Tujadili mambo ya msingi


Sawa kila la kheri...
 
Kukamilika sio lazima kuwa kama wazungu.
Unafahamu wahindi ni matajiri wakubwa hapa bongo, kule kwao ndugu zao huwa wanajisaidia vichakani?
Wao kutoka nchi moja kwenda kuwekeza nchi nyingine, hiyo ndio akili tunayoitaka; kwa nini sisi tunafeli?​
 
Kama huku kuna hiyo mianya, kwa nini bado tuko masikini na tunaenda huko nje kuombaomba?​
Kuombaomba ni mentality mbovu na ya uvivu, hakuna uhalali wowote wa sisi kuwa ombaomba.

Pili kuwepo kwa mianya hakumaanishi maskini watakoma ndio maana kila taifa dunia lina tabaka la maskini bila kujali level ya maendeleo ya taifa husika.
 
Na sahihi sisi kuendelea kuwa tegemezi miaka na miaka?
Sio sahihi ila ndio tuko chini ya social construct, tumetengenezwa hivyo kwa muda mrefu kwa plan mahususi Mkuu. Mfano je unaweza kuishi mwezi mmoja bila internet? Jibu ni utaweza lakn utapitia wakat mgumu sana, vp siku wakiamua kuzima internet mazima unafkr itakuaje? Ndo kama swali lako la tegemezi.. jibu ni tunaweza ila itakua ni patashika.
 
Kwa dunia ya sasa kuna mambo ukiyafanya yanaweza kuwa na maumivu kwa kila upande. Chukulia wewe ni supplier wa spare za pikipiki, ukaamua kutowauzi mafundi hizo spare. Ni kweli kwamba mafundi watateseka na lakini kwa muda huo hata wewe muuzaji hautakuwa unapata faida yoyote na mbaya zaidi unatengeneza mazingira ya hao mafundi kutotegemea huduma zako kwa siku zijazo. Issue ya utegemezi ina hit both ways supplier anafaidika na comsumer anafaidika.
 
Una point ila kumbuka anaetoa msaada ana upper hand na tegemezi lazima afate masharti atakayapewa lasivo mtoa msaada ana options nyingi, supplier hatetereki akipoteza mteja mmoja kati 100,000 alionao na wengine kibao wako pending wanasubiri usajili wa huduma
 
Ni sahihi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…