Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Wahuni wale walikua hawapunguzi ajali Wala nini. Ajali ya gari la wanafunzi Mtwara isingetokea Kama Hawa Wala rushwa wangekua wanakagua magari.

Nimpongeze IGP kwa hatua hii nzuri hasa kumuondoa trafik mmoja wa kike pale Ruvu jirani kabisa na hoteli ya JKT.

Mpangieni Yule mla rushwa kulinda nyumba ya DC wa kike awe anasikiliza miguno usiku.

Aliringa utafikiri daraja la Ruvu kalijenga babake.
Hahaha..

Watu mna matusi aisee...
 
... Bepari2020 ana hoja; tusimbeze. Tuwe wakweli, eneo linaloenda kuongezeka ajali ni wrong overtaking. Uwepo wa trafiki uliwafanya madereva waogope ku-overtake ovyo ovyo. Dereva haoni mbele kuna nini ana-overtake tu halafu analazimisha kuchomekea; wale wa mabasi mnawajua. Ukimkuta anayechomekewa naye ni m`bishi hiyo tayari ni ajali.

Ni kweli trafiki wana kero zao, ila their presence ina msaada mkubwa kuwafanya madereva wa ovyo ovyo kutokuvunja sheria ovyo hususan zile zenye serious impact.
Nipe sababu kwanini pale chalinze mpaka msoga paliponyooka pana mstari usioruhusu kuovertake
 
Kuna siku nipo na Noah,nikatolewa upepo buku tano bila sababu za msingi,sikua na kosa...walikuwa wengi mno barabarani
Hatukatai ndugu kuwa ni kweli kuwa kuna baadhi ya maaskari wamewageuza wenye magari kuwa ndio maduka yao.....lakini hiyo hairamishi uwepo wa wengine WANAOZINGATIA weledi wa kazi....
 
Kuna yeyote humu amewahi kukamatwa na trafiki na akalipishwa faini bila kosa lolote? Be honest; yaliyo moyoni kwako wayajua mwenyewe.

Hizo rushwa za elfu 5 au 10 sio sisi wenyewe tunawabembeleza kukwepa kulipa elfu 30? Tunawalaumu kwa lipi kuhusu rushwa? Unless tunalaumu mapato ya serikali kupotea which I don't think kama ndicho kinacholalamikwa na madereva.
Hivi kwa mfano kukutwa na leseni ya udereva iliyoisha muda wake (kwa wiki kadhaa) ni kosa la kuandikiwa faini?
 
Hivi kwa mfano kukutwa na leseni ya udereva iliyoisha muda wake (kwa wiki kadhaa) ni kosa la kuandikiwa faini?
... na mimi ndio huwa najiuliza hilo swali; kwamba leseni iki-expire automatically na skills za udereva zina-expire? Kimsingi hilo lilitakiwa liwe kosa la onyo tu ila trafiki wa nchi hii hawakuachi aisee; kwao ni bonge la bingo.
 
Nipe sababu kwanini pale chalinze mpaka msoga paliponyooka pana mstari usioruhusu kuovertake
... jukumu la kusimamia sheria ya usalama barabarani ni la polisi/trafiki; sio kazi yao kuweka alama zinazotafsiri sheria. Kuweka alama ni kazi ya TANROADS.
 

Gazeti la Raia Mwema limeripoti kwamba tayari panga limekwisha tembea, huku MCHEZO WA UPATU waliokuwa wanacheza Trafiki hao kila siku ukibaki njia panda , kwa vile wengi wamepangiwa kazi zingine ambazo haziingizi chochote zaidi ya Mshahara , TAARIFA ZINADOKEZA KWAMBA TRAFIKI WENGINE WALIKUWA NA MCHEZO WA UPATU WA KULIPA HADI SH LAKI MOJA KWA SIKU , ambapo inaelezwa kwamba chanzo cha hela hizo ilikuwa ni Rushwa za barabarani .

Kwa mujibu wa gazeti hilo , Trafiki wengi wanamlaumu Kinana kwa kuibua jambo hilo .

Endelea kubaki JF kwa taarifa zaidi.

PIA SOMA: Kinana akerwa na Utitiri wa Traffic barabarani. Atoa maagizo mazito kwa Afande IGP Camilius Wambura

Aiseee walikuwa kero jamani, wilaya moja unakuta vituo vyao vinne au zaidi.... Mbaya zaidi wote wanataka hela.... Mpaka madereva wakajizoesha kutoa hela kila wanapowaona hata kama hawajatajiwa makosa......
 
Kuna siku nipo na Noah,nikatolewa upepo buku tano bila sababu za msingi,sikua na kosa...walikuwa wengi mno barabarani
... mkuu uliamua tu kuwapa pesa kwa utashi wako; kama kweli hukuwa na kosa ulitakiwa kukataa. Kuna siku natokea Mbeya nimevuka Iringa mahali fulani patamu sana "kuokolea muda" pamenyooka sana karibu kuitafuta Ilula.

Kwa mbali kule nikaona kigari kimepaki pembeni kinatazama upande wa Iringa; nikajua tayari ni wenyewe; sikujali nikachochea. Kuwafikia nikawekwa pembeni ndani wako wanne. Naulizwa hujaona katazo la 50 pale? Nikawajibu hakuna katazo. Nikaulizwa, mbona kibao cha 50 kinaonekana pale?

Nikawajibu, 50 ya uelekeo wa Iringa inanihusu nini mimi nayeelekea Morogoro? Nikaulizwa, hata kama hukuona 50, si pana zebra pale? Jibu, hakuna alama yoyote inayoonesha kukariba zebra. Nilikomaa nao hadi wakanifukuza pale bila kuwapa chochote. Kama huna kosa, kuwa jasiri kama simba watakutimua japo utakuwa umepoteza dakika 10 au 15 hivi.

Tatizo ni kwamba kibao cha 50 ukitokea Iringa kuikaribia zebra kilikuwa hakipo japo just before nguzo bila kibao ilikuwepo hamad nilishaikaribia zebra ilikuwa ni hatari kufunga breki za ghafla and in fact mahali penyewe ni kapori fulani unajiuliza pana sababu gani ya kuweka zebra pale. Ila kwa trafiki tayari kwao ni fursa kuwapiga madereva. Narudia tena, huna kosa be CONFIDENT, usitoe pesa.
 

Gazeti la Raia Mwema limeripoti kwamba tayari panga limekwisha tembea, huku MCHEZO WA UPATU waliokuwa wanacheza Trafiki hao kila siku ukibaki njia panda , kwa vile wengi wamepangiwa kazi zingine ambazo haziingizi chochote zaidi ya Mshahara , TAARIFA ZINADOKEZA KWAMBA TRAFIKI WENGINE WALIKUWA NA MCHEZO WA UPATU WA KULIPA HADI SH LAKI MOJA KWA SIKU , ambapo inaelezwa kwamba chanzo cha hela hizo ilikuwa ni Rushwa za barabarani .

Kwa mujibu wa gazeti hilo , Trafiki wengi wanamlaumu Kinana kwa kuibua jambo hilo .

Endelea kubaki JF kwa taarifa zaidi.

PIA SOMA: Kinana akerwa na Utitiri wa Traffic barabarani. Atoa maagizo mazito kwa Afande IGP Camilius Wambura
Hahahahah nashukuru sana kwa hilo muda muafaka sasa wa kuamsha chombo changu 😂😂😂 afadhali nikomae na mafuta sheli ila sio hawa shenzi waliokuwa wametugeuza shamba labibi
 
Back
Top Bottom