Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Mie bhana nakumbuka ilikuwa 2003 nipo Darasa la Tano Kunduchi Dar.

Kisa kenyewe ilikuwa ni ugomvi baina yangu mm na mwanafunzi mwenzangu wa darasa la saba.

Sijui ni utoto au nini tukapanga tupigane baada ya muda wa masomo kuisha. Mie nilikuwa na kundi kubwa la wapambe asikwambie mtu ukiwa na wapambe unajiamini balaaa.

Mwenzangu yupo peke ake baada ya muda wa masomo kuisha tukaruhusiwa, Wana wakanipanga twende zetu na yule mpinzani wangu akatafutwa tukatokomea porini uko.

Nikavua Begi wapambe wakanishikia jamaa akasogea ngumi zikaanza Daah mie nina bonge la nyomi la wapambe Piga huyo!! Mng'oe Meno huyo!!

Bichwa likavimba Mbwembwe nyingi ,Basi mara Ngumi Mara Teke, Kwepa Tena Kwepa Nikampatia Moja Saafi ya Mdomo Akachanika Kidogo Damu Ikaanza Kutoka.

Daah kumbe ndo nimemjeruhi simba, Nilikula mbata za kutosha hadi nikaona kizunguzungu nikazirai.

Wana wote wakakimbia nililala pale sijitambui kwa nusu saa. Bahati kuna mzee alikuwa anapita akaniona nimelala uso umevimba Shati limechanika Daah

Ndo akanibeba kunipeleka shule uku sijitambui kuwaelezea walimu nikamwagiwa maji sijui ndo kunipeleka hospital Wakaitwa wazazi.

Daah Kesi ilikuwa kubwa mno, Wazazi wote wakaitwa.Nashukuru Mungu yaliisha ila nimekoma Kupewa Sifa za Kijinga Inaponza Watu.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] mbavu
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.

Vitu vingine vya hatari ila vinavyohadithiwa inabili tucheke tu....
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.
Hahahahaha jamani jamani, hakika nimecheka mpk nimelia.
Tukio linasikitisha ila namna ya usimuliaji ni balaa hahhaha.
Pole sana lkn!
 
Daah inanikumbusha miaka 1996 nikiwa Mpanda, kipindi hicho nikiwa Secondary ili kila inapofika ijumaa nilikua natoroka kwenda machimboni kwakua kipindi hicho hela ilikua inapatikana kirahisi sana.

Nilikua nikifika huko naingia kwenye shimo lenye urefu wa zaidi ya mita ishirini, chini kabisa nilikua naingia ndani ya "fonka " liliokaa mfano wa chumba ambalo ndio nakwenda kuchimba katika mkondo wenye Dhahabu nyingi.

Kwakua nilihitaji pesa nilizoea kufanya shughuli hiyo kwa siri na sikutaka mtu yeyote shuleni na nyumbani ajue kama naendaga machimboni kwasababu nilikua bado mwanafunzi.

Siku moja tulipata jiwe kubwa la dhahabu na baada ya mgao nilipewa milioni 12 malipo ya mwanzo ila kutokana na umri wangu ilikua ni nyingi sana na siku hiyo niliamua kwenda kumpa dada angu aniwekee kisha nikarudi kwa kusubiria hela nyingine.

Tukiwa ndani walikuja jamaa wakiwa na silaha wakitaka wapewe pesa zote, watu walikula bakora siku hiyo ni balaa. Kuna brother mmoja nakumbuka alijisaidia pale pale. Mimi nilitumbukizwa kweny pipa la maji ikawa kila napotoa kichwa nje nakutana na kibao cha kichwani narudi kwenye maji,ilifikia muda nikapoteza fahamu nimekuja kupata fahamu jamaa wamechukua kila kitu lakini bahati yangu ni kwamba hela nilikua nishazipeleka kwa dada angu.

Pamoja na hayo sikuacha kwenda katika uchimbaji na kipindi hicho nikanunua kipimo cha zahabu ambazo zinapatikana juu juu ya kwenye ardhi nikawa naingiza pesa kwenye mashine na kwenye mashimo marefu niliendelea ku- hustle kama kawaida.

Siku moja nikiwa ndani ya shimo chini kabisa udongo ulikua ukiporomoka na maji yalikua yameanza kujaa hivyo nikawa nachota maji naweka kwenye ndoo kisha inavutwa maji yanamwagwa nje ya shimo lakini wakati shughuli inaendelea ulibomoka ukuta na kurudisha ndoo chini,mimi niliona giza ghafla hivyo nikakimbilia kwenye chumba cha shimo ambako nako hakuna njia ya kutokea. Hewa ilikua inapita lakini maji yalikua yakizidi kuongezeka hivyo nikajua lazima nife.

Kwamba mbaaali sana nilikua nasikia sauti za watu wakigombana kwamba waite polisi ndipo waje waanze kutoa udongo Lakin kuna jamaa yangu mmoja siji kumsahau, yeye alikataa akawaambia wachimbe kwanza wautoe mwili ndipo waite polisi kwasababu wakiacha muda mrefu bila kuwahi kuutoa mwili maji yanaweza kuwa mengi alafu ikawa shida ndipo kazi ikaanza.

Nashukuru Mungu kuna mmoja wao aliona mwanga wa tochi yangu kupitia kitundu kidogo sana,akawaeleza wenzake kwamba nitakua mzima kwasababu kama ningekua nimepoteza uhai tochi ingezama kwenye maji na isingetoa mwanga hivyo wakapiga kazi kwa kufuata mwanga mdogo wa tochi.

Kuna muda nikawa naita ila kwasababu ya kishindo cha sululu ya kuchimbia wakawa hawasikii baada ya muda walitoboa tundu angalau hewa ikaongezeka na tukawasiliana vizuri hadi nilipo okolewa kutoka kwenye fonka hiyo.

Tangu siku hiyo sikutaka kusikia tena habari za machimbo. Huko roho mkononi maana kazi ngumu, hatari ni nyingi na bado ukipata vihela kidogo majambazi wanakuvizia.

Mmh.. pole sana...ama uliponea tunda la sindano. Angalau 'vijisenti' vilikuwa mahali salama...
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Pole sana
 
Nakumbuka kipind niko sekondari tulikua tunapita shortcut njia ya mtoni siku hyo mvua imenyesha mto ukajaa na ujeur wetu tukasema acha tupite huko huko.

Tumevuka kidaraja cha kwanza cha mnazi fresh tu sehem ya pila daraja ni chasis ya roli, tunapita kwa kuruka ruka huku na huku hamadi nmeangusha kiatu.

Nkasema ngoja nikiwah ahaa wapi nilibebwa na maji ya mvua nikazama na kuibuka kama mara mbili hvi ya tatu naona matete haya hapa nikayakamata.

Kumbe ule upande wenye matete ni upande wapil wenzangu wako ng'ambo ikabd washikane mikono kuja kunivuta aisee nmetoka pale nmepoteza viatu vyote na begi la madaftari nkarud home kimyaa mpka leo sijawah kusema kwa familia kama nilnusurika kubebwa na Maji.
Hahaha mzeee.
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.

Hahahaaaaa!! Ulikuwa na vituo viwili, mpapai ulikuwa mrefu balaaa!! Ningekuwa mimi ni wewe ningeyala kwa hasira kuyakomoa hahahaaaa
 
Back
Top Bottom