Tungekopa Ndege (Boeing, Airbus) tungefaidikaje?

Tungekopa Ndege (Boeing, Airbus) tungefaidikaje?

Nafikiri ukizungumzia issue ya Hospital na uboreshwaji wa huduma za afya nchini, ukarabati wa shule kongwe na kampeni kubwa ya madawati iliyokafanyika kipondi cha hayati basi tunapaswa kumpa sifa zake kuwa hapa alipaona zaidi.
Bro unaishi Tanzania kweli?
 
Duh..!! Kama we ni msomi basi Taifa lina safari ndefu. Kaa usubiri ajira brother.
Tatizo la kitaifa hili sijui tuwalaumu wakufunzi wamekuwa wakitoa wahitimu wa ajabu sana.
Hivi kwamfano kuna Kiongozi alipiga trip zaidi ya 300 safari nje ya nchi na huyu mbaya wao akapunguza matumizi ya safari za nje na hiyo chenji iliyobakia akawekeza ili azalishe faida kwaajili ya kuwahudumia wananchi anakuwa ametenda kosa? Hivi pesa hizo angeshindwa kulipia posho za wanufaika?
 
Hujatoa jibu, Hoja ya Aasad kupinga kununua ndege kwa Cash na ndiyo maana nauliza kwani tungekopa tungefaidika vipi zaidi ya tulivyozinunua?
Nitajibu hivi. Hata Assad naye amejichanganya. Hata tungekopa bado tungekuwa kwenye wakati mgumu tu. Kukopa na kununua hakuna tofauti kwani mwisho wa siku kote unalipa, tena mkopo utalipa na riba. Kukopa kuna manufaa iwapo biashara ingekuwa nzuri na faida itumike kulipa deni. Biashara ya kukopa ambayo haingizi faida bado ni kimeo tena hata kuliko kununua cash. Tulitakiwa kwanza tufanye upembuzi, je tunahitaji kufufua shirika letu? Na kama tunahitaji ni kwa namna gani? Biashara ya shirika la ndege ni ngumu na mashirika mengi yanafilisika kila mwaka. Kutia chumvu kwenye kidonda covid ndiyo ilisambaratisha kila kitu.
 
Ok nashukuru kwa ufafanuzi wako.
Basi kwa namna hii kumbe hakuna haja ata kupondea kununua Ndege Cash bali hoja iwe hatukuoaswa kuwa ndege za ATCL kwasasa.
Point kama ulivyoeleweshwa hapa ni kwamba;
1.Hatukupaswa kununua ndege bila uhakika wa biashara zake/soko.
2.Kibaya zaidi tukachukua hela cash ambayo ingetumika kwa kazi za muhimu kwenda kulipia ndege zisizozalisha. Ndani ya nyumba mna uhaba wa chakula na una hela benki, wakati unaelekea benki uko na mtoto wako wa miaka 5 anaona baiskeli ya kisasa analilia na wewe baada ya kudraw fedha unanunua baiskeli.
 
Kwanza ieleweke kwamba tungekuwa tumekopa yamkini tungekuwa na ndege moja mpaka leo hii.. pili ukikopa maana utalipa zaidi ya vile ulivyonunua cash na mwisho kabisa lini sehemu fulani ilikosa pesa yakuendesha mradi fulani kisa tu hizo hela zilienda kununulia ndege?
Niweke wazi msimamo wangu: ndege zilinunuwa kwa pupa bila upembuzi. Lakini pamoja na hayo wanaoponda huo ununuzi hawastahili kufanya hivyo kwa sababu walipokuwa kwenye madaraka hawakuweza kukusanya fedha zilizotumika kununua ndege na pia hawakufanya jingine lolote la ziada. Kwa kifupi ni bora hata tunaona ndege zisizo na faida kuliko fedha zingetafunwa kwa safari, vikao na mambo mengine mengi kama wakati wa Kikwete.
 
Habari za Asubuhi wadau..!
Kwa wakazi wa Dar es Salaam poleni na mvua.

Nimeona taarifa ya Prof: Mussa Assad aliyewahi kuwa CAG wa Tanzania juu ya taarifa yake ya kupondea ununuaji wa ndege kwa Cash, binafsi ile habari imefikirisha sana na naomba wanazengo leo mnisaidie kwa maswali yangu machache ambayo nafikiri yatasaidia ata member wengine humu ndani kupata elimu ya kile tunachokipondea ama kukitetea.

Kwanza nikiri wazi kuwa mimi ni muumini kindakindaki wa Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuli.

Maswali yangu ni haya hapa chini.

1. Tungeenda kukopa ndege zetu kwa
wanaotengeneza ndege (Boeing/ Airbus/
Bomberdier) tungefaidika vipi zaidi ya
tulivyozinunua kwa Cash?

2. Tungekodi Ndege kama ilivyokuwa zamani baada ya kuingia enzi za JK tukaingia ubia na Shirila la ndege la South Africa na mwisho wa siku tukabaki na madeni makubwa tukidaiwa na Shirika hilo kwa ATCL isingetucost?

Nafikiri maswali yangu aya machache yanajitosheleza kama ni bora kukopa au bora kukodi? Maana nimeona ata KQ imepata hasara zaidi ya Mabilioni ya Fedha japo wamekopa pia ndege zao.
You are biased and never will accept any other idea. It is always financially viable that leasing a high value capital asset (i.e. an airplane) is a preference to cash purchase.
 
Kwa kusema wewe ni muumini kindakindaki, ueleweshwaji wako utakuwa ni mgumu sana.
Itoshe kusema kuwa swala la ununuzi wa ndege halikuzingatia vitu vingi zaidi ya kurekebisha kejeli alizopewagwa jk kuwa kaua ATC.
Ilitakiwa research ifanyike jinsi makampuni mengine ya usafiri wa anga yanavyofanya hadi kutengeneza faida.


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu point in kwamba kwa nchi yetu Tanzania ambayo bado in masikini kuanzisha mradi Wa ndege ni sawa na maskini Wa huko kigoma kulazimisha kutembelea v8 wakati hana uhakika Wa kula Milo mitatu kwa siku ...

Kukopa isingetufaidisha ...

Kukodisha isingetufaidisha...


Hapa issue ilikuwa kutengeneza mazingira rafiki ya kibiashara watu waje kuwekeza wenyewe nchini kwetu ,kw a safari za anga ....


Over
Correct. I support you. It is an intelligent answer.
 
Kwani kulikuwa kuna ulazima gani wa kununua hizo ndege? Wakati magufuli anaingia madarakani, Precision na fast jet walikuwa wanafanya vizuri sana kwenye soko la ndani!

Kwa nini tusingewekeza nguvu kubwa kuboresha/kujenga viwanja vingi vya ndege ili kuwavutia wawekezaji wengi zaidi? Tena ni kipindi hicho shirika letu la ATCL lilikuwa na ndege sijui mbili zile (mbovu mbovu) huku likiwa na wafanyakazi 200! Na hivyo kuifirisi tu nchi kwa kuwalipa wafanyakazi wasio fanya kazi!

Sasa mzee wako kwa kupenda sifa na kwa kutokupenda kushaurika au kujiridhisha kwanza, akakurupuka nakununua madege lukuki, likiwemo lile li dreamliner! Ona sasa zinavyo zalisha hasara!
Kabla ya kununua ndege, ATCL iliwahi kuingiza faida? Kama haikuwahi mlishauri nini?
 
Siku dream liner imenunuliwa nilicheka sana. Sikuamini kama vichwa vyote vile vinavyoongoza nchi havifahamu kama ule ulikuwa utoto au sijui nini!
Dream liner ,, kuitunza ni ghrama kubwa sana na tungefanyia biashara gani na B787! Dah! Ile ilikuwa kituko cha ajabu sana.
Lakini nimerudi kuwaunga mkono wanaotaka mabadiriko ya katiba kwani bila rais kuwa na madaraka makubwa kiasi kile asingefajiingiza kwenye huu mkenge.
Kama kweli mama ana nia njema na hii nchi ,,swala ni moja tu; KATIBA.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Good..!! Bajeti ya Wizara ya Afya unaifahamu? Kitu gani kilikwama mara baada ya ununuzi wa ndege nchini?
Kuanzia zahanati, vituo vya Afya, hospitali mpaka za rufaa hazina watumishi, dawa na vitendea kazi vya kutosha, rejea kauli ya Mzee Bigambo kwenye mazishi Chato mbele ya Rais na camera za tv za dunia nzima, na Rais mwenyewe baada ya kuwaapisha makatibu wakuu na manaibu Dar majuzi, upo hapo au utajitoa ufahamu?!
 
Tungekopa, ina maana hiyo cash tungetumia kufanyia mambo mengine ikiwemo kujenga miundombinu ya barabara, kuimarisha miundombinu ya huduma za kijamii kama shule, hospitali za afya n.k.

Tungekodi tungeendelea kulimbikiza madeni na kuendelea kupata hasara

Njia sahihi ni Serikali kuachana na umiliki na uendeshaji wa mashirika ya ndege

Serikali ibaki tu ku-regulate na kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wa sector hiyo
 
Habari za Asubuhi wadau..!
Kwa wakazi wa Dar es Salaam poleni na mvua.

Nimeona taarifa ya Prof: Mussa Assad aliyewahi kuwa CAG wa Tanzania juu ya taarifa yake ya kupondea ununuaji wa ndege kwa Cash, binafsi ile habari imefikirisha sana na naomba wanazengo leo mnisaidie kwa maswali yangu machache ambayo nafikiri yatasaidia ata member wengine humu ndani kupata elimu ya kile tunachokipondea ama kukitetea.

Kwanza nikiri wazi kuwa mimi ni muumini kindakindaki wa Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuli.

Maswali yangu ni haya hapa chini.

1. Tungeenda kukopa ndege zetu kwa
wanaotengeneza ndege (Boeing/ Airbus/
Bomberdier) tungefaidika vipi zaidi ya
tulivyozinunua kwa Cash?

2. Tungekodi Ndege kama ilivyokuwa zamani baada ya kuingia enzi za JK tukaingia ubia na Shirila la ndege la South Africa na mwisho wa siku tukabaki na madeni makubwa tukidaiwa na Shirika hilo kwa ATCL isingetucost?

Nafikiri maswali yangu aya machache yanajitosheleza kama ni bora kukopa au bora kukodi? Maana nimeona ata KQ imepata hasara zaidi ya Mabilioni ya Fedha japo wamekopa pia ndege zao.
Kukopa 1. Mnagawana risk na muuzaji lolote likitokea, ndege kuharibika, kuanguka au biashara kugoma kama kipindi hiki cha covid19
2. Unaanza kuingiza pesa kule unalipa polepole na huku unagharimia mahitaji mengine ya ndani.
 
Sio hatukapaswa tu kuwa na ndege za ATCL kwa SASA. Hatakupaswa kabisa kufanya hiyo biashara kichaa. Hiyo ni biashara ya sekta binafsi.
Ok nashukuru kwa ufafanuzi wako.
Basi kwa namna hii kumbe hakuna haja ata kupondea kununua Ndege Cash bali hoja iwe hatukuoaswa kuwa ndege za ATCL kwasasa.
 
Mzee wa Chato alimwambia Rais hospitali hazina madawa.
Good..!! Bajeti ya Wizara ya Afya unaifahamu? Kitu gani kilikwama mara baada ya ununuzi wa ndege nchini?
 
Hii nchi ya ajabu sana. Yani kuna mambwiga hayaelewi vitu vyepesi kama hivi !
Ngoja nikujibu kijana wangu. Kwanza lazima ujue tuna manunuzi ya aina mbili tu, CASH na CREDIT na nikuweke wazi CREDIT Purchase sio LOAN hapa namaanisha kuna tofauti kubwa sana kati ya MKOPO (LOAN), na kununua kwa MKOPO (CREDIT) nimetaka kwanza uelewe nadharia hizo mbili ili niwekapo faida za kununua kwa mkopo uelewe. Pili lazima ujue kuna vitu lazima ununue kwa CASH kama NCHI na vingine lazima UNUNUE KWA CREDIT kama NCHI. Miradi yote mikubwa huwezi fanya kwa CASH hii ni kwa sababu kuna daily activities ambazo governments ina run hivyo ili kubalance purchasing power ya nchi miradi mikubwa unakopa ili pesa yako iliyopo cash unaiingiza kwenye mzunguko wa uchumi wako ambapo sasa itakufanya uchumi ukue na uweze kukusanya pesa kuweza kulipa lile deni wakati huo wananchi hawafeel economic hardship. Pesa ambazo umenunua ndege CASH zingepelekwa kwenye maboresho ya shule zetu au zahanati zetu ungeona impact katika uchumi wetu kwani watu wangepata huduma muhimu wakati huo serikali inaangalia kwa kina ile biashara kama inafaa kuendelea nayo au la. Wakati pesa hizo unanunua ndege kumbuka hata akiba ya pesa za kigeni unapunguza kwa wingi kwenye akiba yako hivyo kupunguza purchasing power ya nchi yetu. Umeeona hata suala la sukari lilituzidi nguvu? Ni kwakuwa hatukuwa na akiba ya kutosha kuagiza bidhaa hiyo muhimu badala yake tulinunua NDEGE. HIVYO MIRADI YOTE MIKUBWA KIUCHUMI UNASHAURIWA KUNUNUA KWA CREDIT TU ILI KUONDOA VIKWAZO KATIKA MZUNGUKO WA PESA KATIKA NCHI YAKO.
NIMEJARIBU KUKUELEZA KWA UFUPI SANA NA NAIMANI UTAELEWA.
 
Back
Top Bottom