Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Mimi ni Mkristo lakini nakubaliana asilimia zote na Uislamu katika kipengele cha kumhifadhi Marehemu,hiki kinachoendelea ni kumdhalilisha tu Marehemu. Mtu akisha fariki kinachofuata ni kumzika tu,hizi drama zingine hazina mantiki kabisa. Namsikitikia sana Mjane,atateseka sana hadi hiyo Ijumaa.
Yaani kuna mapopoma hawaelewi kabisa katika hili ... Anakokotwa kutoka mwanza to chato hiiiii kama km200 flani na kitorori aseee ... Ni unyama kiwango cha lami
 
Moja katika mambo mazuri katika dini ya Kiislamu ni hili la mazishi. Nawapa pongezi ndugu zangu waislamu katika hili
Leoo hii jpm angekuwa muislamu haya yote usingeyaina angeshazikwa na mambo mengine yangekuwa yanaendelea muda huu.
Hata yale inasemwa alikufa siku nyingi ila haikutangazwa mapema ingekuwa kwa ndugu zetu waislamu kamwe hilo lisingetokea
waislamu wako smart sana kwa kweli, hawa mataga wanadhani sijui ataamka ??
 
waislamu wako smart sana kwa kweli, hawa mataga wanadhani sijui ataamka ??
Angalia Maalim Seif.
Hakuna kuchelewa.
Waislam wamefundishwa mambo matatu yafanyike kwa haraka sana.
1. Kuzika
2. Kufunga ndoa
3. Kumsilimisha anayehitaji kuwa Muislam
 
Tungemcremenate tu majivu yakakaaa ikulu ...
Sasa nalopinga ni usambazaji wa koona tu.

Mwanzo nami nilikuwa na mwelekeo wa kutounga mkono zoezi hili ila nikajiuliza - kama nduguze wameafiki mi nani kupinga? Sababu serikali inafuata matakwa ya ndugu, wanaomwakilisha mwendazake. Mwanae na mdogo wa marehemu wapo sambamba na msafara.
 
Tangu lini mshana jr akaongea zuri la Magufuli?
Inawawauma nini?
Kunyweni sana mfurahi muwaache wanaotaka kumuona japo jeneza lake
 
Kusema kweli hii kitu ni pointless kabisa. Uongozi uliobaki wamedhihirisha kuwa nao bado ni malimbukeni tu.

Haiwezekani kufanya mikusanyiko mikubwa namna hiyo bila kujali uhalisia wa janga la covid-19.

Watu tungeangalia shughuli kupitia kwenye TV na kusikiliza kwenye radio ingetosha. Hakukuwa na haja ya haya yote. Kwanza ni gharama kubwa tu zinatumika na zinaongeza mzigo kwenye kodi za wanaoitwa wanyonge.

Mimi kwangu haileti tofauti kuwa ameagwa na watu wengi au hajaagwa kabisa. Mtu akishakufa amekufa tu hata akiagwa na dunia nzima haimsaidii chochote.

Wangempumzisha tu tuendelee na maisha.

NB: In the end all the people you know (including you) will die.
Huey said to Jasmine...
 
Back
Top Bottom