Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

daah nakumbuka nilikua darasa la tatu nilikua napenda sana mambo ya ufundi umeme na redio, hasa kuna siku alikuja fundi umeme nyumbani kuna vioande vya wire vikabaki, nilikua na kiredio kidogo cha betri nikajiuliza kwa nini ninunue betri wakati nyaya zipo? basi bwana nikajifanya fundi nikachukua mult plug moja nikaifungua nikaunga nyaya nikaja kuunga na sehemu ya kuweka betri kwenye redio.
Ile kuwasha naona redio kimya sijui niliwaza nini asee nikashika zile nyaya daah nilikula shoti moja ya maana sana hadi leo sielewi nilichomokaje pale!! kuanzia hapo hadi leo sitaki kucheza na umeme tena imezidi sana labda nibadili taa!
 
Mimi mwezi wa nane tu nilinusurika kifo ..wanavyosema usiendeshe ukiwa umelewa nimeamini.. Bwana hiyo siku nimepiga vodka nusu chupa nikaamua kuchukua baskeli kuanza kuendesha nikaenda mpaka kilimani sasa kuteremka nikawa sipigi break bwana bwana kuna ya mwisho kunakua na kingo na chuma sasa nikazikosa zile chuma maana zingenitoboa utumbo kabisa .. Nikagonga kingo nikatupwa huko.. Bahati nzuri kuna watu niliwapita nikawa nimekaa nawasubiri maana simu imevunjika vipande u can imagine hiyo crush ilikuwaje suruali imetatuka kila mahali tena sehemu tofauti tofauti.. Wale watu wakapiga simu emergency polisi na ambulance wakatinga.. Hospital wakanipiga ct-scan kucheki kuwa uti wa mgongo na brain ipo sawasawa.. Sasa huko hospital nikaishia kutengua mkono maana niliutwist mwenyewe kwa bahati mbaya wakati nimelazwa...
Huwa nawaza Yale machuma yalivyonikosa
 
Haha pole sana boss
daah nakumbuka nilikua darasa la tatu nilikua napenda sana mambo ya ufundi umeme na redio, hasa kuna siku alikuja fundi umeme nyumbani kuna vioande vya wire vikabaki, nilikua na kiredio kidogo cha betri nikajiuliza kwa nini ninunue betri wakati nyaya zipo? basi bwana nikajifanya fundi nikachukua mult plug moja nikaifungua nikaunga nyaya nikaja kuunga na sehemu ya kuweka betri kwenye redio.
Ile kuwasha naona redio kimya sijui niliwaza nini asee nikashika zile nyaya daah nilikula shoti moja ya maana sana hadi leo sielewi nilichomokaje pale!! kuanzia hapo hadi leo sitaki kucheza na umeme tena imezidi sana labda nibadili taa!
 
Ee usirudie tena mkuu
Mimi mwezi wa nane tu nilinusurika kifo ..wanavyosema usiendeshe ukiwa umelewa nimeamini.. Bwana hiyo siku nimepiga vodka nusu chupa nikaamua kuchukua baskeli kuanza kuendesha nikaenda mpaka kilimani sasa kuteremka nikawa sipigi break bwana bwana kuna ya mwisho kunakua na kingo na chuma sasa nikazikosa zile chuma maana zingenitoboa utumbo kabisa .. Nikagonga kingo nikatupwa huko.. Bahati nzuri kuna watu niliwapita nikawa nimekaa nawasubiri maana simu imevunjika vipande u can imagine hiyo crush ilikuwaje suruali imetatuka kila mahali tena sehemu tofauti tofauti.. Wale watu wakapiga simu emergency polisi na ambulance wakatinga.. Hospital wakanipiga ct-scan kucheki kuwa uti wa mgongo na brain ipo sawasawa.. Sasa huko hospital nikaishia kutengua mkono maana niliutwist mwenyewe kwa bahati mbaya wakati nimelazwa...
 
Story yangu inaanza kama ifuatavyo baada ya kumaliza shughuli zangu za kuuza chipsi usiku napita karbu na nyumba ya jiran namsikia bwana mifugo akimwambia jiran yangu ambae ngombe wake alkuwa kasha dead amzike Mara moja kwani alkuwa ana anthrax basi nikaendelea kupeleleza nkaona alpomzka walipomaliza walivyoondoka nikaenda mfukua skuwa na gloves nikavaa mifuko ya Rambo maana nlsikia akisema ugonjwa ni hatar unaambukzwa na bacteria aina ya bacillus anthrax sjui kama nimepatia spelling au laa ila hayanihusu basi tuendelee na story basi bwana nikamuosha nikamkatakata vipande kesho nikamuuze mishkak vipande vilivyobakia nikampa mshkaj aweke kwenye freezer lake maana anatuchaj per day bwana nikauza wee mara watu wakaanza kuanguka baada ya kula wengne kutapika na kuhara palepale RAIA waliponishtukia wakaanza nikimbiza na mapanga wengine magongo sauti zilisikika zikisema "lazma tukukate vipandevipande" kwa bahat nzur kulikuwa kuna fuso sjui Lori hata skumbuk vzr lilikuwa linaanza kuondoka sjui lilikuwa linaenda WAP bas bwana nikalidandia baada ya masaa mawil mule ndan ya fuso simu yangu inaita mama mwenye nyumba anasema upo WAP mbona kuna polis wanakutafuta hapa nikakata Sm mara tena simu inaitaa kapiga RFK take yule mshkaj anatuifadhia nyama akasema nyama yako ina nn jamaa alikuibia kdogo kaenda itumia gheto sahiv ninavyokwambia tumemuwahisha hospital nikakata Sm .gar likiwa linaenda ktk kukaguakagua mule ndan nikakuta magunia kuyacheck ndani naona bangi pia kulikuwa na madawa mengne syajui kumbe skudandia fuso nilidandia kifo Mara gar likasimama kumbe hlo eneo kulikuwa na police patrol nkasikia shuken wote tukague gari
Mkuu naomba unitumie mwendelezo hata PM
 
Poleee sana,

Kwa upande wangu, kuna simbilis moja almanusra inifanye nipak vitu vyangu niondoke duniani, shenzi sana, mapenzi haya


Anyway.. tuyaache hayo

miaka ya Nyuma kidogo hapo, nikiwa kama standard three hv au two, nikiwa kwa babu mzaa mama moshi vijijin huko, siku moja nimepanda juu ya mti wa mmerez, (kwa wanao ifahamu hii miti ukiwa umekomaa n mrefu sana) nilikua naupunyua matawi, bwana wee huku na huko nimekata tawi lina kama V hv, hiyo V si ikaja ikanivaa shingon kama tai hv... nilijaribu kulivua weee lakn wapi, huku na huko wapi (nilikua bado mdogo, chini ya miaka 10) so uamuz wa haraka ukanijia nijiachie tu nidondoke nalo, nikaachia panga likatangulia kwanza... Yaan ilitokea kama miujiza vile, ile nataka kujiachia tu likanivuka lenyewe, niko hoi bin taaban hapo, nguvu zenyewe zalisha anza kuisha, nikashuka nikaenda kulala

Aisee nimecheka sana maana tukio kama hili lilinitokea nikiwa nakata majani juu ya mti unaoitwa "mhesi" kule Rombo, kumbe nilikuwa nimeshikilia kimti kikavu kikakatika nikashuka kwa kichwa hadi chini phuuh!.
Nilijaribu kuinuka nikae lakini nikashindwa na sauti ya kulia nayo ikawa haitoki. Nikatulia kama dakika moja nguvu zikanijia lakini shingo sidhubutu kuigeuza maana ilikuwa inauma balaa.
Niliposimama nikageuka kumbe pale chini palibakibaki na nywele za kichwani kutokana na kile kishindo nilichoanguka nacho [emoji23][emoji23]
Siku nyingine tena nilitoka shule nikawahi fasta kwenda kupanda juu ya mwembe kujisevia kama ilivyo kawaida yangu, baada ya kula na kushiba hukohuko juu ikawa ni wakati wa kushuka sasa.
Nilikuwa na tabia ya kushuka kwa kutumia matawi ya huo mwembe,, sasa wakati natumia tawi kushuka si likaachia kule juu/likakwanyuka kwa kuzidiwa na uzito! Nilitangulia chini nikiwa nabembea na ule mti hadi chini alafu matawi yake yakanifunika nikalala palepale usingizi mzito hadi usiku wa saa 2 kasoro ndio nilizinduka
 
Story yangu inaanza kama ifuatavyo baada ya kumaliza shughuli zangu za kuuza chipsi usiku napita karbu na nyumba ya jiran namsikia bwana mifugo akimwambia jiran yangu ambae ngombe wake alkuwa kasha dead amzike Mara moja kwani alkuwa ana anthrax basi nikaendelea kupeleleza nkaona alpomzka walipomaliza walivyoondoka nikaenda mfukua skuwa na gloves nikavaa mifuko ya Rambo maana nlsikia akisema ugonjwa ni hatar unaambukzwa na bacteria aina ya bacillus anthrax sjui kama nimepatia spelling au laa ila hayanihusu basi tuendelee na story basi bwana nikamuosha nikamkatakata vipande kesho nikamuuze mishkak vipande vilivyobakia nikampa mshkaj aweke kwenye freezer lake maana anatuchaj per day bwana nikauza wee mara watu wakaanza kuanguka baada ya kula wengne kutapika na kuhara palepale RAIA waliponishtukia wakaanza nikimbiza na mapanga wengine magongo sauti zilisikika zikisema "lazma tukukate vipandevipande" kwa bahat nzur kulikuwa kuna fuso sjui Lori hata skumbuk vzr lilikuwa linaanza kuondoka sjui lilikuwa linaenda WAP bas bwana nikalidandia baada ya masaa mawil mule ndan ya fuso simu yangu inaita mama mwenye nyumba anasema upo WAP mbona kuna polis wanakutafuta hapa nikakata Sm mara tena simu inaitaa kapiga RFK take yule mshkaj anatuifadhia nyama akasema nyama yako ina nn jamaa alikuibia kdogo kaenda itumia gheto sahiv ninavyokwambia tumemuwahisha hospital nikakata Sm .gar likiwa linaenda ktk kukaguakagua mule ndan nikakuta magunia kuyacheck ndani naona bangi pia kulikuwa na madawa mengne syajui kumbe skudandia fuso nilidandia kifo Mara gar likasimama kumbe hlo eneo kulikuwa na police patrol nkasikia shuken wote tukague gari
Eeh, ikawaje rafiki maana inaonekana wewe ulifia palepale kwa pressure
 
Aisee nimecheka sana maana tukio kama hili lilinitokea nikiwa nakata majani juu ya mti unaoitwa "mhesi" kule Rombo, kumbe nilikuwa nimeshikilia kimti kikavu kikakatika nikashika kwa kichwa hadi chini phuuh!.
Nilijaribu kuinuka nikae lakini nikashindwa na sauti ya kulia nayo ikawa haitoki. Nikatulia kama dakika moja nguvu zikanijia lakini shingo sidhubutu kuigeuza maana ilikuwa inauma balaa.
Niliposimama nikageuka kumbe pale chini palibakibaki na nywele za kichwani kutokana na kile kishindo nilichoanguka nacho [emoji23][emoji23]
Siku nyingine tena nilitoka shule nikawahi fasta kwenda kupanda juu ya mwembe kujisevia kama ilivyo kawaida yangu, baada ya kula na kushiba hukohuko juu ikawa ni wakati wa kushuka sasa.
Nilikuwa na tabia ya kushuka kwa kutumia matawi ya huo mwembe,, sasa wakati natumia tawi kushuka si likaachia kule juu/likakwanyuka kwa kuzidiwa na uzito! Nilitangulia chini nikiwa nabembea na ule mti hadi chini alafu matawi yake yakanifunika nikalala palepale usingizi mzito hadi usiku wa saa 2 kasoro ndio nilizinduka
Haha pole mkuu daah hakukuwa na watu eneo hilo?
 
USHUHUDA wangu mimi :


Mimi mwaka 1998, nikiwa nasoma primary huko Arusha tulikuwa na tabia ya kutoroka kipindi cha dini siku ya ijumaa na kuondoka na wanafunzi wa kiislam waliokuwa pekee wanaruhusiwa kwenda nje ya campus ya shule kwenda msikitini.

Tulikuwa tunatembea na manati kulenga ndege na kwenda kuogelea mto themi. (Wakati huo ulikuwa na maji mengi sana hata kuuvuka ni tabu)

Siku moja tukaenda kuogelea wanne...mmoja alikuwa mdg zaidi wakati wa kuogelea tukafika mahali penye kina kirefu haswa na kuogelea penyewe hatujui vizuri...nilikunywa maji haswa mpaka tumbo likajaa tukaja nikaja kutapishwa maji na jamaa mmoja alikuwa anakata ndizi shambani.

Wakati nipo nje natetemeka baridi nikakumbuka yule dogo alikuwa kwny maji...akaibuka mara moja na kuniambia kwa sauti

"MUAGE MAMA YANGU" wakati huo mimi nilikuwa na begi lake la sport, viatu na soksi miguuni kwangu.

Rafiki yangu tena alihamia kutoka shule ya msingi huko Moshi na tulikuwa tunakaa siti moja alifia palepale....sintosahau anaitwa ROMAN ARMANDO MLAKI.

Siku ya kumzika tulienda wanafunzi wa karibu darasa zima na yawezekana hata hapa wapo wanaomkumbuka na siku ya kuvunja matanga nikapewa vile viatu vyake, sox na madaftari.

Ilikuwa ni Mazishi ya KWANZA mimi kuhudhuria na nlikuwa kama naota vile.

Watu wakawa wanasema hajafa kachukuliwa na Chunusi...mpk leo sijui chunusi ni nini.
 
USHUHUDA wangu mimi :


Mimi mwaka 1998, nikiwa nasoma primary huko Arusha tulikuwa na tabia ya kutoroka kipindi cha dini siku ya ijumaa na kuondoka na wanafunzi wa kiislam waliokuwa pekee wanaruhusiwa kwenda nje ya campus ya shule kwenda msikitini.

Tulikuwa tunatembea na manati kulenga ndege na kwenda kuogelea mto themi. (Wakati huo ulikuwa na maji mengi sana hata kuuvuka ni tabu)

Siku moja tukaenda kuogelea wanne...mmoja alikuwa mdg zaidi wakati wa kuogelea tukafika mahali penye kina kirefu haswa na kuogelea penyewe hatujui vizuri...nilikunywa maji haswa mpaka tumbo likajaa tukaja nikaja kutapishwa maji na jamaa mmoja alikuwa anakata ndizi shambani.

Wakati nipo nje natetemeka baridi nikakumbuka yule dogo alikuwa kwny maji...akaibuka mara moja na kuniambia kwa sauti

"MUAGE MAMA YANGU" wakati huo mimi nilikuwa na begi lake la sport, viatu na soksi miguuni kwangu.

Rafiki yangu tena alihamia kutoka shule ya msingi huko Marangu-Moshi na tulikuwa tunakaa siti moja alifia palepale....sintosahau anaitwa Roman Armando Mlaki.

Siku ya kumzika tulienda wanafunzi wa karibu darasa zima na yawezekana hata hapa wapo wanaomkumbuka na siku ya kuvunja matanga nikapewa vile viatu vyake, sox na madaftari.

Ilikuwa ni Mazishi ya KWANZA mimi kuhudhuria na nlikuwa kama naota vile.

Watu wakawa wanasema hajafa kachukuliwa na Chunusi...mpk leo sijui chunusi ni nini.
 
USHUHUDA wangu mimi :


Mimi mwaka 1998, nikiwa nasoma primary huko Arusha tulikuwa na tabia ya kutoroka kipindi cha dini siku ya ijumaa na kuondoka na wanafunzi wa kiislam waliokuwa pekee wanaruhusiwa kwenda nje ya campus ya shule kwenda msikitini.

Tulikuwa tunatembea na manati kulenga ndege na kwenda kuogelea mto themi. (Wakati huo ulikuwa na maji mengi sana hata kuuvuka ni tabu)

Siku moja tukaenda kuogelea wanne...mmoja alikuwa mdg zaidi wakati wa kuogelea tukafika mahali penye kina kirefu haswa na kuogelea penyewe hatujui vizuri...nilikunywa maji haswa mpaka tumbo likajaa tukaja nikaja kutapishwa maji na jamaa mmoja alikuwa anakata ndizi shambani.

Wakati nipo nje natetemeka baridi nikakumbuka yule dogo alikuwa kwny maji...akaibuka mara moja na kuniambia kwa sauti

"MUAGE MAMA YANGU" wakati huo mimi nilikuwa na begi lake la sport, viatu na soksi miguuni kwangu.

Rafiki yangu tena alihamia kutoka shule ya msingi huko Moshi na tulikuwa tunakaa siti moja alifia palepale....sintosahau anaitwa ROMAN ARMANDO MLAKI.

Siku ya kumzika tulienda wanafunzi wa karibu darasa zima na yawezekana hata hapa wapo wanaomkumbuka na siku ya kuvunja matanga nikapewa vile viatu vyake, sox na madaftari.

Ilikuwa ni Mazishi ya KWANZA mimi kuhudhuria na nlikuwa kama naota vile.

Watu wakawa wanasema hajafa kachukuliwa na Chunusi...mpk leo sijui chunusi ni nini.
Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom