Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Niliwahi kuchungulia kisima kipindi natambaa... wakati huo Bi mkubwa karudi kwao mwanza baada ya kugombana na mzee... mimi ndio nina miezi sijui mitatu.. miaka ya 70 huko...

Mama akiwa anasukana nywele kibarazani hana habari mimi natambaa kuelekea kwenye kisima cha maji kirefu kweli kweli...

Mama ananiambia alikurupuka kama mshale alikuja mbio akanidaka mguu huku niko nusu nje nusu ndani ya kisima... akawa anatetemeka huku anapiga kelele za kilio...

Alifanikiwa kunivuta akalia mno! Kesho yake alipanda gari kurudi nyumbani [kwa mumewe] ....

Ningekuwa nimeshakufa zamani!
 
Pambafuu ungekufaa wewe...
 
Duuh maza ikabdi arudi kwa Mzee... Ilikuwa njia ya kuwarusidha pamojaaa kazi ya Mungu bhanaa
 
Daah aisee pole yake mama yako
 

Nimejaribu kuwaza mama aliumwaje tumbo la uzazi kwa presha hii dah
unaeza blid siku si zako
 
Pole ccy but hao (kumbi)Γ—2 wasipo kaushwa vizuri yale mafuta yao ni lazima uendeshe tuuu tena vizuri! Nnaexperience yake kidogo
but siwez acha kamwe kuwakula jmn.. utamu wke na chungu wake naujua

Go ahead ujaribu tena siku nyingiiine
et
 
Pole baby, kwa hiyo hata chakula cha nazi huli?
 
Mungu hua anatulinda sana kwakweli!
.
.
huu uzi umepita muda lakini ngoja na mimi nishee kidogo yangu!
.
.
nina matukio mawili ambayo kiukweli niliona kaburi hili hapa.
.
.
la kwanza miaka ya nyuma kuna zile dawa za malaria zilikua zikiitwa chloroquine kutokana na uchungu wake walizipaka rangi ya blue na utam kidogo kwa juu.
.
.
nilipokuwa na umri wa miaka kama minane hivi nilikuwa nahimizwa sana kulala mchana, sasa katika harakati hizo siku moja baada ya kuamka nikaona kopo la chloroquine, kwa mawazo yangu nilijua ni pipi, nikazichota nyingi nikazitupia mdomoni..
.
.
kwa uchungu wa zile dawa ukisha zitafuna huwezi zitema basi yale mate nikayameza.. dawa ikaanza kuingia.. macho yakanitoka povu likajaa mdomoni hatimae nikaanza kukata roho πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
.
.
katika kutupa tupa miguu niiache hii dunia kwa bahati mama akasikia akamwambia sister mkubwa kuna kitu kimeingia ndani kakifukuze,
.
.
sister kuja alitoka mbio mama mama njoo mwone kindikinyer, mama kufika kuangalia pembeni ananiona ndo nipo kwenye hatua za mwisho.. alikimbia kuomba maziwa kwa mzee maajabu akaambiwa hawezi kupewa kama hajaenda na hela!
.
.
mama alilia lakini wapii!! huku mimi mpaka na miguu nimeshaacha kurusha, bahati nzuri akaja kuna mwalim akasema ukichukua yai bichi na mkaa ukamnywesha atatapika pia..
.
.
basi nikapewa nikatapika walau nikawa nimeponea hapo.
.
.
miez michache baadae yule jamaa aliekuwa akiuza maziwa wakati akicheza ngoma alidondokea mkuki ukamchoma vibaya, utumbo ulitoka nje kwa bahati mbaya watu wakaushika kwa mkono, kitu kilichosababisha baadae uoze, alipelekwa KCMC lakini miezi mitano baadae alifariki! (hua namkumbuka katika sala zangu na mola amlaze pema peponi).
.
.
kila nikikumbuka nawaza nikivyo isogelea kaburi
 


Mzee baba ukawa umetulia unashusha tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…