Tunaanza na Tume Huru Kwanza

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.
Tume ya Nyalali ilisema '' ni lazima kwanza kuwe na Tume huru ya uchaguzi na kuandikwa katiba mpya''. ACT wanakubali mambo hayo yanaenda sambamba!
Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!
Jeshi la Polisi linaingiaje kwenye mambo ya siasa? Kazi ya jeshi ni kusimamia sheria za nchi.
''Kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika''. Kule Zanzibar kumefanyika miafaka mingapi na hali ipoje leo hii. Kuna utayari gani kwa CCM waliopora chaguzi! utayari wanaozungumzia ACT ni upi huo
Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.
ACT wanaamini kukiwa na Tume huru basi Wabunge watachaguliwa kwa uhuru.
Hapa ndipo ninapoona ACT wana tatizo la kufikiri. Hivi si waliwahi kuwa na Tume huru Zanzibar?
Kwa mamlaka gani Jecha aliharibu uchaguzi alioshinda Maalim?
ACT hawakumbuki Jecha aliondolewaje, alipelekwa wapi na aliamriwa aseme nini?

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.
Tume huru haina uhusiano na uhuni unaofanywa. Mtu akiporwa Form si tatizo la tume ni uvunjaji wa sheria na wahusika ni Polisi. Hujuma za mawakala si tatizo la tume ni uratibu wa CCM, Polisi na vyombo vya usalama.
3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.
Tunarudi pale pale kwamba wao wanaamini uchaguzi unahujumiwa na Tume. Hawana habari kuwa uratibu wa hujuma za uchaguzi ni wa mfumo mzima.
4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.
Kule kule wanaamini Tume huru itamaliza tatizo la uhuni. Hawakumbuki Jecha alifanya nini kwa msaada wa nani na kwanini hakukuwepo na hatua dhidi yake. Si Jecha alikuwa na Tume huruiliyowashirikisha CUF ambao ni ACT
ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.
Katiba pendekezwa iliandikwa na CCM, kusema kwamba maoni ya Tume ya Warioba yachanganywe na uhuni wa CCM ni ku adulterate maoni ya Wananchi.
ACT Katiba pendekezwa ni mali ya CCM. Wananchi wanataka kurudi ktk Tume ya Warioba
Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.
Kumbe tayari kuna sheria imeandaliwa!!
3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.
Kwanini Rais awe na mkono wa uteuzi? Rais anatakiwa aidhinishe jina. Rejea tume ya uchaguzi ya Ghana. Rais hana mamlaka yoyote ya kuteua majina au kupewa lundo la ma
Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.
Forget about katiba pendekezwa. Turudi kwa Rasimu ya Warioba.
ACT hii katiba pendekezwa iliandikwa na CCM
Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.
ACT katiba pendekezwa iliandikwa na CCM na haihitaji maboresho yoyote. Hii ilifuta maoni ya Tume ya Warioba ambayo ni maoni ya wananchi. Katiba pendekezwa si maoni ya Watanzani, ni Bunge la CCM.
Ninatilia shaka uelewa wa ACT Wazalendo! kuna tatizo kubwa wanajitahidi kulisukuma mbele
Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Huwezi kuwa na Tume huru ya uchaguzi katika mfumo wa dhulma ACT!

Kuna tatizo kubwa sana na nadhani kuna kitu kipo nyuma! mtakuja baini ikiwa ni too late

ACT na CCM wanaserikali ya pamoja kule Zanzibar, huku bara hatuna GNU na ACT wasijaribu kututumbukiza katika matatizo hayo. Kuna motive behind , ipo siku watu wataelewa tunamaanisha nini. Kuna kitu!
 
Tatizo linaanza hapo kwenye Kamati ya Uteuzi wa Tume maana karibu wote wanaopendekezwa wameishakuwa au wanaweza kuwa compromised katika mazingira ya sasa. Ndio maana watu wanadai Katiba Mpya ambayo itaruhusu uundaji wa Kamati ambayo wananchi watakuwa wana imani kuwa haiegemei upande wowote.
Ni bora kusubiri kuliko kuunda Tume ambayo italeta matokeo yale yale ya 2020 ingawa labda safari hii hawatarudia kosa la kukipa chama kimoja ushindi wa 99%. Wapinzani wenye staha watapewa viti vya kutosha kuunda Kambi Rasmi ya Upinzani na hivyo kuweza kudai kuwa hata Katiba itakayopendekeza itakuwa na uhalali.

Amandla...
Wasi wasi wa ACT ni kuwa kuna uchaguzi wa serikali za mitaa 2024. ACT wanaamini watashinda chaguzi hizo. Hivi wakipata viti 5000 dhidi ya 40,000 kuna maana gani?
ACT wanaamini kuna uchaguzi 2025 na Tume huruikiwepo watashinda. Hivi wakishinda viti 50 vya ubunge dhidi ya 200 vya CCM wataleta mabadiliko gani? Hapo si ndipo watapiga mhuri kwa CCM kufanya mauza uza yao.

Kosa la ACT ni lile walilofanya Chadema mwaka 2010. JK alitangaza kuanzishwa mchakato wa katiba mpya. CDM wakasema Rais amefanya jambo jema na Wamefarijika. Tuliwaambi kuwa hiyo si njia sahihi, mchakato ulitakiwa uanzie Bungeni ili waweze kuuratibu

Matokeo yake mchakato ukawa mali ya 'Rais' na matokeo yake tunayajua
Hilo ndilo kosa la ACT kutaka Tume huru na Wajumbe wake wapatikane kwa mazingira ya sasa

Haraka ni ya nini ACT?
 
Nimesoma Hoja za ACT ni nzuri na zinaeleweka shida ya Chadema ni wanataka Katiba mpya kama wimbo ila hawajaleta hoja za ushawishi kwanini Katiba mpya

ACT wamesema Tume huru kwanza na wametoa sababu

Chadema njooni na sababu kwanini Katiba mpya kwanza

Hapa itaturahisishia kupima kipi kianze, hoja zitoke kwenye Uongozi wa Chama sio kwa watukanaji mitandaoni
 
Wafuasi wa kilichokuwa chama kikuu cha upinzani wanavyoushambulia uzi wa ACT wazalendo ni dhahiri wanatambua 2025 hali ni mbaya kwao.
Mtake msitake 2025 ACT wazalendo wanakwenda kupata wabunge wengi
Labda Pemba
 
Ndio maana nasema ACT wazalendo sijui kama wanajua tatizo ni nini!

Laiti wangalikuwa na kumbukumbu japo 25% yaliyotokea Zanzibar wasingejiunga na hatua ya Msajili hata kwa bahati mbaya. Sielewi kuna pipi gani wamepewa

Kinachoharibu uchaguzi si Tume ya uchaguzi. Mfumo mzima ni mbovu.

Dola inatumika kikamilifu. Zitto ana imani Msajili wa vyama aliyekaa kimya Kenan Kihongosi wa UVCCM akitoa matamshi ya mauaji, atakaa kimya kwa mwanachama wa ACT! Chama kitafutwa siku hiyo hiyo

Msajili aliyeshiriki ''kuua CUF'' ndiye huyo huyo leo wana 'dance' na ACT wazalendo.
ACT wanaamini ana nia njema na mchakato

Polisi walimkamata Zitto akifanya mkutano halali Lindi , ACT wanaamini tume huru Polisi hawataMkamata tena!

Wagombea wananyang'anywa form mbele ya Polisi ACT wanadhani hayatatokea kukiwa na tume huru. ACT wamegombea kila kiti hakuna walichoambulia zaidi ya vipigo, leo wapo meza moja na waporaji wakipanga mipango ya tume huru ya uchaguzi!! kama si kioja sijui

Orodha ni ndefu inatosha kuwaambi hujuma za uchaguzi ni za kimfumo si tume peke yake.

Zanzibar ilikuwa na Tume huru wakiwemo CUF wakaporwa uchaguzi na Jecha na vyombo vya dola. ACT ambao ni CUF wanadhani tume huru ina matokeo tofauti ni ile iliyowapora uchaguzi

Kufanya jambo lile lile kwa namna ile ile ukitegemea matokeo tofauti ni definition ya Insanity

Kwahili siamini kama ACT hawafahamu! nadhani kuna pipi wanapewa , let's hope that I'm wrong

Msoud Othman wa ACT aliacha kuwa AG akitetea Katiba mpya na Zanzibar yenye mamlaka! Kapewa ving'ora hakumbuki yaliyompa Maalim, kama si usaliti sijui ni nini

ACT mna feli na mnafelisha Taifa, hamna hoja. Ushirika wenu na CCM una madhara makubwa sana kwa Taifa hili. ACT si chama kikubwa bara lakini visiwani ni kikubwa

ACT acheni huu uzumbukuku, kumbukeni ya nyuma! msitumike kirahisi haina tija kwa Taifa

True!
mzee kama CCM hawataki hiyo katiba mpya itapatikana vipi? Please explain kwa mfano tu tume hii iliyopo ndio isimamiye kura ya maoni ya katiba mpya itakuwaje please lete fikra zako
 
TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Traitors at work
 
t
Tume ya Nyalali ilisema '' ni lazima kwanza kuwe na Tume huru ya uchaguzi na kuandikwa katiba mpya''. ACT wanakubali mambo hayo yanaenda sambamba!

Jeshi la Polisi linaingiaje kwenye mambo ya siasa? Kazi ya jeshi ni kusimamia sheria za nchi.
''Kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika''. Kule Zanzibar kumefanyika miafaka mingapi na hali ipoje leo hii. Kuna utayari gani kwa CCM waliopora chaguzi! utayari wanaozungumzia ACT ni upi huo

ACT wanaamini kukiwa na Tume huru basi Wabunge watachaguliwa kwa uhuru.
Hapa ndipo ninapoona ACT wana tatizo la kufikiri. Hivi si waliwahi kuwa na Tume huru Zanzibar?
Kwa mamlaka gani Jecha aliharibu uchaguzi alioshinda Maalim?
ACT hawakumbuki Jecha aliondolewaje, alipelekwa wapi na aliamriwa aseme nini?


Tume huru haina uhusiano na uhuni unaofanywa. Mtu akiporwa Form si tatizo la tume ni uvunjaji wa sheria na wahusika ni Polisi. Hujuma za mawakala si tatizo la tume ni uratibu wa CCM, Polisi na vyombo vya usalama.

Tunarudi pale pale kwamba wao wanaamini uchaguzi unahujumiwa na Tume. Hawana habari kuwa uratibu wa hujuma za uchaguzi ni wa mfumo mzima.

Kule kule wanaamini Tume huru itamaliza tatizo la uhuni. Hawakumbuki Jecha alifanya nini kwa msaada wa nani na kwanini hakukuwepo na hatua dhidi yake. Si Jecha alikuwa na Tume huruiliyowashirikisha CUF ambao ni ACT

Katiba pendekezwa iliandikwa na CCM, kusema kwamba maoni ya Tume ya Warioba yachanganywe na uhuni wa CCM ni ku adulterate maoni ya Wananchi.
ACT Katiba pendekezwa ni mali ya CCM. Wananchi wanataka kurudi ktk Tume ya Warioba

Kumbe tayari kuna sheria imeandaliwa!!

Kwanini Rais awe na mkono wa uteuzi? Rais anatakiwa aidhinishe jina. Rejea tume ya uchaguzi ya Ghana. Rais hana mamlaka yoyote ya kuteua majina au kupewa lundo la ma

Forget about katiba pendekezwa. Turudi kwa Rasimu ya Warioba.
ACT hii katiba pendekezwa iliandikwa na CCM

ACT katiba pendekezwa iliandikwa na CCM na haihitaji maboresho yoyote. Hii ilifuta maoni ya Tume ya Warioba ambayo ni maoni ya wananchi. Katiba pendekezwa si maoni ya Watanzani, ni Bunge la CCM.
Ninatilia shaka uelewa wa ACT Wazalendo! kuna tatizo kubwa wanajitahidi kulisukuma mbele

Huwezi kuwa na Tume huru ya uchaguzi katika mfumo wa dhulma ACT!

Kuna tatizo kubwa sana na nadhani kuna kitu kipo nyuma! mtakuja baini ikiwa ni too late

ACT na CCM wanaserikali ya pamoja kule Zanzibar, huku bara hatuna GNU na ACT wasijaribu kututumbukiza katika matatizo hayo. Kuna motive behind , ipo siku watu wataelewa tunamaanisha nini. Kuna kitu!
then what the way forwad kama CCM hawataki Please
 
TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
nani asiye wajua ninyi kuwa ni mapandikizi ya mbogamboga? Ukweli ni kwamba chama chenu hakina ushawishi wowote ule bara ukiondoa zanzibar ambapo wana Cuf waliwajoin kumfata Maalim.Hamna mvuto wa kisiasa kabisa. Udini umewajaa na hamna jipya!
 
Hii katiba iliyopo tu inakanyagwa na nyinyi wapiga kelele mitandaoni mmeufyata! Nini kitasababisha hiyo katiba mpya mnayoitaka isikanyagwe pale itapopatikana? Katiba ya chama unachokishabikia ilikuwa Mkiti awepo kwa awamu 2 za miaka mitano then amuachie mwingine, nini kilitokea? Kupiga makelele ya katiba rahisi sana, ila kama hata kama katiba za vyama vyenu hamuheshimu, mtaheshimu katiba ya nchi? Jamaa wanafiki sana
Katiba ya chama gani inaruhusu vipindi viwili? Tuwekee hapa kifungu kilichosiginwa. Halafu unaonekana mweupe kichwani. Tukishasema rais rais akifanya ujinga anaenda jela anaenda kweli. Muulize baba yako Zuma Nini kikimkuta. Au muulize baba yako wa kambo Kenyatta Nini kikimkuta kwenye BBI.

Rais anajifanyia anayotaka kwa sababu sisi(katiba)Ndio tumempa mamlaka. Kwa katiba hii hata Malaika itamlevya kwa madaraka. Ila tukimwonesha njia yakupita naye atafuta humohumo. Funguka wewe.
 
Si mnatuambia yesu kajizaa , Hivi akili inakubali hii kitu ??
Nakutahadharisha dogo

Kama Huna Ilimu ya deen/Imani piga ukimya!

Nifahamishe hili! Kuna Jambo gani Mwenyezi Mungu Hawezi??
 
Nimesoma Hoja za ACT ni nzuri na zinaeleweka shida ya Chadema ni wanataka Katiba mpya kama wimbo ila hawajaleta hoja za ushawishi kwanini Katiba mpya

ACT wamesema Tume huru kwanza na wametoa sababu

Chadema njooni na sababu kwanini Katiba mpya kwanza

Hapa itaturahisishia kupima kipi kianze, hoja zitoke kwenye Uongozi wa Chama sio kwa watukanaji mitandaoni
Yaani hata wewe unainhia kwenye mitego ya Hawa waramba viaty wa kiongozi mkuu wa chama,
Kati ya Mzazi na mtoto yupi alianza kuzaliwa?
 
Hawezi kuolewa wala kunya
Duuh! Umeandika as if ni mc wake



بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ

[ AL - BAQARA - 117 ]
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.

Kambishie mungu wako kuwa ww ni muongo kuna hili....huwezi??
 
Duuh! Umeandika as if ni mc wake



بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِذَا قَضَىٰ أَمْرًا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُ كُن فَيَكُونُ

[ AL - BAQARA - 117 ]
Yeye ndiye Muumba wa mbingu na ardhi pasina ruwaza; na anapo taka jambo basi huliambia tu: Kuwa! Nalo huwa.

Kambishie mungu wako kuwa ww ni muongo kuna hili....huwezi??
Huyo ni Nani anayesema hapo ?
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom