yao kulipa kodi na tozo za serikali? Tunayo ya kujifunza Kigali.



Athari za kuondoka Wamachinga bila maandalizi ya kutosha Kisera, Sheria, Kanuni na Miongozo husika.

Mgandamizo wa Kijamii (Social Pressure)

1. Ujambazi, Udokozi na Vibaka (Banditry, Pilfering and Thugs)

Akili iliyolala kwa kukosa cha kufanya huvutiwa na uhalifu. Uhalifu uchukuwa sura mbalimbali zikiwemo umalaya ambao utaongeza mzigo wa magonjwa kwa watu na serikali kununua madawa na vifaatiba, aidha, kuna uhalifu wa kuhujumu taasisi kupitia deals za kupiga fedha za taasisi ili watu waweze kuishi.


2. Magereza Kujaa (Prisons Runoff)

Namba moja hapo juu inazua athari za moja kwa moja kwa idara za Magereza na Mahakama na kulazimisha mahitaji ya ajira mpya za Mahakimu na Majaji wa kutosha na pia kutanua bajeti ya Magereza ambayo serikali haijajiandaa nayo.


3. Kutanuka kwa Soko la Mihadarati (Burgeoning of Drugs Market Niche)

Wengi walio mateja ni wale waliokosa cha kufanya kuingizia kipato. Wafalme wa mihadarati mbinu wanayotumia kwenye marketing yao ni kugawa fedha na mihadarati bure kwa wateja wapya kwa muda maalum ambao unatosha kuwatengenezea uraibu hawa newcomers, baada ya muda huo pesa za bure na ngada za bure zinasitishwa ili sasa ununuwe, uraibu uliotengenezewa utakusukuma kutafuta ela hata kwa kukata kiungo cha Albino au hata kumvamia Askari mwenye bunduki na kumpiga sachi ili upate ama ela au mali ya thamani ukauze ukanunue ngada ya kipimo tu cha ukucha ili arosto isikuondoe kwenye uso wa dunia.


4. Migogoro ya Familia (Household Disorders)

Wamachinga wengi wanasomesha, wamejenga, ni bima ya afya kwa ndugu zao, ni breadwinners wa familia zao na jamaa zao. Kama breadwinner akikosa cha kufanya kuleta mkate nyumbani familia itaingia kwenye mgogoro. Taifa lenye migogoro ya kifamilia halina ustawi mzuri. Umoja wa Mataifa umeweka siku maalum kimataifa ya kutafakari juu ya migogoro ya kifamilia na kuna itifaki zake.


Changamoto za Kiuchumi (Economic Challenges)

1. Mikopo (Credit Facility)

Wamachinga wengi wamekopa kwenye masoko ya mitaji ama yasiyo rasmi au yaliyo rasmi. Kuondoka kwa dharura bila fidia ya kutengenezea vizimba vipya kwenye site mpya kutayumbisha mitaji yao na biashara zao na kufanya urejeshaji wa mikopo yao kuyumba pia, masoko haya ya mitaji yatakosa uwezo mkubwa wa kuendelea kuwahudumia wakopaji wapya. Hili wakati wa Corona 2020 liliyumbisha masoko ya hisa duniani. Kenya, serikali ili-guarantee masoko haya ili yarefushe muda wa mikopo kwa mwaka mbele kuwapunguzia waliokopa athari za Corona zilizotokana na lockdown kwamba dhamana zao za mikopo zisiuzwe. Hongera SSH kwa kutenga 5bl za zoezi la ku-relocate Wamachinga hofu iko kwenye usalama wa matumizi ya fungu hili lakini pia fungu linatosha idadi kubwa ya Wamachinga nchini?


2. Nadharia ya Uhitaji na Ugavi (Theory of Demand and Supply)

Kuondoka kwa Wamachinga kutaathiri mnyororo wa ugavi (Supply Chain) ambapo wagavi watakuwa wachache na wahitaji kuwa wengi hivyo bei ya bidhaa na huduma kupanda (Price Elasticity of Demand and Supply) na kufanya uwezo wa manunuzi (Purchasing Power) ya wahitaji hasa wanyonge kuathirika, na huenda tukaona mfumuko wa bei kwenye uchumi wa nchi, ikumbukwe kuwa hatuna takwimu za sensa ya Wamachinga na huenda makisio ni kuwa idadi yao nchini huenda inazidi watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja. Wamachinga walikuwa wana-regulate mfumuko wa bei (Inflation) na kuruhusu nguvu za soko za uhitaji na ugavi (Demand and Supply) kinyume na sasa ambapo tutaona Business Syndicates na Cartels zikiibuka na kujifanya Mawakala wa Kudhibiti Bei (Price Control Agents). Serikali itakapowataka wenye maduka sasa kulipa kodi na tozo halali za serikali (ambazo kimsingi sipingani nazo maana zina manufaa kwangu pia) misuguano itaanza kati ya wafanyabiashara hawa na Mamlaka za Kodi na Ushuru na wimbo utabadilika kwamba serikali inanyanyasa wafanyabiashara, Afrika ndivyo tulivyo, tunapenda kuona serikali ikikosa mapato yake halali sisi pekee wafanyabiashara tupate. Aidha, Wamachinga wanategemewa na Wafanyabiashara wakubwa kabisa maarufu nchini wanaouza vinywaji laini, barafu za kulamba, vitafunwa nk. Hawa nao wanakuwa wahanga wakubwa wa kuondoka Wamachinga katikati ya miji/mitani. Wamachinga kumbe ni injini inayotegemewa na wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa kabisa licha ya mlaji tu. Mafunuo mapya hayo.


3. Kuathiri Tasnia ya Mama na Baba Lishe (Affecting Food Vending Industry)

Mama na Baba Lishe soko lao kubwa mijini ni mamilioni ya Wamachinga wanaouza bidhaa zao maeneo hayo. Mama na Baba Lishe wanategemea Wamachinga kuliko wanavyowategemea Wachina, Wahindi, Waarabu, Wakinga na Wachaga wachache waliosalia (kwa Kariakoo). Biashara za Mama & Baba Lishe na Wamachinga zinategemezana (Solution to one problem contains the seeds for the next problem. Ukiondoa Wamachinga kwa pupa umeleta tatizo la Mama na Baba Lishe ambao wengi hivi sasa wako kisheria kupitia mradi wa Majiji Salama Afrika uliofadhiliwa na UN na serikali kuhalalisha biashara zao kupitia Healthy Cities Project). Case Study: Hoteli ya Kitalii zamani Holiday Inn mkabala na Benki ya Standard Chartered jijini Dsm mwekezaji mpya alipochukuwa hoteli ile akaondoa kibanda cha Mama na Baba Lishe kilichokuwepo jirani kabisa na hoteli, kilichotokea ni kwamba wageni wake wakiwemo wa kizungu walikuwa wanalipia tu malazi hotelini lakini chakula wanawafuata Mama na Baba Lishe wale waliosukumiziwa mita kama 25 hivi, walichokuwa wakifuata wageni wale pale kwa Mama na Baba Lishe ni bei nafuu, African cuisine na wadada wazuri wa Kitz, matokeo yake wageni wale wakawa wanawaambia keep change hata $, hoteli ile ikapoteza asilimia kubwa ya mapato ya chakula hadi pale mamlaka zilipowafuata wale Mama na Baba Lishe na kuwafungia kabisa biashara ile lakini ikaathiri mamia ya wafanyakazi maofisini waliokuwa wakitegemea vibanda vile kwa sababu hawawezi kula hoteli ile ya kitalii.


4. Halmashauri za Dar Hazina Ardhi (Metropolitan Dar Land Scarcity)

Ardhi zote zimeishamilikiwa na watu, serikali ikihitaji ardhi inabidi ifidie watu iwahamishe au iende kwenye wilaya za jirani na mkoa wa Dar (Temeke inapumulia Mkuranga, Ilala inapumulia Kisarawe, Ubungo inapumulia Kibaha, Kinondoni inapumulia Bagamoyo). Population ya Wamachinga Dar pekee ni kubwa kuliko inavyofikiriwa na wanahitaji maeneo mengi ya kutosha. Mwaka 1995 idadi yao ilikuwa sawa na wakazi wa jiji la Mwanza, leo miaka 26 imepita je, idadi yao imeongezeka kiasi gani? Dar inayo ardhi hiyo?


Uzorotefu wa Kisiasa (Political Meltdown)

1. Machafuko (Mayhem)

Tunisia iliingia machafuko yaliyosambaa katika ukanda mzima wa Waarabu wa Kaskazini mwa Jangwa la Sahara na Sahel na baadaye Mashariki ya Kati kwa cheche ndogo tu ya Mmachinga aliyeuawa kwa kipigo cha Mgambo akimtuhumu kujipumzisha kwenye bustani ya ofisi za umma, ndipo jeshi kubwa la Wamachinga wakaungana kukoleza moto. Mazingira ya kwetu siyo ya Tunisia ila for knowledge and reference sake hii inatupa kioo kizuri cha kujitazamia tunaposhughulika na kikundi hiki kinachokuwa siku hadi siku bila kuwa na sera, kanuni, mwongozo au hata sheria ya kuwaratibu moja kwa moja kama wao.


2. Mtaji wa Kisiasa (Political Capital Investment)

Wanasiasa wa wastani pote duniani hupenda kutumia Wamachinga kama mtaji wa kisiasa badala ya kutumia hoja kama mtaji wa kisiasa. Nchini Kenya Wamachinga ni mtaji mkubwa kuelekea 2022 ambapo wamepewa jina la Hustlers na kutoa tafsiri kama ile ya Biblia kwenye kitabu cha Muhubiri.10:5-7 “Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye; ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini mimi nimeona watumwa (uongozi ni utumwa) wamepanda farasi, na wakuu (wenye nchi yao ndiyo wakuu) wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa” Uganda 2021 Wamachinga walikuwa kama mpira wa kona vile, wanasiasa wengine wakiwavuta kwa sanaa ya muziki wengine wakiwavuta kwa sera jadidifu. Zambia, Mhe. Lungu moja ya sababu zilizofanya akapoteza ni China-zation of Zambia Micro Economy ambayo ndiyo wamo Wamachinga kwa 100%. Mchina mchana ni Project Engineer usiku ni Waiter kwenye Chinese Restaurant, lugha ya mitaani inasema ‘wametumwa ela’ (kwa Mtz hii inatafsirika kama Professional Suicide). Siku moja nikapost hapa kwamba kuna Mchina mmoja aliwahi kushangaa kusikia kwamba Afrika kuna kitu kinaitwa fedha haramu/illicit money. Afrika Kusini Wamachinga wanatengenezewa sera yao na sheria vitakavyoratibu shughuli zao rasmi na serikali kujipatia mapato. Hii imekuja baada ya xenophobia kulipuka kila mwaka na kila awamu (kasoro ya Mandela) na hasa baada ya jumuiya za kimataifa kama SADC na AU kuweka chagizo kwa serikali ya ANC kufanya kitu kwa ajili ya ustawi wa Wamachinga. Raia wa nchi zingine walijiuza wenyewe Afrika Kusini kusaka maisha wakawa Wamachinga. Ethiopia iliyokosa sera na sheria ya kuratibu Umachinga ikashuhudia uhamiaji haramu mkubwa toka Ethiopia kwenda Afrika Kusini kupitia EAC kama njia. Hapa ndipo ninapokuja na hoja kwamba kama taifa tunaweza kuanzisha programu kabambe ya kuuza Wamachinga kama rasilimalibinadamu nje ya mipaka kwa tija ya taifa (hii siyo biashara ya utumwa bali ni labour migration protocol kwenda kwenye nchi ambazo zinaendesha chumi zao kwa mfumo wa labour intensive/mitulinga).

3. Kuibuka kwa Mivutano ya Kiitikadi za Kisiasa (Eruption of Political Ideological Tensions)

Ili Afrika Kusini ipone vizuri itahitaji kuondoa sumu kali ya hisia za mapambano ya kizalendo ya kudai ukombozi kila wakati hata baada ya ukombozi huo kupatikana; ambazo ndizo zimewajaa vijana wengi ambao ndiyo wanatengeneza kundi kubwa la Wamachinga. Aidha, Wamachinga wanaotoka nchi zingine kuzamia Afrika Kusini nao wanajifunza mienendo ya Wamachinga wa Afrika Kusini ya mapambano ya kudai ukombozi wa kiuchumi na ajira wanaporudi kwenye nchi zao. Hii hali imeziweka kwenye tahadhari kubwa nchi za Lesotho na eSwatini. Wamachinga ambao ni vijana kwa asilimia kubwa wanaongozwa na hisia kali za kutaka kuona mabadiliko katika mifumo ya maisha wanayoishi. Fursa hii ya mabadiliko inapokosekana tamaa kali (lust) ya kutafuta itikadi sahihi na mrengo sahihi inaibuka ndani yao na inapokutana na wanasiasa uchwara basi unaweza kujuwa kuwa 1 + 1 siyo lazima iwe 2 bali kutegemea mazingira inaweza kuwa hata 11. Mwenye masikio na asikie, mwenye macho na aone, asomaye na afahamu.







R.83e27eaf0fc4e8335d92d5f002b8a7b3

OIP.wrKP-8aI1XLG6NmZ1e85FwAAAA

Taswira zote kwa hisani ya google.
Dah!....uko vizuri sana kwenye kujenga hoja, hongera sana.

Andiko lako linaonyesha wewe ni msomi mkubwa.

Unafanya tafiti nini kuhusu umachinga?
 
Tafakari haya:-

1. Je, Wamachinga ni matokeo au zao la mfumo wa elimu tulio nao?

2. Je, Wamachinga ni zao la Economic Model inayoongoza nchi na sayari?

3. Je, Mamlaka za Kodi zime-engage vipi Wamachinga kwenye mfumo wa kodi maana wako wengi sana?

4. Je, kwanini hakuna Sheria ya Bunge (Act of Parliament) inayoratibu shughuli za Wamachinga kwa tija ya taifa? Ikumbukwe idadi yao ambayo hatujaijuwa ni kubwa kiasi kwamba taifa halipaswi kukosa sheria ya kuwaratibu zaidi ya ile sheria ya uzururaji inayobana madadapoa na mission-town (wapiga misele).

5. Je, Sheria ya Nguvu Kazi ya 1984 inasema nini kuhusu Wamachinga? Au wakati sheria hiyo inatungwa Wamachinga hawakuwepo lakini kwamba sasa wapo ni kwanini sheria hiyo isifanyiwe marekebisho ili iwaongelee na wao pia?

6. Je, kwakuwa Umachinga ni zao la mfumo-liberali wa dunia hasa kwenye uchumi ambapo Ujamaa uliokuwa unasisitiza dola kuzalisha na kuwalisha je, ujio wa mfumo mpya uliowazalisha (siyo Ujamaa) unaowataka wale kwa jasho lao umewaandaliaje mazingira wezeshi na jumuishi ili waendelee kula kwa jasho lao wasijekuitegemea dola?

7. Nachelea kuamini kwamba kama sensa ya Wamachinga nchini ikifanyika idadi yao itazidi idadi ya watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja.

8. Je, mbona uamuzi wa kuwaondoa huwa unafanyika tu baada ya uchaguzi na serikali kusimikwa? Karibu na uchaguzi hawaondolewi? Serikali inakuwa wapi? Bajeti ya kuwaondoa kipindi hicho inakuwa wapi?

9. Mbona ilani za uchaguzi hazisemi moja kwa moja kwamba tukishika madaraka ya nchi tutawaondoa Wamachinga; ili utekelezaji wa kuwaondoa unapofanyika basi ionekane wazi kwamba Ilani inatekelezwa?


10. Je, kama Wamachinga wanachafua miji vipi magereji na vituo holela vya mafuta kwenye makazi vinapamba miji?

11. Pana tofauti gani kati ya Wamachinga waliovamia mitaa nchi nzima na watu waliowekeza na kuishi kwenye hifadhi za barabara za Tanroads na Tarura nchi nzima kwa miaka nenda miaka rudi?

12. Wamachinga walianza mwaka 1985. Wakati wa uchaguzi 1990 Wamachinga hawakuondolewa, 1995 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2000 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2005 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2010 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2015 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2020 hawakuondolewa muda wote wa uchaguzi na ule usio wa uchaguzi. Maswali:-

1. Tatizo ni warasimu au Wamachinga?

2. Tatizo ni Demokrasia mbovu?

3. Tatizo ni ombwe la sheria, sera, kanuni, miongozo, ubovu wa sera ya taifa ya vijana, mfumo wa elimu au nini?

4. Sheria (kama ipo) inayowaondoa muda usio wa uchaguzi kwanini isiwaondoe muda wa uchaguzi pia?

5. 2025 wakati wa mchakato wa uchaguzi hasa kampeni Wamachinga watarejea tena mitaani (na hawataguswa) kwa sababu hatuna utaratibu mzuri endelevu kuhusu Umachinga. Mama atatafuna mfupa huu bila shaka.

NB.
Fikiria, taifa liwe na kundi dogo la watu wa idadi ya nchi za Eswatini na Lesotho ambao hawalipi kodi kutokana na kwamba hakuna mazingira/mfumo wezeshi ulioandaliwa kwa ajili yao kulipa kodi na tozo za serikali? Tunayo ya kujifunza Kigali.



Athari za kuondoka Wamachinga bila maandalizi ya kutosha Kisera, Sheria, Kanuni na Miongozo husika.

Mgandamizo wa Kijamii (Social Pressure)

1. Ujambazi, Udokozi na Vibaka (Banditry, Pilfering and Thugs)

Akili iliyolala kwa kukosa cha kufanya huvutiwa na uhalifu. Uhalifu uchukuwa sura mbalimbali zikiwemo umalaya ambao utaongeza mzigo wa magonjwa kwa watu na serikali kununua madawa na vifaatiba, aidha, kuna uhalifu wa kuhujumu taasisi kupitia deals za kupiga fedha za taasisi ili watu waweze kuishi.


2. Magereza Kujaa (Prisons Runoff)

Namba moja hapo juu inazua athari za moja kwa moja kwa idara za Magereza na Mahakama na kulazimisha mahitaji ya ajira mpya za Mahakimu na Majaji wa kutosha na pia kutanua bajeti ya Magereza ambayo serikali haijajiandaa nayo.


3. Kutanuka kwa Soko la Mihadarati (Burgeoning of Drugs Market Niche)

Wengi walio mateja ni wale waliokosa cha kufanya kuingizia kipato. Wafalme wa mihadarati mbinu wanayotumia kwenye marketing yao ni kugawa fedha na mihadarati bure kwa wateja wapya kwa muda maalum ambao unatosha kuwatengenezea uraibu hawa newcomers, baada ya muda huo pesa za bure na ngada za bure zinasitishwa ili sasa ununuwe, uraibu uliotengenezewa utakusukuma kutafuta ela hata kwa kukata kiungo cha Albino au hata kumvamia Askari mwenye bunduki na kumpiga sachi ili upate ama ela au mali ya thamani ukauze ukanunue ngada ya kipimo tu cha ukucha ili arosto isikuondoe kwenye uso wa dunia.


4. Migogoro ya Familia (Household Disorders)

Wamachinga wengi wanasomesha, wamejenga, ni bima ya afya kwa ndugu zao, ni breadwinners wa familia zao na jamaa zao. Kama breadwinner akikosa cha kufanya kuleta mkate nyumbani familia itaingia kwenye mgogoro. Taifa lenye migogoro ya kifamilia halina ustawi mzuri. Umoja wa Mataifa umeweka siku maalum kimataifa ya kutafakari juu ya migogoro ya kifamilia na kuna itifaki zake.


Changamoto za Kiuchumi (Economic Challenges)

1. Mikopo (Credit Facility)

Wamachinga wengi wamekopa kwenye masoko ya mitaji ama yasiyo rasmi au yaliyo rasmi. Kuondoka kwa dharura bila fidia ya kutengenezea vizimba vipya kwenye site mpya kutayumbisha mitaji yao na biashara zao na kufanya urejeshaji wa mikopo yao kuyumba pia, masoko haya ya mitaji yatakosa uwezo mkubwa wa kuendelea kuwahudumia wakopaji wapya. Hili wakati wa Corona 2020 liliyumbisha masoko ya hisa duniani. Kenya, serikali ili-guarantee masoko haya ili yarefushe muda wa mikopo kwa mwaka mbele kuwapunguzia waliokopa athari za Corona zilizotokana na lockdown kwamba dhamana zao za mikopo zisiuzwe. Hongera SSH kwa kutenga 5bl za zoezi la ku-relocate Wamachinga hofu iko kwenye usalama wa matumizi ya fungu hili lakini pia fungu linatosha idadi kubwa ya Wamachinga nchini?


2. Nadharia ya Uhitaji na Ugavi (Theory of Demand and Supply)

Kuondoka kwa Wamachinga kutaathiri mnyororo wa ugavi (Supply Chain) ambapo wagavi watakuwa wachache na wahitaji kuwa wengi hivyo bei ya bidhaa na huduma kupanda (Price Elasticity of Demand and Supply) na kufanya uwezo wa manunuzi (Purchasing Power) ya wahitaji hasa wanyonge kuathirika, na huenda tukaona mfumuko wa bei kwenye uchumi wa nchi, ikumbukwe kuwa hatuna takwimu za sensa ya Wamachinga na huenda makisio ni kuwa idadi yao nchini huenda inazidi watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja. Wamachinga walikuwa wana-regulate mfumuko wa bei (Inflation) na kuruhusu nguvu za soko za uhitaji na ugavi (Demand and Supply) kinyume na sasa ambapo tutaona Business Syndicates na Cartels zikiibuka na kujifanya Mawakala wa Kudhibiti Bei (Price Control Agents). Serikali itakapowataka wenye maduka sasa kulipa kodi na tozo halali za serikali (ambazo kimsingi sipingani nazo maana zina manufaa kwangu pia) misuguano itaanza kati ya wafanyabiashara hawa na Mamlaka za Kodi na Ushuru na wimbo utabadilika kwamba serikali inanyanyasa wafanyabiashara, Afrika ndivyo tulivyo, tunapenda kuona serikali ikikosa mapato yake halali sisi pekee wafanyabiashara tupate. Aidha, Wamachinga wanategemewa na Wafanyabiashara wakubwa kabisa maarufu nchini wanaouza vinywaji laini, barafu za kulamba, vitafunwa nk. Hawa nao wanakuwa wahanga wakubwa wa kuondoka Wamachinga katikati ya miji/mitani. Wamachinga kumbe ni injini inayotegemewa na wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa kabisa licha ya mlaji tu. Mafunuo mapya hayo.


3. Kuathiri Tasnia ya Mama na Baba Lishe (Affecting Food Vending Industry)

Mama na Baba Lishe soko lao kubwa mijini ni mamilioni ya Wamachinga wanaouza bidhaa zao maeneo hayo. Mama na Baba Lishe wanategemea Wamachinga kuliko wanavyowategemea Wachina, Wahindi, Waarabu, Wakinga na Wachaga wachache waliosalia (kwa Kariakoo). Biashara za Mama & Baba Lishe na Wamachinga zinategemezana (Solution to one problem contains the seeds for the next problem. Ukiondoa Wamachinga kwa pupa umeleta tatizo la Mama na Baba Lishe ambao wengi hivi sasa wako kisheria kupitia mradi wa Majiji Salama Afrika uliofadhiliwa na UN na serikali kuhalalisha biashara zao kupitia Healthy Cities Project). Case Study: Hoteli ya Kitalii zamani Holiday Inn mkabala na Benki ya Standard Chartered jijini Dsm mwekezaji mpya alipochukuwa hoteli ile akaondoa kibanda cha Mama na Baba Lishe kilichokuwepo jirani kabisa na hoteli, kilichotokea ni kwamba wageni wake wakiwemo wa kizungu walikuwa wanalipia tu malazi hotelini lakini chakula wanawafuata Mama na Baba Lishe wale waliosukumiziwa mita kama 25 hivi, walichokuwa wakifuata wageni wale pale kwa Mama na Baba Lishe ni bei nafuu, African cuisine na wadada wazuri wa Kitz, matokeo yake wageni wale wakawa wanawaambia keep change hata $, hoteli ile ikapoteza asilimia kubwa ya mapato ya chakula hadi pale mamlaka zilipowafuata wale Mama na Baba Lishe na kuwafungia kabisa biashara ile lakini ikaathiri mamia ya wafanyakazi maofisini waliokuwa wakitegemea vibanda vile kwa sababu hawawezi kula hoteli ile ya kitalii.


4. Halmashauri za Dar Hazina Ardhi (Metropolitan Dar Land Scarcity)

Ardhi zote zimeishamilikiwa na watu, serikali ikihitaji ardhi inabidi ifidie watu iwahamishe au iende kwenye wilaya za jirani na mkoa wa Dar (Temeke inapumulia Mkuranga, Ilala inapumulia Kisarawe, Ubungo inapumulia Kibaha, Kinondoni inapumulia Bagamoyo). Population ya Wamachinga Dar pekee ni kubwa kuliko inavyofikiriwa na wanahitaji maeneo mengi ya kutosha. Mwaka 1995 idadi yao ilikuwa sawa na wakazi wa jiji la Mwanza, leo miaka 26 imepita je, idadi yao imeongezeka kiasi gani? Dar inayo ardhi hiyo?


Uzorotefu wa Kisiasa (Political Meltdown)

1. Machafuko (Mayhem)

Tunisia iliingia machafuko yaliyosambaa katika ukanda mzima wa Waarabu wa Kaskazini mwa Jangwa la Sahara na Sahel na baadaye Mashariki ya Kati kwa cheche ndogo tu ya Mmachinga aliyeuawa kwa kipigo cha Mgambo akimtuhumu kujipumzisha kwenye bustani ya ofisi za umma, ndipo jeshi kubwa la Wamachinga wakaungana kukoleza moto. Mazingira ya kwetu siyo ya Tunisia ila for knowledge and reference sake hii inatupa kioo kizuri cha kujitazamia tunaposhughulika na kikundi hiki kinachokuwa siku hadi siku bila kuwa na sera, kanuni, mwongozo au hata sheria ya kuwaratibu moja kwa moja kama wao.


2. Mtaji wa Kisiasa (Political Capital Investment)

Wanasiasa wa wastani pote duniani hupenda kutumia Wamachinga kama mtaji wa kisiasa badala ya kutumia hoja kama mtaji wa kisiasa. Nchini Kenya Wamachinga ni mtaji mkubwa kuelekea 2022 ambapo wamepewa jina la Hustlers na kutoa tafsiri kama ile ya Biblia kwenye kitabu cha Muhubiri.10:5-7 “Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye; ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini mimi nimeona watumwa (uongozi ni utumwa) wamepanda farasi, na wakuu (wenye nchi yao ndiyo wakuu) wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa” Uganda 2021 Wamachinga walikuwa kama mpira wa kona vile, wanasiasa wengine wakiwavuta kwa sanaa ya muziki wengine wakiwavuta kwa sera jadidifu. Zambia, Mhe. Lungu moja ya sababu zilizofanya akapoteza ni China-zation of Zambia Micro Economy ambayo ndiyo wamo Wamachinga kwa 100%. Mchina mchana ni Project Engineer usiku ni Waiter kwenye Chinese Restaurant, lugha ya mitaani inasema ‘wametumwa ela’ (kwa Mtz hii inatafsirika kama Professional Suicide). Siku moja nikapost hapa kwamba kuna Mchina mmoja aliwahi kushangaa kusikia kwamba Afrika kuna kitu kinaitwa fedha haramu/illicit money. Afrika Kusini Wamachinga wanatengenezewa sera yao na sheria vitakavyoratibu shughuli zao rasmi na serikali kujipatia mapato. Hii imekuja baada ya xenophobia kulipuka kila mwaka na kila awamu (kasoro ya Mandela) na hasa baada ya jumuiya za kimataifa kama SADC na AU kuweka chagizo kwa serikali ya ANC kufanya kitu kwa ajili ya ustawi wa Wamachinga. Raia wa nchi zingine walijiuza wenyewe Afrika Kusini kusaka maisha wakawa Wamachinga. Ethiopia iliyokosa sera na sheria ya kuratibu Umachinga ikashuhudia uhamiaji haramu mkubwa toka Ethiopia kwenda Afrika Kusini kupitia EAC kama njia. Hapa ndipo ninapokuja na hoja kwamba kama taifa tunaweza kuanzisha programu kabambe ya kuuza Wamachinga kama rasilimalibinadamu nje ya mipaka kwa tija ya taifa (hii siyo biashara ya utumwa bali ni labour migration protocol kwenda kwenye nchi ambazo zinaendesha chumi zao kwa mfumo wa labour intensive/mitulinga).

3. Kuibuka kwa Mivutano ya Kiitikadi za Kisiasa (Eruption of Political Ideological Tensions)

Ili Afrika Kusini ipone vizuri itahitaji kuondoa sumu kali ya hisia za mapambano ya kizalendo ya kudai ukombozi kila wakati hata baada ya ukombozi huo kupatikana; ambazo ndizo zimewajaa vijana wengi ambao ndiyo wanatengeneza kundi kubwa la Wamachinga. Aidha, Wamachinga wanaotoka nchi zingine kuzamia Afrika Kusini nao wanajifunza mienendo ya Wamachinga wa Afrika Kusini ya mapambano ya kudai ukombozi wa kiuchumi na ajira wanaporudi kwenye nchi zao. Hii hali imeziweka kwenye tahadhari kubwa nchi za Lesotho na eSwatini. Wamachinga ambao ni vijana kwa asilimia kubwa wanaongozwa na hisia kali za kutaka kuona mabadiliko katika mifumo ya maisha wanayoishi. Fursa hii ya mabadiliko inapokosekana tamaa kali (lust) ya kutafuta itikadi sahihi na mrengo sahihi inaibuka ndani yao na inapokutana na wanasiasa uchwara basi unaweza kujuwa kuwa 1 + 1 siyo lazima iwe 2 bali kutegemea mazingira inaweza kuwa hata 11. Mwenye masikio na asikie, mwenye macho na aone, asomaye na afahamu.







R.83e27eaf0fc4e8335d92d5f002b8a7b3

OIP.wrKP-8aI1XLG6NmZ1e85FwAAAA

Taswira zote kwa hisani ya google.
Tunafahamu kuwa wamachinga Wana haki zao kama watanzania, lakini tunafahamu pia kuwa waenda kwa miguu Wana haki zao kulindwa. Uhuru wako unakoma pale unapoanza uhuru wa wengine. Wamachinga hawatoi fidia kwa mtu aliyegongwa na chombo Cha mto kwa kutembea kwenye barabara za magari.

Hatuwezi kujiuliza maswali mengiii kama mbegu za papai ili kuwaondoa wavamizi wa maeneo, waliovunja sheria. Hata kupewa maeneo ni hisani TU.

Tunafahamu kuwa wapo wachinga walioletwa mjini na watu wenye kazi zao, hawa ndio watakaopiga kelele nyingi kwa niaba ya machinga, lakini ukweli ni kwamba sio machinga ila wanajificha kwenye mgongo wa machinga.
 
Tunafahamu kuwa wamachinga Wana haki zao kama watanzania, lakini tunafahamu pia kuwa waenda kwa miguu Wana haki zao kulindwa. Uhuru wako unakoma pale unapoanza uhuru wa wengine. Wamachinga hawatoi fidia kwa mtu aliyegongwa na chombo Cha mto kwa kutembea kwenye barabara za magari.

Hatuwezi kujiuliza maswali mengiii kama mbegu za papai ili kuwaondoa wavamizi wa maeneo, waliovunja sheria. Hata kupewa maeneo ni hisani TU.

Tunafahamu kuwa wapo wachinga walioletwa mjini na watu wenye kazi zao, hawa ndio watakaopiga kelele nyingi kwa niaba ya machinga, lakini ukweli ni kwamba sio machinga ila wanajificha kwenye mgongo wa machinga.
Kupanga ni kuchagua na kutekeleza ni kuamua. Machinga wa Ethiopia wanakimbia nchi yao (EAC ndiyo route yao kwenda Kusini mwa Afrika), ni kioo cha kujitazamia hicho. Ila mawazo yako super!
 
Kupanga ni kuchagua na kutekeleza ni kuamua. Machinga wa Ethiopia wanakimbia nchi yao (EAC ndiyo route yao kwenda Kusini mwa Afrika), ni kioo cha kujitazamia hicho. Ila mawazo yako super!
Nchi yetu Ina bahati sana kuwa ni kubwa sana kuliko idadi ya watu. Yako mapori ambayo hajawahi kukanyaga binadamu. Na bahati mbaya hakuna mtanzania ambae familia yake imekosa ardhi. Machinga wooote kabisa Wana kwao ana huko kwao wanayo ardhi kubwa sana ambayo wameiacha bila matumizi.

Machinga hawa wamekuwa machinga kwasababu TU serikali yetu inafahamu kuwa wananchi wameichoka hivyo wanatumia ujanjaujanja kubakia madarakani, ikiwemo hii ya kuwaacha machinga wafanyekazi kiholela kama hivi wakidhani kuwa ni suluhisho, lakini Sasa tatizo linaanza kuwa kubwa sana kuliko walivyotarajia.

Hata hivyo, it is never too late to do the right thing. Tufanye Leo sio kesho. Kama Leo ni ghali basi itakuwa ghali zaidi kesho.
 
Tafakari haya:-

1. Je, Wamachinga ni matokeo au zao la mfumo wa elimu tulio nao?

2. Je, Wamachinga ni zao la Economic Model inayoongoza nchi na sayari?

3. Je, Mamlaka za Kodi zime-engage vipi Wamachinga kwenye mfumo wa kodi maana wako wengi sana?

4. Je, kwanini hakuna Sheria ya Bunge (Act of Parliament) inayoratibu shughuli za Wamachinga kwa tija ya taifa? Ikumbukwe idadi yao ambayo hatujaijuwa ni kubwa kiasi kwamba taifa halipaswi kukosa sheria ya kuwaratibu zaidi ya ile sheria ya uzururaji inayobana madadapoa na mission-town (wapiga misele).

5. Je, Sheria ya Nguvu Kazi ya 1984 inasema nini kuhusu Wamachinga? Au wakati sheria hiyo inatungwa Wamachinga hawakuwepo lakini kwamba sasa wapo ni kwanini sheria hiyo isifanyiwe marekebisho ili iwaongelee na wao pia?

6. Je, kwakuwa Umachinga ni zao la mfumo-liberali wa dunia hasa kwenye uchumi ambapo Ujamaa uliokuwa unasisitiza dola kuzalisha na kuwalisha je, ujio wa mfumo mpya uliowazalisha (siyo Ujamaa) unaowataka wale kwa jasho lao umewaandaliaje mazingira wezeshi na jumuishi ili waendelee kula kwa jasho lao wasijekuitegemea dola?

7. Nachelea kuamini kwamba kama sensa ya Wamachinga nchini ikifanyika idadi yao itazidi idadi ya watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja.

8. Je, mbona uamuzi wa kuwaondoa huwa unafanyika tu baada ya uchaguzi na serikali kusimikwa? Karibu na uchaguzi hawaondolewi? Serikali inakuwa wapi? Bajeti ya kuwaondoa kipindi hicho inakuwa wapi?

9. Mbona ilani za uchaguzi hazisemi moja kwa moja kwamba tukishika madaraka ya nchi tutawaondoa Wamachinga; ili utekelezaji wa kuwaondoa unapofanyika basi ionekane wazi kwamba Ilani inatekelezwa?


10. Je, kama Wamachinga wanachafua miji vipi magereji na vituo holela vya mafuta kwenye makazi vinapamba miji?

11. Pana tofauti gani kati ya Wamachinga waliovamia mitaa nchi nzima na watu waliowekeza na kuishi kwenye hifadhi za barabara za Tanroads na Tarura nchi nzima kwa miaka nenda miaka rudi?

12. Wamachinga walianza mwaka 1985. Wakati wa uchaguzi 1990 Wamachinga hawakuondolewa, 1995 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2000 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2005 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2010 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2015 muda wa uchaguzi hawakuondolewa, 2020 hawakuondolewa muda wote wa uchaguzi na ule usio wa uchaguzi. Maswali:-

1. Tatizo ni warasimu au Wamachinga?

2. Tatizo ni Demokrasia mbovu?

3. Tatizo ni ombwe la sheria, sera, kanuni, miongozo, ubovu wa sera ya taifa ya vijana, mfumo wa elimu au nini?

4. Sheria (kama ipo) inayowaondoa muda usio wa uchaguzi kwanini isiwaondoe muda wa uchaguzi pia?

5. 2025 wakati wa mchakato wa uchaguzi hasa kampeni Wamachinga watarejea tena mitaani (na hawataguswa) kwa sababu hatuna utaratibu mzuri endelevu kuhusu Umachinga. Mama atatafuna mfupa huu bila shaka.

NB.
Fikiria, taifa liwe na kundi dogo la watu wa idadi ya nchi za Eswatini na Lesotho ambao hawalipi kodi kutokana na kwamba hakuna mazingira/mfumo wezeshi ulioandaliwa kwa ajili yao kulipa kodi na tozo za serikali? Tunayo ya kujifunza Kigali.



Athari za kuondoka Wamachinga bila maandalizi ya kutosha Kisera, Sheria, Kanuni na Miongozo husika.

Mgandamizo wa Kijamii (Social Pressure)

1. Ujambazi, Udokozi na Vibaka (Banditry, Pilfering and Thugs)

Akili iliyolala kwa kukosa cha kufanya huvutiwa na uhalifu. Uhalifu uchukuwa sura mbalimbali zikiwemo umalaya ambao utaongeza mzigo wa magonjwa kwa watu na serikali kununua madawa na vifaatiba, aidha, kuna uhalifu wa kuhujumu taasisi kupitia deals za kupiga fedha za taasisi ili watu waweze kuishi.


2. Magereza Kujaa (Prisons Runoff)

Namba moja hapo juu inazua athari za moja kwa moja kwa idara za Magereza na Mahakama na kulazimisha mahitaji ya ajira mpya za Mahakimu na Majaji wa kutosha na pia kutanua bajeti ya Magereza ambayo serikali haijajiandaa nayo.


3. Kutanuka kwa Soko la Mihadarati (Burgeoning of Drugs Market Niche)

Wengi walio mateja ni wale waliokosa cha kufanya kuingizia kipato. Wafalme wa mihadarati mbinu wanayotumia kwenye marketing yao ni kugawa fedha na mihadarati bure kwa wateja wapya kwa muda maalum ambao unatosha kuwatengenezea uraibu hawa newcomers, baada ya muda huo pesa za bure na ngada za bure zinasitishwa ili sasa ununuwe, uraibu uliotengenezewa utakusukuma kutafuta ela hata kwa kukata kiungo cha Albino au hata kumvamia Askari mwenye bunduki na kumpiga sachi ili upate ama ela au mali ya thamani ukauze ukanunue ngada ya kipimo tu cha ukucha ili arosto isikuondoe kwenye uso wa dunia.


4. Migogoro ya Familia (Household Disorders)

Wamachinga wengi wanasomesha, wamejenga, ni bima ya afya kwa ndugu zao, ni breadwinners wa familia zao na jamaa zao. Kama breadwinner akikosa cha kufanya kuleta mkate nyumbani familia itaingia kwenye mgogoro. Taifa lenye migogoro ya kifamilia halina ustawi mzuri. Umoja wa Mataifa umeweka siku maalum kimataifa ya kutafakari juu ya migogoro ya kifamilia na kuna itifaki zake.


Changamoto za Kiuchumi (Economic Challenges)

1. Mikopo (Credit Facility)

Wamachinga wengi wamekopa kwenye masoko ya mitaji ama yasiyo rasmi au yaliyo rasmi. Kuondoka kwa dharura bila fidia ya kutengenezea vizimba vipya kwenye site mpya kutayumbisha mitaji yao na biashara zao na kufanya urejeshaji wa mikopo yao kuyumba pia, masoko haya ya mitaji yatakosa uwezo mkubwa wa kuendelea kuwahudumia wakopaji wapya. Hili wakati wa Corona 2020 liliyumbisha masoko ya hisa duniani. Kenya, serikali ili-guarantee masoko haya ili yarefushe muda wa mikopo kwa mwaka mbele kuwapunguzia waliokopa athari za Corona zilizotokana na lockdown kwamba dhamana zao za mikopo zisiuzwe. Hongera SSH kwa kutenga 5bl za zoezi la ku-relocate Wamachinga hofu iko kwenye usalama wa matumizi ya fungu hili lakini pia fungu linatosha idadi kubwa ya Wamachinga nchini?


2. Nadharia ya Uhitaji na Ugavi (Theory of Demand and Supply)

Kuondoka kwa Wamachinga kutaathiri mnyororo wa ugavi (Supply Chain) ambapo wagavi watakuwa wachache na wahitaji kuwa wengi hivyo bei ya bidhaa na huduma kupanda (Price Elasticity of Demand and Supply) na kufanya uwezo wa manunuzi (Purchasing Power) ya wahitaji hasa wanyonge kuathirika, na huenda tukaona mfumuko wa bei kwenye uchumi wa nchi, ikumbukwe kuwa hatuna takwimu za sensa ya Wamachinga na huenda makisio ni kuwa idadi yao nchini huenda inazidi watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja. Wamachinga walikuwa wana-regulate mfumuko wa bei (Inflation) na kuruhusu nguvu za soko za uhitaji na ugavi (Demand and Supply) kinyume na sasa ambapo tutaona Business Syndicates na Cartels zikiibuka na kujifanya Mawakala wa Kudhibiti Bei (Price Control Agents). Serikali itakapowataka wenye maduka sasa kulipa kodi na tozo halali za serikali (ambazo kimsingi sipingani nazo maana zina manufaa kwangu pia) misuguano itaanza kati ya wafanyabiashara hawa na Mamlaka za Kodi na Ushuru na wimbo utabadilika kwamba serikali inanyanyasa wafanyabiashara, Afrika ndivyo tulivyo, tunapenda kuona serikali ikikosa mapato yake halali sisi pekee wafanyabiashara tupate. Aidha, Wamachinga wanategemewa na Wafanyabiashara wakubwa kabisa maarufu nchini wanaouza vinywaji laini, barafu za kulamba, vitafunwa nk. Hawa nao wanakuwa wahanga wakubwa wa kuondoka Wamachinga katikati ya miji/mitani. Wamachinga kumbe ni injini inayotegemewa na wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa kabisa licha ya mlaji tu. Mafunuo mapya hayo.


3. Kuathiri Tasnia ya Mama na Baba Lishe (Affecting Food Vending Industry)

Mama na Baba Lishe soko lao kubwa mijini ni mamilioni ya Wamachinga wanaouza bidhaa zao maeneo hayo. Mama na Baba Lishe wanategemea Wamachinga kuliko wanavyowategemea Wachina, Wahindi, Waarabu, Wakinga na Wachaga wachache waliosalia (kwa Kariakoo). Biashara za Mama & Baba Lishe na Wamachinga zinategemezana (Solution to one problem contains the seeds for the next problem. Ukiondoa Wamachinga kwa pupa umeleta tatizo la Mama na Baba Lishe ambao wengi hivi sasa wako kisheria kupitia mradi wa Majiji Salama Afrika uliofadhiliwa na UN na serikali kuhalalisha biashara zao kupitia Healthy Cities Project). Case Study: Hoteli ya Kitalii zamani Holiday Inn mkabala na Benki ya Standard Chartered jijini Dsm mwekezaji mpya alipochukuwa hoteli ile akaondoa kibanda cha Mama na Baba Lishe kilichokuwepo jirani kabisa na hoteli, kilichotokea ni kwamba wageni wake wakiwemo wa kizungu walikuwa wanalipia tu malazi hotelini lakini chakula wanawafuata Mama na Baba Lishe wale waliosukumiziwa mita kama 25 hivi, walichokuwa wakifuata wageni wale pale kwa Mama na Baba Lishe ni bei nafuu, African cuisine na wadada wazuri wa Kitz, matokeo yake wageni wale wakawa wanawaambia keep change hata $, hoteli ile ikapoteza asilimia kubwa ya mapato ya chakula hadi pale mamlaka zilipowafuata wale Mama na Baba Lishe na kuwafungia kabisa biashara ile lakini ikaathiri mamia ya wafanyakazi maofisini waliokuwa wakitegemea vibanda vile kwa sababu hawawezi kula hoteli ile ya kitalii.


4. Halmashauri za Dar Hazina Ardhi (Metropolitan Dar Land Scarcity)

Ardhi zote zimeishamilikiwa na watu, serikali ikihitaji ardhi inabidi ifidie watu iwahamishe au iende kwenye wilaya za jirani na mkoa wa Dar (Temeke inapumulia Mkuranga, Ilala inapumulia Kisarawe, Ubungo inapumulia Kibaha, Kinondoni inapumulia Bagamoyo). Population ya Wamachinga Dar pekee ni kubwa kuliko inavyofikiriwa na wanahitaji maeneo mengi ya kutosha. Mwaka 1995 idadi yao ilikuwa sawa na wakazi wa jiji la Mwanza, leo miaka 26 imepita je, idadi yao imeongezeka kiasi gani? Dar inayo ardhi hiyo?


Uzorotefu wa Kisiasa (Political Meltdown)

1. Machafuko (Mayhem)

Tunisia iliingia machafuko yaliyosambaa katika ukanda mzima wa Waarabu wa Kaskazini mwa Jangwa la Sahara na Sahel na baadaye Mashariki ya Kati kwa cheche ndogo tu ya Mmachinga aliyeuawa kwa kipigo cha Mgambo akimtuhumu kujipumzisha kwenye bustani ya ofisi za umma, ndipo jeshi kubwa la Wamachinga wakaungana kukoleza moto. Mazingira ya kwetu siyo ya Tunisia ila for knowledge and reference sake hii inatupa kioo kizuri cha kujitazamia tunaposhughulika na kikundi hiki kinachokuwa siku hadi siku bila kuwa na sera, kanuni, mwongozo au hata sheria ya kuwaratibu moja kwa moja kama wao.


2. Mtaji wa Kisiasa (Political Capital Investment)

Wanasiasa wa wastani pote duniani hupenda kutumia Wamachinga kama mtaji wa kisiasa badala ya kutumia hoja kama mtaji wa kisiasa. Nchini Kenya Wamachinga ni mtaji mkubwa kuelekea 2022 ambapo wamepewa jina la Hustlers na kutoa tafsiri kama ile ya Biblia kwenye kitabu cha Muhubiri.10:5-7 “Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye; ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini mimi nimeona watumwa (uongozi ni utumwa) wamepanda farasi, na wakuu (wenye nchi yao ndiyo wakuu) wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa” Uganda 2021 Wamachinga walikuwa kama mpira wa kona vile, wanasiasa wengine wakiwavuta kwa sanaa ya muziki wengine wakiwavuta kwa sera jadidifu. Zambia, Mhe. Lungu moja ya sababu zilizofanya akapoteza ni China-zation of Zambia Micro Economy ambayo ndiyo wamo Wamachinga kwa 100%. Mchina mchana ni Project Engineer usiku ni Waiter kwenye Chinese Restaurant, lugha ya mitaani inasema ‘wametumwa ela’ (kwa Mtz hii inatafsirika kama Professional Suicide). Siku moja nikapost hapa kwamba kuna Mchina mmoja aliwahi kushangaa kusikia kwamba Afrika kuna kitu kinaitwa fedha haramu/illicit money. Afrika Kusini Wamachinga wanatengenezewa sera yao na sheria vitakavyoratibu shughuli zao rasmi na serikali kujipatia mapato. Hii imekuja baada ya xenophobia kulipuka kila mwaka na kila awamu (kasoro ya Mandela) na hasa baada ya jumuiya za kimataifa kama SADC na AU kuweka chagizo kwa serikali ya ANC kufanya kitu kwa ajili ya ustawi wa Wamachinga. Raia wa nchi zingine walijiuza wenyewe Afrika Kusini kusaka maisha wakawa Wamachinga. Ethiopia iliyokosa sera na sheria ya kuratibu Umachinga ikashuhudia uhamiaji haramu mkubwa toka Ethiopia kwenda Afrika Kusini kupitia EAC kama njia. Hapa ndipo ninapokuja na hoja kwamba kama taifa tunaweza kuanzisha programu kabambe ya kuuza Wamachinga kama rasilimalibinadamu nje ya mipaka kwa tija ya taifa (hii siyo biashara ya utumwa bali ni labour migration protocol kwenda kwenye nchi ambazo zinaendesha chumi zao kwa mfumo wa labour intensive/mitulinga).

3. Kuibuka kwa Mivutano ya Kiitikadi za Kisiasa (Eruption of Political Ideological Tensions)

Ili Afrika Kusini ipone vizuri itahitaji kuondoa sumu kali ya hisia za mapambano ya kizalendo ya kudai ukombozi kila wakati hata baada ya ukombozi huo kupatikana; ambazo ndizo zimewajaa vijana wengi ambao ndiyo wanatengeneza kundi kubwa la Wamachinga. Aidha, Wamachinga wanaotoka nchi zingine kuzamia Afrika Kusini nao wanajifunza mienendo ya Wamachinga wa Afrika Kusini ya mapambano ya kudai ukombozi wa kiuchumi na ajira wanaporudi kwenye nchi zao. Hii hali imeziweka kwenye tahadhari kubwa nchi za Lesotho na eSwatini. Wamachinga ambao ni vijana kwa asilimia kubwa wanaongozwa na hisia kali za kutaka kuona mabadiliko katika mifumo ya maisha wanayoishi. Fursa hii ya mabadiliko inapokosekana tamaa kali (lust) ya kutafuta itikadi sahihi na mrengo sahihi inaibuka ndani yao na inapokutana na wanasiasa uchwara basi unaweza kujuwa kuwa 1 + 1 siyo lazima iwe 2 bali kutegemea mazingira inaweza kuwa hata 11. Mwenye masikio na asikie, mwenye macho na aone, asomaye na afahamu.







R.83e27eaf0fc4e8335d92d5f002b8a7b3

OIP.wrKP-8aI1XLG6NmZ1e85FwAAAA

Taswira zote kwa hisani ya google.
Nimesoma response yako ni nzuri na maswali mengi fikirishi ambayo yanahitaji a good research to come up with good way forward ambao unaweza kupelekea hata kutunga sheria mpya. Machinga walianza kama marching guys watembeza bidhaa mitaani. Wakaongezeka mara wakaanza vibanda vidogo vidogo mara wakaenda kila mahali. Hili lilipaswa kutazamwa kwa undani why do we have these people loitering along our streets. Chanzo cha hawa watu ni nini? Tunakitawala vipi, Elimu, ajira, umaskini, au? Wanapata wapi bidhaa wanazoziuza, je mitaji yao au ni mali za wengine n.k. kwa sasa hatuna tena huo wasaa wa kujiuliza bali ni kuokoa uchumi kwa kuwaondoa na kuwapa maeneo mbadala.
 
Nimesoma response yako ni nzuri na maswali mengi fikirishi ambayo yanahitaji a good research to come up with good way forward ambao unaweza kupelekea hata kutunga sheria mpya. Machinga walianza kama marching guys watembeza bidhaa mitaani. Wakaongezeka mara wakaanza vibanda vidogo vidogo mara wakaenda kila mahali. Hili lilipaswa kutazamwa kwa undani why do we have these people loitering along our streets. Chanzo cha hawa watu ni nini? Tunakitawala vipi, Elimu, ajira, umaskini, au? Wanapata wapi bidhaa wanazoziuza, je mitaji yao au ni mali za wengine n.k. kwa sasa hatuna tena huo wasaa wa kujiuliza bali ni kuokoa uchumi kwa kuwaondoa na kuwapa maeneo mbadala.
Umenena vema kabisa mkuu, lakini kama Kuna kosa serikali inataka kufanya tena ni kuahidi kuwa itaratibu na kuwapatia maeneo machinga wote kabisa hapa mjini. Wamachinga waliopo Sasa ni wengi, wanakuja wengine na wanazaana. Hivyo guarantee ya kuwapatia maeneo wote siioni. Kinachotakiwa ni kanuni za kufanya biashara na mipangomiji zifuatwe kama zilivyo kwa 100%.

Leo hii unakuta bia na vileo/ glossary ziko kila mahali, nchi nzima na maeneo yote yanauzwa bia na pombe nyingine hata kwenye maduka ya hardware. Huu ni uzembe mkubwa sana wa serikali. Mtu ana leseni ya bidhaa nyingine lakini anauza na bidhaa nyingine, na hiyo ni kupambana na umaskini au siasa za bei rahisi TU? Je, wale wenye leseni za kuuza bidhaa hizo kama pombe unawatendea haki?
 
Umenena vema kabisa mkuu, lakini kama Kuna kosa serikali inataka kufanya tena ni kuahidi kuwa itaratibu na kuwapatia maeneo machinga wote kabisa hapa mjini. Wamachinga waliopo Sasa ni wengi, wanakuja wengine na wanazaana. Hivyo guarantee ya kuwapatia maeneo wote siioni. Kinachotakiwa ni kanuni za kufanya biashara na mipangomiji zifuatwe kama zilivyo kwa 100%.

Leo hii unakuta bia na vileo/ glossary ziko kila mahali, nchi nzima na maeneo yote yanauzwa bia na pombe nyingine hata kwenye maduka ya hardware. Huu ni uzembe mkubwa sana wa serikali. Mtu ana leseni ya bidhaa nyingine lakini anauza na bidhaa nyingine, na hiyo ni kupambana na umaskini au siasa za bei rahisi TU? Je, wale wenye leseni za kuuza bidhaa hizo kama pombe unawatendea haki?
Great Mkuu!
Ulielewa presentation ya research report yangu vzr. Kuongezea kwenye points zako mahiri hizo, ni kuwa tunahitaji Machinga Marshal Plan ya kitaifa to address the problem once and for all.
 
Rais Samia hashauriwi vyema,

anatengeneza kundi kubwa sana la wapinzani nchini,

watu hao wakiachwa bila njia za kujipatia kipato wataichukia serikali yake.

Ni kweli tunahitaji miji misafi ila raia nao wanatakiwa kuwa huru kufanya shughuli zao.

CCM itapata wakati mgumu sana kujinadi 2025 kama hali hii ikiendelea.
 
Great Mkuu!
Ulielewa presentation ya research report yangu vzr. Kuongezea kwenye points zako mahiri hizo, ni kuwa tunahitaji Machinga Marshal Plan ya kitaifa to address the problem once and for all.
Nilipata fursa ya kuishi marekani vijijini, wengi wetu tunaokwenda Marekani wanakwenda kuishi mijini, lakini mimi nimeishi kule vijijini kabisa kama Chelsea na kijijini zaidi ambako watu wanajikamulia wenyewe juice za apple na kuweka kwenye galoni na kuuza kiholela tu.

Ukweli ni kwamba hata Marekani wako machinga wengi sana, lakini hawa wako hukohuko vijijini. Watu kutoka mijini siku za weekeend na public holiday utaona misululu ya magari kuelekea huko vijijini kununua bidhaadh
Great Mkuu!
Ulielewa presentation ya research report yangu vzr. Kuongezea kwenye points zako mahiri hizo, ni kuwa tunahitaji Machinga Marshal Plan ya kitaifa to address the problem once and for all.
Ok, Sir pamoja sana.

Mimi nimewahi kuishi Marekani mjini na vijijini pia. Nimeishi kwenye vijiji hasa kama Chelsea na vingine ambako wajasikiamali wadogo wanauza bidhaa zao hukohuko vijijini. Wanajikamulia wenyewe apple zao kupata juice wanazouza kwenye galoni kiholela TU kwa bei ndogo. Wamachinga kule vijijini wanauza bidhaa zenye bei nafuu sana kuliko mjini, bidhaa zao zimeondolewa Kodi mbalimbali hivyo ni rahisi sana kuliko kule mjini. Hivyo, kila weekends na public holidays utaona misululu mirefu ya magari kutoka mijini kwenda vijijini kufuata bidhaa za bei nafuu kuliko kwenye Malls.

Hivyo serikali inaweza kuondoa Kodi fulanifulani kwenye bidhaa zinazouzwa na machinga walioko kule Mlandizi, Mkuranga, kisarawe na bagamoyo ili machinga wavutike kwenda kule na wakazi wa mjini kuvutika kwenda kufanya manunuzi kule ya bei nafuu.

Mfano, kama bei ya seti ya sufuria inayouzwa laki 3 kariakoo itauzwa laki 2 kule Kisarawe kwenye maduka ya machinga watu wengi sana watakwwnda Kisarawe kununua sufuria hizo badala ya kariakoo. Tunahitaji sera na sio kutumia nguvu zaidi.

Kule Marekani bei ya bidhaa inapungua bei kutokana na mambo yafuatayo:

1. Ubora wa bidhaa
2. Umbali kutoka mjini
3. Aina ya bidhaa
4. Parking, kama sehemu haina parking na bei ya bidhaa hapo itakuwa ndogo.
5. Public transport, kama hakuna usafiri wa umma na bei iya bidhaa husika inaweza kushuka pia.

Shida yetu sisi hapa bidhaa ni rahisi mijini kuliko vijijini, bei inaongezeka kadiri mtu anavyotoka city center. Hivyo kuvuta watu kuja kariakoo kufanya biashara na kununua. Inawezekana huku kariakoo yakaweko maduka ya jumla TU basi.
 
Rais Samia hashauriwi vyema,

anatengeneza kundi kubwa sana la wapinzani nchini,

watu hao wakiachwa bila njia za kujipatia kipato wataichukia serikali yake.

Ni kweli tunahitaji miji misafi ila raia nao wanatakiwa kuwa huru kufanya shughuli zao.

CCM itapata wakati mgumu sana kujinadi 2025 kama hali hii ikiendelea.
Hapo kwenye 'huru'

Sio huru

Ni wanatakiwa kufuata taratibu na sheria ambazo kila mtanzania anafuata
 
Niliposema maandalizi ya kutosha yafuatayo aghalabu ni muhali hadi sasa kujulikana:-

1 Je, nani anajuwa takwimu halisi za idadi ya Wamachinga nchini? Mwaka 1995 wale wanaotembeza bidhaa (acha wanaotandika bidhaa chini idadi yao ilikuwa sawa na idadi ya watu wa Mwanza Mjini, over 8K)

2. Je, kuna sera, mwongozo kuhusu Wamachinga kwa miaka yote 36 tangu 1985? Kama havipo, tunahitaji miongo mingapi mbele kuandaa tools hizo?

3. Je, soko la Machinga Complex limeleta matokeo gani (kabla ya Kariakoo kuungua vizimba vilikuwa wazi kwa miaka nenda).

4. Je, kuna sensa ya Wamachinga imefanyika? Wako wangapi? Wanawake wangapi? Wanaume wangapi? Drop outs wangapi waliojiunga na Umachinga? Idadi kwa kila mji nchi nzima ni ngapi (ili wasije kuelemea Dar)? Graduates wangapi? Watanzania wangapi? Wachina wangapi? idadi kwa makabila ikoje ili tujuwe mkoa upi hauna mikakati ya kuwa-absorb wasije Dar? nk.

5. Je, Umachinga siyo jibu la madai ya taifa ya kutaka watu wajiajiri? Lkn katika mazingira gani?

6. Je, kuna sehemu zimeandaliwa za kuwameza wote waondoke mitaani?

7. Je, after-effects za kuwaondoa kwa dharura tumezipima tukazijuwa ni zipi na namna gani tumejiandaa kuzimitigate?

8. Je, Wamachinga ni matokeo au zao la mfumo wa elimu tulio nao?

9. Je, Wamachinga ni zao la Economic Model inayoongoza nchi/dunia?

10. Je, Mamlaka za Kodi zime-engage vipi Wamachinga kwenye mfumo wa kodi maana wako wengi sana?

11. Je, kwanini hakuna Sheria ya Bunge (Act of Parliament) inayoratibu shughuli za Wamachinga kwa tija ya taifa? Ikumbukwe idadi yao ambayo hatujaijuwa ni kubwa kiasi kwamba taifa halipaswi kukosa sheria ya kuwaratibu zaidi ya ile sheria ya uzururaji inayobana madadapoa na mission-town (wapiga misele).

12. Je, Sheria ya Nguvu Kazi ya 1984 inasema nini kuhusu Wamachinga? Au wakati sheria hiyo inatungwa Wamachinga hawakuwepo lakini kwamba sasa wapo ni kwanini sheria hiyo isifanyiwe marekebisho ili iwaongelee na wao pia?

13. Je, kwakuwa Umachinga ni zao la mfumo-liberali wa dunia hasa kwenye uchumi ambapo Ujamaa uliokuwa unasisitiza dola kuzalisha na kuwalisha je, ujio wa mfumo mpya uliowazalisha (siyo Ujamaa) unaowataka wale kwa jasho lao umewaandaliaje mazingira wezeshi na jumuishi ili waendelee kula kwa jasho lao wasijekuitegemea dola?

14. Nachelea kuamini kwamba kama sensa ya Wamachinga nchini ikifanyika idadi yao itazidi idadi ya watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja.


NB.
Fikiria, taifa liwe na kundi dogo la watu wa idadi ya nchi za Eswatini/Lesotho ambao hawalipi kodi kutokana na kwamba hakuna mazingira/mfumo wezeshi yaliyoandaliwa kwa ajili yao kulipa kodi na tozo za serikali? Baghosha!

Wamachinga wako maeneo mengi hata China, Nairobi Kikomba wako tangu enzi za Jomo Kenyatta.

R.e1ec613adc84bf0605423d19b716e466

Taswira kwa hisani ya google
Big up Mkuu
 
Nchi yetu inatakiwa ihakikishe vijana wanafanya kazi kwenye sekta za uzalishaji na huduma zenye tija kubwa siko kuwa wachuuzi wa bidhaa hafifu za Kichina
Niliposema maandalizi ya kutosha yafuatayo aghalabu ni muhali hadi sasa kujulikana:-

1 Je, nani anajuwa takwimu halisi za idadi ya Wamachinga nchini? Mwaka 1995 wale wanaotembeza bidhaa (acha wanaotandika bidhaa chini idadi yao ilikuwa sawa na idadi ya watu wa Mwanza Mjini, over 8K)

2. Je, kuna sera, mwongozo kuhusu Wamachinga kwa miaka yote 36 tangu 1985? Kama havipo, tunahitaji miongo mingapi mbele kuandaa tools hizo?

3. Je, soko la Machinga Complex limeleta matokeo gani (kabla ya Kariakoo kuungua vizimba vilikuwa wazi kwa miaka nenda).

4. Je, kuna sensa ya Wamachinga imefanyika? Wako wangapi? Wanawake wangapi? Wanaume wangapi? Drop outs wangapi waliojiunga na Umachinga? Idadi kwa kila mji nchi nzima ni ngapi (ili wasije kuelemea Dar)? Graduates wangapi? Watanzania wangapi? Wachina wangapi? idadi kwa makabila ikoje ili tujuwe mkoa upi hauna mikakati ya kuwa-absorb wasije Dar? nk.

5. Je, Umachinga siyo jibu la madai ya taifa ya kutaka watu wajiajiri? Lkn katika mazingira gani?

6. Je, kuna sehemu zimeandaliwa za kuwameza wote waondoke mitaani?

7. Je, after-effects za kuwaondoa kwa dharura tumezipima tukazijuwa ni zipi na namna gani tumejiandaa kuzimitigate?

8. Je, Wamachinga ni matokeo au zao la mfumo wa elimu tulio nao?

9. Je, Wamachinga ni zao la Economic Model inayoongoza nchi/dunia?

10. Je, Mamlaka za Kodi zime-engage vipi Wamachinga kwenye mfumo wa kodi maana wako wengi sana?

11. Je, kwanini hakuna Sheria ya Bunge (Act of Parliament) inayoratibu shughuli za Wamachinga kwa tija ya taifa? Ikumbukwe idadi yao ambayo hatujaijuwa ni kubwa kiasi kwamba taifa halipaswi kukosa sheria ya kuwaratibu zaidi ya ile sheria ya uzururaji inayobana madadapoa na mission-town (wapiga misele).

12. Je, Sheria ya Nguvu Kazi ya 1984 inasema nini kuhusu Wamachinga? Au wakati sheria hiyo inatungwa Wamachinga hawakuwepo lakini kwamba sasa wapo ni kwanini sheria hiyo isifanyiwe marekebisho ili iwaongelee na wao pia?

13. Je, kwakuwa Umachinga ni zao la mfumo-liberali wa dunia hasa kwenye uchumi ambapo Ujamaa uliokuwa unasisitiza dola kuzalisha na kuwalisha je, ujio wa mfumo mpya uliowazalisha (siyo Ujamaa) unaowataka wale kwa jasho lao umewaandaliaje mazingira wezeshi na jumuishi ili waendelee kula kwa jasho lao wasijekuitegemea dola?

14. Nachelea kuamini kwamba kama sensa ya Wamachinga nchini ikifanyika idadi yao itazidi idadi ya watu wa Zanzibar (1.5ml), watu wa Shelisheli (0.9ml) na huenda ikakaribiana na idadi ya watu wa Lesotho na Eswatini kwa pamoja.


NB.
Fikiria, taifa liwe na kundi dogo la watu wa idadi ya nchi za Eswatini/Lesotho ambao hawalipi kodi kutokana na kwamba hakuna mazingira/mfumo wezeshi yaliyoandaliwa kwa ajili yao kulipa kodi na tozo za serikali? Baghosha!

Wamachinga wako maeneo mengi hata China, Nairobi Kikomba wako tangu enzi za Jomo Kenyatta.

R.e1ec613adc84bf0605423d19b716e466

Taswira kwa hisani ya google
 
Wewe Kipato cha kati hujui tabu ya mtu asiye hata na buku la kumpa uhakika wa mlo wa kesho.
Kwanini mtu akose buko wakati Tanzania Kuna uhaba wa Mayai, kuku, nyama ya mbuzi, mihogo, machungwa, nyanya, mafenesi, malimao, pilipili, samaki, alizeti, maharagwe, nk? Bado uhitqji ni mkubwa kuliko uzalishaji. Tutiane moyo tufanye kazi za uhakika hadi hapo rasilimali zetu zitakapokuwa zimeisha.
 
Rais Samia hashauriwi vyema,

anatengeneza kundi kubwa sana la wapinzani nchini,

watu hao wakiachwa bila njia za kujipatia kipato wataichukia serikali yake.

Ni kweli tunahitaji miji misafi ila raia nao wanatakiwa kuwa huru kufanya shughuli zao.

CCM itapata wakati mgumu sana kujinadi 2025 kama hali hii ikiendelea.
Hii sio kweli, Kuna kijana niliwahi kumshauri arudi mkoani na kuachana na kazi ya kuuza urembo kwa njia ya kutembezea wateja kwenye kapu, alinichukia sana lakini akarudi mkoani na kuanza kazi ya kufuga kuku wa kienyeji na kulima pilipili. Sasa hivi Yuko mbali sana, ana zaidi ya kuku 1000, Bata 200 na mbuzi 100. Anauza kuku na Mayai ya kuku wa kiejeji anapata hela hata kumzidi mtu aliyeajiliwa kwa mtu, amejenga na amepanua shamba lake kwa kulima kwa Trekta. Leo hii ni rafiki yangu na ananisifu kila siku.

Vijana hawa machinga kwa kuishi hapa mjini wamepata exposure kubwa sana, wanafahamu kitu gani kinatakiwa mjini, hivyo ukiwatimua hapa na kurudi kijijini watafanya vitu vya maana sana vya kimaendeleo. Unachosema wewe ni kinyume chale.

Mfano, sisi tulikulia mjini kwenye nyumba ya serikali ambako baba alikuwa akifanyakazi, nyumba ilikuwa Ina fanicha zote, maji na umeme wa bure. Siku baba alipotuambia tunahamia nyumbani kwetu huko salasala tulimchukia sana kwa kututoa kwenye mtaa na nyumba tuliozoea. Lakini hivi Sasa tunamsifu kwa kufanya uwamuzi ule badala angesubiri kustaafu au tuondolewe baada ya baba kuacha kazi. Tulipohamia kule tukajikuta tuko kwenye nyumba yenye nafasi hata ya kucheza na kulala. Badala ya kumchukia tukamuona shujaa.

Hata machinga ukiwatimua kwenye njia za waenda kwa miguu na chini ya nyaya za umeme Leo lazima kesho watakusifu TU kwa kuwaondolea mateso na hatari.
 
Mkuu, ukizungumzia masuala ya kilimo na ufugaji hakuna Kijana atakayekuelewa. Wewe leta story za kubet na kushinda milioni kadhaa utaona watakavyomiminika.
Uko sahihi. Sijui kama viongozi huwa wanatafakari kuona kijana mwenye nguvu za kutunza shamba au mifugo kwa faida anatembeza saa na handkerchief kutoka china. Kikubwa Barabara zijengwe maeneo ya mashambani vijana wajiajiri kwenye kilimo na mifugo.
 
Back
Top Bottom