Nakumbuka siku kama ya leo tarehe 21/04/2016 nilikuwa katika mtihani mzito ambao sitakuja usahau katika maisha yangu yaliyobakia hapa duniani, Niliondokewa na mama yangu mzazi Duniani tarehe 19/04/2016 na tulimzika tarehe 21/04/2016 mkoani Tanga Wilayani Muheza. Ndugu zangu had leo hii sina mama mwenzenu, kitu hiki kinaniumiza sana katika maisha yangu ya kila siku. Siwezi kusahau na huwa halinitoki moyoni. Naumia sana. Bali namuomba mwenyezi mungu amuepushe na adhabu ya kaburi na amuwekee mwanga katika kaburi lake. "Ameen"