Sahihi kabisa lugha za kimagharibi huwa zinatuzuzua hakuna kitu kinaitwa 'fall in love' au 'love at the first sight' hakuna kitu kama hicho ulimwenguni.
Kitu kilichopo ni 'growth of love' ambayo inachukua muda mpaka kukua na kupevuka hivyo hapa katikati ni jukumu la _me na _ke kumwagilia na kupalilia ili penzi lao listawi, ambapo kunakuwa na changamoto nyingi sana ila somo ni uvumilivu na uaminifu.
Kinyume nakuijua hiyo definition tutaishia kulalama ooh mapenzi hakuna siku hizi sio siku hizi hata zamani kulikuwa hakuna hayo mapenzi ya 'european version' ambayo mnayataka baada ya kupumbazwa na utandawazi, ukitaka kupata mpenzi wa kweli fuata sheria za asili ambazo wengi mnaziita za kizamani au zimepitwa na wakati ila nakuhakikishia ukizifuata na Mungu akakujalia kumpata mwenza anayezifahamu na kuzifuata mtazeeka wote pamoja, kinyume na hapo hakuna na hatakuwepo sio bar, shuleni, kazini, kanisani wala msikitini.
#Back_to_my_roots