Baada ya TUNDU LISU kupigwa risasi bila Shaka damu yake ilimwagika sana, alipigwa, tena alipigwa risasi nyingi mno, hakika aliusikilizia mwili wake vyuma vya moto vikiingia mwilini. Hakika vile vyuma viliuchana mwili wake mithili ya NYAMA bucha. Aliyemimina RISASI alizimimina Kweli Kweli, alimimina kwa lengo la kuua, kwa lengo la kutoa roho, kwa lengo la kuiangamiza NAFSI iliyohai, alivaa sura, sura ya kutenganisha nafsi, mwili, na Roho.
Lakini LISU alipona, yupo hai, anavuta pumzi, pumzi ya Baba wa mbinguni, Mungu aliye hai, yawezekana alikosa, tena Kosa kubwa, yawezekana ni msaliti, muongo, mwizi, mhalifu asiyesameheka, yawezekana, hafai kabisa. Lakini cha ajabu asiyefaa amepona kwa jinsi ya ajabu, kwa namna tusiyoijua, maana kanuni ya uhai ni fumbo.
Nakumbuka wakati nikiwa mdogo miaka ya sabini pale kurasini shimo la udongo, wakati eneo lile lilijaa mikorosho mingi sana, haukuwa mji kama Leo. Enzi za Mzee bongo Lolo. Nakumbuka watu walipiga mwizi, walikuwa mamia ya watu, na yule mwizi alipigika hasa, mwili wote ulijaa damu, walimwacha waliamini amekufanya, walimwacha, kila mtu alirudi nyumbani kwake, baada sisi wadogo tulishuhudia Yule mwizi akiinuka, damu ilikuwa imejaa hata USO haukuonekana, alianguka tena chini, msamalia mmoja alimsaidia kusimama, akitia huruma SANA sijui kama alipona.
Inawezekana LISU ni alama tusiyoijua, ni ujumbe tusioujua, maana sisi tu wanadamu. Kwani wangapi tunawaombea mabaya? Wangapi tunatamani wafe, kwa sababu tunahisi ni vikwazo kwenye maisha yetu? Ila hatuna bunduki? LISU survived, NI mzima, mwache aombe, aombe, mwache roho na nafsi yake vihangaike, tumwache, hakuna anayejua mwisho wake, kuna watu walimuombea vibaya LOWASA Leo hawapo, kuna watu wanamuombia raisi mabaya sisi wanadamu tuna roho ngumu SANA. Mwacheni LISU ahangaike, mwacheni. Kupona kwake ni nafuu kwa familia yake, hapo NDIPO tumaini lake lilipo. Pia tuache USHABIKI.