Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha.

Tunapenda kuufahamisha umma na jamii kwa ujumla kuwa, Mamlaka haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCMA).

Bw. Emmanuel Gadi alifikisha malalamiko yake kwa njia ya barua tarehe 27 Februari, 2023 akidai kupewa uthibitisho na TRA wa kuingiza mzigo wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges’’ kupitia kampuni ya Tosh Logistics Ltd. TRA ilifanya uchunguzi wa kutosha na kuthibitisha kwamba, hapakuwa na mzigo wowote ulioingizwa nchini kwa jina la Wintech Tanzania Ltd wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges” kupitia kadhia yenye namba TZDL-22-1382193 ya tarehe 18 Agosti 2022 kama anavyodai.

Hivyo, TRA ilimjibu mhusika kupitia barua yenye kumbukumbu namba CF 8/92/01 ya tarehe 25 Julai 2023 ikimjulisha kuwa, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa “House Bill of Lading” na kutoonekana kwa mzigo huo kwenye kadhia iliyowasilishwa na kampuni ya Tosh Logistics Ltd, TRA isingeweza kuthibitisha kuingizwa kwa mzigo huo nchini.

Kupitia taarifa yake aliyoitoa kwenye vyombo vya habari tumebaini kuwepo viashiria vya ukwepaji kodi kwani ni dhahiri kuwa mzigo huu uliingizwa kwa njia za magendo. TRA inamtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe.


1697052593980.png


===========
Video ya Mfanyabiashara akiituhumu TRA
 
Jamaa kawaeleza mizigo inaingia kwa magendo wanamtaka yeye alete nyaraka as if yeye ni TRA. Mtu katoa taarifa, badala ya wafanyie kazi wao wanajitetea tu.

Rais Samia, mtimue Boss wa TRA. Wamezidi. wananchi Masikini wanaibiwa hakuna anaye jali.

WANALINDANA
 
Sakata la malalamiko ya mfanyabiashara Bw. Emmanuel Gadi, Mmiliki wa Kampuni ya Wintech Tanzania Ltd., dhidi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imechukua sura mpya baada ya TRA kubaini kile ilichotaja kuwepo viashiria vya ukwepaji kodi na kutuhumu kwamba mzigo wake uliingizwa kimagendo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata amesema kwamba ni dhahiri kuwa mzigo wa mlalamikaji huyo uliingizwa nchini kwa njia za magendo.

“TRA inamtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe”, imeeleza taarifa hiyo.

Bw. Kidata ametoa taarifa hiyo kufuatia taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijami inayohusu malalamiko ya Bw. Gadi kuwa TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria va Forodha.

Akifafanua Bw. Kidata amesema kwamba TRA haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo chini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCMA).

Akifafanua zaidi Kamishna huyo wa TRA amesema Bw. Emmanuel Gadi alifikisha malalamiko yake kwa njia ya barua tarehe 27 Februari, 2023 akidai kupewa uthibitisho na TRA wa kuingiza mzigo wa vifurushi 471 vya "Toner Cartridges" kupitia kampuni ya Tosh Logistics Ltd.

“TRA ilifanya uchunguzi wa kutosha na kuthibitisha kwamba, hapakuwa a mzigo wowote ulioingizwa nchini kwa jina la Wintech Tanzania Ltd wa vifurushi 471 vya "Toner Cartridges" kupitia kadhia yenye namba TZDL-22-1382193 ya tarehe 18 Agosti 2022 kama anavyodai.

“Hivyo, TRA ilimjibu mhusika kupitia barua yenye kumbukumbu namba CF 8/92/01 ya tarehe 25 Julai 2023 ikimjulisha kuwa, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa "House Bill of Lading" na kutoonekana kwa mzigo huo kwenye kadhia iliyowasilishwa na kampuni ya Tosh Logistics Ltd, TRA isingeweza kuthibitisha kuingizwa kwa mzigo huo nchini,’ amesema Bw. Kidata kwenye taarifa yake hiyo.

Bw. Kidata amesisitiza kwamba kupitia taarifa yake (mlalamikaji) aliyoitoa kwenye vyombo vya habari TRA imebainika kuwepo kwa viashiria vya ukwepaji kodi na kwamba ni dhahiri kuwa mzigo huu ulingizwa kwa njia za magendo.

Kamishna huyo wa TRA amemtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe.
fe3fda71-fdbb-4a91-a96a-91508e48f1a2.JPG
 
Sikiliza clip hii halafu soma majibu ya TRA.View attachment 2779614
Emma wanamuonea kabisa Kabisa na ile ajari ya mzigo ndio imezibua uozo wa TRA hata ingekua Nani Lazima angekua katika situation Kama hii, Taasisi ya Bima haiwezi kunilipa bila ya valid documents za forodha under a valid process with EACCMA, kitu ambach TRA hawaku a bid hapo mwanz na Emma hawezi kutupilia mbali malipo yake kutoka kwa Kampuni ya Bima

TRA wamtoe tu mtu sadaka tu
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya taarifa inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu malalamiko ya Bw. Emmanuel Gadi kuwa, TRA imetengeneza mfumo wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo halali wa Serikali kinyume na Sheria ya Forodha.

Tunapenda kuufahamisha umma na jamii kwa ujumla kuwa, Mamlaka haina mfumo wowote mwingine inaouendesha wa kuingiza mizigo nchini nje ya mfumo wa Forodha wa TANCIS ambao unatumika kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCMA).

Bw. Emmanuel Gadi alifikisha malalamiko yake kwa njia ya barua tarehe 27 Februari, 2023 akidai kupewa uthibitisho na TRA wa kuingiza mzigo wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges’’ kupitia kampuni ya Tosh Logistics Ltd. TRA ilifanya uchunguzi wa kutosha na kuthibitisha kwamba, hapakuwa na mzigo wowote ulioingizwa nchini kwa jina la Wintech Tanzania Ltd wa vifurushi 471 vya “Toner Cartridges” kupitia kadhia yenye namba TZDL-22-1382193 ya tarehe 18 Agosti 2022 kama anavyodai.

Hivyo, TRA ilimjibu mhusika kupitia barua yenye kumbukumbu namba CF 8/92/01 ya tarehe 25 Julai 2023 ikimjulisha kuwa, kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa “House Bill of Lading” na kutoonekana kwa mzigo huo kwenye kadhia iliyowasilishwa na kampuni ya Tosh Logistics Ltd, TRA isingeweza kuthibitisha kuingizwa kwa mzigo huo nchini.

Kupitia taarifa yake aliyoitoa kwenye vyombo vya habari tumebaini kuwepo viashiria vya ukwepaji kodi kwani ni dhahiri kuwa mzigo huu uliingizwa kwa njia za magendo. TRA inamtaka mlalamikaji kuwasilisha nyaraka na uthibitisho wa kampuni yake kuingiza mzigo huo nchini mara moja ili hatua stahiki zichukuliwe.


View attachment 2779318
Kama Bwana Gadi katoa bidhaa yake kwa magendo hilo tatizo ndiyo linakuwa la TRA zaidi. Hapo TRA unatoaje mzigo kwa magendo bila kuhusisha Taasisi za TRA.
Clearing and Forwarding Agent aliyetoa mzigo huo ni wakala wa Kamishna wa Forodha na anateuliwa na anasimamiwa na Kamishna wa Forodha, je mbona TRA haitoi ufafanuzi kama huyu alimtendea haki Gadi na kwa nini TRA isimhusishe kwenye sakata hilo. Wafanya biashara watakuwa na imani gani na Kamishna wa Forodha na TRA kama watakuwa wanateua majangili kuwa wakala wao? Lazima pande zote zitazamwe. Hii rufaa inakwenda kwa Rais, je huu ndiyo ushauri wa TRA wa namna ya kushughulikia tatizo hili? Nchi zetu hizi zinatakiwa kujifunza maana ya utawala wa uwazi (transparency) kama kigezo kimoja wapo cha utawala makini (good governance) au haya nayo ni kama demokrasia ilivyo, inabidi tutafute utawala wetu wa Kitanzania tusijifunze kwa wengine?
 
Back
Top Bottom