mke wangu ni mzuri sana hata nikifa leo nikifufuka nitamchagua tena yeye kuwa mke wangu nampenda sana, hivi karibuni nilichepuka na dada mmoja wa ofisini kwetu, ilikua siku ya jumamosi ilipofika jumanne tumbo lilianza kumuuma ghafla mke wangu aliyekuwa ni mjamzito wa miezi sita lilipozidi tukaenda hospital na bahati mbaya ile mimba ikawa imeharibika wakampa madawa akajifungua kitoto cha kike kikiwa kimekufa, hadi leo nawaza labda ni ule mchepuko ndo ulitia gundu, juzi umenipigia kuulizia gemu nyingine nasikia moyo mzito sana!