Tukio ambalo sitoweza kulisahau daima

Tukio ambalo sitoweza kulisahau daima

Hasira wapi wewe acha kujifanya una hisia za matatizo yasiyo kuhusu wewe!!!

Una uhakika gani kama hiyo habari ni ya kweli... Ulikuepo???

Wapi uliona Simba anakula nyama na kubakiza mifupa!!
Simba anakunywa damu tu, akishiba damu anasepa zake...
Kula mizoga ni kazi ya Fisi.
Hakuna sehemu jamaa kaongelea mzoga, by the way simba akikamata shingo sio kuwa lengo anywe damu, NOPE.

Lengo ni kumbana pumzi mnyama ili afe...
 
Pole sana Mkuu. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya mama yetu mahali pema peponi.

Nakumbuka siku kama ya leo tarehe 21/04/2016 nilikuwa katika mtihani mzito ambao sitakuja usahau katika maisha yangu yaliyobakia hapa duniani, Niliondokewa na mama yangu mzazi Duniani tarehe 19/04/2016 na tulimzika tarehe 21/04/2016 mkoani Tanga Wilayani Muheza. Ndugu zangu had leo hii sina mama mwenzenu, kitu hiki kinaniumiza sana katika maisha yangu ya kila siku. Siwezi kusahau na huwa halinitoki moyoni. Naumia sana. Bali namuomba mwenyezi mungu amuepushe na adhabu ya kaburi na amuwekee mwanga katika kaburi lake. "Ameen"
 
Duh! Hili ni tukio la kutisha sana kulishuhudia. Pole sana Mkuu.

HESHIMA KWENU WANAJUKWAA.

Mnamo mwaka 2000 mwezi February tukiwa shamba kwa kilimo cha mpunga katika wilaya ya Kilombero(Ifakara) maeneo ya Mchombe mashambani sehemu inayoitwa Simbagungile tulivamiwa na simba majira ya saa 6 kasoro.

Nyumba ilikuwa ya chini yaani imejengwa kwa miti tu na kutumia nyasi kama ukuta na juu nkuezeka kwa nyasi, walikuwa simba wawili na sisi ndani tulikuwa watu wanne, punde tukajikuta katika shambulio nashukuru nifakiwa kupanda juu ya kitanda chetu cha miti na kupanda juu ya nguzo moja wapo ya kile kinyumba chetu.

Huku nikiwa juu nilishuhudia simba wakiwatafuna wale ndugu zangu bila huruma hadi kuwaua wote watatu na kuwatafuna na kubakiza mabaki kama ngozi, fuvu la kichwa na miguu na mikono kwa wote. Walipomaliza wakaingia huku na kule na kutoka nje ya nyumba baadae mmoja akarudi ndani na kutoka pia wale simba walienda kuvamia nyumba zingine mbili.

R.I.P ALL.

JE WEWE MWENZANGU NI TUKIO LIPI AMBALO HUTOWEZA KULISAHAU?

Karibu
 
Nakumbuka siku kama ya leo tarehe 21/04/2016 nilikuwa katika mtihani mzito ambao sitakuja usahau katika maisha yangu yaliyobakia hapa duniani, Niliondokewa na mama yangu mzazi Duniani tarehe 19/04/2016 na tulimzika tarehe 21/04/2016 mkoani Tanga Wilayani Muheza. Ndugu zangu had leo hii sina mama mwenzenu, kitu hiki kinaniumiza sana katika maisha yangu ya kila siku. Siwezi kusahau na huwa halinitoki moyoni. Naumia sana. Bali namuomba mwenyezi mungu amuepushe na adhabu ya kaburi na amuwekee mwanga katika kaburi lake. "Ameen"
Pole sana mkuu
 
Hasira wapi wewe acha kujifanya una hisia za matatizo yasiyo kuhusu wewe!!!

Una uhakika gani kama hiyo habari ni ya kweli... Ulikuepo???

Wapi uliona Simba anakula nyama na kubakiza mifupa!!
Simba anakunywa damu tu, akishiba damu anasepa zake...
Kula mizoga ni kazi ya Fisi.
Acha uongo wewe.
 
Yani watu wanne wote mnakubali kushambuliwa na simba wabee tu kweli mnatakiwa kuja masaini kuchukua course ya ujasiri na kupambana na viumbe kama hao
 
HESHIMA KWENU WANAJUKWAA.

Mnamo mwaka 2000 mwezi February tukiwa shamba kwa kilimo cha mpunga katika wilaya ya Kilombero(Ifakara) maeneo ya Mchombe mashambani sehemu inayoitwa Simbagungile tulivamiwa na simba majira ya saa 6 kasoro.
Hadithi ya uongo hii. Ni mtoto wa darasa la kwanza ndio atakuamini. Mtu anayejua tabia za simba anavyowinda anajua kabisa huu ni uongo wa mchana kweupe.
 
Hamna kitu hapo...
Mimi naona huu ni uongo kama sio ukweli uliozidishwa chumvi.

Simba wakikamata windo huwa wanakunywa damu tu na kuondoka.
Hawali mizoga Simba, hiyo ni kazi ya Mbweha (Hyena).

Hata kwenye Animal Planet tunaonaga sana tu.
Duh mkuu usingecoment tu
 
Pole sana kwenu nyoote mlioondokewa na wapendwa wetu kwa namna yoyote ile.
 
Hamna kitu hapo...
Mimi naona huu ni uongo kama sio ukweli uliozidishwa chumvi.

Simba wakikamata windo huwa wanakunywa damu tu na kuondoka.
Hawali mizoga Simba, hiyo ni kazi ya Mbweha (Hyena).

Hata kwenye Animal Planet tunaonaga sana tu.
Hata siku moja simba hanywi wala hanyonyi damu.

Unavyomuona simba amemkamata mnyama kwenye koromeo huwa anamziba pumzi afe na sio kunyonya damu.
 
Nakumbuka siku kama ya leo tarehe 21/04/2016 nilikuwa katika mtihani mzito ambao sitakuja usahau katika maisha yangu yaliyobakia hapa duniani, Niliondokewa na mama yangu mzazi Duniani tarehe 19/04/2016 na tulimzika tarehe 21/04/2016 mkoani Tanga Wilayani Muheza. Ndugu zangu had leo hii sina mama mwenzenu, kitu hiki kinaniumiza sana katika maisha yangu ya kila siku. Siwezi kusahau na huwa halinitoki moyoni. Naumia sana. Bali namuomba mwenyezi mungu amuepushe na adhabu ya kaburi na amuwekee mwanga katika kaburi lake. "Ameen"

Pole Gololi ata mim sina mama ila jipe moyo,Mungu anajua yote,R.I.P mom..
 
Hivi mkuu kweli umeshikilia hoja yako ya simba kunywa damu tu? Na unaitaje windo jipya (a fresh kill) mzoga asee? Mzoga ni mabaki ya mnyama yaliofikia hatua ya kuoza baada ya kufa, kuliwa (au kutokuliwa) na kuacha to the mercy of Mother Nature.

Simba dume katika mlo mmoja/one seating (pale wanapowinda mnyama mkubwa kama nyati, zebra, etc) anaweza kula mpaka kilo 20-25 za nyama na pengine zaidi ya hapo. Na hivi mnyama kama simba angekuwa wa kunywa damu tu, angekuwa na ufanisi wa ku'survive kiasi hiki tunavyomjua kama mfalme wa nyika?

Labda kama hauko serious (I'm not questioning your seriousness though) na unachosema, lakini kama uko serious... Again, check your facts sheet, bro!.
Yaani hapa wewe King Shaat ndo unaonekana mbu mbu mbu...sababu ya kupoteza muda kwa kuelimisha kichwa kigumu cha huyo mpuuzi.......Anajiona anajua...kumbe jinga tu......mbaya zaidi uko serious kabisa....hawa ndo wamekua juzi tu....
 
Hasira wapi wewe acha kujifanya una hisia za matatizo yasiyo kuhusu wewe!!!

Una uhakika gani kama hiyo habari ni ya kweli... Ulikuepo???

Wapi uliona Simba anakula nyama na kubakiza mifupa!!
Simba anakunywa damu tu, akishiba damu anasepa zake...
Kula mizoga ni kazi ya Fisi.
Mkuu ina maana Simba chakula chake ni damu tupuuu
 
Hamna kitu hapo...
Mimi naona huu ni uongo kama sio ukweli uliozidishwa chumvi.

Simba wakikamata windo huwa wanakunywa damu tu na kuondoka.
Hawali mizoga Simba, hiyo ni kazi ya Mbweha (Hyena).

Hata kwenye Animal Planet tunaonaga sana tu.

We jamaa bure kabisa, hebu kuwa na staha.

By the way, Simba huwa hanyonyi damu, Simba huwa anabana windo lake shingoni ili mnyama a-suffocate ili afe. Kifupi anambana pumzi ili afe, sio kunyonya damu.
 
HESHIMA KWENU WANAJUKWAA.

Mnamo mwaka 2000 mwezi February tukiwa shamba kwa kilimo cha mpunga katika wilaya ya Kilombero(Ifakara) maeneo ya Mchombe mashambani sehemu inayoitwa Simbagungile tulivamiwa na simba majira ya saa 6 kasoro.

Nyumba ilikuwa ya chini yaani imejengwa kwa miti tu na kutumia nyasi kama ukuta na juu nkuezeka kwa nyasi, walikuwa simba wawili na sisi ndani tulikuwa watu wanne, punde tukajikuta katika shambulio nashukuru nifakiwa kupanda juu ya kitanda chetu cha miti na kupanda juu ya nguzo moja wapo ya kile kinyumba chetu.

Huku nikiwa juu nilishuhudia simba wakiwatafuna wale ndugu zangu bila huruma hadi kuwaua wote watatu na kuwatafuna na kubakiza mabaki kama ngozi, fuvu la kichwa na miguu na mikono kwa wote. Walipomaliza wakaingia huku na kule na kutoka nje ya nyumba baadae mmoja akarudi ndani na kutoka pia wale simba walienda kuvamia nyumba zingine mbili.

R.I.P ALL.

JE WEWE MWENZANGU NI TUKIO LIPI AMBALO HUTOWEZA KULISAHAU?

Karibu
Pole sana mkuu,ila samahani kwa swali langu,uliposhuka baada ya hao simba kuondoka nguo zako hazikuchafuka kweli?hasa kaputula au suruali yako...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom