Tunaanza na Tume Huru Kwanza

TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Act ndio chama gani hiki,mbona cha hovyo kiasi hicho!chama akijui hata nguvu ya rais aliyonayo kwenye tume ya uchaguz bila katiba mpya usitegemee ccm kutoka madarakani.
 
Tatizo wapinzani ni ndumila kuwili ni ACT haohao walikuwa pamoja na wenzao kutokuutambua uchaguzi uliopita waliporushiwa mfupa wa serekali ya mseto Zanzibar tayari uchaguzi ukawahalali kwao utafikri siyo wale waliokuwa wanapinga uchaguzi.

Na hata hili la Rais la kukutana na wapinzani nalo linawatia doa wapinzani kuwa hawako kitu kimoja, baadhi ya wapinzani wanakubali vipi kwenda wakati wapinzani wenzao wako jela kwa makosa ya kubambikizwa wakati ilitakiwa wakomae wote kwa pamoja wasiende mpaka wapanzani wenzao watakapoachiwa huru.
 
TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Hawala" kingereza mnaitwa concubine wa ccm au siyo mwami?

Kumbe mnapewa mil,370 kila mwezi KWA siri Ili kuiua CDM
 
ACT ni zao la CUF chini ya hayati Maalim Seif.
Mwaka 2010 CUF na CCM walikubaliana uwepo wa serikali ya umoja wa kitaifa (GNU)

Walikubaliana uwepo wa TUME HURU ya Uchaguzi, iliyoundwa na Wajumbe kutoka CCM na CUF

Mwaka 2015 Tume ikiwa karibu kutangaza matokeo ambayo CUF Walishinda, Mwenyekiti Bw Jecha akabanwa na '' kuhara na kubebwa na watu maalumu kisha kupata matibabu'' TV Zanzibar akibatilisha matokeo

Serikali ya CCM na vyombo vyake vikakubali uhuni uliofanyika.
Mahakama haikuwa na nguvu, maamuzi ya Tume huru iliyokuwa na CUF hayahojiwi mahakamani.

CUF ambayo ni ACT ya leo wakapoteza uchaguzi na Maalim Seif akabaki kuwa mhanga hadi kifo

Tume huru haihakikishi uchaguzi huru. ACT wameshiriki chaguzi nyingi hawakuhujumiwa na Tum
Kazi ilifanywa na vyombo vya dola kwa baraka.ACT hawajashinda hata mtaa mmoja

Serikali za mitaa hazisimamiwi na tume! ACT hawakumbuki uhuni uliofanywa

Kama kuna kundi linalohujumu katiba mpya, ACT ni sehemu kubwa sana na muhimu ya kundi hilo

Kuna jambo la kujiuliza ikiwa ACT wanakumbukumbu, wanafikiri sawasawa au Wanatumika

JokaKuu Mag3 Pascal Mayalla Matola
 
TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Tume huru utaipataje chini ya Raisi mfalme, kwanza Raisi apunguzwe nguvu, ndo tume itakuwa huru
 
ACT wanafanya siasa za kuifurahisha CCM, ACT inataka ifanye siasa za kuonekana wastaarabu mbele ya CCM. Ukitazama vizuri kwa sasa, ACT inafanya siasa za Zito alizokuwa anazifanya miaka yote alipokuwa CDM. Ni vyema wapinzani wa kweli wakawa makini sana na siasa za ACT/Zito, ambazo ni za ghiliba. Wapinzani wa kweli wabaki na hoja kuu ambayo ni katiba mpya na sio kutekeleza matakwa ya CCM ya tume huru ya uchaguzi, ambayo lengo ni kuipa ACT viti kadhaa lakini CCM ikijihakikishia inabaki madarakani kwa shuruti.
 
Hapo kwenye baada ya usaili majina yapelekwe kwa rais kwa ajili ya uteuzi ndipo mm binafsi nina mashaka napo uwezekano wa mteuliwa kutii maagizo ya mteuaji Ni mkubwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
..tatizo haliko ktk tume ya uchaguzi peke yake.

..tatizo liko ktk MNYORORO mzima wa uchaguzi hapa nchini.

..mfumo mzima unatakiwa ufumuliwe kuanzia ktk uandikishaji wapiga kura, kuteua wagombea, kampeni, ...mpaka hatua ya mwisho.

..kwa maoni yangu, michakato yote miwili ianze kwa pamoja, lakini ni lazima MFUMO WA UCHAGUZI uwe umebadilishwa kwa kuboreshwa kabla ya 2024.

Cc Nguruvi3
 
..tatizo haliko ktk tume ya uchaguzi peke yake.
..tatizo liko ktk MNYORORO mzima wa uchaguzi hapa nchini.

..mfumo mzima unatakiwa ufumuliwe kuanzia ktk uandikishaji wapiga kura, kuteua wagombea, kampeni, ...mpaka hatua ya mwisho.
Ndio maana nasema ACT wazalendo sijui kama wanajua tatizo ni nini!

Laiti wangalikuwa na kumbukumbu japo 25% yaliyotokea Zanzibar wasingejiunga na hatua ya Msajili hata kwa bahati mbaya. Sielewi kuna pipi gani wamepewa

Kinachoharibu uchaguzi si Tume ya uchaguzi. Mfumo mzima ni mbovu.

Dola inatumika kikamilifu. Zitto ana imani Msajili wa vyama aliyekaa kimya Kenan Kihongosi wa UVCCM akitoa matamshi ya mauaji, atakaa kimya kwa mwanachama wa ACT! Chama kitafutwa siku hiyo hiyo

Msajili aliyeshiriki ''kuua CUF'' ndiye huyo huyo leo wana 'dance' na ACT wazalendo.
ACT wanaamini ana nia njema na mchakato

Polisi walimkamata Zitto akifanya mkutano halali Lindi , ACT wanaamini tume huru Polisi hawataMkamata tena!

Wagombea wananyang'anywa form mbele ya Polisi ACT wanadhani hayatatokea kukiwa na tume huru. ACT wamegombea kila kiti hakuna walichoambulia zaidi ya vipigo, leo wapo meza moja na waporaji wakipanga mipango ya tume huru ya uchaguzi!! kama si kioja sijui

Orodha ni ndefu inatosha kuwaambi hujuma za uchaguzi ni za kimfumo si tume peke yake.

Zanzibar ilikuwa na Tume huru wakiwemo CUF wakaporwa uchaguzi na Jecha na vyombo vya dola. ACT ambao ni CUF wanadhani tume huru ina matokeo tofauti ni ile iliyowapora uchaguzi

Kufanya jambo lile lile kwa namna ile ile ukitegemea matokeo tofauti ni definition ya Insanity

Kwahili siamini kama ACT hawafahamu! nadhani kuna pipi wanapewa , let's hope that I'm wrong

Msoud Othman wa ACT aliacha kuwa AG akitetea Katiba mpya na Zanzibar yenye mamlaka! Kapewa ving'ora hakumbuki yaliyompa Maalim, kama si usaliti sijui ni nini

ACT mna feli na mnafelisha Taifa, hamna hoja. Ushirika wenu na CCM una madhara makubwa sana kwa Taifa hili. ACT si chama kikubwa bara lakini visiwani ni kikubwa

ACT acheni huu uzumbukuku, kumbukeni ya nyuma! msitumike kirahisi haina tija kwa Taifa
..kwa maoni yangu, michakato yote miwili ianze kwa pamoja, lakini ni lazima MFUMO WA UCHAGUZI uwe umebadilishwa kwa kuboreshwa kabla ya 2024.
True!
 
ACT wanafanya siasa za kuifurahisha CCM, ACT inataka ifanye siasa za kuonekana wastaarabu mbele ya CCM. Ukitazama vizuri kwa sasa, ACT inafanya siasa za Zito alizokuwa anazifanya miaka yote alipokuwa CDM. Ni vyema wapinzani wa kweli wakawa makini sana na siasa za ACT/Zito, ambazo ni za ghiliba. Wapinzani wa kweli wabaki na hoja kuu ambayo ni katiba mpya na sio kutekeleza matakwa ya CCM ya tume huru ya uchaguzi, ambayo lengo ni kuipa ACT viti kadhaa lakini CCM ikijihakikishia inabaki madarakani kwa shuruti.

ACT ni CUF ya zamani, hakuna kilichobadilika. Hoja ya CUF ya Maalim ni Zanzibar yenye mamlaka kamili. Hoja hiyo ya CUF na shinikizo la CDM ndivyo vilimshinikiza JK kuanzisha mchakato wa Katiba

Mchakato wa katiba ulilenga kurekebisha mifumo ya nchi ikiwemo wa kupata Tume huru ya uchaguzi. Tume ni zao la Katiba kwani uwepo wake umeanzishwa na Katiba.

CUF ya Maalim walienda Bunge la Katiba chini ya Ukawa. Mwanasheria mkuu wa SMZ alikuwa Maosud Othman. Mwanasheria (AG) alijiuzulu kufuatia kutokubaliana na mambo ambayo serikali ya CCM iliyafanya ikiwemo kuhujumu mchakato wa katiba mpya

Masoud Othman sasa ni VP akitembea na ving'ora , ulinzi na kila faraja za uongozi, kasahau alisimamia nini na kwanini alijiuzulu kuwa AG.

Mh Masoud ambaye ni kiongozi wa ACT yeye na wenzake hawakumbuki madhila yaliyomkuta maalim Seif chaguzi nyingi ikiwemo ya CUF kuwa sehemu ya tume ya uchaguzi , Jecha akatenda

Masoud Othman kuongoza CUF kuingia makubaliano na CCM inachekesha wala haifikirishi
Kwamba lini CCM wamekuwa wema sana kwa wapinzani katika Taifa hili ?

Wale wanaohisi tu kuwa kuna kutumika na ''quid pro quo' ni ngumu sana kuwashawishi hakuna

ACT hawajiulizi ni kwa mapenzi yapi CCM wanataka Tume huru ya uchaguzi ikiwa hata mikutano hawaruhusiwi? Juzi kule Pemba Polisi wameshushwa vyeo kwa kuruhusu mikutano ya ACT, bado ACT wanadhani ipo namna tofauti na zile zilizofeli huko nyuma

Kwahili, ACT wanaharibu mchakato wa katiba, na kuna kila sababu ya kuamini lipo jambo!
 
ACT ni zao la CUF chini ya hayati Maalim Seif.
Mwaka 2010 CUF na CCM walikubaliana uwepo wa serikali ya umoja wa kitaifa (GNU)

Walikubaliana uwepo wa TUME HURU ya Uchaguzi, iliyoundwa na Wajumbe kutoka CCM na CUF

Mwaka 2015 Tume ikiwa karibu kutangaza matokeo ambayo CUF Walishinda, Mwenyekiti Bw Jecha akabanwa na '' kuhara na kubebwa na watu maalumu kisha kupata matibabu'' TV Zanzibar akibatilisha matokeo

Serikali ya CCM na vyombo vyake vikakubali uhuni uliofanyika.
Mahakama haikuwa na nguvu, maamuzi ya Tume huru iliyokuwa na CUF hayahojiwi mahakamani.

CUF ambayo ni ACT ya leo wakapoteza uchaguzi na Maalim Seif akabaki kuwa mhanga hadi kifo

Tume huru haihakikishi uchaguzi huru. ACT wameshiriki chaguzi nyingi hawakuhujumiwa na Tum
Kazi ilifanywa na vyombo vya dola kwa baraka.ACT hawajashinda hata mtaa mmoja

Serikali za mitaa hazisimamiwi na tume! ACT hawakumbuki uhuni uliofanywa

Kama kuna kundi linalohujumu katiba mpya, ACT ni sehemu kubwa sana na muhimu ya kundi hilo

Kuna jambo la kujiuliza ikiwa ACT wanakumbukumbu, wanafikiri sawasawa au Wanatumika

JokaKuu Mag3 Pascal Mayalla Matola
Kujadili sinema za Zitto Kabwe ni kupoteza muda wenu bure.

Aliombewa kazi ikulu kaunda suti zimemkataa, msitumie muda wenu kuwajadili wahuni kama Zitto Kabwe.

Wazanzibar wanajipanga kukichukuwa hicho chama jumla na Ayatollah hatoamini macho yake.
 
ACT ni CUF ya zamani, hakuna kilichobadilika. Hoja ya CUF ya Maalim ni Zanzibar yenye mamlaka kamili. Hoja hiyo ya CUF na shinikizo la CDM ndivyo vilimshinikiza JK kuanzisha mchakato wa Katiba

Mchakato wa katiba ulilenga kurekebisha mifumo ya nchi ikiwemo wa kupata Tume huru ya uchaguzi. Tume ni zao la Katiba kwani uwepo wake umeanzishwa na Katiba.

CUF ya Maalim walienda Bunge la Katiba chini ya Ukawa. Mwanasheria mkuu wa SMZ alikuwa Maosud Othman. Mwanasheria (AG) alijiuzulu kufuatia kutokubaliana na mambo ambayo serikali ya CCM iliyafanya ikiwemo kuhujumu mchakato wa katiba mpya

Masoud Othman sasa ni VP akitembea na ving'ora , ulinzi na kila faraja za uongozi, kasahau alisimamia nini na kwanini alijiuzulu kuwa AG.

Mh Masoud ambaye ni kiongozi wa ACT yeye na wenzake hawakumbuki madhila yaliyomkuta maalim Seif chaguzi nyingi ikiwemo ya CUF kuwa sehemu ya tume ya uchaguzi , Jecha akatenda

Masoud Othman kuongoza CUF kuingia makubaliano na CCM inachekesha wala haifikirishi
Kwamba lini CCM wamekuwa wema sana kwa wapinzani katika Taifa hili ?

Wale wanaohisi tu kuwa kuna kutumika na ''quid pro quo' ni ngumu sana kuwashawishi hakuna

ACT hawajiulizi ni kwa mapenzi yapi CCM wanataka Tume huru ya uchaguzi ikiwa hata mikutano hawaruhusiwi? Juzi kule Pemba Polisi wameshushwa vyeo kwa kuruhusu mikutano ya ACT, bado ACT wanadhani ipo namna tofauti na zile zilizofeli huko nyuma

Kwahili, ACT wanaharibu mchakato wa katiba, na kuna kila sababu ya kuamini lipo jambo!

Hao Wapemba walioko ACT wameingizwa mkenge na siasa za Zito, watatumika hadi wakija kustuka muda utakuwa umekwisha.
 
Hao Wapemba walioko ACT wameingizwa mkenge na siasa za Zito, watatumika hadi wakija kustuka muda utakuwa umekwisha.
Kwa mtu makini ''hesabu' za ACT Wazalendo hazieleweki kwa namna yoyote

Miaka 30 ya vyama vingi CCM hawakuwahi kujadili Tume huru ya uchaguzi.

Pressure ya Katiba mpya inawafanya watafute uhalali 'legitimacy' ya kuhujumu uchaguzi wakitumia vyombo vya dola na kujisafisha na tume huru.

Kwamba, Wapinzani wametaka Tume huru wamepewa na wameshindwa vibaya.
Mbele ya uso wa dunia itaonekana kweli na CCM watafanikiwa na kuduwaza watu.

Baada ya kupata uhalali wa uchaguzi kwa Tume huru inayoshirikisha ACT, CCM wataandika katiba wanayotaka wao. Bungeni watakuwa kama walivyo sasa .

Watu wajiulize, ACT kweli walikaa chini na kufikiri sawa sawa au walikaa chini na kutafakari kingine tusichojua na kuamua kuingia chaka hili. Kuna motive ya hili jambo! si bure
 
Tume huru ya uchaguzi bila katiba mpya ni sawa na kuziba mashimo ya panya kwa mikate!

Maana Tanzania uchaguzi ni mfumo sio tume tu.Nguvu ya Rais na wateule wake, polisi, TISS, Jeshi, Tume, Tamisemi na wengineo lazima viangaliwe kwa pamoja kupitia katiba mpya kwa kuwa vinahusika na uchaguzi mkuu.

Hiki kinachoitwa ni Tume huru ya uchaguzi ni changa la macho kwa wajinga ambao ndiyo wengi kwenye hii nchi ikiwa ni pamoja na ninyi ACT wazalendo.
Umesema yote mkuu,tukisema Zitto hamna kitu kichwani na yuko upande CCM,mtu wa siasa maslahi,mnakasirika.

Anapoipeleka ACT ndiko Lipumba alikoizika CUF. Zanzibar wanashabikia ACT kwa sababu za kidini tu.
 
Tume huru ya uchaguzi bila katiba mpya ni sawa na kuziba mashimo ya panya kwa mikate!

Maana Tanzania uchaguzi ni mfumo sio tume tu.Nguvu ya Rais na wateule wake, polisi, TISS, Jeshi, Tume, Tamisemi na wengineo lazima viangaliwe kwa pamoja kupitia katiba mpya kwa kuwa vinahusika na uchaguzi mkuu.

Hiki kinachoitwa ni Tume huru ya uchaguzi ni changa la macho kwa wajinga ambao ndiyo wengi kwenye hii nchi ikiwa ni pamoja na ninyi ACT wazalendo.
ACT nyinyi ni hopeless kabisa. Utapataje tume huru ya uchaguzi bila kufumua katiba ya nchi ???

Mmepewa tenda ya kuneutralize agenda kuu ya katiba mpya kwa kuchukua kiagenda kidogo ndani ili mpunguze nguvu ya uhitaji wa katiba mpya.
 
TUNAANZA NA TUME HURU YA UCHAGUZI

Hoja ya ACT Wazalendo Juu ya Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya.

Utangulizi.

Tangu kurejeshwa upya kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, hoja ya kuanzishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi imetawala medani ya siasa nchini.

Tume ya Jaji Nyalali ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi iliweka bayana kuwa, kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, ni lazima kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na kuandikwa kwa Katiba Mpya.

Hoja hizi zimeendelea kutawala medani ya siasa katika miaka 30 ya uwepo wa siasa za Vyama vingi nchini.

Kikao cha Wadau wa Tasnia ya Siasa Dodoma: Ukurasa Mpya?

Utawala wa Awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ulijipambanua bayana kuwa dhidi ya vyama vya upinzani. Wito wa viongozi wa upinzani wa kuwepo kwa muafaka wa kitaifa na maridhiano ya kisiasa ulipuuzwa. Haki za vyama vya upinzani kufanya shughuli za kisiasa kwa uhuru iliangamizwa. Shughuli halali kama vile mikutano ya hadhara ziliharamishwa!

Katika mazingira hayo, ni dhahiri kuwa Kikao cha Wadau wa Siasa Tanzania Kujadili Hali ya Demokrasia Tanzania kilichofanyika Jijini Dodoma kati ya tarehe 15 hadi 17 Desemba 2021 kilikuwa mwanzo mpya uliokosekana katika miaka sita iliyopita!

Kikao hicho kilichowakutanisha viongozi waandamizi wa vyama vya siasa, Mawaziri wenye dhamana, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, Jeshi la Polisi, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini kilikuwa ni jukwaa muafaka la kutafakari tulipojikwaa kwenye chaguzi zilizopita, hasa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 na kutafakari kwa pamoja mwelekeo unaopaswa kuchukuliwa na Taifa kurekebisha dosari hizo kwa maslahi mapana ya Taifa. Makosa hurekebishwa kwa watu kukutana, kuambiana ukweli na kuwa na utayari wa kubadilika!

Kwa Hali yetu, Nini Kianze? Tume Huru ya Uchaguzi au Katiba Mpya?

Moja ya masuala ambayo yalijadiliwa kwa uwazi na kina kwenye Kikao cha Wadau wa Siasa cha Dodoma ni kuhusu Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya. Baada ya kikao, masuala haya mawili, hasa kuhusu nini hasa kinapaswa kutangulia yamepata mjadala mkubwa.

Tunaanza na Tume Huru!

Kalenda ya Uchaguzi inaonesha kuwa mwaka 2024 kutakuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na 2025 Uchaguzi Mkuu. Kwa maoni yetu, ACT Wazalendo tunaamini kuwa tunapaswa kwanza kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kisha Katiba Mpya. Sababu zetu zipo wazi;

1. Mchakato wa Katiba Mpya unahitaji kutungwa kwa Sheria Mpya ya kusimamia suala hilo kwa sababu Sheria iliyokuwepo imeshapitwa na muda. Kutokana na unyeti wa suala hilo, ACT Wazalendo tungefurahi jukumu hili nyeti, litekelezwe na Bunge lililochaguliwa Kidemokrasia na Wananchi tofauti na Bunge la sasa ambalo asilimia kubwa ya Wabunge wake ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hawakutokana na matakwa (will) ya Wananchi.

2. Kura ya maoni ya Katiba Mpya itasimamiwa na Tume ya Uchaguzi. Hatuna imani kuwa Tume ya Uchaguzi inaweza kusimamia zoezi hilo nyeti kwa weledi na haki. Tunahitaji Tume Huru ya Uchaguzi ambayo itasimamia mchakato wa kura ya maoni ya Katiba Mpya. Tume hiyo ni lazima iundwe sasa.

3. Hata baada ya Katiba Mpya kupitishwa na Wananchi kwenye kura ya maoni, Katiba haitaanza kutumika mara moja. Kutakuwa na kipindi cha mpito kisichopungua Miaka minne. Katika kipindi hicho Sheria mbalimbali zitafanyiwa marekebisho ili kuendana na Katiba Mpya. Kipindi hicho cha mpito lazima tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi kwa ajili ya kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025 na chaguzi ndogo zozote zitakazokuwa zinatokea kabla ya Katiba Mpya kuanza kutumika.

4. Iwapo kwa sababu zozote zile, Mchakato wa Katiba Mpya hautakamilika hadi wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025, Tume Huru itakayoundwa itaweza kusimamia chaguzi hizo kwa uhuru na haki.

Tume Itapatikanaje?

Tume ya Uchaguzi ni zao la Katiba na Sheria. ACT Wazalendo tunapendekeza kuandikwa upya kwa Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zake ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi. Tunapendekeza kuwa Tume Huru ya Uchaguzi iwe na uwezo wa kuajiri Wasimamizi wa Uchaguzi katika ngazi zote na kuondokana kabisa na Mfumo wa sasa wa makada wa Chama tawala kuwa Wasimamizi wa Uchaguzi.

ACT Wazalendo tunapendekeza Mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba na ya Katiba Pendekezwa Kuhusu Tume ya Uchaguzi yachukuliwe kama yalivyo au na marekebisho kulingana na hali ya sasa. Msingi wa hoja hii ni ukweli kuwa maoni hayo yanatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi Wapatikanaje?

1. Sheria mpya ya Uchaguzi (National Elections Act 2022) iweke utaratibu kuwa Watanzania wanaotaka kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi waombe kazi kufuatia tangazo la wazi kwa umma.

2. Sheria mpya ya Uchaguzi ianzishe Kamati Maalum ya Uteuzi wa Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.

3. Kamati ya Uteuzi ifanye usaili (interview) kwa uwazi kwa waombaji wote na kuchuja majina ambayo yatapelekwa kwa Rais kwa ajili ya uteuzi.

4. Mara baada ya wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi kupatikana wataajiri Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye nafasi itatangazwa, kufanyiwa usaili wa wazi na kisha jina kupelekwa kwa Rais kuteua Mkurugenzi wa Uchaguzi.

5. Kamati ya Uteuzi wa Tume itamkwe kisheria kuongozwa na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano kama Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Zanzibar kama Makamu wa Mwenyekiti, Wajumbe wawe ni Rais wa Tanganyika Law Society, Rais wa Zanzibar Law Society, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni, Mtu mmoja atakayeteuliwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na kama hakuna Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni basi kutoka chombo kinachojumuisha Vyama vyenye Wabunge Bungeni, Mtu mmoja kutoka Asasi ya Kitaifa ya masuala ya Sheria na Haki za Binaadam Tanzania Bara na mtu mmoja kutoka asasi kama hiyo Tanzania Zanzibar. Kwa vyovyote vile angalau theluthi ya wajumbe wa Kamati ya Uteuzi lazima wawe Wanawake.

6. Kutakuwa na sifa maalum za Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ili kuhakikisha wanakuwa watu wenye weledi na hawaegemei upande wowote.

7. Baada ya kuteuliwa na Rais, Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume wataidhinishwa na Bunge kwa utaratibu utakaowekwa na Sheria ya Uchaguzi. Kisha watakula kiapo mbele ya Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.


Masuala haya, na mengine yatakayoonekana yanafaa kutokana na mashauriano ya wadau, yanaweza kujumuishwa kwenye Sheria Mpya ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata Tume Huru ya Uchaguzi.

Katiba Mpya Itapatikanaje?

Katiba Mpya ni jambo pana! Inahitaji kuwepo kwa muafaka wa kitaifa juu ya jambo hilo.

Jambo la kutia matumaini, mchakato wa Katiba Mpya ulikwishaanza. Tume ya kukusanya maoni ilikwishaundwa, maoni yalishakusanywa na kuwasilishwa kwenye Bunge la Katiba ambalo lilitoka na Katiba Pendekezwa. Changamoto pekee ni kuwa Katiba Pendekezwa haikutokana na maoni ya pande zote kwa sababu Wabunge wengi wa Upinzani walisusia upigaji kura.

Hivyo basi, Taifa litahitaji Katiba Pendekezwa kufanyiwa maboresho. Mchakato wa namna ya kuifanyia maboresho lazima uelezwe kwenye Sheria ya Mchakato wa Katiba Mpya itayoandikwa upya na Bunge. Bunge linaweza kuamua kuundwa kwa Kamati ya Wataalamu (Committee of Experts) ili kutafuta namna nyingine ya kumalizia mchakato bila kuligharimu Taifa.

Hitimisho.

Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya ni chanda na pete, vinategemeana. Kwa mazingira yetu kama Taifa kwa sasa, kutangulia kupata Tume Huru ya Uchaguzi kunaweka mazingira mazuri ya kupatikana kwa Katiba Mpya inayotokana na maoni na matakwa ya Wananchi.
Yan Zitto ni Yuda Iskariote

Mpe tu vipande 30 vya fedha and you own him, he is the cheapest political commodity in the land, so very sad😔
 
Wafuasi wa kilichokuwa chama kikuu cha upinzani wanavyoushambulia uzi wa ACT wazalendo ni dhahiri wanatambua 2025 hali ni mbaya kwao.
Mtake msitake 2025 ACT wazalendo wanakwenda kupata wabunge wengi
 
Back
Top Bottom