China yaweza kutembea kifua mbele na kuingia kwenye ushindani na makampuni ya kutengeneza ndege kama vile Boeing na Airbus

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111439263658.jpg


Sekta ya utengenezaji ya China imekuwa ikipewa kipaumbele na kuangaliwa kwa jicho la kuona mbali tangu kuwepo kwa utawala wa Chama cha Kikomunisti cha China. Kitakwimu pato la jumla la viwanda vya utengezaji mara nyingi limekua kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10 kila mwaka, na nguvu kazi ya sekta hii nchini China pengine inazidi jumla ya nchi nyingine zote zinazoendelea ikichanganywa pamoja. Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba sekta ya utengenezaji ya China imepita sekta nyingine zote katika ukuaji wa uchumi na kiwango cha kisasa.

Kupitia sekta hii ya utengenezaji, China sasa inaweza kutembea kifua mbele huku ikiweza kuingia kwenye ushindani na makampuni makubwa ya kutengeneza ndege kama vile Boeing na Airbus kwenye soko la ndege la kimataifa, baada ya kufanikiwa kutengeneza ndege yake ya kwanza kwenye historia ya China, na kuweka alama ya kuingia hatua mpya na ya juu ya kutengeneza ndege yake yenyewe ya abiria.

Baada ya Shirika la Biashara la Usafiri wa Anga la China, kutengeneza ndege aina ya C919 na ARJ21, mwaka huu ndege hiyo ya C919 ilianza kufanyiwa majaribio kadhaa na kufaulu vizuri tu kwenye majaribio yake. Katika safari zake za majaribio ndege hiyo ilibeba takriban abiria 130, ikapaa kutoka uwanja wa Ndege wa Shanghai Hongqiao na kutua chini ya saa mbili baadaye hapa mjini Beijing.

Mfanikio hayo yametoa matumaini na imani kubwa kwa kampuni hiyo kutengeneza ndege nyingi zaidi, ambapo kila mwaka inapanga kutengeneza jumla ya ndege 150 za C919. Habari njema ni kwamba hadi hivi sasa oda ilizopokea Shirika la Biashara la Usafiri wa Anga la China ambalo linatengeneza ndege zitakazosafiri katika maeneo mbalimbali kuanzia safari za kikanda, ndege za mwendo mfupi mwendo wa kati zenye mwili mwembamba, hadi miili mipana za masafa marefu, zimefikia 1,061. Wakati huohuo jumla ya ndege 112 za ARJ21, ndege ya kwanza ya kikanda kutengenezwa na China, zimeanza kutumika, na idadi ya oda imefikia 775.

Sekta hii ya utengezaji ya China sasa imepanua mbawa zake hadi kwenye utengenezaji wa meli za kifahari za kitalii ‘cruise ship’, ambapo meli yake ya kwanza kubwa kabisa iliyotengeneza kwa nguvu na jasho lake ijulikanayo kama ‘Adora Magic City’, imeanza safari yake ya pili na ya mwisho ya majaribio Alhamis 7, 2023 ili kuangalia utendaji wake na kama inaweza kuaminika na kutegemewa.

Kwa mujibu wa Yang Xin, Naibu Mkuu wa Idara ya Mradi wa Meli za Kifahari wa Kampuni ya Kutengeneza Meli ya Shanghai Waigaoqiao (SWS), meli hii ya kifahari ya Adora Magic City ina sehemu nyingi za kazi zikiwemo kutoa huduma za upishi, burudani, starehe na malazi kwa abiria, na vile vile ina zaidi ya vyumba 2,000 vya aina tofauti.

Hatua hii iliyopiga China inapaswa kupongezwa sana kwani utengenezaji wa vyombo vya usafiri wa baharini ni miongoni mwa sekta tata na ngumu zaidi, ambapo ni nchi tano pekee ndio zinajikita na kazi hii ya kuzitengeneza zikiwemo China, Ujerumani, Ufaransa, Italia na Finland na kuwa na uwezo wa kuwasilisha.

Sekta hii ya utengenezaji ya China imekuwa chachu kubwa kwa nchi nyingine za nje hasa nchi za Afrika, kwani kupitia miradi ya ujenzi mathalan ya reli, hasa reli ya mwendo kasi SGR, nchi hizi za Afrika pia zimenufaika sana. Ikizingatiwa kwamba China ni rafiki mwema wa Afrika, tuna imani kwamba bidhaa hizi zinazotengezwa na China zikiwemo ndege na meli za kifahari za kitalii zitafika katika nchi za Afrika na kupatikana kwa bei nafuu kama zinavyopatikana bidhaa nyingine muhimu.
 
View attachment 2756535

Sekta ya utengenezaji ya China imekuwa ikipewa kipaumbele na kuangaliwa kwa jicho la kuona mbali tangu kuwepo kwa utawala wa Chama cha Kikomunisti cha China. Kitakwimu pato la jumla la viwanda vya utengezaji mara nyingi limekua kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10 kila mwaka, na nguvu kazi ya sekta hii nchini China pengine inazidi jumla ya nchi hari za kitalii zitafika katika nchi za Afrika na kupatikana kwa bei nafuu kama zinavyopatikana bidhaa nyingine muhimu.
Ni kweli Airbus na Boing watapewa changamoto ya kipekee sana kibiashara na China, na haya ni matokeo ya uwekezaji, ubunifu , ugunduzi, mipango na maono ya mbali sana ya china kitechnoligia kwa siku za usoni.
 
Sawa, lakini kutangulia siyo kufika
kweli mkuu,kikubwa juhudi katika utendaji,na kujifunza,.ukitaka kujua vizuri china imetokaje,angalia documentary ya televisheni yao ya taifa,inaitwa CHINA REINVENT ITS SELF..ipo youtube,mle ndio nimeheshimu wazungu,.wasomi wakubwa wa china karibu 90% wamesoma USA na ulaya
 
Back
Top Bottom