Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,989
Mkazi wa Kijiji cha Namiungo, Wilaya ya Tunduru, Mohamed Saudi Ngwelekwe mwenye umri wa miaka 25 amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia kumlawiti mwanaye wa kumzaa mvulana wa miaka minne.
Hukumu hiyo imetolewa tarehe 03.03.2023 mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Tunduru, Honorius Kando. Mtoto huyo ameeleza kuwa kila alipokuwa anakataa kufanyiwa kitendo hicho, baba yake mzazi alikuwa anamng'ata na kumpiga na kumtishia.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro amelipongeza Jeshi la Polisi wilayani humo kupitia Kitengo cha Dawati la Jinsia kwa jitihada walizozifanya tangu Serikali ilipopata taarifa hizo.
DC Mtatiro amesema mtoto huyo (hamtaji jina) amefanyiwa kitendo hicho kwa muda mrefu na inasikitisha.
Mtatiro amewaasa wananchi wa Tunduru popote pale walipo kutoa taarifa Serikalini kila wanapobaini vitendo vya kikatili dhidi ya Watoto kwani vitendo hivyo vinahatarisha maadili na maisha ya kizazi kijacho.
Mtuhumiwa Mohamed Saudi Ngwelekwe ambaye kwa sasa ameanza kifungo chake
Hukumu hiyo imetolewa tarehe 03.03.2023 mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Tunduru, Honorius Kando. Mtoto huyo ameeleza kuwa kila alipokuwa anakataa kufanyiwa kitendo hicho, baba yake mzazi alikuwa anamng'ata na kumpiga na kumtishia.
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro amelipongeza Jeshi la Polisi wilayani humo kupitia Kitengo cha Dawati la Jinsia kwa jitihada walizozifanya tangu Serikali ilipopata taarifa hizo.
DC Mtatiro amesema mtoto huyo (hamtaji jina) amefanyiwa kitendo hicho kwa muda mrefu na inasikitisha.
Mtatiro amewaasa wananchi wa Tunduru popote pale walipo kutoa taarifa Serikalini kila wanapobaini vitendo vya kikatili dhidi ya Watoto kwani vitendo hivyo vinahatarisha maadili na maisha ya kizazi kijacho.