Tukio la Arusha: Nchimbi ajichanganya Bungeni

Tukio la Arusha: Nchimbi ajichanganya Bungeni

Magesi

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2012
Posts
2,590
Reaction score
589
Waziri EMMANUEL NCHIMBI katika taarifa yake ndani ya bunge amejichanganya juu ya idadi ya watuhumiwa waliokwisha kukamatwa kuhusiana na mlipuko wa Arusha.

Jana wakati akiongea na STAR TV alinukuliwa akisema idadi ya waliokamatwa ni sita lakni leo ndani ya bunge amesema ni watatu.

Je umakini wake uko wapi?
 
Waziri EMMANUEL NCHIMBI katika taarifa yake ndani ya bunge amejichanganya juu ya idadi ya watuhumiwa waliokwisha kukamatwa kuhusiana na mlipuko wa Arusha.Jana wakati akiongea na STAR TV alinukuliwa akisema idadi ya waliokamatwa ni sita lakni leo ndani ya bunge amesema ni watatu.Je umakini wake uko wapi?

umakini wake upo kwenye kumtetea kinana......kuwamaliza ndovu wetu
 
Anasahau kuwa ukiwa muongo unatakiwa kuwa na kumbukumbu. Kashasahau jana alidanganya vipi
 
Naskia kama kawaida wanakamata machizi na mateja mitaani ili wawasakizie kesi!
 
Kwa nini wana Jf hatuungani kumtaka Nchimbi ajiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani?mauaji mangapi yameshatokea na bado yanaendelea kutokea huku tukiendelea kumlalamikia juu juu tuu na sharubu zake?
 
unategemea aongee nini mpiga tunguli mkubwa yule aka phd ya tunguli
 
Kwan wazir ndo anaekamata hao watuhumiwa? Si anapewa taarifa tu yeye ana deliver?...lawama apewe anaempa hizo information! That means polis ndo mambulula plus intelijensia
 
Hawa ndio aina ya mawaziri wa serikali ya CCM. Ukumbuki Maghembe alikitaja kijiji alichosema kipo Arumeru Mashariki, alipoambiwa hakuna kijiji kama hicho alibakia anabung'aa tu.
 
Inawezekana pia hakuna aliyekamatwa.Nadhani walikua wanataka kumwoshesha lema kuwa wanauwezo wa kuwakamata. Vinginevyo watuonyeshe picha na video.

Kwanini wanatoa matamko bila kuwaleta wahalifu na kuwaonyesha ni hawa ndo tuliowakamata mpaka sasa?
 
Jamani wale wafuga ndevu na wavaa suruali fupi,wavaa kanzu na bakarashia kaeni chonjo maana intelijensia yao imekalia huko,Mungu atunusuru na balaa hili maana tulizoea kuyaona haya mambo toka nchi nyingine leo yamefika kwetu.
 
umakini wake upo kwenye kumtetea kinana......kuwamaliza ndovu wetu

Kilaza mwingine huyu....

Mwongo msahaulifu

Ivi Tanzania tuna mawaziri basi?

Anasahau kuwa ukiwa muongo unatakiwa kuwa na kumbukumbu. Kashasahau jana alidanganya vipi

Lini aliwahi kusema ukweli?..
Mnatakiwa kufahamu kuwa sio kila anaeshukiwa au kukamatwa ni mualifu, polisi inakamata inahoji ikiridhika na maelezo yako unaachiwa.. sasa mnataka kama wamekamatwa watu kumi basi ndio hao waliolipua bomu?
Hata nyie na lema wenu tunaweza kuja kuwadabua na kuwapoteza ndani kwa muda tukiridhika na maelezo tunakuachia.

 
Mimi ninamuomba mungu ili watu wasio husika wasisingiziwe,wala kubambika kesi kwani suala kama hili lina hitaji inteligensia
Mara nyingi hawa huwa wanakurupuka
 
Waziri EMMANUEL NCHIMBI katika taarifa yake ndani ya bunge amejichanganya juu ya idadi ya watuhumiwa waliokwisha kukamatwa kuhusiana na mlipuko wa Arusha.

Jana wakati akiongea na STAR TV alinukuliwa akisema idadi ya waliokamatwa ni sita lakni leo ndani ya bunge amesema ni watatu.

Je umakini wake uko wapi?

Tangulini Nchimbi akawa makini? hata bosi wake hayuko makini sasa unategemea nini hapo?
 
Mnatakiwa kufahamu kuwa sio kila anaeshukiwa au kukamatwa ni mualifu, polisi inakamata inahoji ikiridhika na maelezo yako unaachiwa.. sasa mnataka kama wamekamatwa watu kumi basi ndio hao waliolipua bomu?
Hata nyie na lema wenu tunaweza kuja kuwadabua na kuwapoteza ndani kwa muda tukiridhika na maelezo tunakuachia.

Hii sasa gesi, nadhani unahitaji Magnesium
 
Back
Top Bottom