Mkuu Kasana umenikumbusha mbali sana maana ishu ya tebo ilikuwa soo hasa pale wale walimu wanoko waliokuwa wanavuka hataile tebo ya 12 na kwenda mpaka ya ishirini, maana tebo ya saba, tisa ni noma sasa huko kwenye 13, 17, 19 je?. Oyaa mnakumbuka sayansi kimu, ile ya kutengeneza maakuli skuli halafu mnapata maksi. Pia kun ishu moja huwa inaniboa nikikumbuka mpaka leo; NAMBA Yaani mtu unawahi shule kinoma ili uwe namba moja. Mnakumbuka tobo bao, usiombe hiyo ichezwe darasani wakati nje mvua inanyesha! Mnakumbuka mtihani wa mwisho wa darasa la saba, pale ambapo mnaanza say na hisabati baada ya hapo mnaenda kucheza mpaka mnajisahau mnakuja kuitwa mtihaniiiiiiiiii!!! mnaenda tena mkimaliza the same. HALAFU MWISHO KABISA MNAVUNJA PENI, KALAMU N.K