Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake
Lakini isifike mahari tukakufuru”
 
Hatukosoi utaratibu wa imani fulani, bali utaratibu wa kisiasa. Na kukosoa au kuwa na mtazamo tofauti kisiasa au hata kijamii si dhambi
Utofauti wa kisiasa mpaka kwenye misiba?

Au kisiasa mtu akifa anatakiwa kuzikwa vipi?Manake mimi ndio nasikia leo MTU KUZIKWA KWA UTARATIBU WA KISIASA.

Kabisa kuwa na mtizamo tofauti ya kisiasa si dhambi,ila usitake uharibu taratibu za kiimani za marehemu kwa sababu zako za kisiasa ambazo hazina maana,kwani hii shughuli ni ya KIROHO na si KISIASA.
 
Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Kwani unateseka? lini ulisikia aliyefariki anatesekaga? we poyoyo sana wewe.
 
Kama una uchungu na fedha twambie bil. >200 za Tegeta Escrow zilifanya kazi gani?
 
Mkuu huu ni msiba wa aina yake unalipata taifa letu kwa mara ya kwanza, kuondokewa na Rais aliyepo madarakani. Hivyo lazima kuwe na sintofaham za hapa na pale.

Lakini pia huyu ni Jemedari aliyekua anaahirisha baadhi ya sikukuu za kitaifa kuokoa matumizi na gharama zisizo na ulazima, sifikirii angekuwepo angeliafiki hili.

Kwangu kubwa na la hatari zaidi ni kutokuona kuzingatiwa kwa tahadhari za Covid kwenye hili zoezi, hasa kwa viongozi wetu...tunasahau mapema sana.
Ya watanzania...aliowapenda jpm.
 
The picture is real heartbreaking
Screenshot_20210321-202650.jpg
 
Maafa ya leo...Misiba mikubwa maafa hayakosekani..poleni wafiwa
TANZIA!
TUNASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MWALIMU JANE NGONDE (MWALIMU MKUU WA S.M MGEULE) KILICHOTOKEA LEO MCHANA UWANJA WA BENJAMIN MKAPA ALIPOKUWA AKISHIRIKI KUTOA SALAMU ZA MWISHO. TARATIBU ZA MAZISHI ZINAFANYIKA NA TUTAENDELEA KUJULISHANA. AIDHA TUNAITAARIFU KAMATI YA MAAFA- UVEMI KUENDELEA NA TARATIBU ZETU. R. I.P
Screenshot_20210321-201552.jpg
 
TANZIA
Habari za jioni Mates mwenzetu Mbasa Mtua amepata msiba mkubwa sana kwa kumpoteza mwanae mmoja watoto wa mdogo wake watatu na mtoto wa kaka yake mmoja baada ya kukanyagwa uwanja wa Taifa walipokwenda kumuaga JPM,na hadi sasa hawajui house girl yuko wapi,watoto waliongozana na mke wa mdogo wake,msiba uko kimara nyumbani kwao,tuwaombee wako kwenye wakati mgumu sana,mwenyezi mungu awapumzishe kwa Amani[emoji120]
 
Naona nikuache na msimamo wako unaoona utaratibu wa maombolezo hauongozwi na serikali. Mimi naona unaongozwa na serikali yenye wanasiasa.

Naheshimu sana mtazamo wako hata kama sikubaliani nao. Una haki na uhuru wa kushikilia msimamo huo, ila usitake kila mtu aone kama unavyoona.
Utofauti wa kisiasa mpaka kwenye misiba?

Au kisiasa mtu akifa anatakiwa kuzikwa vipi?Manake mimi ndio nasikia leo MTU KUZIKWA KWA UTARATIBU WA KISIASA.

Kabisa kuwa na mtizamo tofauti ya kisiasa si dhambi,ila usitake uharibu taratibu za kiimani za marehemu kwa sababu zako za kisiasa ambazo hazina maana,kwani hii shughuli ni ya KIROHO na si KISIASA.
 
Haya sasa, msiba umeleta misiba!
Maafa ya leo...Misiba mikubwa maafa hayakosekani..poleni wafiwa
TANZIA!
TUNASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MWALIMU JANE NGONDE (MWALIMU MKUU WA S.M MGEULE) KILICHOTOKEA LEO MCHANA UWANJA WA BENJAMIN MKAPA ALIPOKUWA AKISHIRIKI KUTOA SALAMU ZA MWISHO. TARATIBU ZA MAZISHI ZINAFANYIKA NA TUTAENDELEA KUJULISHANA. AIDHA TUNAITAARIFU KAMATI YA MAAFA- UVEMI KUENDELEA NA TARATIBU ZETU. R. I.PView attachment 1731161
 
Poleni sana wafiwa!
TANZIA
Habari za jioni Mates mwenzetu Mbasa Mtua amepata msiba mkubwa sana kwa kumpoteza mwanae mmoja watoto wa mdogo wake watatu na mtoto wa kaka yake mmoja baada ya kukanyagwa uwanja wa Taifa walipokwenda kumuaga JPM,na hadi sasa hawajui house girl yuko wapi,watoto waliongozana na mke wa mdogo wake,msiba uko kimara nyumbani kwao,tuwaombee wako kwenye wakati mgumu sana,mwenyezi mungu awapumzishe kwa Amani[emoji120]
 
Mawazo kweli ni mazuri, ilaaaaa..Wacha wapige hakuna shida. Hata alipokuepo DR bado hamkukubali alichofanya sasa leo hayupo wacha wapige wapigaji. Binadam hatueleweki nini twataka.
 
Back
Top Bottom