Mpinzire
JF-Expert Member
- Jan 18, 2013
- 7,845
- 14,071
Habari za Asubuhi wadau!
Kwa wakazi wa Dar es Salaam poleni na mvua.
Nimeona taarifa ya Prof: Mussa Assad aliyewahi kuwa CAG wa Tanzania juu ya taarifa yake ya kupondea ununuaji wa ndege kwa Cash, binafsi ile habari imefikirisha sana na naomba wanazengo leo mnisaidie kwa maswali yangu machache ambayo nafikiri yatasaidia ata member wengine humu ndani kupata elimu ya kile tunachokipondea ama kukitetea.
Kwanza nikiri wazi kuwa mimi ni muumini kindakindaki wa Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuli.
Maswali yangu ni haya hapa chini.
1. Tungeenda kukopa ndege zetu kwa wanaotengeneza ndege (Boeing/ Airbus/ Bomberdier) tungefaidika vipi zaidi ya tulivyozinunua kwa Cash?
2. Tungekodi Ndege kama ilivyokuwa zamani baada ya kuingia enzi za JK tukaingia ubia na Shirila la ndege la South Africa na mwisho wa siku tukabaki na madeni makubwa tukidaiwa na Shirika hilo kwa ATCL isingetucost?
Nafikiri maswali yangu aya machache yanajitosheleza kama ni bora kukopa au bora kukodi? Maana nimeona ata KQ imepata hasara zaidi ya Mabilioni ya Fedha japo wamekopa pia ndege zao.
Kwa wakazi wa Dar es Salaam poleni na mvua.
Nimeona taarifa ya Prof: Mussa Assad aliyewahi kuwa CAG wa Tanzania juu ya taarifa yake ya kupondea ununuaji wa ndege kwa Cash, binafsi ile habari imefikirisha sana na naomba wanazengo leo mnisaidie kwa maswali yangu machache ambayo nafikiri yatasaidia ata member wengine humu ndani kupata elimu ya kile tunachokipondea ama kukitetea.
Kwanza nikiri wazi kuwa mimi ni muumini kindakindaki wa Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuli.
Maswali yangu ni haya hapa chini.
1. Tungeenda kukopa ndege zetu kwa wanaotengeneza ndege (Boeing/ Airbus/ Bomberdier) tungefaidika vipi zaidi ya tulivyozinunua kwa Cash?
2. Tungekodi Ndege kama ilivyokuwa zamani baada ya kuingia enzi za JK tukaingia ubia na Shirila la ndege la South Africa na mwisho wa siku tukabaki na madeni makubwa tukidaiwa na Shirika hilo kwa ATCL isingetucost?
Nafikiri maswali yangu aya machache yanajitosheleza kama ni bora kukopa au bora kukodi? Maana nimeona ata KQ imepata hasara zaidi ya Mabilioni ya Fedha japo wamekopa pia ndege zao.