Financial Analyst
JF-Expert Member
- Nov 27, 2017
- 2,296
- 5,248
#HABARI Kijana mmoja mfanyabiashara mkazi wa Mbugani Jijini Mwanza, anayejulikana kwa jina la Mzafaru Yunus (26), amefariki dunia baada ya kudaiwa kushambuliwa kikatili ndani ya Baa iliyopo Kona ya Bwiru, Kata ya Nyamanoro wilayani Ilemela, kufuatia kushindwa kulipa bili ya vinywaji yenye thamani ya Sh 8,000.
Tukio hilo limeibua taharuki miongoni mwa wakazi huku Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza likiwashikilia watu tisa wanaodaiwa kuhusika, wakiwemo walinzi wawili maarufu kama mabaunsa.
Akizungumza kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa amesema marehemu alishambuliwa kwa ngumi, mateke, vipande vya mbao pamoja na bomba la chuma sehemu mbalimbali za mwili wake hadi kupoteza maisha.
Soma Pia: Arusha: Polisi auawa na wananchi akidhaniwa kuwa mwizi, Sita wakamatwa kwa tuhuma za mauaji
Amesema miongoni mwa waliokamatwa ni meneja wa baa hiyo, wafanyakazi wa usafi na walinzi wawili, huku watuhumiwa wengine wakidaiwa kutoroka kabla ya kukamatwa na polisi wanaoendelea na uchunguzi wa tukio hilo. #EastAfricaTV