Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Trafiki wapukutishwa barabarani, Vilio vyatawala

Tuliweka uzi humu kuhusu Polisi wa barabara kupunguzwa , huku wengi wao wakipangiwa kulinda Mabenki Usiku , lakini kwa bahati mbaya Moderator akaunga uzi ule kwa mafundo mengi utadhani HIRIZI WANAZOTAPIKA WAUMINI WA MWAMPOSA .

Lakini leo Gazeti la Raia Mwema limeripoti kwamba tayari panga limekwisha tembea , huku MCHEZO WA UPATU waliokuwa wanacheza Trafiki hao kila siku ukibaki njia panda , kwa vile wengi wamepangiwa kazi zingine ambazo haziingizi chochote zaidi ya Mshahara , TAARIFA ZINADOKEZA KWAMBA TRAFIKI WENGINE WALIKUWA NA MCHEZO WA UPATU WA KULIPA HADI SH LAKI MOJA KWA SIKU , ambapo inaelezwa kwamba chanzo cha hela hizo ilikuwa ni Rushwa za barabarani .

Kwa mujibu wa gazeti hilo , Trafiki wengi wanamlaumu Kinana kwa kuibua jambo hilo .

Endelea kubaki JF kwa taarifa zaidi .
Walikula vya watu Bure Bure Sasa wakubali kutapishwa,na kuwekwa juu ya mawe🤔
 
Spidi gavana hata ikiwepo kwenye gari dereva akiuondoa waya mmoja haifanyi kazi !! Kwahiyo spidi gavana ya kweli ni matrafiki kuwa wengi na tochi zao !! Vinginevyo tusubiri tuone !! Kisha wengine wataandika tuliwaonya wakadharau !!
Speed gavana ilikuwa ni dili la lowasa kutakatisha kodi zetu
 
Waweza kuwa mmoja wa uliyekuwa kikaangoni.🤔
Sio kweli Mkuu !! Mimi ni raia mwema tu ! Najaribu kutoa tahadhari maana mimi nimesafiri sana barabarani nawajua vizuri sana madereva wetu wa sasa huko barabarani akili zao huwa zinahama sijui huwa zinaenda wapi ! Ndio maana utaona kila wakati wanaulizana kwa ishara kama Trafiki wapo mbele au hawapo? Ili tu akanyage mafuta kisawasawa na bila kuchukua tahadhari yeyote !!
 
Askari wa barabarani wapo na wanaendelea na kazi zao kama kawaida.
Kilichopungua ni ule wingi na kero ambao ulikuwa unapunguza ufanisi na kusumbua raia kwa sababu binafsi zaidi.
Taasisi za udhibiti zisizo za kitaalamu, zinatakiwa kuwa na watendaji wchache wanaoendana na hali halisi, ili kupunguza rushwa na kero kwa wananchi.
 
Askari wa barabarani wapo na wanaendelea na kazi zao kama kawaida.
Kilichopungua ni ule wingi na kero ambao ulikuwa unapunguza ufanisi na kusumbua raia kwa sababu binafsi zaidi.
Taasisi za udhibiti zisizo za kitaalamu, zinatakiwa kuwa na watendaji wchache wanaoendana na hali halisi, ili kupunguza rushwa na kero kwa wananchi.
Umenena !!
 
Wakati mwingine unazitafakari akili za raia wa Tanzania katikati ya tafakuri yako ndio inakujia picha kwanini CCM bado ipo madarakani........kwa lugha nyepesi watanzania tuna uwezo mdogo sana wa kutafakari kwa kina na kuchanganua mambo.......ni kama mtoto mdogo anayepokonywa noti ya elfu kumi na kupoozwa na pipi ya mia akifurahia.....
Kwahiyo ww ulikuwa ukiona sawa trafick kukaa makundi makundi vile barabarani utadhani pundamilia tena highway??
 
Kuna yeyote humu amewahi kukamatwa na trafiki na akalipishwa faini bila kosa lolote? Be honest; yaliyo moyoni kwako wayajua mwenyewe.

Hizo rushwa za elfu 5 au 10 sio sisi wenyewe tunawabembeleza kukwepa kulipa elfu 30? Tunawalaumu kwa lipi kuhusu rushwa? Unless tunalaumu mapato ya serikali kupotea which I don't think kama ndicho kinacholalamikwa na madereva.
 
Tuliweka uzi humu kuhusu Polisi wa barabara kupunguzwa , huku wengi wao wakipangiwa kulinda Mabenki Usiku , lakini kwa bahati mbaya Moderator akaunga uzi ule kwa mafundo mengi utadhani HIRIZI WANAZOTAPIKA WAUMINI WA MWAMPOSA .

Lakini leo Gazeti la Raia Mwema limeripoti kwamba tayari panga limekwisha tembea , huku MCHEZO WA UPATU waliokuwa wanacheza Trafiki hao kila siku ukibaki njia panda , kwa vile wengi wamepangiwa kazi zingine ambazo haziingizi chochote zaidi ya Mshahara , TAARIFA ZINADOKEZA KWAMBA TRAFIKI WENGINE WALIKUWA NA MCHEZO WA UPATU WA KULIPA HADI SH LAKI MOJA KWA SIKU , ambapo inaelezwa kwamba chanzo cha hela hizo ilikuwa ni Rushwa za barabarani .

Kwa mujibu wa gazeti hilo , Trafiki wengi wanamlaumu Kinana kwa kuibua jambo hilo .

Endelea kubaki JF kwa taarifa zaidi .
 

Attachments

  • C25C05EF-F564-464A-8D6F-A24815ADC812.jpeg
    C25C05EF-F564-464A-8D6F-A24815ADC812.jpeg
    86.2 KB · Views: 17
Back
Top Bottom