Tujiandae na 'lock down' nyingine kubwa

Tujiandae na 'lock down' nyingine kubwa

Madhila ya vita ya Iran na Marekani/Israel yameanza kuonekana tangu mwanzo mwa mwezi huu kwenye usafiri wa ndege

Baada ya airport za Qatar na Dubai kufungwa tickets za ndege zilipanda maradufu.. Imagine ticket ya ndege kutoka China kurudi Bongo ilipanda kutoka 2M mpaka 10M

Hii vita haina dalili na kumalizika leo wala kesho na ukosefu wa mafuta umeshaanza kushika kasi duniani .. Leo pipa moja la mafuta ghafi limefikia dola 175
Mataifa mengi yameshaanza kutoa tahadhari kwa wananchi wake kupunguza matumizi ya nishati (mafuta na gesi) sisi bado.. Lakini hatuko mbali

Lockdown ijayo si ya maradhi na barakoa na kujivukiza tena! Bali ni lockdown ya " movement limitations" kwakuwa mafuta yatapanda bei kupitiliza na yatakuwa hayapatikani kwa urahisi

Fursa fursana! Lockdown ya mafuta wakati itakapokuwa janga kwa wengine, kwingineko itakuwa ni neema na fursa ya kupiga ndefu
Jiandae ufaidike ama ujipange lockdown yaja!
Chai
 
Hii Ngoma ingenoga zaidi kama makombora ya Iran yangekuwa yanafika Washington😀🤓🤓🤓
Mwaka huu mtaona mzigo unashuka ndani ya USA, utashukaje tusikilizie kayakoroga lazima ayanywe. Jana muajemi ameuakana mzigo wake uliopiga zaidi ya 4000km..😁😁 Kila kukicha Trump anajitekenya na kucheka mwenyewe kuhusu Iran
 
Tutanyooka, nasubiri mwezi wa 4 tareh 5, mafuta tutatangaziwa lita 1 kuwa 4000
Trump na Nyau wakiendeza mambo yao ya kipuuzi wese litaondoka kabisa hata hilo la 4000 litakuwa linapatikana kwa kulenga, jamaa wameharibu uchumi wa dunia kwa kuingia kwenye vita ambayo haina kichwa wala miguu, ila mradi wao wamesababisha maafa
 
Hilo eneo si tumeambiwa,yanapita mafuta asilimia 20 tu..ina maana duniani patakuwa na uhaba wa mafuta asilimia 20
20% ni yale yanayopitia pale hormuz, vipi na vile viwanda vilivyoharibiwa? Vimepunguza asilimia ngapi katika soko?
Hapo huenda ikawa tayari ni 30%, ni nyingini sana katika soka la mafuta, chukua sisi mafuta tunanunua km 2800 hivi, tafuta 30% ya 2800, ni kama 840 hivi jumlisha kwenye 2800, hapo inakuwa kama 3640 hivi, maana yake hamna hamna hapo mafuta tutanunua kwa 3640, usishangae ikawa ni 4000 kabisa kwa lita, (factor ni nyingi)
na je Vipi houthi wakizuia ule mlango bahari wa kwao, kifuatacho ni kipi?
 
Madhila ya vita ya Iran na Marekani/Israel yameanza kuonekana tangu mwanzo mwa mwezi huu kwenye usafiri wa ndege

Baada ya airport za Qatar na Dubai kufungwa tickets za ndege zilipanda maradufu.. Imagine ticket ya ndege kutoka China kurudi Bongo ilipanda kutoka 2M mpaka 10M

Hii vita haina dalili na kumalizika leo wala kesho na ukosefu wa mafuta umeshaanza kushika kasi duniani .. Leo pipa moja la mafuta ghafi limefikia dola 175.

Mataifa mengi yameshaanza kutoa tahadhari kwa wananchi wake kupunguza matumizi ya nishati (mafuta na gesi) sisi bado.. Lakini hatuko mbali

Lockdown ijayo si ya maradhi na barakoa na kujivukiza tena! Bali ni lockdown ya " movement limitations" kwakuwa mafuta yatapanda bei kupitiliza na yatakuwa hayapatikani kwa urahisi

Fursa fursana! Lockdown ya mafuta wakati itakapokuwa janga kwa wengine, kwingineko itakuwa ni neema na fursa ya kupiga ndefu.

Jiandae ufaidike ama ujipange lockdown yaja!
Blaza Bob Marley said there comes a time total destruction is the only solution.Tunakwenda huko kwa kasi ya SGR.
 
Back
Top Bottom