Tumefika hapa kwa sababu ya Kikwete kumlea vibaya Ridhiwani kuihusisha familia yake kwenye masuala ya uongozi

Kikwete Urais wake ulikuwa wa ubia na familia na rafiki zake wakina 'ShKubar"! Kama ataruhusiwa kuturudisha huko kutatokea backlash kubwa kutoka kwa wananchi na Samia hata kuwa salama na utawala wake!
Sijuwi kama watakuelewa...
 
Kikwete alipokuwa akitaka kugombea Urais mwaka 1995 Nyerere alimwambia kwamba wewe bado mdogo muachie Ben watu weengi waliamini hivyo ila ukweli Nyerere alimaanisha kuwa Kikwete alikuwa mdogo kwenye mambo ya kupewa kuiongoza Nchi yaani alimsoma mwenendo wa maisha yake na kugundua kuwa ni msumbufu na hafai kuwa Rais wa nchi Nyerere aliona mbali sana.

Kosa kubwa la kwanza alilolifanya Kikwete kwenye uongozi wake ni kuiruhusu familia yake kujiingiza moja kwa moja kwenye mamlaka ya Rais.

Tulishuhudia awamu ya Kikwete kijana mdogo kama Ridhiwani kujimilikisha makampuni meengi ya kilaghai na waliokuwa wasaidizi wa Ridhiwani nao kujiingiza moja kwa moja kwenye Utawala wa nchi.

Rais Mstaafu Kikwete aliporuhusu hata marafiki wake wa karibu kuingia kwenye masilahi ya Urais wake kwa njia ya utapeli hali hii imepelekea sasa kuhangaika sana wanapopata mtu ambaye hajali maslahi yao hii ni kwa sababu moja tu wanaendeleza biashara zao za kitapeli kipindi wawapo kwenye mifumo.

Ndio maana Nyerere alisema ni hatari sana kuingiza Ikulu Rais mfanyabiashara hali ikiendelea hivi kuna umuhimu sasa wa kuwa na mgombea binafsi ambaye bila huruma atakuja kuisafisha nchi.
Pia mwalimu Nyerere alisema.. kwa katiba tuliyonayo tukipata Rais ambae haeshimu katiba bas atakalosema ndilo litakua sheria na usipofuata utakiona cha mtema kuni.
 
Afadhali ya Kikwete Mara milioni kuliko ibilisi .
Swali la ziada hivi ni Ridhwani aliyefukuza wawekezaji? Je ni yeye aliyeshusha kiwango cha ukusanyaji kodi miaka miwili iliyopita? Je ni yeye aliyepora fedha za watu kutoka kwenye akaunti zao benki? Je ni yeye aliyeuza nyumba za serikali na kuhonga mahawara? Je ni yeye aliyebomoa nyumba za wananchi mbezi huku za mwanza akiziacha? Je ni yeye aliyepora korosho na hatimae kupoteza soko la korosho mazima? Je ni yeye aliyefanya miradi ya miala mitano iliyopita "baadhi" ijengwe chini ya kiwango na utaalamu hafifu hata mingine kubomoka na kusababisha majanga? Daaah kuna mlolongo mrefu vema mgetulia ili upepo usivume na kusababisha nyeti zianikwe
 
Magufuli alitaka Rostam awe ndiye mbunge wa Morogoro mjini badala ya Aboud umesahau?
Magufuli kutaka awe mbunge wa Morogoro hakuondowi ufisadi Rostam aliofanya kama archirect wa mpango wa kuiba fedha BOT Kupitia EPA!! Roastam ni bingwa wa kuwaingia watawala wasiojitambua !!! Fikiria aliweza hata kumuingia marehemu Mkapa Kupitia kwa Balozi Ruhinda!!
Kumbuka kuwa Rostam alinunua viwanda vya Ngozi hata vya kule Mwanza lakini miaka yote hiyo alikuwa hajaviendeleza na sina hata hakika kama alimaliza hata kuvilipia!!
Hawa wanaojiita wawekezaji wa bongo ni wakuwaangalia sana kwani sio wazalendo!
 
Magufuli kutaka awe mbunge wa Morogoro hakuondowi ufisadi Rostam aliofanya kama archirect wa mpango wa kuiba fedha BOT Kupitia EPA!! Roastam ni bingwa wa kuwaingia watawala wasiojitambua !!! Fikiria aliweza hata kumuingia marehemu Mkapa Kupitia kwa Balozi Ruhinda!!
Kumbuka kuwa Rostam alinunua viwanda vya Ngozi hata vya kule Mwanza lakini miaka yote hiyo alikuwa hajaviendeleza na sina hata hakika kama alimaliza hata kuvilipia!!
Sasa iweje Magufuli atake fisadi awe mbunge? , Au Magufuli alikuwa anafuga mafisadi papa?
 
Sasa iweje Magufuli atake fisadi awe mbunge? , Au Magufuli alikuwa anafuga mafisadi papa?
Kule kufanya manunuzi makubwa bila kufuata utaratibu wewe unadhani kulikuwa kunaashiria nini? Kumuweka mtoto wa dada yake kuwa Paymaster General kulikuwa na maana gani? Not to mention MAYANGA construction waliokuwa wanapewa tender za mabillion bila kushindanishwa!!!
 
Acheni huu Ujinga jamani,mbona mnapenda kuwakosea watu,sio Tabia nzuri,kama una chuki binafsi ni Bora Kukaa kimya.Tuko na mama ngoja tuijenge Nchi haya au huu Ujinga Haunaa Maana kabisa.
 
Ibilidi mkubwa alikuwa Mkapa. Yeye ndiye rais wa Kwanza kufanya biashara ikulu, yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kununua wapinzani na kudhoofisha Demokrasia, yeye ndiye aliyeasisi ufisadi Kagoda , deep green , meremeta etc. Yeye ndiye aliyetuletea Kikwete ingawa alikuwa na watu wengi Safi akiwemo Ahmed Salim, yeye ndiye aliyemleta Magufuri na kuwa mentor wake. Kale kazee kanischt sana. Najua Mwl.alijilaumu sana kukaamini
WEWE CHIFU UNAELEWA USHETANI ULIPOANZIA TANZANIA. PIA NI MSEMA KWELI.
 
Kwanza wewe ni kilaza. Hakuna probability zaidi ya 100% na ikiwa ni 100% maana yake event will happen, hivyo umeboa. Unajua nani alipendekeza Samia awe mgombea mwenza 2015?
HAPANA PROBABILITY IKIWA 100% BADO NI PROBABILITY HAINA MAANA KUWA THE EVENT WILL HAPPEN INA MAANA UWEZEKANO NI ASILI 100. BADO NI UWEZEKANO WA JAMBO KUTOKEA. SHUKRAN.
 
HAPANA PROBABILITY IKIWA 100% BADO NI PROBABILITY HAINA MAANA KUWA THE EVENT WILL HAPPEN INA MAANA UWEZEKANO NI ASILI 100. BADO NI UWEZEKANO WA JAMBO KUTOKEA. SHUKRAN.
Wewe kilaza nenda shule na acha kupiga kelele katika mtandao (herufi kubwa)
 
Acheni huu Ujinga jamani,mbona mnapenda kuwakosea watu,sio Tabia nzuri,kama una chuki binafsi ni Bora Kukaa kimya.Tuko na mama ngoja tuijenge Nchi haya au huu Ujinga Haunaa Maana kabisa.
Sasa wewe ndo umeandika upuuzi. Wakati wenzio wenye akili wametoa angalizo la maana
 
Mwendazake alipoona anaweza kuchemka uchaguzi wa 2020 haraka haraka akajiweka karibu na Rostam na Kinana....unafiki nafiki tu.
Magufuli hakumhitaji Kinana wala mjinga yoyote kushinda ule uchaguzi Magufuli alikuwa na mkono wa chuma na ndio uliomrudisha Ikulu.
 
Back
Top Bottom