UKRISTO NA UISILAMU ni imani na ustaarabu ulio letwa na waarabu na wazungu, nia yao ilikuwa ni kututawala, walijua kuwa ukoloni wa kawaida unamwisho wake, wakabuni mbinu ya kutupatia dini zao, japokuwa hatutawaliwi tena, bado kiimani sisi ni watumwa wa wazungu na waarabu. Babu na bibi zetu hapo awali waliishi maisha ya amani, japo tunayabeza na kuyaita ya kishenzi. Walikuwa wakifanya ibada zao kwa mungu wasie mjua, lakini bado baraka na neema zilikuwa juu yao, hapakuwa na majanga kama wakati huu, magojwa yasiyo na tiba kama wakati huu, ukame na njaa kama wakati huu.
Pamoja na kujisifia na kupigania hizi imani za kikristo na kiisilamu, lakini Mungu hayupo nasi kabisa, Dunia imejaa dhambi na laana, magojwa yasiyo na tiba, kuaribika kwa maadili, wizi watu kijipenda na kujijali wenyewe, ukame na njaa. Tunadhani tukipigania dini tunamtetea Mungu kumbe wala hayupo nasi, tunaishi kwa mazoea tu.
Badala ya kubishania dini, ni bora kila mmoja na imani yake, kukaa na kutafakari, maisha tuliyo nayo yanakwenda wapi, kwanini tuko kama tulivyo, tujaribu kumtafuta Mungu, Kutubu kwa niaba ya nchi yetu na ulimwengu kwa ujumla ili Mungu aturehemu atuondolee majanga.
Ninaamini dini hizi mbili, zina mafundisho yanayo zungumzia amani na utulivu, ndugu zangu kama nilivyochangia awali, tusikubali Imani zetu zikatugombanisha, kwasababu ninaamini hatuta pata thawabu yeyote kutoka kwa huyo Mungu tunayedhani tunamtetea.