Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Wanakagua nini kila km 100!? Acha kuhalalisha rushwa
Km 100 au 200 zinatosha kabisa kukaguliwa. Tena kuwe na logbook kituo kilichopita umetoka saa ngapi ili speed unayoenda idhibitiwe. Ukaguzi mkubwa wa ubora wa gari ufanyike stand na ukaguzi wa vituo usiwe juu ya dk 3. Chap chap.

"Dereva naomba logbook ya muda, Abiria salama? Mnaridhika na uendeshaji wa dereva? Safari njema".
 
FB_IMG_1659337962903.jpg
 
Kuna yeyote humu amewahi kukamatwa na trafiki na akalipishwa faini bila kosa lolote? Be honest; yaliyo moyoni kwako wayajua mwenyewe.

Hizo rushwa za elfu 5 au 10 sio sisi wenyewe tunawabembeleza kukwepa kulipa elfu 30? Tunawalaumu kwa lipi kuhusu rushwa? Unless tunalaumu mapato ya serikali kupotea which I don't think kama ndicho kinacholalamikwa na madereva.
Rushwa ni zile 10% zinazopeanwa kwenye mikataba mikubwa mikubwa, hivi vielfu elfu ni virushwa uchwara tu !!
 
Km 100 au 200 zinatosha kabisa kukaguliwa. Tena kuwe na logbook kituo kilichopita umetoka saa ngapi ili speed unayoenda idhibitiwe. Ukaguzi mkubwa wa ubora wa gari ufanyike stand na ukaguzi wa vituo usiwe juu ya dk 3. Chap chap.

"Dereva naomba logbook ya muda, Abiria salama? Mnaridhika na uendeshaji wa dereva? Safari njema".
Njia nyingine ni kuweka speed monitor cameras huko kwenye highways!!
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Njia nyingine ni kuweka speed monitor cameras huko kwenye highways!!
Hii nayo ni nzuri. Ila sasa kuzilinda maana watanganyika kwa vipuli. Mwanakijiji anaweza chomoa sababu anataka tule tunyaya mule ndani akatengeneze mtego wa ndegepori.
 
Hii nayo ni nzuri. Ila sasa kuzilinda maana watanganyika kwa vipuli. Mwanakijiji anaweza chomoa sababu anataka tule tunyaya mule ndani akatengeneze mtego wa ndegepori.
Kweli kabisa !!
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Kiyakacho tokea ni kama ya Jerry Muro watamuandali mitego ya kumtuhumu na kumkuta na hatia.
 
... mkuu uliamua tu kuwapa pesa kwa utashi wako; kama kweli hukuwa na kosa ulitakiwa kukataa. Kuna siku natokea Mbeya nimevuka Iringa mahali fulani patamu sana "kuokolea muda" pamenyooka sana karibu kuitafuta Ilula.

Kwa mbali kule nikaona kigari kimepaki pembeni kinatazama upande wa Iringa; nikajua tayari ni wenyewe; sikujali nikachochea. Kuwafikia nikawekwa pembeni ndani wako wanne. Naulizwa hujaona katazo la 50 pale? Nikawajibu hakuna katazo. Nikaulizwa, mbona kibao cha 50 kinaonekana pale?

Nikawajibu, 50 ya uelekeo wa Iringa inanihusu nini mimi nayeelekea Morogoro? Nikaulizwa, hata kama hukuona 50, si pana zebra pale? Jibu, hakuna alama yoyote inayoonesha kukariba zebra. Nilikomaa nao hadi wakanifukuza pale bila kuwapa chochote. Kama huna kosa, kuwa jasiri kama simba watakutimua japo utakuwa umepoteza dakika 10 au 15 hivi.

Tatizo ni kwamba kibao cha 50 ukitokea Iringa kuikaribia zebra kilikuwa hakipo japo just before nguzo bila kibao ilikuwepo hamad nilishaikaribia zebra ilikuwa ni hatari kufunga breki za ghafla and in fact mahali penyewe ni kapori fulani unajiuliza pana sababu gani ya kuweka zebra pale. Ila kwa trafiki tayari kwao ni fursa kuwapiga madereva. Narudia tena, huna kosa be CONFIDENT, usitoe pesa.
Kuna shule pale napafahamu
 
... mkuu uliamua tu kuwapa pesa kwa utashi wako; kama kweli hukuwa na kosa ulitakiwa kukataa. Kuna siku natokea Mbeya nimevuka Iringa mahali fulani patamu sana "kuokolea muda" pamenyooka sana karibu kuitafuta Ilula.

Kwa mbali kule nikaona kigari kimepaki pembeni kinatazama upande wa Iringa; nikajua tayari ni wenyewe; sikujali nikachochea. Kuwafikia nikawekwa pembeni ndani wako wanne. Naulizwa hujaona katazo la 50 pale? Nikawajibu hakuna katazo. Nikaulizwa, mbona kibao cha 50 kinaonekana pale?

Nikawajibu, 50 ya uelekeo wa Iringa inanihusu nini mimi nayeelekea Morogoro? Nikaulizwa, hata kama hukuona 50, si pana zebra pale? Jibu, hakuna alama yoyote inayoonesha kukariba zebra. Nilikomaa nao hadi wakanifukuza pale bila kuwapa chochote. Kama huna kosa, kuwa jasiri kama simba watakutimua japo utakuwa umepoteza dakika 10 au 15 hivi.

Tatizo ni kwamba kibao cha 50 ukitokea Iringa kuikaribia zebra kilikuwa hakipo japo just before nguzo bila kibao ilikuwepo hamad nilishaikaribia zebra ilikuwa ni hatari kufunga breki za ghafla and in fact mahali penyewe ni kapori fulani unajiuliza pana sababu gani ya kuweka zebra pale. Ila kwa trafiki tayari kwao ni fursa kuwapiga madereva. Narudia tena, huna kosa be CONFIDENT, usitoe pesa.
Nilikua na mishe nyingi
 
Wahuni wale walikua hawapunguzi ajali Wala nini. Ajali ya gari la wanafunzi Mtwara isingetokea Kama Hawa Wala rushwa wangekua wanakagua magari.

Nimpongeze IGP kwa hatua hii nzuri hasa kumuondoa trafik mmoja wa kike pale Ruvu jirani kabisa na hoteli ya JKT.

Mpangieni Yule mla rushwa kulinda nyumba ya DC wa kike awe anasikiliza miguno usiku.

Aliringa utafikiri daraja la Ruvu kalijenga babake.
Dah....yupi? Asia? 😂😂😂😂
 
Wakati mwingine unazitafakari akili za raia wa Tanzania katikati ya tafakuri yako ndio inakujia picha kwanini CCM bado ipo madarakani.

Kwa lugha nyepesi watanzania tuna uwezo mdogo sana wa kutafakari kwa kina na kuchanganua mambo ni kama mtoto mdogo anayepokonywa noti ya elfu kumi na kupoozwa na pipi ya mia akifurahia.
Sure
 
Mimi hapa nilisingiziwa mara kadhaa
  • Niliambiwa nimeovertake sehemu isiyo sahihi wakati mimi ndiye nimepitwa na mabasi - Sokoine Mvomero
  • Niliambiwa nimeoverspeed wakati waliooverspeed ili wanipite ni magari ya serikali nikiwa naendesha 50 - Mdaula
  • Niliambiwa chupa ya maji ya whipper haina maji ya kutosha - Chalinze
  • Windi shield ilipigwa na kokoto iliyoorushwa na gari la mbele wakati barabara inaongezwa layer ya lami pale Doma, nikaenda simama Mikumi nikatoa taarifa kwa traffic police, wakasema wataaminije kama nimepigiwa Doma, nikaomba kuonana na kiongozi wao, wakanielekeza alipo, nikamfuata, akasema nenda ila ukirudi Dar kabadili kioo, nikaomba maandishi ili yanisaidie mbele ya safari akasema kwa muda huo hana vitendea kazi (alikuwa na wageni kwenye restaurent moja inaitwa Halfway na ilikua giza limeingia) ila wakinishika niwaambie wampigie simu kupata ushahidi, Iringa nikashikwa nikawaambia nimeripoti Mikumi nikawapa namba za simu za askari wa Mikumi, wakaniambia niko mkoa mwingine, wakazuia leseni yangu, baada ya wiki nikaenda kulipa faini nikaondoka.
Pole sana,.
Traffic wa Iringa waliendekeza sana njaa. Kuna mwanamke mmoja ana ndevu, anakuwaga na mwenzake wa kiume, kuanzia eneo la Ilula kibaoni, ni msheeeeeeenzi sana. Wengine huwa wanavizia pale Nyololo na Mafinga. Wajinga sana. Wanabambikiza makosa.
 
Back
Top Bottom