Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Watu sijui wanawazaga nini na kawaza kabisa kurekodi na ile inaonekana ni zile kamera za siri sio simu
Kuna miwani
Kuna vifungo
Kuna urembo
Vyote hivi unaweza kuvifunga secret cameras
 
Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Sasa mnaanza kutetea sera zake,mnaanza kukusanya hoja ambazo kimsingi alizifanyia kazi kwa matendo .Mlipokosa hoja kutokana na jemedari kuzifuta kwa matendo mkasingizia uhuru wa habari,mara kwa sababu hakuna Bunge live.Najua kwa sasa zinakusanywa data za garama ya msiba na kuwasilishwa Ubelgiji ili mpate pa kuanzia.
Bahati mbaya msiba huu nguvu yake ni kubwa sana,hivyo itapidi tu mchukue hiyo hoja ikae kwenye makabrasha ya ubelgiji.
 
Mie ninayo,
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Iko format ya gif, watu maspai. Huyu jamaa aliweka kamera kwenye mfuko wa shati nafikiri, mzee kalala kabisa na miwazi zake kwenye jeneza.
Ngoja niku zoom
 
Cha kushangaza haya maneno yapo tu humu mitandaoni ila mitaani huku akuna anaethubutu kupaza sauti yake kusema lolote.

Nyuma ya keyboard wengi wanamkosoa sana marehemu lakini kila nikijaribu kuangalia idadi ya watu wanaoaga najifunza kitu. Acheni watu wamuage mpendwa wao(kila mtu akiri upendo/chuki binafsi mwenyewe ndani yake). Acha watu waage ndio nafasi ya mwisho kwao.
 
Playtime ni ya muda gani? Visibility je?
Hii niliyonayo ni ndogo sana, waliiformat kwenda gif na imecapture the actual moment yaani pale anafika mbele ya mwili na kuinama hivyo mzee kaonekana vizuri tu ndani ya jeneza...muda ni mchache sana. Sekunde kama 3 hivi..aliyerekodi atakua na clip ndefu toka anaiseti alikotoka ila hapa atakua amei-crop kwenye moment. Visibility iko super..
 
Hii niliyonayo ni ndogo sana, waliiformat kwenda gif na imecapture the actual moment yaani pale anafika mbele ya mwili na kuinama hivyo mzee kaonekana vizuri tu ndani ya jeneza...muda ni mchache sana. Sekunde kama 3 hivi..aliyerekodi atakua na clip ndefu toka anaiseti alikotoka ila hapa atakua amei-crop kwenye moment. Visibility iko super..
Katumia super spy cam
 
 
Back
Top Bottom