Pythagoras
JF-Expert Member
- Sep 24, 2013
- 2,334
- 6,121
daah mleta mada umenikumbusha kitambo sanaa, ni kijiji alichokuwa anaishi bibi yangu (RIP), kinaitwa Mngeta.
kipindi hicho kulikuwa na sifa kubwa ya kuvamiwa na simba sema wenyeji wanasema simba wengi wa kule ni wakutumwa na watu siyo simba halisi. mfano labda kulikuwa na ugomvi wa shamba au umedhurumu mpunga wa mtu bas rafiki yangu jiandae kuonana na simba mubashara.
nakumbuka mwaka 2004 nilienda kupeleka dawa ya kuua majani kwenye mpunga, kufika kule waliokuwa wanalima wakanambia yaani leo alfajiri tu simba walipita wakanionyesha na alama za miguu. nakumbuka ilitakiwa nirudi mapema ila nilikaa hadi wale jamaa wamalize kazi nirudi nao
kipindi hicho kulikuwa na sifa kubwa ya kuvamiwa na simba sema wenyeji wanasema simba wengi wa kule ni wakutumwa na watu siyo simba halisi. mfano labda kulikuwa na ugomvi wa shamba au umedhurumu mpunga wa mtu bas rafiki yangu jiandae kuonana na simba mubashara.
nakumbuka mwaka 2004 nilienda kupeleka dawa ya kuua majani kwenye mpunga, kufika kule waliokuwa wanalima wakanambia yaani leo alfajiri tu simba walipita wakanionyesha na alama za miguu. nakumbuka ilitakiwa nirudi mapema ila nilikaa hadi wale jamaa wamalize kazi nirudi nao